Monday 29 June 2015

[wanabidii] MAABARA YA MAFUNZO ITEMBEAYO YAZINDULIWA RASMI

Habari za mchana, tafadhali pokea CODES


<a href="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2015/06/DSC_00801.jpg"><img class="aligncenter size-full wp-image-139360" src="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2015/06/DSC_00801.jpg" alt="DSC_0080" width="640" height="427" /></a>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000080;"><em><strong>Mganga Mkuu Wizara ya Afya na Ustawi wa jamiii, Dk. Magreth Mhando akisoma hotuba ya uzinduzi wa maabara itembeayo kwa ajili ya mafunzo ya upasuaji. Kulia ni Naibu Balozi wa Ireland nchini, Maire Matthews na kushoto ni Mkurugenzi wa ECSA anayeshughulikia Afya ya jamii Prof Yoswa Dambisya.</strong></em></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>Na Mwandishi wetu</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>Mganga Mkuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii,  Dk. Magreth Mhando mwishoni mwa juma alizindua maabara ya upasuaji ya mafunzo inayotembea iliyotolewa kwa chuo kitembeacho cha COSECSA na serikali ya Ireland.</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>Alifanyakazi hivyo kwa niaba ya Waziri wa Afya na Ustawi wa jamii, Dk Seif Rashid.</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>Maabara hiyo ambayo ni mradi wa majaribio wa chuo hicho wenye lengo la kufundisha wapasuaji pale walipo imegharimu dola za Marekani 100,000.</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>Kwa mujibu wa taarifa za COSECSA maabara hiyo itakuwa nchini kwa miezi kama mitatu kabla ya kwenda Kenya na baadae Malawi.</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>Mradi huo wenye lengo la kufundisha wapasuaji zaidi kwa kufika eneo ambalo wanafanyia kazi, ni moja ya miradi ya chuo kitembeacho ambacho toka kimeanzishwa mwaka 1990 kimeshatoa wapasuaji 200.</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>Hafla ya uzinduzi wa maabara hiyo yenye vifaa vya kisasa vya kufundishia na kufanyia upasuaji ikiwamo ya upasuaji kwa kutumia darubini ulifanyika katika hospitali ya kumbukumbu ya Hubert Kairuki.</strong></span></p>
<a href="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2015/06/DSC_0053.jpg"><img class="aligncenter size-full wp-image-139363" src="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2015/06/DSC_0053.jpg" alt="DSC_0053" width="427" height="640" /></a>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000080;"><em><strong>Rais wa COSECSA , Profesa Stephen Ogendo akisoma taarifa kwa mgeni rasmi kabla ya uzinduzi.</strong></em></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>Akizindua maabara hiyo Dk. Mhando alisema kwamba ni matumaini yake italeta mabadiliko makubwa katika kuwezesha taifa kuwa na wataalamu wengi wa upasuaji.</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>Aidha alisema changamoto ya kutosajiliwa kama chuo kamili wakati mataifa mengine yamefanya atayafuatilia ili kuweza kuona ya kukiwezesha chuo hicho kutambuliwa rasmi nchini Tanzania.</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>Maabara hiyo mali ya College of Surgeons of East Central and Southern Africa (COSECSA)  iliwasili mapema  mwezi huu na jana ndio ilikuwa uzinduzi rasmi ambao ulishuhudiwa na wanafunzi wa upasuaji, wataalamu na maofisa mbalimbali wa afya wakiwemo watu wa Mfuko wa taifa wa Bima ya Afya (NHIF).</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>Kaimu mkurugenzi wa Mfuko huo Michael Mhando alisema kwamba wamefurahishwa na juhudi za wadau wao katika kuimarisha vifaa tiba na utoaji wa wataalamu.</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>Alisema anaamini kwamba maabara hiyo ni moja ya mambo muhimu yanayotakiwa kufanywa na wadau ili kuimarisha tiba nchini.</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>Alisema kwamba wataangalia namna ya kufanya ili kusaidia huduma hiyo kwani inahitajika sana vijijini ambako wengi wa watu hawapati fursa ya kufanyiwa upasuaji hata ule mdogo.</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><a href="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2015/06/DSC_0130.jpg"><img class="aligncenter size-full wp-image-139367" src="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2015/06/DSC_0130.jpg" alt="DSC_0130" width="640" height="427" /></a></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000080;"><em><strong>Baadhi ya wadau wa sekta ya afya na wanafunzi waliohudhuria hafla hiyo.</strong></em></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>Maabara hiyo yenye uzito wa tani 30 inatarajia kufanya mafunzo ya upasuaji katika hospitali zenye uhusiano na COSECSA.</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>Aidha maabara hiyo inaweza kufunza wapasuaji 10 kwa mkupuo mmoja.</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>Kuletwa kwa maabara hiyo kutoka Ireland ambako kuna uzoefu wa miaka mingi wa kutumia maabara zitembeazo za upasuaji kumefanikishwa na mahusiano yaliyopo kati ya Royal College of Surgeons in Ireland (RCSI), Shirika la misaada la Ireland (Irish Aid) na College of Surgeons of East, Central and Southern Africa (COSECSA).</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>Maabara ya mafunzo ya upasuaji itembeayo ilianzishwa na RCSI kwa mara ya kwanza duniani  mwaka  2006 na kwa uzinduzi  uliofanyika dare s Salaam jana umedhihirisha dhamira njema ya COSECSA na RCSI ya kutoa mafunzo bora kwa lengo la kuimarisha afya za wanadamu.</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>Akizungumza kwenye tukio hilo Rais wa COSECSA , Profesa Stephen Ogendo alisema kwamba kuwepo kwa maabara hiyo kutasababisha mabadiliko makubwa katika utoaji mafunzo katika ukanda wa Afrika Mashariki, kati na Kusini ( ECSA).</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>Alisema kwamba kutokana na uasili wa maabara hiyo wanafunzi hawatakuwa wanalazimika kufuata kituo cha mafunzo na badala yake kituo hicho kitawafuata pale walipo.</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>Aidha alisema kwamba muundo na mfumo wa ufundishaji umeshatengenezwa kwa ajili ya kusaidia mafunzo hayo kwa nchi wanachama.</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><a href="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2015/06/DSC_0023.jpg"><img class="aligncenter size-full wp-image-139368" src="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2015/06/DSC_0023.jpg" alt="DSC_0023" width="640" height="427" /></a></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>Naye Mkurugenzi wa ECSA anayeshughulikia Afya ya jamii Prof Yoswa Dambisya alisema  kwamba wataendelea kuwa mstari wa mbele kufundisha wataalamu wa afya kwa kutumia mbinu mbalimbali za kisasa na zenye kutoa tija kama kuwepo kwa mabara hiyo.</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>Alisema kutokana na haja kubwa ya wataalamu wa upasuaji kuwepo kwa maabara hiyo itembeayo kutasaidia kufunza wanafunzi wengi katika eneo ambalo uwiano wa wataalamu na wagonjwa ni mtaalamu mmoja kwa wagonjwa 190,000 ukilinganisha na Uingereza ambako uwiano ni mtaalamu mmoja kwa wagonjwa 2,800.</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>Alisema raslimali kama ya maabara itasaidia kufunza watu wengi zaidi ili kuendelea kupunguza pengo la wataalamu wa upasuaji.</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>Alisema pia kwamba takwimu za dunia zinaonesha kuwa asilimia 6.5 ya magonjwa yanatokana na kukosekana kwa huduma za upasuaji.</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>Alisema vifo vingi vinatokana na kukosekana kwa huduma za upasuaji kuliko Malaria, Ukimwi na kifua kikuu kwa pamoja.</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>COSECSA ambayo ilianzishwa mwaka 1999 kwa malengo ya kutoa elimu ya upasuaji ilianzishwa na  shirikisho la wapasuaji Afrika Mashariki ambalo lina miaka takaribani 60.</strong></span></p>
<a href="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2015/06/DSC_00871.jpg"><img class="aligncenter size-full wp-image-139358" src="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2015/06/DSC_00871.jpg" alt="DSC_0087" width="640" height="427" /></a>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000080;"><em><strong>Mganga Mkuu Wizara ya Afya na Ustawi wa jamiii, Dk. Magreth Mhando akikata utepe kuzindua maabara ya upasuaji ya mafunzo inayotembea iliyotolewa kwa chuo kitembeacho cha COSECSA na serikali ya Ireland.</strong></em></span></p>
<a href="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2015/06/DSC_0097.jpg"><img class="aligncenter size-full wp-image-139365" src="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2015/06/DSC_0097.jpg" alt="DSC_0097" width="640" height="427" /></a>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000080;"><em><strong>Mmoja wa walimu ambaye ni daktari bingwa wa upasuaji akitoa maelezo kwa mgeni rasmi Mganga Mkuu Wizara ya Afya na Ustawi wa jamiii, Dk. Magreth Mhando aliyemwakilisha Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii na Naibu Balozi wa Ireland nchini, Maire Matthews.</strong></em></span></p>
<a href="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2015/06/DSC_0146.jpg"><img class="aligncenter size-full wp-image-139370" src="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2015/06/DSC_0146.jpg" alt="DSC_0146" width="640" height="427" /></a>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000080;"><em><strong>Wageni mbalimbali wakiangalia namna maabara hiyo inavyofanyakazi.</strong></em></span></p>
<a href="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2015/06/IMG_2862.jpg"><img class="aligncenter size-full wp-image-139369" src="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2015/06/IMG_2862.jpg" alt="IMG_2862" width="640" height="427" /></a>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000080;"><em><strong>Mganga Mkuu Wizara ya Afya na Ustawi wa jamiii, Dk. Magreth Mhando (kulia) akishuhudia zoezi la upasuaji kwa vitendo ndani ya maabara hiyo.</strong></em></span></p>
<a href="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2015/06/DSC_0151.jpg"><img class="aligncenter size-full wp-image-139361" src="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2015/06/DSC_0151.jpg" alt="DSC_0151" width="640" height="427" /></a>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000080;"><em><strong>Rais wa COSECSA , Profesa Stephen Ogendo akizungumza na vyombo vya habari mara baada ya kukagua maabara hiyo katika uzinduzi huo.</strong></em></span></p>
<a href="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2015/06/DSC_0090.jpg"><img class="aligncenter size-full wp-image-139366" src="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2015/06/DSC_0090.jpg" alt="DSC_0090" width="640" height="427" /></a>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000080;"><em><strong>Picha ya pamoja baada ya uzinduzi.</strong></em></span></p>
<p style="text-align: center;"><a href="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2015/06/DSC_0047.jpg"><img class="aligncenter size-full wp-image-139371" src="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2015/06/DSC_0047.jpg" alt="DSC_0047" width="640" height="427" /></a></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000080;"><em><strong>Maabara ya upasuaji ya mafunzo inayotembea iliyotolewa kwa chuo kitembeacho cha COSECSA na serikali ya Ireland.</strong></em></span></p>

KAWAIDA

DSC_0080

Mganga Mkuu Wizara ya Afya na Ustawi wa jamiii, Dk. Magreth Mhando akisoma hotuba ya uzinduzi wa maabara itembeayo kwa ajili ya mafunzo ya upasuaji. Kulia ni Naibu Balozi wa Ireland nchini, Maire Matthews na kushoto ni Mkurugenzi wa ECSA anayeshughulikia Afya ya jamii Prof Yoswa Dambisya.

Na Mwandishi wetu

Mganga Mkuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii,  Dk. Magreth Mhando mwishoni mwa juma alizindua maabara ya upasuaji ya mafunzo inayotembea iliyotolewa kwa chuo kitembeacho cha COSECSA na serikali ya Ireland.

Alifanyakazi hivyo kwa niaba ya Waziri wa Afya na Ustawi wa jamii, Dk Seif Rashid.

Maabara hiyo ambayo ni mradi wa majaribio wa chuo hicho wenye lengo la kufundisha wapasuaji pale walipo imegharimu dola za Marekani 100,000.

Kwa mujibu wa taarifa za COSECSA maabara hiyo itakuwa nchini kwa miezi kama mitatu kabla ya kwenda Kenya na baadae Malawi.

Mradi huo wenye lengo la kufundisha wapasuaji zaidi kwa kufika eneo ambalo wanafanyia kazi, ni moja ya miradi ya chuo kitembeacho ambacho toka kimeanzishwa mwaka 1990 kimeshatoa wapasuaji 200.

Hafla ya uzinduzi wa maabara hiyo yenye vifaa vya kisasa vya kufundishia na kufanyia upasuaji ikiwamo ya upasuaji kwa kutumia darubini ulifanyika katika hospitali ya kumbukumbu ya Hubert Kairuki.

DSC_0053

Rais wa COSECSA , Profesa Stephen Ogendo akisoma taarifa kwa mgeni rasmi kabla ya uzinduzi.

Akizindua maabara hiyo Dk. Mhando alisema kwamba ni matumaini yake italeta mabadiliko makubwa katika kuwezesha taifa kuwa na wataalamu wengi wa upasuaji.

Aidha alisema changamoto ya kutosajiliwa kama chuo kamili wakati mataifa mengine yamefanya atayafuatilia ili kuweza kuona ya kukiwezesha chuo hicho kutambuliwa rasmi nchini Tanzania.

Maabara hiyo mali ya College of Surgeons of East Central and Southern Africa (COSECSA)  iliwasili mapema  mwezi huu na jana ndio ilikuwa uzinduzi rasmi ambao ulishuhudiwa na wanafunzi wa upasuaji, wataalamu na maofisa mbalimbali wa afya wakiwemo watu wa Mfuko wa taifa wa Bima ya Afya (NHIF).

Kaimu mkurugenzi wa Mfuko huo Michael Mhando alisema kwamba wamefurahishwa na juhudi za wadau wao katika kuimarisha vifaa tiba na utoaji wa wataalamu.

Alisema anaamini kwamba maabara hiyo ni moja ya mambo muhimu yanayotakiwa kufanywa na wadau ili kuimarisha tiba nchini.

Alisema kwamba wataangalia namna ya kufanya ili kusaidia huduma hiyo kwani inahitajika sana vijijini ambako wengi wa watu hawapati fursa ya kufanyiwa upasuaji hata ule mdogo.

DSC_0130

Baadhi ya wadau wa sekta ya afya na wanafunzi waliohudhuria hafla hiyo.

Maabara hiyo yenye uzito wa tani 30 inatarajia kufanya mafunzo ya upasuaji katika hospitali zenye uhusiano na COSECSA.

Aidha maabara hiyo inaweza kufunza wapasuaji 10 kwa mkupuo mmoja.

Kuletwa kwa maabara hiyo kutoka Ireland ambako kuna uzoefu wa miaka mingi wa kutumia maabara zitembeazo za upasuaji kumefanikishwa na mahusiano yaliyopo kati ya Royal College of Surgeons in Ireland (RCSI), Shirika la misaada la Ireland (Irish Aid) na College of Surgeons of East, Central and Southern Africa (COSECSA).

Maabara ya mafunzo ya upasuaji itembeayo ilianzishwa na RCSI kwa mara ya kwanza duniani  mwaka  2006 na kwa uzinduzi  uliofanyika dare s Salaam jana umedhihirisha dhamira njema ya COSECSA na RCSI ya kutoa mafunzo bora kwa lengo la kuimarisha afya za wanadamu.

Akizungumza kwenye tukio hilo Rais wa COSECSA , Profesa Stephen Ogendo alisema kwamba kuwepo kwa maabara hiyo kutasababisha mabadiliko makubwa katika utoaji mafunzo katika ukanda wa Afrika Mashariki, kati na Kusini ( ECSA).

Alisema kwamba kutokana na uasili wa maabara hiyo wanafunzi hawatakuwa wanalazimika kufuata kituo cha mafunzo na badala yake kituo hicho kitawafuata pale walipo.

Aidha alisema kwamba muundo na mfumo wa ufundishaji umeshatengenezwa kwa ajili ya kusaidia mafunzo hayo kwa nchi wanachama.

DSC_0023

Naye Mkurugenzi wa ECSA anayeshughulikia Afya ya jamii Prof Yoswa Dambisya alisema  kwamba wataendelea kuwa mstari wa mbele kufundisha wataalamu wa afya kwa kutumia mbinu mbalimbali za kisasa na zenye kutoa tija kama kuwepo kwa mabara hiyo.

Alisema kutokana na haja kubwa ya wataalamu wa upasuaji kuwepo kwa maabara hiyo itembeayo kutasaidia kufunza wanafunzi wengi katika eneo ambalo uwiano wa wataalamu na wagonjwa ni mtaalamu mmoja kwa wagonjwa 190,000 ukilinganisha na Uingereza ambako uwiano ni mtaalamu mmoja kwa wagonjwa 2,800.

Alisema raslimali kama ya maabara itasaidia kufunza watu wengi zaidi ili kuendelea kupunguza pengo la wataalamu wa upasuaji.

Alisema pia kwamba takwimu za dunia zinaonesha kuwa asilimia 6.5 ya magonjwa yanatokana na kukosekana kwa huduma za upasuaji.

Alisema vifo vingi vinatokana na kukosekana kwa huduma za upasuaji kuliko Malaria, Ukimwi na kifua kikuu kwa pamoja.

COSECSA ambayo ilianzishwa mwaka 1999 kwa malengo ya kutoa elimu ya upasuaji ilianzishwa na  shirikisho la wapasuaji Afrika Mashariki ambalo lina miaka takaribani 60.

DSC_0087

Mganga Mkuu Wizara ya Afya na Ustawi wa jamiii, Dk. Magreth Mhando akikata utepe kuzindua maabara ya upasuaji ya mafunzo inayotembea iliyotolewa kwa chuo kitembeacho cha COSECSA na serikali ya Ireland.

DSC_0097

Mmoja wa walimu ambaye ni daktari bingwa wa upasuaji akitoa maelezo kwa mgeni rasmi Mganga Mkuu Wizara ya Afya na Ustawi wa jamiii, Dk. Magreth Mhando aliyemwakilisha Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii na Naibu Balozi wa Ireland nchini, Maire Matthews.

DSC_0146

Wageni mbalimbali wakiangalia namna maabara hiyo inavyofanyakazi.

IMG_2862

Mganga Mkuu Wizara ya Afya na Ustawi wa jamiii, Dk. Magreth Mhando (kulia) akishuhudia zoezi la upasuaji kwa vitendo ndani ya maabara hiyo.

DSC_0151

Rais wa COSECSA , Profesa Stephen Ogendo akizungumza na vyombo vya habari mara baada ya kukagua maabara hiyo katika uzinduzi huo.

DSC_0090

Picha ya pamoja baada ya uzinduzi.

DSC_0047

Maabara ya upasuaji ya mafunzo inayotembea iliyotolewa kwa chuo kitembeacho cha COSECSA na serikali ya Ireland.


--
Zainul A. Mzige,
Operation Manager,
MO BLOG,
+255714940992.

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

0 comments:

Post a Comment