Sunday 17 July 2016

[wanabidii] UNESCO YAKUTANISHA WADAU KUJADILI USAFI WA MAJI, HALI YA USALAMA BADO SI NZURI

Habari za asubuhi,

Tafadhali pokea CODES hapa chini.



<div style="text-align: center;">
Katika kuhakikisha kunakuwa na usalama wa maji duniani kutokana na kuwepo kwa idadi kubwa ya vifo ambavyo vinatokana na uchafu katika maji, Shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) limefanya kongamano la siku moja ambalo limewakutanisha viongozi wa idara za maji za mikoa mbalimbali nchini na kutoka nje ya nchi.</div>
<div style="text-align: center;">
<br /></div>
<div style="text-align: center;">
Katika kongamano hilo mgeni rasmi alikuwa ni Mkurugenzi Msaidizi wa Rasilimali za Maji kutoka Wizara ya Maji na Umwagiliaji, George Lugomela alisema sehemu kubwa ya vyanzo vya maji zimekuwa vikichafuliwa kutokana na usafi wa binadamu.</div>
<div style="text-align: center;">
<br /></div>
<div style="text-align: center;">
Alisema kuwa takwimu zinaonyesha ni asilimia 24 ya watu Afrika ndiyo wanajisaidia katika maeneo ambayo ni salama na idadi iliyobakia wamekuwa wakijisaidia mazingira ambayo yanahatarisha vyanzo vya maji na wengi wao wakijisaidia maporini.</div>
<div style="text-align: center;">
<div style="text-align: center;">
Mkurugenzi Msaidizi wa Rasilimali za Maji kutoka Wizara ya Maji na Umwagiliaji, George Lugomela akitoa hotuba kwa niaba ya serikali katika kongamano hilo. (Picha na <a href="http://www.modewjiblog.com/">Modewjiblog</a>)</div>
<div>
"Kongamano hili linaangalia kuhusu vijidudu vilivyo katika maji ambavyo kwa asilimia kubwa yanachafuka kutokana na usafi ambao anaufanya binadamu na ukiangalia kwa nchi zetu inaonyesha bado uhifadhi wa hizo taka kama kinyesi ambacho baadae huathiri vyanzo vya maji ni mdogo," alisema Lugomela.<br /><br />Aidha alisema pamoja na maeneo mengine kufanya ujenzi wa vyoo lakini jambo hilo bado sio salama kwa asilimia 100 na hivyo inahitajika kufanyika jitihada za ziada ili kuweza kuviweka vyanzo vya maji katika hali ya usalama.<br /><img height="425" src="https://blogger.googleusercontent.com/img/proxy/AVvXsEj4iAEBmzIlAC6zF7bDPe30sdBvOCWzJRSS47703t-nJEPx_fRqTgcU_ZKWfqkzWZmmzOzTrh12NCF4DQDWgjS6zybavhTojvDkLefq8czFEgW_qjSNXRGE1EgmpZVbQhx5jsyFhc2JFHbFtO3eJ0hbHkc5EccJVsk7kjjy=" width="640" /><br />Mshauri Mwandamizi wa UNESCO, Bruno Nguyen, akielezea umuhimu wa kongamano hilo.<br /><br />Nae Mshauri Mwandamizi wa UNESCO, Bruno Nguyen, alisema kuwa kongamano hilo lina malengo ya kupata suluhisho ili kuhakikisha watu ambao wanaishi bara la Afrika wanapata maji safi na salama.<br /><br />Katika ripoti ya mwaka 2014 ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya (WHO) inaonyesha kuwa watu bilioni 1.8 duniani kote wanatumia maji ambayo yana vijidudu.<br /><img height="425" src="https://blogger.googleusercontent.com/img/proxy/AVvXsEjqewKAeH5LhzRrP6wOjlfFAH9blAWe5swApP15m46qAuuA5zNjLIie3Z8I1W4gj4nDXYwn0cPENe8s9RUc_qPYbvNnUhhQZrVDWvOtaEZ8o7FEiog3pPw0lUA5GIEjZ6z79uvaOiV1hYDTXQG-SxogmFonX9-UL_StjdLl=" width="640" /><br />Mtaalam wa programu wa UNESCO, Alexandros Makarigakis akitoa takwamu za usalama wa maji na jinsi taka mwili za binadamu zinavyoyafanya maji yasiwe salama.<br /><img height="425" src="https://blogger.googleusercontent.com/img/proxy/AVvXsEhONhFeECq35TK1SIfEgqXSYlI7vIb1DrTYyUM6jARuXPNYCJ2hg_tT-IdUK1GWNWjfky5zagN9ZGAHrywbX61a-G6xgz3k-aVbsB6IeS7kO9Fbl_2w3VCpjgeIG-w6lBBAhgnc_eDOek1dMzmErEIhdcKg39F6IQHuRNZA=" width="640" /><br /><br /><img height="425" src="https://blogger.googleusercontent.com/img/proxy/AVvXsEhaRYd0mcZoafzh45TgeQRIp-aDzij42pTEuvAnwdt4W6xZ23_1fjmzfuHXQkeMgAEmgkrED8mJG8cfKqou3gl-noYyPS_0B3NyaJZFit54Et23rkAQHWt2CVT5kuKPfPW_U4OqZfCpZc6KWhviMtAliYtIqWNufwl-PVy2=" width="640" /><br />Baadhi ya watu waliohudhuria kongamano hilo la siku moja kutoka mikoa mbalimbali na nchi jirani.<br /><img height="425" src="https://blogger.googleusercontent.com/img/proxy/AVvXsEhfYedGJteHh3VtcUlZ1cQg2V0TBHlKtXIHjnNGf4SXt_gxuUFVtN3w7Hvmy0gYnoMi7-CjmRhHDwnVmi1VrndO3-ww-L87JTffFzKxAQ7YROfJ0X8vgQNOfY76vYIrM7brXU3kVvK0_ppafQrBN6OIfzrUorzqV1MoiJXl=" width="640" /><br /><br /><img height="425" src="https://blogger.googleusercontent.com/img/proxy/AVvXsEjRClYNlEFnByG5RmOFa2hb_KBFLUBOKKiIeBkTqwO7KQpTslo3GF9r2ZS9EIVcJXPwIsMpBck9lHvB94CdLXeMQq3WQxqd9hVUe4ZFaAwTdi52fwYtdUL5h2cTdwf6ahg0fkjSofeSJHWI5Szu2ZeBfKpJLGuOXNcRSNHQ=" width="640" /><br /><br /><img height="425" src="https://blogger.googleusercontent.com/img/proxy/AVvXsEjOzzW_f8JDNDQMNBz2pYkCbfitKlBIp3q9TF46ze1i6Yq6nn7PPJfQEHQOJkGRllegQ311vgF-JTxJhV2HQPvi_mHz3Feax8Z7bx26m-9ai-3TCMtWgz9QqYsdshqNasUjuGdJaxjhyndRYLdrYCXEoqGvNzvaVPIJ_ZvP=" width="640" /><br /><br /><img height="425" src="https://blogger.googleusercontent.com/img/proxy/AVvXsEgkC55zotrzsi_1oDFHqb3nVHIfFD9LYGeAxFXcbjnKSPzrbltEpxQYvdHuZiQ98ElK3oxGBPGhO4apS-q6W5sCQHeKbyetUtPV7DeLD1LQIaRY3XZM50bL9DKjpj3UM_9Gq9ckiVRgmbdwDNMvBoOY1gW5zD4_dNv0w_Zm=" width="640" /><br /><br /><div style="text-align: center;">
Washiriki wakiwa katika picha ya pamoja.</div>

--
Zainul A. Mzige,
Operation Manager,
MO BLOG,
+255714940992.

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

0 comments:

Post a Comment