Friday 31 July 2015

RE: [wanabidii] TULIOMWITA LOWASSA FISADI TUMUOMBE RADHI

Kwa mfumo tuliokuwa nao tangu tupate uhuru asili mia 80% ya watanzania ni mafisadi kila mmoja kwa nafasi yao.  Mkulima ataongeza maji na mawe na takataka ili kilo ziongezeke, mnunuzi atachakachua mizani ili kilo zipunguwe na afisa ugani atabariki uuzaji wa mbolea na madawa feki ali mradi kapata mshiko.  Muuza duka atapanga bei ya ulanguzi.  Mfanyakazi ambaye ana kipata cha Shs 500,000 kwa mwezi atajenga nyumba ya zaidi ya Shs150 million - 1 billion bila mkopo na wote tunaona.  Utakumbuka tulikotoka kulikuwa hakuna mikopo ya nyumba na wengi wetu tumejenga kwa njia za ajabu.

Kwa sasa hivi mshahara wa mfanyakazi hautoshi kuishi zaidi ya wiki mbili lakini unaona wanaishi kwa mwezi mzima na ukiuliza anaishi je anakujibu kwa kubangaiza.

Kinachotakiwa ni kujipanga na kuanza upya kurudi huko nyuma hakutamsaidia mtu yeyote.  Tuanze na katiba ambayo itatoa fursa kwa kila mtanzania kupata kipato halali kutokana na jasho lake.  Tuanze na mkulima mdogo kuzalisha, kusindika na kuuza mazao yaliyoongezewa thamani ili kumwezesha kushiriki kupanga bei badala ya kupangiwa bei.  Kwa mfano tuuwe soko la mpunga na kuuza mchele uliopangwa kwenye madaraja, wakulima wawezeshwe wauze unga wa mahindi badala ya kuuza mahindi, na wauze pamba iliyochambuliwa badala ya kuuza pamba mbegu.

Nchi hii bila umaskini ule uliokithiri inawezekana na ndio mwanzo wa siasa safi na demokrasia ya kweli.

Herment A. Mrema

> Date: Fri, 31 Jul 2015 02:38:17 +0300
> Subject: Re: [wanabidii] TULIOMWITA LOWASSA FISADI TUMUOMBE RADHI
> From: wanabidii@googlegroups.com
> To: wanabidii@googlegroups.com
>
> Report ili bias bana
> Lesian
>
> 'ELISA MUHINGO' via Wanabidii <wanabidii@googlegroups.com> wrote:
>
> >Ukikumbuka sana ripoti aliyoitoa Mwakyembe bungeni ni wazi kuwa tume iliacha kumshitaki Lowasa maana baada ya hapo boss wake ndiye angeambiwa apime mazingira achukue hatua. badala yake tume ilikomea kwa kumwambia Lowasa apime mwenenyewe. Hii ilikuwa wazi kuwa boss wa Lowasa ana kosa ila tume imemstahi labda kwa kuzingatia ushauri wa Nyerere kuwa waziri mkuu kujiuzulku si tatizo sana kama rais kujiuzulu.
> >Hata hivyo ripoti hiyo haikuacha mashaka kuwa Lowasa alikuwa na maslahi katika sakata la Richmond. kwa hiyo kumuomba msamaha Lowasa inabidi uwe huyakumbuki yote na ripoti hatunayo hadharani. Pia kama mtu ukianzia na kuishia kwenye YouTube ambayo nitaisikiliza baadaye unaweza kuishia kumuomba Lowasa msamaba. lakini ukianzia nyuma. ukaja mazindira ya sakata la Richmond ukapima mazingira ya uchunguzi wa TAKUKURU kuhusu richmond na ripoti yake kukataliwa ba watu ikiwa ni bunge pia. Ukakumbuka picha z\ bunge na ukamkumbuka Lowasa baada ya bunge kuamua kuunda tume. Ukikumbuka zawaqdi alizokuwa akitoa siku za karibuni. Michango makanisani na misikitini. Ukikumbuka jinsi alivyobanwa akasema ni marafikizake wanampa lakini hakusema wanatarajia nini kwake. ukimumbuka mateso ya mtandao tuliyoyapata Huwezi kumuomba msamaha maana hapo utakuwa unapalilia njia yake kuelekea Ikulu na kulitumbukiza taifa kuongozwa na mtandao uliotutesa mia\ka hiiyote 10. Utakuwa
> > unaelekea kukivunja chama kikuu cha upinzani kilichomkaribisha maana baada ya yeye kwenda Ili;u kitabaki jina. Hii itakuwa jinai kwa vizazi vijavyo na nadhni tusione aibu kuepuka hilo
> >--------------------------------------------
> >On Thu, 7/30/15, 'ananilea nkya' via Wanabidii <wanabidii@googlegroups.com> wrote:
> >
> > Subject: [wanabidii] TULIOMWITA LOWASSA FISADI TUMUOMBE RADHI
> > To: mabadilikotanzania@googlegroups.com
> > Cc: "WANA BIDII" <wanabidii@googlegroups.com>
> > Date: Thursday, July 30, 2015, 2:43 AM
> >
> >
> > Nimemsikiliza Edward  Lowassa  kwenye you tube
> > tuliyowekewa humu jukwaani akiulizwa maswali na wanahabari
> > kuhusu kashfa ya Richmond iliyotokea alipokuwa Waziri Mkuu
> > miaka minane iliyopita. Kulingana na  majibu aliyoyatoa
> > hata mimi kama mwanahabari niliwahi kumwita fisadi kwa
> > sababu ya  kashfa hiyo. Lakini kulingana na maelezo
> > aliyoyatoa ninakiri nilifanya dhambi maana kumsingizia mtu
> > uongo ni dhambi na binafsi baada ya kusikia upande wake mimi
> > kwa upande wangu namuomba radhi.
> >  
> > Kumbe kinara wa  kashfa ya Richmond alikuwa bosi wake.
> > Lo!  Sasa inaingia akilini ni kwa nini TOR za Mwakyembe
> > hakikumuweka Lowassa kama sample ya kuhojiwa kashfa ya
> > Richmond ilipotokea. Lakini kwa unyenyekevu Lowassa
> > alijiuzulu kuinusuru serikali nzima  isianguke. Mungu
> > mwema miaka minane  baadaye ukweli kamili wa Richmond
> > unajulikana. Kama ulichokisema ni kweli Lowassa, Mungu
> > atakupigania kwa sababu ni wewe  na Mzee Mwinyi peke
> > yenu mna rekodi ya kujiuzulu kuonyesha uwajibikaji kutokana
> > na nafasi zenu na siyo kosa mlilolitenda  ninyi
> > wenyewe. Viongozi wengine mpaka umma upige kelele sana ndipo
> > wajibaraguze kujiuzulu mfano kashfa ya escrow 2014. Sasa
> > ninaelewa ni kwa nini baadhi ya watu wana hofu baada ya
> > LOwassa  kukubaliwa na UKAWA kuwa mgombea Urais.
> >
> > Namshukuru sana aliyetuwekea hii you-tube huku jukwaani
> > maana baadhi yetu ambao hatuko site tungeweza kuendelea
> > kufanya uchambuzi wetu kwa kutumia habari nusu nusu
> > tulizopewa miaka iliyopita kuhusu kashfa ya Richmond.
> >
> > Ananilea Nkya
> >  E-mail:ananilea_nkya@yahoo.com
> >
> > --
> > Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
> >
> > Kujiondoa Tuma Email kwenda
> > wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com 
> > Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
> >
> > Disclaimer:
> > Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility
> > for any legal consequences of his or her postings, and hence
> > statements and facts must be presented responsibly. Your
> > continued membership signifies that you agree to this
> > disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
> > ---
> > You received this message because you are subscribed to the
> > Google Groups "Wanabidii" group.
> > To unsubscribe from this group and stop receiving emails
> > from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
> > For more options, visit
> > https://groups.google.com/d/optout.
> >
> >--
> >Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
> >
> >Kujiondoa Tuma Email kwenda
> >wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
> >
> >Disclaimer:
> >Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
> >---
> >You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
> >To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
> >For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.
>
> --
> Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
>
> Kujiondoa Tuma Email kwenda
> wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
>
> Disclaimer:
> Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
> ---
> You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
> To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
> For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

0 comments:

Post a Comment