Tuesday 1 April 2014

[wanabidii] Programu ya kompyuta kuvuruga ATM wiki ijayo

Wiki moja kabla ya kusitishwa huduma za programu ya kompyuta (OS) ya Windows Xp, imefahamika kuwa waathirika wakubwa watakuwa ni benki na taasisi za fedha ambazo hutumia mfumo huo katika mashine za kutolea fedha (ATMs)

Shirika la Microsoft limethibitisha kuwa benki ni miongoni mwa taasisi nyingi zitakazoathirika na mabadiliko hayo.

Baadhi zimeanza kufanyia kazi tatizo hilo, ikiwamo benki moja ambayo jana alasiri ilituma ujumbe kwa wateja wake kuwa, "Ndugu mteja, kuanzia Jumamosi saa 2:00 usiku Aprili 5, mpaka Jumapili saa 12:00 asubuhi tutakuwa tunaboresha mashine zetu za ATM, hivyo kadi yako haitafanya kazi kwa kipindi hiki. Asante."

Kwa mujibu wa Microsoft asilimia kubwa ya benki katika nchi zinazoendelea zinatumia programu ya Windows XP katika kuendesha ATM, hivyo kuwa moja ya waathirika wa mpango huo.

Katikati ya Machi, Microsoft ilitangaza kusitisha huduma zote zinazohusiana na bidhaa zake za Windows Xp kufikia Aprili 8, mwaka huu. Pia shirika hilo litasitisha ufanisi wa programu ya kuzuia na kupambana na virusi ya Microsft Security Essentials katika mfumo wa Windows Xp, hivyo kufanya urahisi wa kompyuta zinazoitumia kukosa ulinzi.

Mkurugenzi wa Kampuni ya Twiga Hosting, Jacob Urassa alisema Watanzania hawatakiwi kupuuza onyo hilo kwa kuwa ikifika Aprili 9 usalama wa taarifa zao utakuwa hatarini.

"Windows XP ni dhaifu mara tano zaidi ya Windows 7 na 8, kwa hiyo Microsoft wameona ni bora wakaitoa sokoni. Kwa maana hiyo ATM na kompyuta zote zinazotumia programu hizo hazitakuwa na ulinzi wa uhakika," alisema Urassa ambaye ni mtaalamu wa masuala ya Teknolojia ya Mawasiliano (IT).

Alisema kuwa kuna idadi kubwa sana ya Watanzania wanaoendelea kutumia bidhaa hizo zikiwemo taasisi kubwa nchini hivyo kuna haja kubwa ya kuchukua hatua za kubadilika na teknolojia.

Naye, Ofisa Uhusiano wa Benki ya Posta, Noves Moses aliwatoa wasiwasi wateja wake kuwa licha ya kusitishwa kwa matumizi ya Windows XP, bado benki hiyo itaendelea kutoa huduma zenye kiwango kile kile.

http://www.mwananchi.co.tz/kitaifa/Programu-ya-kompyuta-kuvuruga-ATM-wiki-ijayo/-/1597568/2264804/-/mj380v/-/index.html

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

0 comments:

Post a Comment