Friday, 2 October 2015

Re: [wanabidii] Bomu la Magufuli

Elisa,
Hizo ni siasa za kipendaroho. Magufuli si msafi. Soma makala ya Rweyemamu.
em

2015-10-02 8:26 GMT-04:00 'ELISA MUHINGO' via Wanabidii <wanabidii@googlegroups.com>:
Siku zile watu walijitahidi kumchafua Mrema. Wengine wakasem ni mla rushwa. Wenye kuona mbali wakawaonya wanaomchafua kuwa mkitaka kumchafua Mrema msimuunganishe na rushwa kwa sababu hakuna atakayewaamini. Nimelikumbuka sasa watu wanapotaka kumchafulia Magufuli.
--------------------------------------------
On Fri, 10/2/15, fatma_elia via Wanabidii <wanabidii@googlegroups.com> wrote:

 Subject: Re: [wanabidii] Bomu la Magufuli
 To: wanabidii@googlegroups.com
 Date: Friday, October 2, 2015, 10:37 AM

 Sent
 from my BlackBerry® smartphone provided by Airtel
 Tanzania.From:  Emmanuel Muganda
 <emuganda@gmail.com>
 Sender:  wanabidii@googlegroups.com
 Date: Thu, 1 Oct 2015 14:48:22
 -0400To: TANZANET Mailing
 List<list@tanzanet.org>;
 Wanazuoni@yahoogroups.com<Wanazuoni@yahoogroups.com>;
 wanabidii@googlegroups.com<wanabidii@googlegroups.com>ReplyTo:
  wanabidii@googlegroups.com
 Subject: [wanabidii] Bomu la
 Magufuli
 Habari
 hii ilichapishwa kwenye gazeti la RAI miaka michache
 iliyopita ikisomeka...
 Huyu Ndiye
 Pombe Magufuli:

 -
 Wasema nyumba 8,000 kauza kwa mkono wake mwenyewe
 - Apuuza maonyo ya wataalamu- Mafaili ya Sundi
 na Musa aliyabeba kwapani

 ALIYEKUWA Waziri wa Ujenzi, John Magufuli,
 katika Serikali ya awamu ya tatu, aliteka madaraka na kuwa
 mwenyekiti wa zoezi la kuuza nyumba za serikali ambazo hadi
 sasa, zimeshauzwa 8,288 imefahamika.

 Habari zilizopatikana ndani ya wakala wa
 Majengo ya Serikali (TBA), zimethibitishia Rai wiki hii
 kwamba Magufuli alihakikisha anashiriki kama Mwenyekiti
 katika zoezi zima la kuuza nyumba, ambalo kimsingi
 lilistahili kusimamiwa na Mtendaji Mkuu wa TBA.

 Kwa mujibu wa vyanzo kadhaa
 vya habari ndani ya TBA, Magufuli alifanya kila aina ya
 'fujo' katika zoezi la kuuza nyumba hizo, wakati
 mwingine akibatilisha maamuzi yaliyofanywa na Kamati ya TBA
 ya kuuza nyumba hizo, akiwapangia watu nyumba kwa utashi
 wake na wakati mwingine akiwakemea wale wote waliomshauri
 kinyume na matakwa.

 Ni
 chini ya utaratibu huo, habari zinaeleza kwamba Magufuli,
 aliyabeba yeye mwenyewe mafaili ya ndugu zake; Musa Magufuli
 ambaye ni mdogo wake, na Sundi Malomo ambaye ni mzazi
 mwenzake na kuwalazimisha watendaji wa TBA wafuate matakwa
 yake katika kuwapatia nyumba ndugu zake hao.

 Habari hizo zinaeleza kwamba
 awali Mtendaji Mkuu wa TBA alimshauri Magufuli kwamba suala
 la mauzo ya nyumba kwa ndugu zake ni kinyume cha utaratibu.
 Hata hivyo, imeelezwa kwamba Magufuli alilazimisha huku
 akisema mdogo wake hana tatizo kwa sababu alikuwa tayari
 mfanyakazi wa Serikali.

 Musa aliajiriwa kwa mkataba wa miezi mitatu,
 baada ya mwezi mmoja akauziwa nyumba na baada ya miezi
 miwili akaacha kazi.

 "Kwa
 upande wa Sundi, kwanza ilikuwa Sundi auziwe nyumba moja kwa
 moja. Lakini Magufuli alipoonywa akashtuka na kusema suala
 hilo aachiwe yeye mwenyewe. Na ndipo akaibuka na jina la
 Stanley Manongi kwamba ndiye mnunuzi halisi na baba yake
 Sundi," vinasema vyanzo hivyo vya habari, vingine ambavyo
 vilishiriki moja kwa moja katika mchakato wa uuzaji nyumba
 hizo.

 Habari hizo
 zinaendelea kueleza kwamba baadaye, Sundi alishtuka akitilia
 shaka uaminifu wa Manongi, kwamba angeweza kumdhulumu nyumba
 hiyo.

 "Ndipo Magufuli
 aliibuka na mpango wa Sundi kuwa mtoto wa Manongi na mrithi
 wake na kisha kwa kuhakikisha kwamba hakuna dhuluma yoyote,
 mtoto wa Sundi naye akarithishwa na kama mrithi wa pili,"
 chanzo hicho cha habari kinaeleza.

 Chini ya sheria ya Executive Agency Act No. 30
 ya mwaka 1997, TBA ilipewa madaraka yote ya kuuza nyumba za
 Serikali, kujenga nyumba mpya, kuzikarabati zilizopo pamoja
 na kugawa nyumba za madaraja A, B na C kwa wafanyakazi wa
 Serikali.

 Sheria hiyo
 inaipa mamlaka ya kipekee ya kufanya shughuli zote bila
 kuingiliwa na chombo chochote.

 Chini ya sheria hiyo, Waziri anaruhusiwa kuteua
 wajumbe wa bodi ya ushauri watakaomshauri Katibu Mkuu wa
 Wizara juu ya namna nzuri ya TBA kusimamia mamlaka yake.

 Hadi Machi mwaka huu, wajumbe
 hao walikuwa ni J. Kijazi, E. Lipambila, E. Lugwisha,
 Msangi, E. Mwakalinga, D. Kisasi, P. Ncheye, F. Werema na A.
 Bukuku.

 Hata hivyo, sheria
 haitoi nafasi yoyote kwa Waziri kusimamia shughuli za
 uuzwaji au upangaji wa nyumba za serikali.

 Mtendaji Mkuu wa TBA Togolayi
 Makumba Kimweri, alipoulizwa kupitia kwa Katibu Muhtasi
 wake, alimwambia mwandishi wa Rai aandike maswali kisha
 asubiri kuruhusiwa kuingia ndani ya ofisi.

 Hata hivyo, baada ya kusubiri
 kwa muda wa saa moja, mwandishi alipokwenda kuuliza
 akaambiwa kwamba Kimweri tayari alikwishaondoka ofisini
 kupitia mlango wa nyuma na asingeweza kurudi ofisini.

 Lakini baadhi ya wafanyakazi
 wa TBA wameiambia Rai kwamba kinachoandikwa kwenye magazeti
 kuhusu ushiriki wa Magufuli kuuza nyumba za Serikali ni
 kidogo mno kuliko hali halisi.

 Kama ilivyokuwa kwa mdogo wake Musa, waziri
 Magufuli alishinikiza mtoto wa dada yake anayeitwa James
 Doto Mgosha auziwe nyumba za serikali kwa kumtengenezea
 ajira ya muda mfupi katika TANROADS.

 Tofauti na Musa, Doto ameuziwa nyumba hiyo kwa
 jina la mtu mwingine lakini anaishi katika nyumba hiyo,
 namba 64 iliyopo Kinondoni Flats.

 Habari kutoka TBA zinaonyesha jina la mtu
 mwingine (tunalihifadhi) kuwa ndiye aliyeuziwa nyumba hiyo
 mtu huyo alipata kupitia utaratibu wa Magufuli kupeleka jina
 lake kwenye wakala wa majengo na kulazimisha apewe
 nyumba.

 Alipoulizwa kwa
 njia ya simu, Doto alisema suala la ajira na nyumba waulizwe
 waliomwajiri na kumpa nyumba. Akakata simu.

 Mfanyakazi mwingine alieleza
 Rai kwamba msichana mwingine (jina tunalihifadhi) akiwa na
 miezi minne tu kazini alipelekwa na Magufuli katika Wakala
 wa Majengo akilazimisha auziwe nyumba hata kabla ya
 kuthibitishwa kazini. Nyumba hiyo iko Block A, Ocean
 Road.

 Hata hivyo, habari
 hizo zinaeleza kwamba msichana huyo ambaye hadi sasa anaishi
 na wazazi wake, ameipangisha nyumba hiyo kwa mfanyakazi
 mmoja wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa na
 analipwa kwa dola za kimarekani.

 "Kuuza nyumba za serikali sawa, lakini kweli
 katika mtindo huu? Sisi tunaoshiriki kuzikagua na kuziratibu
 tukiomba hatupati, lakini wengine wanaingia serikalini miezi
 miwili wanapata nyumba. Na wengine hata si wafanyakazi,
 wanapata, hii si sahihi, alilalamika mfanyakazi mmoja
 aliyeandikia Rai kwa njia ya barua pepe.

 Hadi Machi mwaka huu Wakala wa Majengo wa
 Serikali (TBA) walishauza nyumba 8,288 ambazo hata hivyo
 zilitakiwa kuuzwa kwa watumishi wa serikali.

 Katika mauzo hayo, Serikali
 ilitarajia kupata jumla ya shilingi 60,016,556,439.00. Hata
 hivyo hadi sasa Serikali imepata shilingi
 22,684,108,115.08.

 Kwa
 sasa, Serikali imebakiwa na nyumba 1,098 zinazosimamiwa na
 TBA. Kati ya hizo, nyumba 692 zimetengwa kwa wafanyakazi wa
 Serikali, nyumba 675 kama tied quarters, nyumba 111
 zinatumika kama Rest House za Serikali, wakati nyumba 40
 zinatumika kama state lodges. Nyumba 24 zinatumika kama
 ofisi na nyingine 29 ni kama karakana na bohari.

 SALVA RWEYEMAMU
 RAIEmail This BlogThis! Share to Twitter Share to Facebook 
 0
 Comments :Post a
 CommentNewsreelPopularArchiveRecentRSS
 Feed WidgetSince February 1st,
 20149960220 



 --

 Send Emails to wanabidii@googlegroups.com

  

 Kujiondoa Tuma Email kwenda

 wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com  Utapata Email ya
 kudhibitisha ukishatuma

  

 Disclaimer:

 Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility
 for any legal consequences of his or her postings, and hence
 statements and facts must be presented responsibly. Your
 continued membership signifies that you agree to this
 disclaimer and pledge to abide by our Rules and
 Guidelines.

 ---

 You received this message because you are subscribed to the
 Google Groups "Wanabidii" group.

 To unsubscribe from this group and stop receiving emails
 from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.

 For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.




 --

 Send Emails to wanabidii@googlegroups.com

  

 Kujiondoa Tuma Email kwenda

 wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com  Utapata Email ya
 kudhibitisha ukishatuma

  

 Disclaimer:

 Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility
 for any legal consequences of his or her postings, and hence
 statements and facts must be presented responsibly. Your
 continued membership signifies that you agree to this
 disclaimer and pledge to abide by our Rules and
 Guidelines.

 ---

 You received this message because you are subscribed to the
 Google Groups "Wanabidii" group.

 To unsubscribe from this group and stop receiving emails
 from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.

 For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.


--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com

Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com  Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma

Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

0 comments:

Post a Comment