Friday 29 January 2016

Re: [wanabidii] Membe mwache Magufuli

Yes Dominick;
There you are,nakuunga mkono sana.
Huwezi kuwabembeleza watu kutimiza wajibu wao.
Kama hawawezi waache kufanya biashara mana itakuwa imewashinda kwa kushindwa kutimiza ya Kaisari.
Huu sio wakati wa kubembelezwa wakati shamba linabaki mabua tu.
 
Reuben



On Friday, January 29, 2016 7:24 PM, 'Dominick Rukokelwa' via Wanabidii <wanabidii@googlegroups.com> wrote:


Wafanyakazi walipe kodi zao kwa wakati na kwa lazima, wafanyabiashara wabembelezwe,waombwe kulipa kodi. huu utakuwa mfumo wa kipumbavu. Taifa liko hapa tulipo kwa sababu hii. Membe anajua uzembe uliofanywa na serikali aliyokuwa anaitumikia. Lakini kila aliyekuwa na mlango wa kuiibia nchi hii na sisi raia masikini tukiteseka MUNGU atashughulika nao kupitia Rais Magufuli. MUNGU atakuwa kinyume nao. Haiwezekani kabisa MUNGU akawaacha na hakika wote walioiibia nchi hii kwa kutumia madaraka waliyopewa na MUNGU wakawadhulumu raia wanyonge wajue hakika mkono hodari wa MUNGU na hasira ya MUNGU huu ndio wakati wenyewe. kupatilizwa.
Dominick.


On Thursday, January 28, 2016 1:43 PM, 'ELISA MUHINGO' via Wanabidii <wanabidii@googlegroups.com> wrote:


Kubwa jinine alilolsema Membe ni kumtaka Rais ''awabembeleze'' wafanhya biasharia. nalo lijadiliwe. Tafsiri sahihi ya wafanya biashara ni wale ambao wanalipa kodi. Membe kutaka waliokwepa kodi wapewe  miezi mitatu ni aina nyingine ya kutaka kuendeleza ufisadi. Membe alikusudia taifa liendeshweeje bila kodi? kama wafanyabiashara watabembelezwa KULIPA kodi na kwa hiyo siyo hiyari nchi iendelee kutegemea mama ntilie kulipa kodi kama miaka ya mateso ambayo watu wanatarajia mabadiliko? Maana yake Membe alipokuwa anagombea urais alikusudia kuendelea kuwabada wafaya biashara wadogo na kuwaachia uhuru wakibwa kuendelea kukwepa kodi?
N\ hilo linahitaji ahojiwe. Tuna tatizo la wsauliza maswali katika mijadala hii. nasema hivyo kama maswali yamnakuwa hayakupangwa na muulizwaji
--------------------------------------------
On Thu, 1/28/16, 'ananilea nkya' via Wanabidii <wanabidii@googlegroups.com> wrote:

Subject: Re: [wanabidii] Membe mwache Magufuli
To: wanabidii@googlegroups.com
Date: Thursday, January 28, 2016, 1:35 PM


Fadhili,
Hii makala uliyoweka hapa nimeisoma. Ni nzuri. Ina ujumbe
mzuri kwa taifa. Nakubaliana na mwandishi Evarist Chachali
kwamba safari nyinyi za nje zilizofanywa na serikali
iliyopita, kwa kiwango kikubwa zilikuwa ni mkakati wa
kifisadi wa kunufaisha watawala wachache. Hivyo hatua ya
Rais Dr Magufuli ya kudhibiti ufisadi huo uliofanyika kwa
kisingizio cha ushirikiano wa kimataifa kukuza uchumi kumbe
ni biashara mahususi ya kuneemesha zaidi watawala wachache.
Namtia shime Rais Dr Magufuli asitetereke kwa hili la KUBANA
SAFARI UFISADI na wala asitiwe hofu na mwana CCM yoyote hai
au mfu maana umma mpana,uliofukarishwa ili hali watawala
wachache wakiwa matajiri kufuru kwa kunufaika kwa fedha na
rasilimali za nchi, uko nyuma yake. Mungu ibariki Tanzania

Ananilea Nkya
 E-mail:ananilea_nkya@yahoo.com

--------------------------------------------
On Thu, 1/28/16, fadhil fadhil <fadhil.fadhil96@gmail.com>
wrote:

  Subject: [wanabidii] Membe mwache Magufuli
  To: "'Hildegarda Kiwasila' via Wanabidii" <wanabidii@googlegroups.com>
  Date: Thursday, January 28, 2016, 9:35 AM
 
  Evarist Chachali
 
 
 
  KATIKA tasnia ya ushushushu kuna kitu kinachoitwa Moscow
  Rules (yaani
  Kanuni za Moscow). Hizi ni kanuni za zama za Vita Baridi
  ambazo majasusi
  waliopangiwa kazi nchini Urusi walipaswa
kuzizingatia, kwa
  sababu nchi
  hiyo ilikuwa nguli wa kukabiliana na majasusi. Moja ya
  kanuni hizo
  inasema; "Once is an accident. Twice is a coincidence.
  Three times is an
  enemy action." Kwa tafsiri isiyo rasmi; kitu
kinachojiri
  mara moja ni
  ajali; kikijiri mara ya pili ulinganifu wa bahati mbaya,
sio
  makusudi;
  kikijiri mara ya tatu ni kitendo cha adui."
 
 
 
  Nimeanza makala hii na angalizo hilo kwani ndio wazo
  lililoniingia
  kichwani mara baada ya kusoma kauli za aliyekuwa Waziri wa
  Mambo ya Nje
  na Ushirikiano wa Kimataifa, katika Serikali ya Awamu ya
  Nne, Bernard
  Membe.
 
 
 
  Wiki iliyopita, Membe alinukuliwa na vyombo vya habari
  akimkosoa Rais
  Dk. John Magufuli, angalau katika maeneo matatu. Kwanza,
  Membe alidai
  kuwa kiuhalisi, Dk. Magufuli hajapunguza idadi ya wizara
  kama
  alivyoahidi bali amepunguza idadi ya mifuko, na
kutanabaisha
  kuwa Rais
  hajabana matumizi yoyote kwa kupunguza ukubwa wa baraza la
  mawaziri,
  bali alichofanya ni kupunguza idadi ya mawaziri na sio
  wizara.
 
 
 
  "Alichofanya ni sawa na kuwa na mayai kumi halafu
ukaamua
  kuyaweka
  kwenye mifuko kumi, maana yake ni kwamba utakuwa na mifuko
  kumi yenye
  mayai," alisema waziri huyo wa zamani ambaye pia alikuwa
  miongoni mwa
  makada wa CCM waliowania kuteuliwa kugombea urais kwa
tiketi
  ya chama
  hicho tawala.
 
 
 
  "Lakini unaweza kuwa na idadi hiyo hiyo ya mayai na
  ukaamua kuyagawanya;
  mayai matatu unayaweka kwenye mfuko mmoja, mawili
kwenye
  mfuko mwingine
  na yaliyobaki kwenye mfuko mmoja. Maana yake ni
kwamba
  utaendelea kuwa
  na mayai kumi lakini idadi ya mifuko imepungua. Hapa sasa
  utakuwa
  hujapunguza gharama za kuyatunza hayo mayai,"aliongeza
  Membe.
 
 
 
  Membe alidai kwamba Magufuli ameendeleza wizara zile zile
  lakini kaamua
  kuzikusanya pamoja, na kuona kuwa mfumo huo mpya wa wizara
  unaweza
  kuathiri uwasilishaji wa bajeti bungeni kwa vile mawaziri
  sasa
  watahitaji muda mwingi zaidi kuliko ilivyokuwa awali.
 
 
 
  Hilo tutaliona kwenye Bajeti ya Serikali ya mwaka huu.
Tuone
  kama bajeti
  itaongezeka au itapungua? Kwa sababu kama wizara
zimepungua
  kama
  tunavyoamini, lazima bajeti ipungue, sasa bajeti
ikiongezeka
  au ikibaki
  vile vile maana yake hakuna
  kilichofanyika,"alitahadharisha.
 
 
 
  Eneo la pili ambalo Membe alimkosoa Magufuli ni udhibiti
wa
  safari za
  nje, akidai kuwa Tanzania si kisiwa. Membe, aliyekuwa
  mtetezi mkuu wa
  safari mfululizo za Rais (mstaafu) Jakaya Kikwete nje ya
  nchi, alisema
  kuwa safari za nje zina manufaa kwa taifa, na kusisitiza
  kuwa lazima
  Rais Magufuli asafiri kwenda nje ya nchi.
 
 
 
  "Tanzania si kisiwa, hata ukiwa tajiri namna gani lazima
  utoke nje ya
  nchi yako," alisema Membe, na kutahadharisha kuwa nchi
  yetu inaweza kuwa
  kama Zimbabwe kwani ukijitenga, utatengwa.
 
  Alisema nchi ina mabalozi 36 tu duniani kote kati ya nchi
  194
  zinazohitaji uwakilishi huo na kibaya zaidi, mabalozi
  hawaruhusiwi
  kuingia kwenye baadhi ya vikao, na hata wakiingia wakifika
  kwenye hatua
  ya uamuzi watazuiwa kushiriki.
 
 
 
  Eneo la tatu ambalo japo hakumtaja Magufuli wala kukosoa
  moja kwa moja
  lakini linaloweza kutafsiriwa kama kuikosoa serikali kuhusu

  wafanyabiashara, ambapo alitahadharisha serikali
  kutowachezea.
 
 
 
  Waziri huyo ambaye pia ni mbunge wa zamani wa Mtama (CCM)
  alipongeza
  kasi ya Magufuli katika vita dhidi ya ufisadi na kudhibiti
  mianya ya
  kukwepa kodi lakini akatahadharisha kuhusu haja ya kuwa
  mwangalifu
  katika kuwashughulikia wafanyabiashara. Alidai kuwa
  wafanyabiashara wana
  masikitiko makubwa dhidi ya serikali, na anaona suala
hilo
  litaibuka
  kwa kishindo bungeni.
 
 
 
  Licha ya maeneo hayo matatu, Membe alizungumzia kauli ya
  aliyekuwa
  mgombea urais kwa tiketi ya Chadema, Edward Lowassa,
  aliyedai
  wafanyabiashara waliomuunga mkono wananyanyaswa. Alieleza
  kuwa si dhambi
  kwa wafanyabiashara kufadhili vyama vya siasa wakati
wa
  uchaguzi, na
  kwamba serikali ya chama kilichoshinda uchaguzi inapaswa
  kuwakusanya
  wafanyabiashara wote na kufanya nao kazi na sio
kuwaburuza.
 
 
 
  Kadhalika, mwanasiasa huyo alizungumzia kuhusu "timua
  timua" ya watumishi wa umma wanaohusishwa na tuhuma za
  ufisadi.
 
 
 
  "Ni rahisi kumshughulikia mtu usiyemfahamu lakini siyo
  rahisi
  kumshughulikia mtu unayemfahamu," alidai Membe, na
  kuongeza kuwa
  haitokuwa shida kwa Magufuli kuwashughulikia watendaji
  aliowakuta
  serikalini ambao kimsingi hakuwateua, na hawafahamu.
Alihoji
  iwapo Rais
  ataweza kuwatimua aliowateua mwenyewe.
 
 
 
  Kauli hizo za Membe zimezua mjadala mkubwa, hususan kwenye
  mitandao ya
  kijamii. Japo kabla yake, aliyekuwa Naibu wa Kazi, Ajira
na
  Maendeleo ya
  Vijana, Makongoro Mahanga, alimkosoa Magufuli kuhusu
ukubwa
  wa kabineti
  yake, ukweli kwamba Membe bado ni kiongozi wa juu wa
CCM
  ilhali Mahanga
  alihamia upinzani, unaashiria mengi.
 
 
 
  Lakini binafsi sikushangazwa na kauli hizo za Membe, hasa
  kwa vile
  awali, katika kitabu nilichokichapisha hivi karibuni
kuhusu
  safari ya
  urais wa Magufuli, mafanikio na changamoto katika urais
  wake,
  nilibainisha kuwa moja ya changamoto zinazoweza kumkabili
  Rais huyo wa
  Awamu ya Tano ni maadui wa ndani ya chama chake.
 
  Kimsingi, hoja zote za Membe hazina mashiko. Kuhusu
  anachoita ukubwa wa
  baraza la mawaziri, la muhimu kwa Watanzania si ukubwa au
  udogo bali
  uchapakazi. Ni bora kuwa na mawaziri, manaibu na makatibu
  wakuu hata
  1,000 wachapakazi, kuliko kuwa na serikali ndogo
  inayokumbatia mafisadi.
 
 
 
  Pia Membe alipaswa kufahamu kuwa utendaji kazi wa viongozi
  wa serikali
  unategemea sana utendaji kazi na msimamo wa bosi wao,
yaani
  Rais
  aliyewateua. Ni dhahiri kuwa Membe anatambua kuwa Magufuli
  si mtu wa
  porojo, mtoa ahadi anazoshindwa kuzitekeleza mwenyewe
(rejea
  kauli ya
  "ninawajua wala rushwa kwa majina" ya Kikwete), na
  kimsingi Watanzania
  na dunia nzima wanafahamu kuwa kaulimbiu ya Hapa Kazi Tu
ya
  Magufuli ni
  tofauti na zama za nchi kujiendesha yenyewe (on
autopilot).
 
 
 
  Kuhusu safari za nje, Membe amepotoka mno, pengine kwa
  sababu kwa
  wadhifa wake wakati huo, alikuwa mmoja wa wasafiri nje ya
  nchi mara kwa
  mara. Kwanza, Rais Magufuli hajawahi kutamka kuwa
  hatosafiri. Kwa hiyo,
  kauli ya Membe kuwa lazima atasafiri ni fyongo.
 
 
 
  Pili, zuio la safari za nje sio 'blanket ban' bali ni
  kwa safari zisizo
  na tija. Lakini kwa nini tushangazwe na kauli hiyo ya
Membe
  ilhali
  tunafahamu misafara ya serikali iliyopita ilivyosheheni
  wajumbe kwa
  kutumia fedha za umma? Ni mtu mwenye matatizo tu anayeweza
  kutetea
  safari zenye manufaa zinazoligharimu taifa matrilioni ya
  shilingi huku
  faida tarajiwa zikiwa pungufu ya gharama husika.
 
 
 
  Mwanadiplomasia msomi kama Membe alipaswa kuangalia hapo
  jirani tu kwa
  Rais Paul Kagame, kulinganisha idadi ya safari zake nje na
  zile za
  Kikwete kisha kuangalia hali ya uchumi kati ya nchi hizo
  mbili.
 
 
 
  Vilevile ni rahisi kwa Membe kuzungumzia mafanikio ya
safari
  hizo kwa
  vile ni Watanzania wachache wanaofahamu vituko
  vilivyoambatana na safari
  hizo. Ni mara ngapi safari hizo za 'manufaa'
  zilijumuisha shopping,
  kuhudhuria birthday parties, na matukio mengine yasiyo na
  tija kwa
  serikali?
 
 
 
  Kuhusu wafanyabiashara, ni upuuzi wa hali ya juu kuhisi tu
  kuwa kuna
  uonevu dhidi ya mfanyabiashara yeyote. Kama kuwabana
  wafanyabiashara
  wakwepa kodi ni uonevu basi Magufuli aongeze dozi, maana
  hizi sio zama
  za Tanzania kuwa shamba la bibi.
 
 
 
  Membe anadai wafanyabiashara wana masikitiko na suala hilo
  linaweza
  kuibuka bungeni. Anamaanisha Bunge limejaa wafanyabiashara
  au? Na kama
  masikitiko yao ni kutokana na Serikali ya Awamu ya Tano
  kuwabana ili
  wasikwepe kodi na kwamba masikitiko hayo yanaweza
  kusababisha kupoteza
  wawekezaji, basi na waondoke hata kesho. Hatuhitaji
wakwepa
  kodi nchini.
  Kimsingi, wanaolalamika wala hawastahili kuitwa
  wafanyabiashara bali
  wahujumu wa uchumi wetu.
 
 
 
  Na hoja yake kuhusu 'timua timua' haishangazi kwani
moja
  ya udhaifu wa
  serikali ambayo Membe alikuwa waziri ilikuwa ni kuwaonea
  aibu
  wanaoboronga, na matokeo yake hali hiyo ilivutia
waborongaji
  wapya kwani
  walishabaini kuwa hakuna wa kuwachukulia hatua. Hivi
Membe
  anaweza
  kutuambia lolote kuhusu ahadi ya Riais Kikwete aliyoitoa
  Februari 2006
  kwamba anawafahamu wala rushwa kwa majina na anawapa muda
  wajirekebishe?
  Sawa,
 
 
 
  Magufuli alipoingia Ikulu alikuta orodha hiyo ya wala
rushwa
  aliowajua Kikwete na kuamua kuifanyia kazi?
 
  Nimeeleza awali kuwa nimelizungumzia suala hilo kwa kirefu
  kitabuni.
  Sitaki kabisa kuamini kuwa kauli za Membe ni zake peke
yake.
  Hisia
  zinanituma kuamini kuwa huu ni moshi tu unaoashiria moto
  unaowaka ndani
  kwa ndani ya CCM kati ya makundi makuu mawili: la Hapa
Kazi
  Tu la
  Magufuli linalotaka kuiondoa Tanzania katika lindi la
  ufisadi unaoifanya
  nchi yetu kuzidi kuwa masikini, na kundi la wanufaika
wa
  ufisadi
  linalomwona Magufuli kama mtu anayewaziba pumzi. Naam,
  ufisadi ni
  'lifeline' ya watu walioigeuza nchi yetu Shamba la
Bibi,
  wakivuna
  wasichopanda.
 
 
 
  Nimalizie makala hii kwa kutoa wito kwa makada wa CCM,
ambao
  wengi wao
  wanaimba Hapa Kazi Tu, lakini wakisikia madhambi
  yaliyofanywa na
  mwana-CCM fulani wanakimbilia kuwanyooshea vidole
wapinzani.
  Wapinzani
  wakuu wa Magufuli hawapo Chadema au nje ya nchi bali wapo
  ndani ya chama
  hicho tawala. Na njia pekee ya kupambana nao ni
kuweka
  mbele maslahi ya
  taifa badala ya kutanguliza umoja na mshikamano wa
chama.
  Kuna usemi
  mchawi akimaliza kuroga mtaa hugeukia familia yake. Majipu
  yaliyomo
  ndani ya CCM yasipotumbuliwa mapema yatamkwaza Magufuli na
  nchi yetu kwa
  ujumla.
 
 
 
  Raia Mwema
 
 
 
 
  --
 
  Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
   
 
  Kujiondoa Tuma Email kwenda
 
  wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com 
Utapata Email ya
  kudhibitisha ukishatuma
 
   
 
  Disclaimer:
 
  Everyone posting to this Forum bears the sole
responsibility
  for any legal consequences of his or her postings, and
hence
  statements and facts must be presented responsibly. Your
  continued membership signifies that you agree to this
  disclaimer and pledge to abide by our Rules and
Guidelines.
 
  ---
 
  You received this message because you are subscribed to
the
  Google Groups "Wanabidii" group.
 
  To unsubscribe from this group and stop receiving emails
  from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
 
  For more options, visit
https://groups.google.com/d/optout.

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com

Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com 
Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma

Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility
for any legal consequences of his or her postings, and hence
statements and facts must be presented responsibly. Your
continued membership signifies that you agree to this
disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the
Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails
from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit
https://groups.google.com/d/optout.

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com

Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com  Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma

Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.


0 comments:

Post a Comment