Wednesday 30 March 2016

Re: [wanabidii] KUHUSU MCC KUSITISHA MSAADA WA MCC 2 NA SHUGHULI ZAKE TANZANIA: MTIZAMO

Mbowe na ukawa walikuwa wanatulaghai na mabadiliko ya kuzunguusha
mikono wtz tukawashitukia

On 3/31/16, Joseph Ludovick <josephludovick@gmail.com> wrote:
> Polepole siyo mtu wa kufukuzia ukuu wa wilaya. Na mbowe aliposema
> hatuhitaji kuishi kwa misaada ya MCC alikuwa anafukuzia nini?
> On Mar 30, 2016 9:59 PM, "Emmanuel Muganda" <emuganda@gmail.com> wrote:
>
>> Achana naye Polepole. Anafukuzia ukuu wa wilaya.
>> em
>>
>> 2016-03-30 9:33 GMT-04:00 fadhil fadhil <fadhil.fadhil96@gmail.com>:
>>
>>> KUHUSU MCC KUSITISHA MSAADA WA MCC 2 NA SHUGHULI ZAKE TANZANIA: MTIZAMO
>>>
>>> Nianze na nukuu hizi mbili kuntu za Baba wa Taifa Mwalimu Julius K.
>>> Nyerere- Mwenyezi Mungu amrehemu.
>>>
>>> "Democracy is not a bottle of Coca-Cola which you can import. Democracy
>>> should develop according to that particular country". June 1991 in Rio
>>> De
>>> Janeiro, Brazil
>>>
>>> "Demokrasia sio chupa ya Coca-Cola ambayo unaweza kuagiza. Demokrasia
>>> lazima ikue na kuendelezwa kulingana na nchi husika". Juni 1991 Rio De
>>> Janeiro, Brazil (Tafsiri ni yangu)
>>>
>>> "No nation has the right to make decisions for another nation; no people
>>> for another people". From 'A Peaceful New Year' speech, Tanzania,
>>> January
>>> 1968
>>>
>>> "Hakuna Taifa lina haki ya kufanya maamuzi juu ya Taifa lingine; wala
>>> watu juu ya watu wengine ". Hotuba ya Amani ya Mwaka Mpya, Tanzania,
>>> Januari 1968 (Tafsiri ni yangu)
>>>
>>> Hili la Marekani na uamuzi wa MCC ni jambo la mpito na haliwezi kuua
>>> mahusiano yetu na Marekani. Tanzania na Marekani zinashirikiana kwa
>>> mambo
>>> mengi na MCC ni sehemu tu tena ni eneo jipya la ushirikiano. Uamuzi huu
>>> ni
>>> jaribio kwa uhuru wa Taifa letu. Hakuna namna nyingine ila kushinda hili
>>> kama tulivyoshinda mengine huko nyuma. Kwa wale ambao wameuona umri
>>> watakumbuka namna tulivunja uhusiano na Ujerumani Magharibi 1964 pale
>>> walipotaka kuwa na kauli hasi dhidi ya Muungano wa Tanganyika na
>>> Zanzibar.
>>>
>>> Tulivunja uhusiano na Ujerumani Magharibi baada ya kutaka kuingilia
>>> Uhuru
>>> wa Mataifa Mawili huru yaliyoamua kuungana na kuunda Nchi Mpya ambayo
>>> leo
>>> tunajivunia, Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. 1965 Tulivunja uhusiano na
>>> Uingereza kufuatia na kitendo cha wazungu wachache kujitangazia Uhuru
>>> (Unilateral Declaration of Independence) kule Rhodesia na uingereza
>>> kukaa
>>> kimya na kushindwa kuchukua hatua stahiki.
>>>
>>> Tulivunja Uhusiano na Uingereza kuieleza Dunia kwamba Uhuru wa nchi za
>>> Afrika ni kipaumbele muhimu kwa Tanzania. Jambo tunalopaswa kufahamu ni
>>> kuwa MCC 2 toka mwanzo imekuwa ni mtihani dhidi ya uhuru wetu. Napenda
>>> ieleweke kwamba kipindi hiki kilichotokea sio kuvunjika kwa uhusiano
>>> wetu
>>> na Marekani bali taasisi ya MCC ndio imesitisha msaada wao kwetu, lakini
>>> mahusiano yetu na marekani bado yako pale pale, na si Marekani au
>>> Tanzania
>>> inayoweza kuugharimu uhusiano wetu.
>>>
>>> MCC 1 ilikuwa ni chambo cha kutuvuta na tulipewa bila masharti tena hela
>>> nyingi dola milioni 698 na ni fedha tulizopewa moja kwa moja na kupewa
>>> uhuru wa kuamua tuzitumieje. Tanzania ilitakiwa kuainisha maeneo kisha
>>> wao
>>> wanatoa hela. Ndio maana miradi kama ile barabara ambazo hazikuwa
>>> zikipata
>>> ufadhili kwa kuwa hazikuonekana ni za kiuchumi na miradi ya maji ya
>>> Morogoro na kwingineko iliingizwa humu na kupata ufadhili. MCC 2 sio
>>> hivyo.
>>> Kwenye MCC 2 walengwa wakubwa ni sekta binafsi ya Marekani, hapa kuna
>>> mtego
>>> hapa, hapa ni biashara hapa.
>>>
>>> Mchakato wa MCC 2 ulipoanzishwa, wafanyabiashara kwa kushirikiana na
>>> Maseneta wakaanzisha hoja kuwa kwanini Marekani inatoa fedha kwa
>>> ufadhili
>>> katika nchi ambazo China ndio wenye kufaidika na fedha hizo? Wakaleta
>>> hoja
>>> ya kuwa Serikali ya Marekani ifanye jitihada ya kuweka fedha kwa
>>> kusaidia
>>> Sekta Binafsi ya Marekani kupenya Afrika.
>>>
>>> Ukaitishwa mkutano wa US-Africa Summit na agenda kubwa ikawa Power
>>> Africa. Katika Power Africa, Marekani ikalichagua eneo la Nishati (si
>>> uzalishaji viwanda) kwa kutambua kuwa ndio eneo pekee wanaloweza
>>> kushindana
>>> na wachina. Wakasema wataelekeza fedha huko kuisaidia Afrika kutatua
>>> tatizo
>>> la nishati ambalo ndio pembejeo ya viwanda. Wakaweka sharti kuwa fedha
>>> hizo
>>> na miradi hiyo itatekelezwa na Sekta Binafsi ya Marekani.
>>>
>>> Ndio sababu wengi wenu mtakumbuka hata Rais Obama alitangazia dhamira
>>> ile
>>> pale Ubungo kwenye Mitambo ya Symbion Power na sio kwamba alipenda
>>> kwenda
>>> kutembea Ubungo. Kuanzia hapo kumekuwepo na shinikizo kubwa sana na
>>> masharti magumu na yenye kuhamahama (shifting goal post) kutaka kuibaka
>>> sekta ya nishati nchini ikiwemo mageuzi ya TANESCO. Zikaainishwa hatua
>>> kadhaa,ambazo utekelezaji wake baadhi ni kisheria na kisera na hivyo
>>> haziwezi kwenda kwa deadline walizotaka. Kila bodi ikikutana wanaibua
>>> hiki
>>> na kile lakini wakisema hela watatoa. Hela hizi zikawa zimeshikiliwa
>>> kama
>>> chambo ukisogelea zinasogea, ni sawa na ule mchoro wa Mpanda Punde
>>> aliyeshika fimbo yenye majani na akiielekeza mbele ya punda, kwamba
>>> punda
>>> ataendelea kuyafuata majani akidhani atayafikia kumbe ndio anaupiga
>>> mwendo.
>>> Hatimaye wakasema wanasubiri uchaguzi mkuu jambo ambalo halihusiani na
>>> madai ya mwanzoni. Baada ya uchaguzi wakaibuka na suala la Zanzibar.
>>>
>>> Hivyo, uamuzi wao wa leo ni uamuzi uliotarajiwa. Pia ni uamuzi wenye
>>> madhara kwa sekta binafsi ya Marekani pia ambayo ndio ilikuwa itekeleze
>>> miradi hiyo. Kama Taifa ni muhimu kulinda utu na uhuru wetu. Ndio msingi
>>> wa
>>> sera yetu ya nje toka mwanzo na hata sasa. Tumetofautiana na Marekani
>>> katika hili tutapatana katika mengine. Ndio uhai wa maisha ya
>>> diplomasia.
>>>
>>> Wao nao wanayo hadhira ya wapiga kura wao wanayojaribu kuituliza huko
>>> nchini kwao kwa uamuzi huu. Tunapaswa kuheshimu uamuzi wao kama ambavyo
>>> wanapaswa kuuheshimu wetu. Hatimaye baadae tutapatana. Marekani
>>> inaihitaji
>>> Tanzania zaidi na Tanzania inaihitaji Marekani. Marekani inahitaji MCC 2
>>> zaidi hali kadhalika Tanzania inahitaji MCC 2.
>>>
>>> Mahusiano ya Tanzania na Marekani hayakuanza na hayataisha na MCC. MCC
>>> imeyakuta na itayaacha.
>>>
>>> Kama marudio ya uchaguzi wa Zanzibar ndio kigezo, basi Marekani
>>> isingekuwa inatoa zaidi ya Dola Bilioni 3 kila mwaka kwa Egypt iliyo
>>> chini
>>> ya utawala wa kijeshi kwa sababu ya kuununua ugomvi wa Egypt na Israel
>>> na
>>> isingetoa kiasi cha dola bilioni 6 kwa Israel kila mwaka kwa yale
>>> wanayoyafanya dhidi ya Wapalestina.
>>>
>>> Huu ni wakati ambao Taifa linawaita Wazalendo wake. Wazalendo wasimame
>>> na
>>> kusema 'Nchi yangu KWANZA, iwe Sahihi au Imekosea" na Makuwadi
>>> watashangilia na kusema "si mnaona sasa kiko wapi?".
>>>
>>> Huu ni wakati wa kujifunga mikanda na kulinda heshima yetu kama Taifa
>>> letu. Tuna vyanzo vya mapato vingi sana ambavyo hatujaanza kukusanya
>>> mapato, tuwe wabunifu na tusibweteke na kutegemea mapato yataongezeka
>>> maradufu kwa vyanzo vile vile.
>>>
>>> Niseme kwa uchache, sababu walizotoa MCC, na ieleweke aliyetoa tamko ni
>>> MCC, heri lingetoka tamko hili Wizara ya Mambo ya Nje au Ikulu ya
>>> Marekani,
>>> moja ni Zanzibar na pili ni Sheria ya Makosa ya Mitandao (Cyber crimes
>>> Act).
>>>
>>> Sasa hebu tujadili kidogo, hivi kule Zanzibar tulitaka kitokee nini pale
>>> ambapo wanasiasa walikuwa hawataki kujadiliana? Tume ile ile ya Uchaguzi
>>> ambayo bado ilikuwa na uhalali wa kikatiba na kisheria kuuitisha,
>>> kuufuta
>>> na kuuitisha tena uchaguzi ikachukua nafasi yake. Wanasiasa wasio makini
>>> wakaishia kuhamishia malumbano mitandaoni badala ya kuitafuta suluhu ya
>>> kisiasa na pale siasa iliposhindikana basi wangeitafuta suluhu katika
>>> mahakama za Zanzibar. Mezani wakashindwa, mahakamani hawakwenda. Tume
>>> ikachukua uongozi, uchaguzi ukaitishwa Wananchi wakapiga kura na sasa
>>> huko
>>> Zanzibar kuna serikali na baraza la wawakilishi. Hata mimi sifurahii
>>> sana
>>> njia waliyoichukua Zanzibar lakini ilibidi siasa za madaraka zisite ili
>>> tuanze kufanya siasa za maendeleo. Je wamarekani walitaka muujiza gani
>>> utokee huko.?
>>>
>>> Kuhusu Sheria ya Mitandao, hata mimi siipendi, si twende mahakamani,
>>> bunge litaanza vikao muda si mrefu je wabunge si wapeleke hoja ya
>>> kuifanyia
>>> marekebisho sheria hii. Sasa Marekani (MCC) inapoweka shinikizo kwa
>>> suala
>>> la Sheria ambayo ni jambo la ndani na linaloweza kujadilika, sijaelewa.
>>> Mbona sie hatujapiga kelele Yule jamaa yao Trump alipotutusi waafrika na
>>> kusema sisi stahili yetu ni kuwekwa tena chini ya ukoloni (hapa
>>> nimechomekea tu).
>>>
>>> INDHARI
>>>
>>> Ni aibu kwa viongozi wa kisiasa kufurahia jambo hili, ni ishara ya
>>> ukuwadi wa kisiasa na ambao uko tayari kukumbatia mahusiano yanayotweza
>>> Uhuru wetu. It is now high time kufanya siasa safi za maendeleo
>>> (politics
>>> of development) na sio kujikita katika katika siasa za madaraka
>>> (Politics
>>> of Power).
>>>
>>> Mwandishi, Ndg. Humphrey Polepole amenufaika na uelewa wa watu wenye
>>> uzoefu wa mahusiano ya Tanzania na nchi za Nje. Aidha, ni mnufaikaji
>>> (alumni) wa programu ya uongozi chini ya Wizara ya Mambo ya Nje ya
>>> Marekani.
>>>
>>> --
>>> Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
>>>
>>> Kujiondoa Tuma Email kwenda
>>> wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha
>>> ukishatuma
>>>
>>> Disclaimer:
>>> Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any
>>> legal consequences of his or her postings, and hence statements and
>>> facts
>>> must be presented responsibly. Your continued membership signifies that
>>> you
>>> agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and
>>> Guidelines.
>>> ---
>>> You received this message because you are subscribed to the Google
>>> Groups
>>> "Wanabidii" group.
>>> To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send
>>> an
>>> email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
>>> For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.
>>>
>>
>> --
>> Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
>>
>> Kujiondoa Tuma Email kwenda
>> wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha
>> ukishatuma
>>
>> Disclaimer:
>> Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any
>> legal
>> consequences of his or her postings, and hence statements and facts must
>> be
>> presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree
>> to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
>> ---
>> You received this message because you are subscribed to the Google Groups
>> "Wanabidii" group.
>> To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an
>> email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
>> For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.
>>
>
> --
> Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
>
> Kujiondoa Tuma Email kwenda
> wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha
> ukishatuma
>
> Disclaimer:
> Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal
> consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be
> presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to
> this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
> ---
> You received this message because you are subscribed to the Google Groups
> "Wanabidii" group.
> To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an
> email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
> For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.
>

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com

Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma

Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

0 comments:

Post a Comment