Thursday 8 September 2016

Re: [wanabidii] Kumbe Mbowe msaliti wa nguvu ya umma?

Hapa sioni mjadala ulioenda shule hata kidogo!

2016-09-08 12:38 GMT+03:00 'ELISA MUHINGO' via Wanabidii <wanabidii@googlegroups.com>:
Kosa la kuchanganya mtu na taasisi katika sakata hili lilianza pale Mbowe aliposema NHC imefanya hivyo kwa kuwa yeye ni M'kiti wa chadema. Hapo ndipo ilipoanzia kujadili deni hilo na uongozi wa chama
--------------------------------------------
On Thu, 9/8/16, 'misangocharles' via Wanabidii <wanabidii@googlegroups.com> wrote:

 Subject: Re: [wanabidii] Kumbe Mbowe msaliti wa nguvu ya umma?
 To: wanabidii@googlegroups.com
 Date: Thursday, September 8, 2016, 8:11 AM

 Nadhani tuweke pembeni wakati
 mwingine ushabiki wenye makengeza. Kumchanganya mtu na
 taasisi sidhani kama ni sahihi. Huwezi kushutumu watu kwa
 ujumla wake kwa kosa la mtu mmoja. Deni lake lielekezwe
 kwake na sio kwa taasisi.
 Hivi hamkumbuki, kuna kada na kiongozi maarufu wa CCM
 alituhumiwa kusambaza arv feki na akajipatia fedha lukuki.
 Huyu aliyeua watu kwa dawa feki kwa nini hakuhusishwa na CCM
 na mbona povu halikututoka kiasi hiki? Sina maana ya
 kumtetea Mbowe maana hanisaidii kwa lolote na niseme wazi
 niliacha kazi kwake kwa sababu sikukubaliana na mambo fulani
 yasiyo sawa kwangu.
 Lkn hii hainifanyi nisiseme ninapoona tunachanganya hoja ya
 msingi kwa kuchafua na wasiohusika

 Sent from my Huawei Mobile

 'mpombe mtalika' via Wanabidii
 <wanabidii@googlegroups.com> wrote:


        SHIRIKA la Nyumba la Taifa (NHC) limefanya uamuzi mgumu
 dhidi ya
 Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema),
 Freeman
 Mbowe. Uamuzi wa kumshinikiza alipe malimbikizo ya deni lake
 la kodi kwa
  shirika hilo la taifa, deni la zaidi ya shilingi bilioni
 moja. 



        Mbele ya NHC, Mbowe kupitia kampuni yake ya Mbowe Hotels
 Ltd ni mdaiwa
 sugu na hili limethibitishwa na Mkurugenzi Mkuu wa NHC,
 Nehemia Mchechu
 katika mkutano wake na waandishi wa habari jijini Dar es
 Salaam, Agosti
 24, mwaka huu.


        Pengine si tu mbele ya NHC bali hata mbele ya Watanzania
 wengi, Mbowe
 ni mdaiwa sugu kwa kurejea takwimu hizo rasmi za NHC, ambalo
 ni shirika
 mali ya wananchi linalojiendesha kibiashara ili hatimaye
 kutoa gawiwo
 kwa serikali kuu na kuboresha hali za makazi ya wananchi
 nchini.



        Kwa
 hiyo na kwa vyovyote vile, hujuma yoyote dhidi ya shirika la
 umma
 ikiwamo hii ya kutolipa kodi ni sawa na hujuma dhidi ya umma
 ambao chama
  anachokiongoza Mbowe kimekuwa kikijinadi kupitia salamu
 yake ya "nguvu
 ya umma."


        Tayari Mbowe amekwishafanya utetezi dhidi ya tuhuma hizi za
 kuitwa
 mdaiwa sugu wa NHC. Kwa bahati mbaya, utetezi wake umebeba
 siasa,
 pengine kwa sababu tu ya kutafuta kichaka na kuficha aibu ya
 kihistoria
 ya kuwa miongoni mwa wadaiwa vinara na sugu wa NHC.



        Katika utetezi wake wa Agosti 24, mwaka huu,
 baada ya Mkurugenzi Mkuu
 wa NHC kutangaza kuwa mwanasiasa huyo ni mdaiwa sugu, Mbowe
 alitoa
 taarifa kwa umma akijitetea kwa kupiga porojo za kisiasa,
 kwanza akikiri
  kuwapo deni ama mgogoro wa kibiashara wa miaka mingi baina
 ya kampuni
 yake na NHC.



        "Kumekuwepo
 na ukakasi wa muda mrefu kuhusiana na mkataba wetu wa
 umiliki, uendelezaji na uendeshaji wa jengo hili
 unaochagizwa na msimamo
  wangu wa kisiasa," anasema Mbowe na kuendelea; "Haki na
 Uhuru wetu wa
 kufanya biashara kama raia wengine umekuwa ukiingiliwa mara
 kwa mara
 katika mazingira yanayoambatana na vitisho kiasi ambacho
 maamuzi kadhaa
 hayafanyiki kwa hofu ya kisiasa kwamba itakuwa kumwongezea
 nguvu
 mpinzani."



        Anasisitiza
 akitaka Watanzania waelewe kuwa hadaiwi. Bado anapiga siasa
  akisema; "Sitafungwa fikra, sitafungwa mdomo na sitaacha
 kuutetea
 ukweli, haki na demokrasia katika nchi hii kwa misingi ya
 kulinda
 kinachodhaniwa ni maslahi yangu ya kibiashara." Anasema
 wafanyabiashara
 wengi wamekuwa wakifungwa fikra na midomo ndani ya nchi hii
 kwa kuogopa
 hila na ghiliba za watawala.



        Anasema;
 "Ni heri kufa masikini nikiwa nimesimamia ukweli, kuliko
 kuishi tajiri niliyetawaliwa na ubinafsi, woga, hofu na
 ubatili."


        Lakini pamoja na kauli hiyo ya kukanusha kudaiwa katikati
 ya hoja za
 kisiasa, NHC kwa niaba ya Watanzania, uongozi wake umesimama
 imara kudai
  haki ya umma. Unaweza kujiuliza Mbowe ni mtu wa namna gani
 pale maslahi
  yake yanapokinzana na umma? Je, yuko tayari kwa kiasi gani
 kulinda
 maslahi yake bila kujali athari kwa umma? Mbowe anapaswa
 kufahamu haya.



 NHC
 kudai wadaiwa si siasa


        Pengine historia ya Shirika la Nyumba la Taifa (NHC)
 imemkalia kando
 Mbowe huyu wa Chadema. Nitamkumbusha jambo ili afute hoja
 zake nyepesi
 kwamba kitendo cha NHC kudai wadaiwa sugu ni ajenda ya
 kisiasa.



        Takriban
 miaka 44 iliyopita, yaani mwaka 1972, Freeman Mbowe akiwa na

 umri wa miaka 11 tu kwani alizaliwa Septemba 14, 1961,
 Shirika la Nyumba
  la Taifa lilifanya uamuzi mzito wa kudai wadaiwa wake sugu.



        Katika
 kutangaza uamuzi wake huo, Ofisa Uhusiano wa NHC kwa wakati
 huo,
  E. Musabalala, aliutangazia umma namna shirika hilo la umma

 litakavyolinda maslahi ya umma. Akasema shirika limefanya
 uamuzi wa
 kuunda kamati maalumu nchini ili hatimaye kuwafukuza
 wapangaji ambao ni
 wadaiwa sugu, waliolimbikiza kodi za shirika hilo.



        Kwa kumkumbusha tu Mbowe ni kwamba, kamati ya
 kwanza kuundwa ilikuwa na
  watu 14 na ilifanya uchambuzi kwa wapangaji sugu katika
 nyumba za
 shirika hilo la umma maeneo ya Ilala, Upanga, Ukonga na
 Barabara ya
 Morogoro, mjini Dar es Salaam. Kazi hiyo ilianza Oktoba,
 mwaka 1972.



        Na uamuzi huo wa kuuda kamati ulikuwa wa
 mwendelezo tu kwa sababu
 tayari uamuzi wa shirika kuwafukuza wapangaji wadaiwa sugu
 ulikwishaanza
  mwezi Mei, mwaka huo wa 1972.



        Kwa
 hiyo, Mbowe asilete siasa kwamba anakandamizwa kwa sababu
 eti ni
 mwanasiasa wa upinzani. Ajue tu kwamba rekodi zinaonesha
 uamuzi wa NHC
 kushughulika na wadaiwa sugu kama yeye, wenye kufanya hila
 za hapa na
 pale, ulianza zamani tena akiwa na umri wa miaka 11.
 Asimuonee
 Mkurugenzi Mkuu wa NHC, Mchechu, ajue shughuli hii ni pevu,
 uamuzi wa
 busara kwake ni kulipa fedha za umma, asiishie tu kutamka
 jukwaani ….
 Peopleees … power, bali ajue nguvu ya umma sasa inadai
 chake kupitia
 NHC.



 Si wa
 kwanza kutupiwa virago


        Katika utetezi wake, Mbowe anasema ametupiwa virago na
 kwamba
 utekelezaji wa uamuzi wa NHC kupitia dalali wake ni wa
 uonevu kwake,
 watu wake wanadai hata taasisi mbalimbali za serikali
 zinadaiwa lakini
 kwa nini hazikutupiwa virago kama yeye. Anahoji, iweje yeye
 pekee na
 anahitimisha kwamba anapigwa siasa.



        Hapa niweke wazi kwamba kuna tatizo la
 kumbukumbu kuhusu NHC kufanya
 uamuzi mgumu kwa wateja wake ambao wadaiwa sugu, wadaiwa
 wanaohujumu
 umma. Nitajadili mambo mawili muhimu hapa.



        Mosi,
 Mbowe akumbuke kuhusu kile kilichoandikwa katika gazeti
 linalomilikiwa na familia yake la Tanzania Daima la Oktoba
 12, mwaka
 2013, habari iliyoandikwa na mwandishi na mpiga picha wa
 gazeti hilo,
 Joseph Senga (Mungu amrehemu).


        Habari ile ilieleza uamuzi mgumu wa NHC kuwatupia virago
 madaktari
 wawili wa Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa sababu mwajiri
 wao, yaani
 Muhimbili kulimbikiza deni.



        Madaktari
 hao wawili ni Dk. Wambura Chacha na mwenzake bingwa wa
 upasuaji katika Kitengo cha Mifupa (MOI), Profesa Joseph
 Kahamba. Hawa
 wanaweza kuwa mashahidi kwamba NHC haifanyi siasa, bali
 inadai fedha za
 umma.



        Madaktari
 hao, kwa mujibu wa habari hiyo ya Tanzania Daima walikuwa
 wakiishi katika nyumba namba 355 mali ya NHC, Mtaa wa Umoja
 wa Mataifa
 jijini Dar es Salaam. Mwajiri wao alikuwa amelimbikiza deni
 la miezi 15
 lililokuwa limefikia Sh 9,738,000. Sasa itakuwa Mbowe mwenye
 deni la
 bilioni takriban 1.2? Halafu unadai eti siasa!



        Operesheni hiyo ya wakati ule ya kudai fedha za
 umma kutoka kwa wadaiwa
  sugu kama Mbowe iliendeshwa na Meneja wa Kitengo cha
 Kukusanya Madeni
 wa NHC, Japhet Mwanasenga. Kwa wakati ule wa operesheni hiyo
 Muhimbili
 ilikuwa ikidaiwa Sh milioni 135.6, yakiwa ni malimbikizo ya
 malipo ya
 pango kwa vipindi tofauti.



        Kwa
 hiyo ya Mbowe na wenzake kwamba anaonewa kwa kutupiwa virago
 wakati
  serikali na taasisi zake ni wadaiwa sugu haina ukweli, bali
 ni porojo
 za kusaka huruma ya kisiasa. Kama ataweka kumbukumbu zake
 vizuri,
 atakumbuka pia kwamba hata Wizara ya Habari, Utamaduni na
 Michezo wakati
  huo ikiongozwa na

 Waziri Dk. Emmanuel Nchimbi, ilitupiwa virago na
 NHC.
  Asilete ndoto za mchana.


        Pili, kuna jambo analopaswa kulielewa Mbowe. Kwamba
 serikali na taasisi
  zake zinaweza kufanya mawasiliano ambayo Mbowe kama mmoja
 wa wadaiwa
 sugu si lazima apewe taarifa za namna wadaiwa wenzake
 walivyojipanga
 kulipa madeni yao. Serikali inayo bajeti yake na hili Mbowe
 anapaswa
 kulijua vizuri kwa sababu ni kiongozi wa kambi rasmi ya
 upinzani
 bungeni, na ajue yeye kama mtu binafsi au kampuni zake
 bajeti yake ni
 siri yake.



        Kwa
 hiyo si sahihi kudai kuwa umetupiwa virago na wenzake
 hawajatupiwa.
  Usahihi kuwa, na kwa kweli kwa mtu makini anapaswa kutambua
 kuwa jambo
 la msingi ni kulipa deni, tena deni linalohusu fedha za umma
 si
 kujitetea kuhusu muda wa kulipa kwa wadaiwa wenzako. Kila
 mdaiwa anaweza
  kuwa na makubaliano tofauti na anayedai.



 Haenei
 katika ubepari, ujamaa


        Chadema, ambacho Mbowe ni mwenyekiti wake kinajinadi kuwa
 na mrengo wa
 kibepari. Ni kweli ubepari unahusu kutumikisha watu ili
 bepari anufaike
 zaidi lakini katika huo huo ubepari, hasa kwa mabepari wa
 kweli ni
 lazima unayemtumikisha aendelee kula, kubaki katika afya
 njema ili
 endelee kuishi na uendelee kumtumikia. Hili inaonekana
 halimo kichwani
 mwa Mbowe, wale anaojinadi nao kuwa ni nguvu ya umma sasa
 hao hao ndio
 wanaomdai kodi aliyolimbikiza kupitia shirika lao la umma
 – NHC.



        Tazama,
 utu wa mabepari wa kale kwa kurejea kijiji Saltaire, kule
 Shipley, kijiji ambacho ni sehemu ya Jiji la Bradford, pale
 Yorkshire ya
  Magharibi, England, miaka 163 iliyopita, yaani mwaka 1853
 au kijiji cha
  Port Sunlight kule Merseyside, England, mwaka 1888, miaka
 128
 iliyopita. Hoja ni kwamba mabepari hawa wa kale walisaidia
 umma wao
 karne zaidi ya moja lakini Mbowe, Mwenyekiti wa chama cha
 kibepari,
 anadaiwa kodi ya umma na bado anakuwa mbishi. Ni kama vile
 hafafani hata
  na ubepari wa kale enzi za kikoloni, achilia mbali upebari
 wa kisasa.



        Wakoloni
 ambao mwaka 1885, baada ya ripoti ya Tume ya Kifalme England

 walianzisha, kwa mara ya kwanza, mpango wa makazi kwa
 wafanyakazi
 kupitia sheria iliyoitwa Housing of the Working Classes Act
 ya mwaka
 1885. Sasa Mbowe hajui kwamba lengo la NHC kudai kodi ya
 umma ni
 kusaidia wafanyakazi wa nchi hii katika suala la makazi,
 wafanyakazi
 ambao Rais John Magufuli aliahidi kuboresha maslahi yao,
 maslahi ambayo
 bila shaka ni pamoja na makazi bora kwa kadiri
 inavyowezekana.



        Mbowe kalipe deni lako, usikwaze umma. Umma
 unahitaji kufaidika na
 jengo ulilohodhi kwa kulimbikiza kodi, lile jengo lililopo
 makutano ya
 mitaa ya Mkwepu na Indira Gandhi, katikati ya jiji la Dar es
 Salaam.
 Hima hima Mbowe, jitahidi kuheshimu na kutunza haki ya kiapo
 ya uadilifu
  na maadili ya utumishi wa umma, kwa nafasi yako kama
 mbunge, kiongozi
 wa kambi ya upinzani bungeni na zaidi ya hapo, mwenyekiti wa
 chama kikuu
  cha upinzani nchini. Lipa deni kuleta utulivu ndani ya umma
 wa
 Watanzania, uamuzi wa kulipa unaweza kusaidia kuepusha
 mpasuko kitaifa
 na kifamilia.

 Raia Mwema




 --

 Send Emails to wanabidii@googlegroups.com

  

 Kujiondoa Tuma Email kwenda

 wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com  Utapata Email ya
 kudhibitisha ukishatuma

  

 Disclaimer:

 Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility
 for any legal consequences of his or her postings, and hence
 statements and facts must be presented responsibly. Your
 continued membership signifies that you agree to this
 disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.

 ---

 You received this message because you are subscribed to the
 Google Groups "Wanabidii" group.

 To unsubscribe from this group and stop receiving emails
 from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.

 For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.




 --

 Send Emails to wanabidii@googlegroups.com

  

 Kujiondoa Tuma Email kwenda

 wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com  Utapata Email ya
 kudhibitisha ukishatuma

  

 Disclaimer:

 Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility
 for any legal consequences of his or her postings, and hence
 statements and facts must be presented responsibly. Your
 continued membership signifies that you agree to this
 disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.

 ---

 You received this message because you are subscribed to the
 Google Groups "Wanabidii" group.

 To unsubscribe from this group and stop receiving emails
 from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.

 For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.


--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com

Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com  Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma

Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

0 comments:

Post a Comment