Friday 30 October 2015

[wanabidii] RE: [Wanazuoni] Neno La Leo: Mabadiliko

Neno halikutumika vibaya sema tu mfumo dola ulilitumia vibaya lisilete maaana kwani lilikua dhidi ya mfumo.
Hata hivi leo maneno mapya yanaanza kutumika kwa mfano "nimeagizwa na mamlaka ya juu"
Ulipata bure tusitoe bure kwanini? MADINI YETU TULIPATA BUTE TUSIYATOE BURE KWANINI
SHUKRANI

On Oct 30, 2015 11:47 AM, "Surumedia majiydsuru@gmail.com [Wanazuoni]" <Wanazuoni@yahoogroups.com> wrote:
 

Uko sahihi ndugu Mjendwa!
Wakati wa kampeni nilipata taabu sana kuhusu matumizi ya neno mabadiliko. Kiasi kwamba neno hilo lilikosa maana halisi ya neno lenyewe. Ilinishangaza hasa pale mwandishi mwanazuoni anaposahau kawaida ya matumizi ya maneno kwa makusudi.  Ilifikia baadhi ya wanazuoni walitumia neno mabadiliko wakimaanisha kuhama chama, kuacha ukweli, kupotosha, kujikataa, kujidharau na kufuata upepo wa ufisadi. Iliandikwa wakati fulani kwamba, wananchi ni wale tu watakaoweza kuchagua waliohama chama tawala, wanaokataa ukweli, wanaopotosha, wanaojikataa, wanaodharau, wanaobeza na wanaofuata upepo wa ufisadi unakoelekea. Ilichukuliwa kwamba, watakao chagua wasiohama chama tawala, wanaosema ukweli, wasiopotosha, wasiojikataa, wasiotudharau, wasiotubeza na wasiofuata upepo wa ufisadi kwamba hao siyo wananchi. Kwa Ujumla neno mabadiliko na neno wananchi wamepotoshwa sana katika kampeni za uchaguzi mkuu mwaka huu 2015. Tunayo nafasi ya kujirekebisha na kurejesha ufahamu wetu na Uanazuoni wetu.
Wakatabahu!

..........................................................................
"Ni bora kukaa kimya kuliko kuzungumza yasiyowafaa watu, lakini ni bora zaidi kusema yanayowafaa watu kuliko kukaa kimya".

Baba Nouman,
Bongonyika, East Africa

From: Maggid Mjengwa mjengwamaggid@gmail.com [Wanazuoni]
Sent: ‎30/‎10/‎2015 09:24
To: mabadilikotanzania; wanabidii; Wanazuoni@yahoogroups.com
Subject: [Wanazuoni] Neno La Leo: Mabadiliko [1 Attachment]

 


Ndugu zangu,

Uchaguzi umeshapita. Tunafungua sasa ukurasa mwingine. Lakini, haina maana ya kuacha kufanya tathmini yakinifu ili tuweze kujifunza.

Tumeona, kuwa dhana ya mabadiliko ilitawala uchaguzi wa mwaka huu. Ni sahihi, kuwa mwanadamu, kwa asili, ni kiumbe mwenye kutamani mabadiliko. Ni kuanzia kwenye mavazi, chakula na mengineyo.

Tumekuwa wavivu sana wa kutafakari kwa kina juu ya tunamaanisha nini tunaposema tunataka mabadiliko katika nchi. Bahati mbaya, baadhi ya wanasiasa wameonyesha udhaifu mkubwa katika kuielewa dhana ya mabadiliko, ikawa kama wimbo wa taarab tu.

Ikafika mbali, kuwa waliosimama majukwaani kuhubiri mabadiliko hawakujua kama walifanya kazi pia ya kumhujumu mgombea ama wagombea wao wenyewe.

Sifa moja kubwa ya Watanzania ni dhamira na utayari wao wa kukataa kudharauliwa. Ilipofika mahali, watu wazima wanaojiita viongozi wakasimama majukwaani na kutamka; " CCM imechoka, nendeni mkachague hata jiwe!"

Huko ni kuwadharau Watanzania. Ni kauli kama hiyo ndio iliyowafanya Watanzania wengi waviache vitanda vyao alfajiri na mapema siku ya Uchaguzi Mkuu, waende kuhakikisha wanazuia 'mawe' yasipite. Maana, haikuwaingia akilini kuwa kwa miaka 54 CCM haikufanya chochote na kwamba imefika wakati wa kufanya mabadiliko kwa kuyaweka ' mawe' na CCM kuichimbia shimo kabisa. Kwenye siasa kauli zinaweza kupelekea kupanda au kuanguka kwa chama na mwanasiasa.

Na tuendelee kuitafakari dhana ya mabadiliko.

Ni Neno La Leo.

Maggid,

Iringa.

__._,_.___

Posted by: Surumedia <majiydsuru@gmail.com>
Reply via web post Reply to sender Reply to group Start a New Topic Messages in this topic (2)

Check out the automatic photo album with 1 photo(s) from this topic.
0.jpg


.

__,_._,___

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

0 comments:

Post a Comment