Kinyawela- Waambie hao atumie research method ya Historical transect wawaulize wananchi kama yupo mzee kuliko wote 80+ years awaeleze kuhusu matatizo waliyoyaona, mwaka gani, sababu, walisurvive vipi au mitigation measures zilikuwa nini. Utaona majanga ya dharuba ya mvua, uipepo, jua kali na ukame, wanyamapori kuvamia mashamba, vita vya kikabila, mkoloni kupokonya ardhi na walifanya nini; walikula nini. Waulize kwa nini kuna tribal norms hizi na zile kuhusu kilimo, mazao ya kupanda au aina fulani ya ulinzi wa mazingira au kilimo na upandaji wa namna fulani. Utaona majibu yao kuwa-walikwisha kufikwa na kuziona climate change effects, wakaweka survival strategies and mitigation measures. Ndio unakuta kuna mashamba ya malungulu, kilimo cha ngoro; kilimo milimani cha kutandika mawe au kupiga matuta na mashimo ya kukinga maji na mchanga; kilimo mchanganyiko cha maharage au kunde na mahindi huruhusiwi kulima bila ya kuchanganya; sheria ndogo ndogo hukusu namna ya kulima, kusafisha mifereji ya kumwagilia maji, kulinda mabwawa ya irrigation (Ndiwa/Ndiva); kuweka mifereji ya maji kupeleka mbugani wanyamapori wapate maji huko wasije mashambani; mifugo kutengwa na mashamba na mwiko kunyweshea mtoni, mwiko kutumia dawa za kemikali kupiga mazao (maji ya mifereji ipitayo mashambani hupeleka kemikali mtoni watu wanakunywa wanapata matatizo). Kuna miti haikatwi-husaidia mboga wakati wa ukame na mizizi huwa chakula au dawa. Wana sheria za kimila za kutunza misitu (Nyumba Ngitu) kutishia watu kuwa ukiingia huko kukata miti miti italia na kukauka Mungu anakasirika na utaadhibiwa na mizimu utaumwa na kufa. Kumbe ni catchment forest ni vyanzo vya mito na tegemewa katika maji na mvua. Siku hizi nyumba ng'itu miti inakatwa na wayoto wao na wala hawafi!
Kuna mengi waliyafanya wazee wetu na makabila mbali mbali kama mila, miiko ya kabila katika mazingira, kilimo, uvuvi, ufugaji, misitu, maji ertc ambayo iliwasaidia kuishi na ulizi wa mazingira. Hakuna jipya hapa katika mabadiliko ya tabia nchi wazee wetu wanajua. Hata Mzee I. Kimambo ktk vitabu vyake ameziandika njaa zilizotokea Upareni na mitigation measures zake zilikuwa nini-Nzala ya Mnyime, Nzala ya Nkebe etc. Watu walihama kutoka eneo moja kwenda lingine kutokana na mabadiliko ya tabia nchi, vita au ardhi kuwa ndogo. Climate change iliwaleta Wasukuma-kabila kuu nchini kutoka Chad West Africa mpaka TZ lake zone. Vita ya Zulu Mfekane imewaleta Wangoni kutoka South Africa-kabila kuu la Pili nchini.
Raha za kutembea na majahazi akiwa Holiday zilimleta mtawala toka Oman akaja ZNZ akatawala baada ya kukipenda kisiwa. Pia Mfalme wa Kilwa aliyetawala Mafia Pia watoto wakishika madaraka huko. Walitoka Uajemi au uarabuni wakasafiri na kufa na kuzikiwa Tongoni Mafia au Kaole Bagamoyo. Makaburi yao yapo. Walikuwa juu milimani Udzungwa range au Pare mountains lakini wakawa na adaptation ya kuishi milimani na kulima mazao yasiyokuwa katika baridi huko mabondeni. Midizi milimani-mpunga bondeni kwenye wetlands na kumwagilia maji huko upareni upogoroni na Uvidundani ni kutumia wetlands ambazo sasa wamezichukua wanalima miwa wananchi wanaharimu milima kupanda vinavyochukua badala ya miezi 6 mwaka kutokana na baridi. Adaptation to climate change wanaijua wananchi na ndio maana wana mashamba maeneo tofauti kutokana na ekjolojia. Anaishi Milimani iringa au Njombe mfano Uhafiwa lakini analima mazao mengine kilometa 5 kwa babu au mjomba, analima mengine kwa shangazi amepewa ardhi huko analima nyanya, vitunguu. Milimani analima chai na kupanda miti ya mbao. Wewe land officer unampimia ardhi akae hapo alime hapo-msomi hujui Ecology na usefulness of Ecological Niches kwamba walizitumia kutokana na uwezo wake wa kuzalisha aina mbali mbali za mimea/mazao hivyo kila msimu analima kwingine. Ukisema alime pale alipo-utawaua wananchi kwa njaa. Fanya land use planning, mpe hati miliki ya maeneo yake, mtoze kodi ila mwache alime mpunga unakolimika na maharage yanapokua na chai inapoweza kulimika.
Hata Tsunami mimi niliiona nikiwa darasa la pili au la tatu huko Bagamoyo-bahari ilijaa mawimbi yake yalifika mpaka pale kwenye kanisa katoliki. Sikuisikia na kuiona tena mpaka miaka 50+ hivi karibuni yaani nusu karne. Kila mwaka kuna mabadiliko na kila baada ya miaka 3 hadi 5, yapo ikifika 10 ni makubwa kuliko ile 3 na ikifika 20 hivyo 50 ndio a big bang ikifika 100 tetemeko na kupatwa kwa sayari au kuonekana nyinginezo mpya na hata wanyama wa ajabu kuonekana walikotokea hao nyangumi, papa, samaki wa sura ya mtu etc inakuwa maajabu ya dunia. sasa tunashangaa nini? Ikiwa huyo mama na mumewe wanakata miti wanachoma mkaa, wanakausha mito, kisha mama anatembea kilometa 5 kusaka maji kutwa. Hiyo ni shule ya yeye kukataza mumewe kukata miti katika misitu maji na kando ya mito. Bado kubakwa akienda kuchota maji na kusaka kuni. Kazungukwa na msitu lakini hawana choo. Wanakwenda porini-wanaliwa na simba au kuumwa na nyoka ila choo jirani na nyumba-hachimbi. Wakiwekewa borehole yenye hand pump-wanabomoa pampu kuuza chuma chakavu na mtoni mto umekauka. Kutengeneza pampu wachange kila kaya shs 1,000/= hapana ila daily wanakunywa pombe mume na mke ya angalau 2,000/= ila kesho atatembea km 5 kusaka maji kwa pombe anatumia 60,000/= bado mengineyo. Trump wa USA-anasema kweli kuhusu akili zetu!!
Nani akufundishe kuwa mabadiliko ya tabia nchi yanaweza kuleta mafuriko na unayaona yanatokea kila mwaka na hutaki kuhama bondeni Jangwani na kwingineko vijijini na mijini. Maji yanajaa mpaka darini tena yana takataka na kemikali, vinyesi, unapoteza mali na watu na hutaki kuhama. Unapewa plot, vifaa vya ujenzi unauza unarudi bondeni ambako umevamia baada ya kuuza nyumba yako ya magomeni uliyouziwa kwa 60,000/= vyumba sita zile za NHC. Unaelewa ajali za moto lakini unabananisha nyumba na hata kama moto utawaka ukipita kuzimwa mnajenga tena-mnabananisha kuliko kwanza kuziba feeder roads zote bar hapa, pale maguduria ya gesi, pale nyama choma moto unawaka, pale pharmacy! Kama vile kufa hukujui na umekuona na iliwaka umeanza upya ila kubadilika hutaki akili za ngedere. Walihamishwa na kubebwa na boat maji yalivyojaa -mabadiliko ya tabia nchi-wamerudi na kujenga bondeni kabisa! Walibebwa kwa Ndege Rufiji mid 1970s wakwanza kupanda helikopta TZ-waliambiwa wakae milimani wakalime bondeni huo mpunga. Wamerudi kuishi mabonde ya mpunga jirani na wetlands na mto Rufiji. Mafuriko yanawabeba mabadiliko ya tabia nchi wameyaona karne lakini wanajenga mtoni na kusimulia jinsi wanavyopoteza mali kila mara-tumezoea kuishi hapa!!
Bado wanatupa viroba ktk open drainage system pamoja na kufurika mtaamzima maji ya kinyesi na taka zote. Viroba vinaziba mapito ya maji kwenda baharini. wanatupa daily pamoja na Mangufuli kuweka siku ya usafi kwa lazima wanatupa na kuunganisha vyoo vyao mitaro wazi!! Akili za zombie!!
Wanakolimbikiza mifugo mpaka ardhi inakuwa kipara-wanachojali ni social status kuwa na mingi ndio unapata jina wewe ni tajiri hata iwe imekonda. Lakini ardhi na mito inavyokauka mke anatembea kilometa nyingi na punda kusaka maji. Watoto hawasomi ni kuchunga mifugo hiyo. Kubadilika ufanye ufugaji wa kisasa- nani anataka? labda 1% ya wafugaji wenye mifugo mingi. Class ni muhimu kuliko ulinzi wa mazingira. Mke asipotembea mbali kutafuta maji atafanyakazi gani? Nimemlipia mahari ya mifugo! hali ikiwa mbaya tutahamia mkoa mwingine misitu bado mingi Tanzania.
Elimisha mpaka PhD; ukiuliza maswali hata wasio na PhD watatoa majibu sahihi. Tatizo bongoland na suala la elimu jamii sio ukosefu wa elimu au ufahamu-UKOSEFU WA POSITIVE ACTION na UKOSEFU WA SUSTAINABLE POSITIVE ACTION. ELIMU NA KUKUZA UFAHAMU WA ISSUES NI MUHIMU LAKINI HAIKUPI GARANTII/UKAKIKA KUWA ALIYEELIMISHWA ATAFANYA INAVYOTAKIWA. Anaweza akawa na maelezo mengi, mawazo ya kijinga pamoja na ushirikina, kuona hawajibiki eti analipa kodi, ana haki ya kukaa au kutokufanya hivyo kwani hiyo si kazi yake; kazi ya mungu akipenda mafuriko hayatotokea; serikali haitujali tunalipa kodi ila wanajaza takataka mitaroni au kukata miti hovyo. Nini ulinzi wa mazingira kukwepa mabadiliko ya tabia nchi, matumizi ya kondom-elimu inatolewa, wanaokufa au kuumwa anawaona ila-tulitumia tulipoanza sasa baada ya kuzoeana-Tumeacha. Elimu anayo lakini ameacha anasema hataki kula pipi na maganda yake sasa wamezoeana lakini huyo ni mchepuko wake si mkewe!!
Sheria inapoingia SIASA za kukataa kukemea na kuadhibu waharibifu mazingira bali kutofa faini-kila mtu atalipa faini na kuendelea tena kufanya yale yale. Atalima milimani na atafuga isivyo endelevu, atakata miti na kuchoma mkaa; watakata mikoko kuisafirisha uarabuni hata wakikamatwa si watalipa faini? Hata vibari au leseni za mbao na kuchoma mkaa zinatolewa na GVT bila ya kuhakikisha kuwa anayepewa leseni ana msitu wake wa mila au wa kupanda atakata mbao na kuchomba mkaa pia. Unapewa leseni-ukaharibu misitu ambayo ni muhimu kwa kuzuia athari za mabadiliko ya tabia nchi. Unamifugo beyond land's carrying capacity hulazimishwi kupunguza bali hiyo elfu 10 kila mmoja aliyo nayo anaambiwa na GVt officer/respective ministries-ahamie mkoa huu au ule kuna ardhi kubwa! Huko mapigano, mapambano, mauaji na uharibifu mazingira unakuwa exported na wataalamu wa serikali. Badala ya kulazimisha kisheria kilimo, uvuvi na ufugaji endelevu-lipa leseni ya mifugo, hamisha kwa gari (na wanahama kwa miguu usiku na hawafiki walikopangiwa), huko ardhi kubwa. Miti inabaki mirefu ktk misitu husika wanakokwenda ila ardhi chini inakuwa nyeupe kama imelimwa na kufagiliwa kutokana na kuzidiwa mifugo, Mito inavamiwa inakauka na mabwawa ya wengine ya maji kujaa kinyesi na kukaushwa-mapigano. Nani wa kuelimisha hapa masuala ya Tabia Nchi kama GVt inajali kodi kuliko kufanikisha uchumi wa kisasa unaolinda mazingira ili kuzuia bad climate change effects kwa jamii, mazingira na uchumi wa taifa?
Kama kawa
--------------------------------------------
On Tue, 15/3/16, francis kinyawela <kinyawela@yahoo.co.uk> wrote:
Subject: Re: [wanabidii] WANAWAKE WASHIRIKISHWE ZAIDI KATIKA MABADILIKO YA TABIANCHI : WAZIRI UMMY MWALIMU
To: wanabidii@googlegroups.com
Date: Tuesday, 15 March, 2016, 13:10
Wanajamvi mi naona kuwa hizi kauli
zinatupeleka kwenye ubaguzi wa kijinsia. Pili, hivi wapi
kuna mafundisho ya mabadiliko ya tabia nchi inatolewakwa
wanaume tu. Nadhani tufike pahala tuwe tunaongea siyo mradi
kuongea.
Franci
--------------------------------------------
On Tue, 15/3/16, Zainul Mzige <zmzige@gmail.com>
wrote:
Subject: [wanabidii] WANAWAKE WASHIRIKISHWE ZAIDI KATIKA
MABADILIKO YA TABIANCHI : WAZIRI UMMY MWALIMU
To:
Date: Tuesday, 15 March, 2016, 11:43
Habari za mchana,
Tafadhali pokea CODE hapa chini.
<img class="wp-image-8150 aligncenter" src="
http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2016/03/ummm.jpg"
alt="ummm"
width="629" height="354" />
<p style="text-align: center;"><span
style="color:
#000080;"><strong><em>Waziri wa Afya,
Maendeleo ya Jamii, Masuala ya
Wanawake, Wazee na Watoto wa Tanzania, Mh. Ummy Mwalimu
akiwasilisha mada
kuu ambapo aliwakilisha kundi la Afrika katika mkutano huo
mkubwa
unaoendelea nchini
Marekani.</em></strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><span
style="color:
#000000;"><strong>Bara
la Afrika na hasa wanawake ndio wanaobeba mzigo zaidi wa
madhara ya
mabadiliko ya tabianchi, huku wakinyimwa fursa ya
kushiriki
katika kutafuta
suluhu kwa tatizo hilo, ameeleza leo Ummy Mwalimu, Waziri
wa
Afya,
Maendeleo ya Jamii, Masuala ya wanawake, wazee na watoto
wa
Tanzania.</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><span
style="color:
#000000;"><strong>Bi
Mwalimu amesema hayo akihutubia kikao cha 60 cha Kamisheni
ya Umoja wa
Mataifa kuhusu hali ya wanawake, CSW60 kwa niaba ya kundi
la
nchi za
Afrika, akisisitiza umuhimu wa kushirikisha zaidi wanawake
katika uongozi
wa kimataifa kuhusu suala la mabadiliko ya
tabianchi.</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><span
style="color:
#000000;"><strong>"Wanawake wanapaswa kuweza
kuongoza katika ngazi za
kitaifa na serikali za mitaa. Ubunifu wao, ujuzi wa
kiasili,
matarajio yao
yanaweza kusaidia katika kubuni na kushawishi suluhu
kuhusu
mabadiliko ya
tabianchi.</strong>"</span></p>
<p style="text-align:
center;"><strong><span
style="color: #000000;">Aidha
amezungumzia suala la kilimo ambacho hushughulisha
wanawake
zaidi, akisema
la msingi ni kusaidia sekta binafsi ili kukuza ukuaji wa
uchumi katika
sekta hiyo na hivyo kuwezesha
wanawake.</span></strong></p>
<p style="text-align: center;"><strong><img
class="alignnone wp-image-8148"
src="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2016/03/umm.jpg"
alt="umm"
width="631" height="295" /><em><span
style="color: #000080;">Baadhi ya
washiriki wa mkutano mkuu wa mwaka wa wanawake unaofanyika
nchini Marekani
ulioanza jana Machi 14-24, wakiwa nje ya jengo la Umoja wa
Mataifa
unapofanyika mkutano
huo</span></em></strong></p>
<p style="text-align: center;"><span
style="color:
#000080;"><strong><img
class=" wp-image-8151 aligncenter" src="
http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2016/03/unwomen.jpg"
alt="unwomen"
width="630" height="420"
/></strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><em><span
style="color:
#000080;"><strong>Baadhi ya washiriki
wakifuatilia
mkutano huo wa
#CSW60</strong></span></em></p>
<p style="text-align: center;"><img class="
wp-image-8149 aligncenter" src="
http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2016/03/ummy.jpg"
alt="ummy"
width="630" height="630" /></p>
KAWAIDA
*Bara la Afrika na hasa wanawake ndio wanaobeba mzigo
zaidi
wa madhara ya
mabadiliko ya tabianchi, huku wakinyimwa fursa ya
kushiriki
katika kutafuta
suluhu kwa tatizo hilo, ameeleza leo Ummy Mwalimu, Waziri
wa
Afya,
Maendeleo ya Jamii, Masuala ya wanawake, wazee na watoto
wa
Tanzania.*
*Bi Mwalimu amesema hayo akihutubia kikao cha 60 cha
Kamisheni ya Umoja wa
Mataifa kuhusu hali ya wanawake, CSW60 kwa niaba ya kundi
la
nchi za
Afrika, akisisitiza umuhimu wa kushirikisha zaidi wanawake
katika uongozi
wa kimataifa kuhusu suala la mabadiliko ya tabianchi.*
*"Wanawake wanapaswa kuweza kuongoza katika ngazi za
kitaifa
na serikali za
mitaa. Ubunifu wao, ujuzi wa kiasili, matarajio yao
yanaweza
kusaidia
katika kubuni na kushawishi suluhu kuhusu mabadiliko ya
tabianchi.*"
*Aidha amezungumzia suala la kilimo ambacho hushughulisha
wanawake zaidi,
akisema la msingi ni kusaidia sekta binafsi ili kukuza
ukuaji wa uchumi
katika sekta hiyo na hivyo kuwezesha wanawake.*
*[image: umm]Baadhi ya washiriki wa mkutano mkuu wa mwaka
wa
wanawake
unaofanyika nchini Marekani ulioanza jana Machi 14-24,
wakiwa nje ya jengo
la Umoja wa Mataifa unapofanyika mkutano huo*
*[image: ummm]Pichani ni Waziri wa Afya, Maendeleo ya
Jamii,
Masuala ya
wanawake, wazee na watoto wa Tanzania, Mh. Ummy Mwalimu
akiwasilisha mada
kuu ambaapo aliwakilisha kundi la Afrika katika mkutano
huo
mkubwa
unaoendelea nchini Marekani.*
*[image: unwomen]*
*Baadhi ya washiriki wakifuatilia mkutano huo wa #CSW60*
[image: ummy]
--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com
Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole
responsibility
for any legal consequences of his or her postings, and
hence
statements and facts must be presented responsibly. Your
continued membership signifies that you agree to this
disclaimer and pledge to abide by our Rules and
Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to
the
Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails
from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit
https://groups.google.com/d/optout.
--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com
Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility
for any legal consequences of his or her postings, and hence
statements and facts must be presented responsibly. Your
continued membership signifies that you agree to this
disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the
Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails
from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit
https://groups.google.com/d/optout.
--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.
0 comments:
Post a Comment