Monday, 11 January 2016

[wanabidii] TAARIFA KWA UMMA KUHUSU MWENENDO WA UGONJWA WA KIPINDUPINDU NCHINI

Habari za jioni,

Tafadhali pokea CODES hapo chini.

<a href="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2016/01/DSC_0063.jpg" rel="attachment wp-att-155343"><img class="aligncenter size-full wp-image-155343" src="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2016/01/DSC_0063.jpg" alt="DSC_0063" width="640" height="426" /></a>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000080;"><em><strong>Naibu Waziri wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Dkt. Hamis Kigwangalla akizungumza na waandishi wa habari leo. Kulia ni Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Afya Duniani (WHO) nchini, Dkt. Rufaro Chatora</strong></em></span></p>

<div class="MsoNormal">
<p style="text-align: center;"><strong><span style="color: #000000;">Taarifa kwa umma, kuhusu mwenendo wa ugonjwa wa kipindupindu hapa nchini ni kama ifuatavyo; Tangu ugonjwa huu uanze, jumla ya watu 13,491 wameugua Kipindupindu, na kati yao jumla ya watu 205 wameshafariki kwa ugonjwa huu.</span></strong></p>
<p style="text-align: center;"><strong><span style="color: #000000;">Katika kipindi cha wiki iliyoanza tarehe 04 hadi 10 Januari 2016, kumekuwa na jumla ya wagonjwa 615 walioripotiwa nchini kote na vifo vitatu (3).  Mikoa ambayo bado imeripoti kuwa  na ugonjwa huu ndani ya wiki moja iliyopita ni 11 kati ya 21 iliyokuwa imeripoti ugonjwa hapa nchini. Mikoa hiyo ni pamoja na Morogoro, Arusha, Singida, Manyara, Pwani, Dodoma, Geita, Mara, Tanga, Mwanza na Simiyu. Kati ya hiyo, mikoa inayoongoza kwa kuripoti idadi kubwa ya wagonjwa wapya ndani ya wiki moja iliyopita ni pamoja na  Morogoro (Manispaa ya Morogoro  87, Halmashauri ya Morogoro  66), ukifuatiwa na Arusha (Arusha Manispaa 50), Singida (Iramba 40) na   Manispaa ya Dodoma ( 33).</span></strong></p>
<p style="text-align: center;"><strong><span style="color: #000000;">Aidha, mikoa  iliyokuwa na maambukizi lakini  kwa muda wa wiki moja iliyopita hakukuwa na mgonjwa yoyote wa kipindupindu ni pamoja na  Mbeya, Rukwa, Katavi, Kigoma, Kagera, Lindi. Vile vile mkoa wa Dar es Salaam ambako ndiko ugonjwa ulianzia na kudumu kwa muda wa miezi minne (4) haujaripoti mgonjwa wa kipindupindu kuanzia tarehe 22/12/2015.</span></strong></p>
<p style="text-align: center;"><strong><span style="color: #000000;">Mikoa ambayo ilikwisha kuwa na ugonjwa huo lakini hapajakuwepo na wagonjwa wowote kwa muda wa zaidi ya miezi miwili iliyopita ni pamoja na Shinyanga, Kilimanjaro na Iringa. Pia mikoa ambayo haijawahi kutoa taarifa ya ugonjwa wa kindupindu tangu mlipuko huu uanze hapa nchini ni  Njombe, Ruvuma na  Mtwara.</span></strong></p>
<p style="text-align: center;"><strong><span style="color: #000000;">Bado Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, inaendelea kusisitiza kuwa, ili kudhibiti ugonjwa huo na kuokoa vifo vinavyotokana na ugonjwa huu, wananchi wanasisitizwa kunywa maji yaliyo safi na salama, kuepuka kula chakula kilichoandaliwa katika mazingira yasiyo safi na salama, kunawa mikono kwa sabuni na maji safi yanayotiririka:-</span></strong></p>
<p style="text-align: center;"><strong><span style="color: #000000;">-kabla na baada ya kula</span></strong></p>
<p style="text-align: center;"><strong><span style="color: #000000;">- baada ya kutoka chooni</span></strong></p>
<p style="text-align: center;"><strong><span style="color: #000000;">-baada ya kumnawisha mtoto aliyejisaidia</span></strong></p>
<p style="text-align: center;"><strong><span style="color: #000000;">-baada ya kumhudumia mgonjwa</span></strong></p>
<p style="text-align: center;"><strong><span style="color: #000000;">Aidha, jamii inaaswa kutumia vyoo wakati wote na kutokujisaidia ovyo katika vyanzo vya maji vya mito, maziwa na mabwawa.</span></strong></p>
<p style="text-align: center;"><strong><span style="color: #000000;">Hivyo, Mamlaka za Mikoa na Halmashauri pamoja na watendaji wake kote  nchini zinaagizwa kuendeleza juhudi za kuzuia kusambaa kwa mlipuko pamoja na kuchukua hatua stahiki za tahadhari kwa kusimamia utekelezaji wa yafuatayo:</span></strong></p>
<p style="text-align: center;"><strong><span style="color: #000000;">*Ushirikishwaji wa viongozi ngazi mbali mbali, hasa ngazi za Halmashauri kwa kushirikisha madiwani na viongozi wa kata, vijiji, na mitaa.</span></strong></p>
<p style="text-align: center;"><strong><span style="color: #000000;">*Mamlaka husika kuhakikisha upatikanaji wa maji safi na salama ikiwa ni pamoja na uwekaji wa dawa ya klorini kwenye maji na kupima usalama wa maji mara kwa mara.</span></strong></p>
<p style="text-align: center;"><strong><span style="color: #000000;">*Upatikanaji wa dawa za kutibu maji (Water Guard, Aqua Tabs) katika maeneo ya mlipuko.</span></strong></p>
<p style="text-align: center;"><strong><span style="color: #000000;">*Juhudi kubwa ziongezwe kuhakikisha upatikanaji na matumizi ya vyoo bora kwa kila kaya.</span></strong></p>
<p style="text-align: center;"><strong><span style="color: #000000;">*Uelimishwaji wa Baba na Mama Lishe, na wauzaji wengine wa vyakula kuhusu kanuni za afya.</span></strong></p>
<p style="text-align: center;"><strong><span style="color: #000000;">*Kusimamia utekelezwaji wa Sheria ya Afya ya Mazingira na Sheria ndogo ndogo (By-Laws).</span></strong></p>
<p style="text-align: center;"><strong><span style="color: #000000;">*Uhamasishaji wa Wananchi wanaopata ugonjwa kuwahi kutumia maji ya chumvi  chumvi (ORS) na kuripoti mapema katika vituo vya huduma.</span></strong></p>
<p style="text-align: center;"><strong><span style="color: #000000;">*Uboreshwaji wa vituo vya kutolea huduma za afya.</span></strong></p>
<p style="text-align: center;"><strong><span style="color: #000000;">Hitimisho</span></strong></p>
<p style="text-align: center;"><strong><span style="color: #000000;">Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, inawashukuru wadau wote wanaoshirikiana na Serikali katika harakati za kupambana na ugonjwa huu. Aidha, Wizara inaipongeza mikoa ambayo ilikuwa na ugonjwa na sasa umetoweka au kupungua kwa kiasi kikubwa na pia kuikumbusha mikoa ambayo bado haijaathirika kuchukua hatua za tahadhari za kuzuia ili isipate mgonjwa yeyote wa Kipindupindu.</span></strong></p>
<p style="text-align: center;"></p>

</div>


KAWAIDA

DSC_0063

Naibu Waziri wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Dkt. Hamis Kigwangalla akizungumza na waandishi wa habari leo. Kulia ni Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Afya Duniani (WHO) nchini, Dkt. Rufaro Chatora

Taarifa kwa umma, kuhusu mwenendo wa ugonjwa wa kipindupindu hapa nchini ni kama ifuatavyo; Tangu ugonjwa huu uanze, jumla ya watu 13,491 wameugua Kipindupindu, na kati yao jumla ya watu 205 wameshafariki kwa ugonjwa huu.

Katika kipindi cha wiki iliyoanza tarehe 04 hadi 10 Januari 2016, kumekuwa na jumla ya wagonjwa 615 walioripotiwa nchini kote na vifo vitatu (3).  Mikoa ambayo bado imeripoti kuwa  na ugonjwa huu ndani ya wiki moja iliyopita ni 11 kati ya 21 iliyokuwa imeripoti ugonjwa hapa nchini. Mikoa hiyo ni pamoja na Morogoro, Arusha, Singida, Manyara, Pwani, Dodoma, Geita, Mara, Tanga, Mwanza na Simiyu. Kati ya hiyo, mikoa inayoongoza kwa kuripoti idadi kubwa ya wagonjwa wapya ndani ya wiki moja iliyopita ni pamoja na  Morogoro (Manispaa ya Morogoro  87, Halmashauri ya Morogoro  66), ukifuatiwa na Arusha (Arusha Manispaa 50), Singida (Iramba 40) na   Manispaa ya Dodoma ( 33).

Aidha, mikoa  iliyokuwa na maambukizi lakini  kwa muda wa wiki moja iliyopita hakukuwa na mgonjwa yoyote wa kipindupindu ni pamoja na  Mbeya, Rukwa, Katavi, Kigoma, Kagera, Lindi. Vile vile mkoa wa Dar es Salaam ambako ndiko ugonjwa ulianzia na kudumu kwa muda wa miezi minne (4) haujaripoti mgonjwa wa kipindupindu kuanzia tarehe 22/12/2015.

Mikoa ambayo ilikwisha kuwa na ugonjwa huo lakini hapajakuwepo na wagonjwa wowote kwa muda wa zaidi ya miezi miwili iliyopita ni pamoja na Shinyanga, Kilimanjaro na Iringa. Pia mikoa ambayo haijawahi kutoa taarifa ya ugonjwa wa kindupindu tangu mlipuko huu uanze hapa nchini ni  Njombe, Ruvuma na  Mtwara.

Bado Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, inaendelea kusisitiza kuwa, ili kudhibiti ugonjwa huo na kuokoa vifo vinavyotokana na ugonjwa huu, wananchi wanasisitizwa kunywa maji yaliyo safi na salama, kuepuka kula chakula kilichoandaliwa katika mazingira yasiyo safi na salama, kunawa mikono kwa sabuni na maji safi yanayotiririka:-

-kabla na baada ya kula

- baada ya kutoka chooni

-baada ya kumnawisha mtoto aliyejisaidia

-baada ya kumhudumia mgonjwa

Aidha, jamii inaaswa kutumia vyoo wakati wote na kutokujisaidia ovyo katika vyanzo vya maji vya mito, maziwa na mabwawa.

Hivyo, Mamlaka za Mikoa na Halmashauri pamoja na watendaji wake kote  nchini zinaagizwa kuendeleza juhudi za kuzuia kusambaa kwa mlipuko pamoja na kuchukua hatua stahiki za tahadhari kwa kusimamia utekelezaji wa yafuatayo:

*Ushirikishwaji wa viongozi ngazi mbali mbali, hasa ngazi za Halmashauri kwa kushirikisha madiwani na viongozi wa kata, vijiji, na mitaa.

*Mamlaka husika kuhakikisha upatikanaji wa maji safi na salama ikiwa ni pamoja na uwekaji wa dawa ya klorini kwenye maji na kupima usalama wa maji mara kwa mara.

*Upatikanaji wa dawa za kutibu maji (Water Guard, Aqua Tabs) katika maeneo ya mlipuko.

*Juhudi kubwa ziongezwe kuhakikisha upatikanaji na matumizi ya vyoo bora kwa kila kaya.

*Uelimishwaji wa Baba na Mama Lishe, na wauzaji wengine wa vyakula kuhusu kanuni za afya.

*Kusimamia utekelezwaji wa Sheria ya Afya ya Mazingira na Sheria ndogo ndogo (By-Laws).

*Uhamasishaji wa Wananchi wanaopata ugonjwa kuwahi kutumia maji ya chumvi  chumvi (ORS) na kuripoti mapema katika vituo vya huduma.

*Uboreshwaji wa vituo vya kutolea huduma za afya.

Hitimisho

Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, inawashukuru wadau wote wanaoshirikiana na Serikali katika harakati za kupambana na ugonjwa huu. Aidha, Wizara inaipongeza mikoa ambayo ilikuwa na ugonjwa na sasa umetoweka au kupungua kwa kiasi kikubwa na pia kuikumbusha mikoa ambayo bado haijaathirika kuchukua hatua za tahadhari za kuzuia ili isipate mgonjwa yeyote wa Kipindupindu.

 



--
Zainul A. Mzige,
Operation Manager,
MO BLOG,
+255714940992.

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

0 comments:

Post a Comment