Wednesday 30 March 2016

[wanabidii] Karata Pekee Kwa CHADEMA Kwa Sasa!

Baada ya kuizika rasmi Ajenda/karata ya ufisadi hasa pale walipomsafisha na kumkumbatia  Edward Lowassa karata pekee iliyobaki ni ku-sympathise na Wazanzibari hasa kuhusu suala la Muungano!

CUF ni wapinzani wakuu wa Muungano, kwa hiyo wamepata mwenza huku Bara!
CHADEMA hawana mpango na kutawala nchi kwa sasa kwa kuwa wana lengo la kugawa nchi! Kazi yao ni kushangilia failures huku kukiwa na success wako kimya kama wamemwagiwa maji.

Anayofanya Magufuli mazuri wako kimya, limekuja la MCC eti ndo wanatoa tamko!
Kama upinzani ni kupinga tu basi watabaki wapinzani milele! Endeleeni na kick yenu ya kuwapa joto Wazenj!

0 comments:

Post a Comment