Wednesday 28 September 2016

Re: [wanabidii] Hoja 11 zamrejesha Prof. Lipumba CUF

Hivi uzalendo kwa nchi yako lazima uwe mwenyekiti wa chama hicho hicho. kwani hawezi kuanzisha chama kingine na akatafuta wafuasi wengine? there's must be something fishy behind our Prof. 

Kinachokera zaidi ni msomi ambaye angeweza kuisaidia nchi kutokana na profession yake lakini huu uking'ang'anizi wake naona kama anadhalilisha taaluma yake

2016-09-27 15:04 GMT+03:00 'ELISA MUHINGO' via Wanabidii <wanabidii@googlegroups.com>:
Sio Emma. Msajili hakuamua.. Amesema kilichopo.
Walimpelekea malalamiko. (waliompelekea walitaka awasaidie kutafsiri kinachowashinda) Akaamua kuwasikiliza waye nza akawatangazia kwa mujibu wa malalamiko hyao na kwsa kuzingatia katiba na myongozo waliyojiwekea basi Lipumba ni mwenyekit. Ni kama kumu liza kuwa leo ni siku gani> Akikujibu ni Jumanne hawi yeye kaifanya jumanne bali ndiyo
--------------------------------------------
On Sun, 9/25/16, Emmanuel Muganda <emuganda@gmail.com> wrote:

 Subject: Re: [wanabidii] Hoja 11 zamrejesha Prof. Lipumba CUF
 To: "wanabidii@googlegroups.com" <wanabidii@googlegroups.com>
 Date: Sunday, September 25, 2016, 8:35 PM

 Suali
 linalouliza ni lini msajili wa vyama akawa na mamlaka
 kuamulia vyama vya siasa mambo yao ya
 ndani?em
 2016-09-25 9:34 GMT-04:00
 'Lesian' via Wanabidii <wanabidii@googlegroups.com>:
 Mamluki
 wa ccm na kwa kua anatumiwa lazima watafute namna ya
 kuhakikisha anakuja kuharibu ukawa
 Bytheway...mgogoro huu una lengo la kuharibu
 ukawa na haswa Chadema lakini kwa navyofaham chadema
 wanalijua hilo, kwa kua mzee seif nae kashindwa na huyu ma
 luki wake, sasa bora watimke ukawa, na wale watu wanaoamini
 ktk mabadi.iko walioko Cuf warud chadema CUF bora iishie
 hapo Chadema in uwezo wa kusonga mbele yenyewe bila hawa
 mamluki
 Wanaofurahia ni ccm kwamba
 wameshinda lakini ukitizama kwa jicho la ndani utaona
 tu.....lipumba na pumba zake anavyotumika kuua jitihada za
 upinzani nchini......aluta continuaaaaa

 'mpombe mtalika' via
 Wanabidii <wanabidii@googlegroups.com>
 wrote:

 HOJA 11 zilizotolewa na
 Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, Jaji
 Francis Mutungi, zimetosha kumrejesha katika wadhifa wake,
 Mwenyekiti
 'aliyejiuzulu' wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa
 Ibrahim Lipumba.

 Mbali ya Lipumba viongozi wengine ambao msimamo wa
 Msajili
 unawarejesha madarakani moja kwa moja baada ya kusimamishwa
 na Baraza
 Kuu la Uongozi la CUF, katika kikao chake cha Agosti 30,
 mwaka huu
 kilichofanyika jijini Dar es Salaam ni Naibu Katibu Mkuu
 Bara Magdalena
 Sakaya ambaye pia ni Mbunge wa Kaliua na Naibu Mkurugenzi wa
 Habari
 Taifa, Abdul Kambaya.
 Wengine ni Mbunge wa Mtwara, Maftaha Nachuma, wajumbe
 wa Baraza Kuu
 Taifa, Masudi Omari Mhina, Thomas Malima, Ashura Mustafa na
 Kapasha
 Kapasha. Pia Musa Haji Kombo, Habibu Mnyaa na Haroub Shamis
 ambao
 wataendelea kuhesabika kama wanachama halali wa chama
 hicho.
 Katika barua yake kwa viongozi wa CUF, Msajili alieleza
 kuwa amefikia
  msimamo wake huo baada ya kupata nafasi ya kusikiliza pande
 zote
 zinazosigana katika mgogoro huo wa uongozi ndani ya chama
 hicho.
 Alisema katika kufikia maamuzi hayo amezingatia Mamlaka
 na wajibu wa
 Msajili kushughulikia mgogoro huo, Kujiuzulu kwa Profesa
 Lipumba,
 Profesa Lipumba kutengua barua yake ya kujiuzulu, Uhalali wa
 Mkutano
 Mkuu Maalumu wa CUF wa Agosti 21, mwaka huu na baadhi ya
 wajumbe wa
 Mkutano Mkuu Maalumu kuhitaji Profesa Lipumba aitwe katika
 chumba cha
 mkutano kujieleza.
 Nyingine ni uhalali wa kura zilizopigwa kukubali au
 kukataa Profesa
 Lipumba kujiuzulu, uhalali wa kikao cha Baraza Kuu la
 Uongozi la Taifa
 la Agosti 28, mwaka huu, utaratibu wa kuchukua hatua za
 kinidhamu,
 uhalali wa kamati iliyoundwa na Baraza Kuu la Uongozi la
 Agosti 28 ili
 kufanya kazi ya Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti wa Taifa na
 mwisho ni
 kuhusu uhalali wa uteuzi wa viongozi wa kitaifa uliofanywa
 na kikao cha
 Baraza Kuu la Uongozi la Taifa cha Agosti 28, mwaka
 huu.
 Kutokana na hoja hizo, Jaji Mutungi katika taarifa yake
 kwa vyombo
 vya habari jana alisema: "Hivyo, baada ya upembuzi kama
 nilivyobainisha
 hapo juu, msimamo na mwongozo wangu ni kwamba Profesa
 Ibrahim Lipumba
 bado ni Mwenyekiti halali wa Taifa wa CUF na walalamikaji
 wanachama
 waliosimamishwa na waliofukuzwa uanachama wote bado ni
 wanachama halali
 wa CUF.
 "Aidha viongozi ambao uongozi wao uliathirika na
 maamuzi yasiyo
 halali ya kikao cha Baraza Kuu la Uongozi la Taifa cha
 Agosti 28, mwaka
 huu, bado ni viongozi halali. Natumia fursa hii kuwapa
 angalizo kwamba,
 kwa kuwa kamati iliyoundwa kuongoza chama na viongozi
 walioteuliwa na
 kikao hicho si halali na kwa kifungu cha 88 (2) cha Sheria
 ya Vyama vya
 Siasa Sura ya 258, hawaruhusiwi kufanya shughuli yoyote ya
 chama."
 Msajili kushughulikia mgogoro
 Msajili akifafanua hilo alisema kwa kifungu cha 10 (f)
 cha Sheria ya
 Vyama vya Siasa Sura ya 258 kinahitaji chama cha siasa
 kuwasilisha
 orodha ya viongozi wake wa kitaifa kwa Msajili wa Vyama vya
 Siasa na kwa
  kuwa Kifungu 8A (1) kinampa mamlaka Msajili kuhifadhi
 taarifa za
 viongozi wa kitaifa wa vyama vya siasa na kwa kuwa Kanuni ya
 5 (1) ya
 Kanuni za Usajili wa Vyama vya Siasa toleo namba 111 la
 mwaka 1992
 inakitaka kila chama kuwasilisha taarifa kwa Msajili
 panapotokea
 mabadiliko ya uongozi wa kitaifa wa chama husika.
 "Hivyo kwa mustakabali wa majukumu yanayotolewa na
 vifungu hivyo,
 Msajili wa Vyama vya Siasa anao wajibu wa kuhakikisha
 taarifa za
 mabadiliko ya uongozi anazoletewa na chama cha siasa ni
 sahihi, kwa
 maana ya kujiridhisha kuwa mabadiliko hayo ya uongozi
 yamefanyika na
 mamlaka halali ya chama na pia yametekelezwa kwa mujibu wa
 Katiba na
 Kanuni za chama husika. "Kwa mantiki hiyo basi na
 nikijielekeza kwenye
 vifungu vya sheria nilivyoainisha, ni dhahiri kwamba Msajili
 wa Vyama
 vya Siasa anayo mamlaka na wajibu wa kisheria, kuchunguza na

 kujiridhisha kuhusu usahihi wa mabadiliko katika uongozi wa
 kitaifa wa
 chama yaliyofanyika na masuala yote yanayohusiana na
 mabadiliko hayo,"
 alisema Msajili.
 Kujiuzulu kwa Profesa
 Lipumba Kuhusu hilo Msajili alisema kwa mujibu wa Ibara
 ya 117 (2),
 kiongozi wa Chama cha CUF, hata kama mhusika amebainisha
 tarehe ya
 kujiuzulu katika barua yake ya kujiuzulu, atahesabika kuwa
 amejiuzulu
 baada tu ya mamlaka iliyomchagua au kumteua kukubali.
 Alisema kwa mujibu wa Ibara hiyo, ni sahihi kusema
 kwamba Profesa
 Lipumba alikuwa bado ni Mwenyekiti halali wa Taifa wa CUF
 hata wakati wa
  kufanyika kwa Mkutano Mkuu wa Agosti 21, hivyo hata yeye
 kujiita
 Mwenyekiti wa Taifa mstaafu kabla ya kujiuzulu kwake
 kukubaliwa na
 mamlaka husika si sahihi.
 Kutengua barua yake ya kujiuzulu
 Akizungumzia hilo Msajili alisema, "Katiba ya CUF iko
 kimya kuhusu
 hilo, hivyo hapakuwa na kizuizi kwa Profesa Lipumba kutengua
 barua yake
 ya kujizulu kwa kuzingatia ukimya huo kwa upande wa uongozi
 wa CUF
 kuchukua hatua pindi walipopokea barua yake ya kujiuzulu na
 hivyo kutoa
 mwanya kwa mhusika kuitengua barua yake ya kujiuzulu.
 "Si hivyo tu, bali pia barua yake ya kutengua
 kujiuzulu haikukataliwa
  na uongozi wa CUF.Alichoelezwa Profesa Lipumba ni kwamba
 asianze kazi
 tarehe aliyopanga kuanza kazi ili asubiri kwanza Katibu Mkuu
 ashauriane
 na wanasheria wa chama, ambapo mpaka suala hili
 linawasilishwa mbele
 yangu, Profesa Lipumba alikuwa bado hajapewa mwongozo wowote
 kuhusiana
 na barua yake ya kutengua kujiuzulu," alisema
 Msajili.
 Uhalali wa hoja
 Msajili akitoa msimamo wake kuhusu hoja ya uhalali wa
 Mkutano Mkuu wa
  Agosti 21, alisema pamoja na malumbano kuhusu akidi ya
 wajumbe lakini
 kwa vyovyote vile mkutano huo ulikidhi matakwa ya Ibara ya
 114 inayosema
  kuwa ili akidi kutimia idadi ya wajumbe waliohudhuria kikao
 inapaswa
 kuzidi nusu ya wajumbe wote, na hivyo idadi ya wajumbe 700
 ilikidhi
 matakwa ya Katiba.
 Kuhusu hoja ya baadhi ya wajumbe kuhitaji Profesa
 Lipumba aitwe
 katika chumba cha mkutano kujieleza, Msajili alisema hata
 kama Profesa
 Lipumba angekuwa si mjumbe wa Mkutano Mkuu Maalumu ili mradi
 uwepo wake
 yalikuwa ni matakwa ya wajumbe wa mkutano huo, basi alipaswa
 kupewa
 fursa katika mkutano huo kuthibitisha kuwa, barua iliyosomwa
 na Katibu
 Mkuu kuhusu kujiuzulu kwake ni yake na kueleza sababu za
 kujiuzulu na
 hivyo kumkatalia ilikuwa ni kukiuka Ibara ya 116 ya Katiba
 ya chama
 hicho.
 Kwa hoja za uhalali wa kura zilizopigwa kukubali au
 kukataa Profesa
 Lipumba kujiuzulu, Msajili alisema zoezi la kupiga kura za
 kukubali au
 kukataa kujiuzulu kwa Profesa Lipumba lilifanyika katika
 mazingira ya
 vurugu na hivyo kufanya zoezi hilo kukosa uhalali na kutoa
 mfano kuwa
 zoezi la kujua idadi ya wapiga kura kabla ya kupiga kura
 halikufanyika,
 ukizingatia kuwa baada ya vurugu kuzuka, kuna wajumbe
 walitoka nje ya
 ukumbi kuogopa vurugu na watu wasio wajumbe kuingia ndani ya
 ukumbi.
 Kuhusu uhalali wa uteuzi wa viongozi wa kitaifa
 uliofanywa na kikao
 cha Baraza Kuu la Uongozi la Taifa cha Agosti 28, Msajili
 alisema kwa
 mujibu wa Ibara ya 115 (1) iwapo nafasi ya kiongozi yeyote
 ipo wazi,
 basi mamlaka yake ya uteuzi itamteua mtu wa kukaimu nafasi
 hiyo.
 "Kwa mujibu wa Ibara ya 91 (1) (m) mamlaka ya uteuzi
 wa Naibu Katibu
 Mkuu ni Baraza Kuu la Taifa, hivyo laiti uamuzi wa kikao cha
 Baraza Kuu
 la Uongozi Taifa cha Agosti 28 ungekuwa si batili, basi
 uteuzi wa Joran
 Bashange kuwa Kaimu Naibu Katibu Mkuu ungekuwa sahihi, kwa
 maana ya
 kwamba Baraza Kuu la Uongozi lina mamlaka hayo.
 "Hata hivyo kwa upande mwingine, uteuzi wa Mbaraka
 Maharagande kuwa
 Kaimu Naibu Mkurugenzi wa Habari, Uenezi na Mawasiliano kwa
 Umma una
 dosari nao si sahihi kwa sababu kwa mujibu wa Ibara ya 91
 (1) (f)
 mamlaka yake ya uteuzi ni Mwenyekiti wa Taifa na si Baraza
 Kuu la
 Taifa," alisema Msajili na kusema adhabu kwa mtu
 anayefanya shughuli za
 chama bila kufuata taratibu ni kifungo cha miezi sita, faini
 isiyozidi
 Sh milioni moja au vyote kwa pamoja.
 Lipumba atinga ofisini kwa mdundiko
 Katika tukio lingine mchana jana Profesa Lipumba
 alifika katika ofisi
  za chama hicho zilizopo Buguruni jijini Dar es Salaam huku
 akiandamana
 na umati wa wafuasi wa chama hicho huku wakisindikizwa na
 ngoma maarufu
 katika ukanda wa Pwani ya Mdundiko.
 Wafuasi wa Profesa
 Lipumba walianza kukusanyika katika ofisi hizo kuanzia
 asubuhi baada
 ya kupata taarifa za kuwepo kwa barua kutoka kwa Msajili wa
 Vyama vya
 Siasa, ikimtambua mwanasiasa huyo kama Mwenyekiti halali wa
 chama hicho
 kwa mujibu wa Katiba ya chama.
 Ilipotimu saa saba mchana Profesa Lipumba alifika
 katika eneo zilipo
 ofisi hizo akiwa na kundi la wafuasi wake waliokuwa
 wakicheza kwa ustadi
  ngoma ya mdundiko, lakini walikumbana na kizuizi cha
 kuingia ndani
 kutokana na geti kuu kuwa limefungwa.
 Zuio hilo lilidumu kwa muda usiozidi dakika nne, ambapo
 baadaye
 baadhi ya wafuasi wa kiongozi huyo waliamua kuruka ukuta ili
 kuingia
 ndani kumfungulia geti kumwezesha kuingia ndani.
 Wakati matukio hayo yakiendelea, polisi waliokuwa
 wamefika mapema ili
  kudhibiti usalama katika eneo hilo walikuwa wakishuhudia
 wakiwa ndani
 ya magari matatu yaliyokuwa yamesimama kando ya geti,
 wakiwatazama
 wafuasi hao wakitumia nguvu ili kuingia ndani ya ofisi
 hizo.
 Hata hivyo haikuwa kazi rahisi kuingia ndani ya ofisi
 hizo kwani
 wakati wakiendelea kuruka ukuta, zilisikika risasi zikipigwa
 na askari
 wa kampuni binafsi ya ulinzi aliyekuwa analinda ofisi hizo,
 lakini
 alidhibitiwa baadaye na wafuasi hao ambao walimnyang'anya
 silaha na
 kuikabidhi kwa polisi.
 Baadaye wafuasi hao walianza kumpa kichapo askari huyo
 wa ulinzi
 kabla ya wazee wa chama hicho kujitokeza na kumuokoa na
 kulazimika
 kumfungia katika choo kimojawapo cha ofisi hiyo.
 Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya
 kuingia ofisini
 kwake, Profesa Lipumba alisema kurejea kwake kunatokana na
 uamuzi
 uliotolewa na Msajili wa Vyama vya Siasa, huku akieleza
 hatua mbalimbali
  alizochukua tangu alipoandika barua ya kujiuzulu, barua ya
 kutengua
 uamuzi wake na yaliyotokea katika vikao mbalimbali vya chama
 hicho,
 ambazo kimsingi zinamfanya kuwa na sifa ya kuendelea kuwa
 Mwenyekiti
 halali kwa mujibu wa Katiba ya chama hicho.




 --

 Send Emails to wanabidii@googlegroups.com

  

 Kujiondoa Tuma Email kwenda

 wanabidii+unsubscribe@
 googlegroups.com  Utapata Email ya kudhibitisha
 ukishatuma

  

 Disclaimer:

 Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility
 for any legal consequences of his or her postings, and hence
 statements and facts must be presented responsibly. Your
 continued membership signifies that you agree to this
 disclaimer and pledge to abide by our Rules and
 Guidelines.

 ---

 You received this message because you are subscribed to the
 Google Groups "Wanabidii" group.

 To unsubscribe from this group and stop receiving emails
 from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@
 googlegroups.com.

 For more options, visit https://groups.google.com/d/
 optout.






 --

 Send Emails to wanabidii@googlegroups.com

  

 Kujiondoa Tuma Email kwenda

 wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com  Utapata Email ya
 kudhibitisha ukishatuma

  

 Disclaimer:

 Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility
 for any legal consequences of his or her postings, and hence
 statements and facts must be presented responsibly. Your
 continued membership signifies that you agree to this
 disclaimer and pledge to abide by our Rules and
 Guidelines.

 ---

 You received this message because you are subscribed to the
 Google Groups "Wanabidii" group.

 To unsubscribe from this group and stop receiving emails
 from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.

 For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.


--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com

Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com  Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma

Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

0 comments:

Post a Comment