Sunday 30 March 2014

[wanabidii] TAARIFA YA MAFANIKIO YA UTENDAJI KAZI YA BANDARI YA DAR ES SALAAM KWA KIPINDI CHA MIEZI SITA (JULAI - DISEMBA 2013)

TAARIFA YA MAFANIKIO YA UTENDAJI KAZI YA BANDARI YA DAR ES SALAAM KWA KIPINDI CHA MIEZI SITA (JULAI – DISEMBA 2013)

Katika kipindi cha miezi sita ya Julai – Disemba 2013, Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) kwa kushirikiana na wadau imefanikiwa kwa kiasi kikubwa katika kuongeza ufanisi katika bandari ya Dar es Salaam. Mafanikio hayo ni pamoja na ongezeko la shehena, kuongezeka kwa tija katika kuhudumia shehena na meli, kupunguza msongamano wa meli na mlundikano wa mizigo bandarini na kukomesha vitendo vya upotevu wa mizigo wateja bandarini.

1.HUDUMA KWA SHEHENA

Katika kipindi cha miezi sita ya Julai – Disemba, 2013 bandari ilihudumia tani milion 7.50 ukilinganisha na tani 
million 6.38 zilizohudumiwa katika kipindi cha Julai – Disemba, 2012, ongezeko la 17.6%. Sababu za kuongezeka kwa shehena ni pamoja na:

(i)Kukua kwa uchumi wa nchi zinazotumia bandari.

(ii)Jitihada zinazofanywa na serikali katika kuimarisha miundombinu ya usafirishaji

(iii)Jitihada za kimasoko zinazofanywa na bandari pamoja na wadau

(iv)Kuwepo kwa amani na utulivu bandarini kutokana na uhusiano mzuri 

2.HUDUMA KWA MELI

Idadi ya meli (Ships call) katika kipindi cha miezi sita ya Julai – Disemba, 2013 bandari ilihudumia jumla ya meli 868 zenye ukubwa wa GRT million 15.4 ukilinganisha na meli 677 zenye ukubwa wa GRT million 11.7 zilizohudumiwa kipindi cha Julai – Disemba, 2012. Ongezeko la meli ni 28.2% na ongezeko la GRT 31.6%.

3. UFANISI KATIKA UTENDAJI KAZI
Ufanisi na utendaji kazi bandarini umeongezeka katika kipindi cha nusu mwaka Julai – Disemba, 2013 ukilinganisha na Julai-Disemba, 2012 kwa kutumia viashiria mbali mbali ikiwa ni pamoja na:

(i)Idadi ya siku meli kukaa bandarini imepungua katika kipindi cha Julai – Disemba 2013, ilipungua hadi siku 5.6 ukilinganisha na siku 5.9 kipindi cha Julai – Disemba, 2012, ikiwa ni asilimia 5.1 za kupungua

(ii)Muda wa ukaaji wa kontena bandariniumepungua kutoka wastani wa siku 9.5 kipindi cha Julai-Disemba, 2012 hadi wastani wa siku 8.5 kipindi cha Julai-Disemba, 2013, punguzo la asilimia 10.5.

(iii)Katika kipindi cha Julai – Disemba 2012, utendaji wa krini kwa upande wa TPA (Kitengo cha Mizigo mchanganyiko) uliongezeka kutoka mizunguko 249 kwa saa 24 Julai-Disemba, 2012 hadi mizunguko 418 kwa saa 24 Julai-Disemba, 2013, ongezeko la asilimia 67.9. Kwa upande wa TICTS utendaji ulikuwa mizunguko 605 kwa saa 24 kipindi cha Julai – Disemba 2012 ukilinganisha na mizunguko 611 kwa saa 24 kipindi cha Julai-Disemba, 2013, ongezeko la asilimia 1.0.

(iv)Upakuaji wa magari umeongezeka hadi kufikia magari 672 kwa shifti (kuna shifti 3 kwa saa 24 na kila shifti ina saa 8) kwa kipindi cha Julai-Disemba, 2013 ikilinganishwa namagari 634 kwa shifti kwa kipindi cha Julai-Disemba, 2012, ikiwa ni ongezeko la asilimia 5.7.

3.1 SABABU ZA KUONGEZEKA KWA UFANISI

(i)Hatua zilizochukuliwa na Serikali kupitia Wizara ya Uchukuzi katika kusimamia kwa karibu utendaji kazi wa Mamlaka.

(ii) Ununuzi wa vitendea kazi kwa ajili ya kuboresha huduma kwa meli na mizigo.

(iii) Mafunzo kwa wafanyakazi

(iv) Kuongezeka kwa maeneo ya kufanyia kazi nakuhifadhiamizigo,mfano “EX-AMI” (1,200 TEUS) na “EX-NASACO” (3,600 TEUS), ICDS 10 (15,550 TEUs) naCFS3 (Magari 5,630).

(v)Matumizi ya TEHAMA katika kuhudumia wateja (Harbour View, Cargo System, Billing System na epayment)

(vi) Kuanzishwa kwa One Stop Centre: Wadau wa bandari wamepewa ofisi bandarini ambapo kwa sasa wanapatikana katika eneo moja na hivyo kurahisisha huduma kwa wateja.

(Vii)baadhi ya mizigo (ya Tanzania) bandarini mara tu inapoteremshwa (direct delivery)

(viii)Kuwepo na nguvu kazi yenye ujuzi wa kutosha na iliyo motishwa

4.MATUMIZI

Mapato ya bandari ya Dar es Salaam kwa kipindi cha Julai – Disemba, 2012 yalikuwa ni jumla ya shilingi 191,637,360,000 wakati kwa kipndi cha Julai – Disemba 2013, mapato yalikuwa ni jumla ya shilingi 224,196,470,000/= hii ikiwa ni ongezeko la asilimia 16.9

5.ULINZI NA USALAMA

Ulinzi na usalama katika bandari ya Dar es Salaam umekuwa unaboreshwa na kuimarishwa kila wakati. Ulinzi na usalama ni changamoto ambapo mikakati inachukuliwa ili kuweza kufanya bandari kuwa salama kwa wafanyakazi, wateja, meli, mizigo na mali kwa ujumla. Matukio ya uhalifu/wizi yamekua yakipungua kila mwaka kwa sababu ya juhudi za Mamlaka katika kukabiliana na changomoto hizo. Mikakati ya kupambana na wizi kwa lengo la kuondoa kabisa vitendo vya wizi ni pamoja na:

(i)Matumizi ya TEHAMA katika upokeaji na utoaji wa mizigo bandarini, ambao umepunguza matumizi ya karatasi zilizokuwa zikighushiwa.

(ii)Kutoruhusu bandari kutumika kama sehemu ya kuhifadhia mizigo.

(iii)Kutofumbia macho udokozi wa mali za wateja (Zero tolerance).

(iv)Kuwashirikisha wafanyakazi na wateja katika ulinzi wa mali za wateja na wafanyakazi (Ulinzi shirikishi).

5. CHANGAMOTO

Pamoja na mafanikio yaliyopatikana katika kipindi cha Julai – Disemba 2013 kuna changamoto kadhaa ambayo bandari imekutana nazo katika utendaji kazi wake. Changamoto hizo ni pamoja na:

(i)Ufinyu wa maeneo ya kuhudumia meli na shehena

(ii)Mahitaji makubwa ya fedha kwa ajili ya kuboresha na kupanua huduma za bandari

(iii)Kina kifupi cha maji na ufinyu wa lango la kuingilia meli

(iv)Mabadiliko ya teknologia ya meli

(v)Huduma hafifu ya reli

6. MIKAKATI YA KUBORESHA ZAIDI HUDUMA

(i)Kuongeza kina cha gati Na. 1 hadi 7 na lango la kuingilia bandarini ili kuwezakuhudumia meli kubwa.

(ii)Kujenga gati Na. 13 na 14 kwa ajili yakuhudumia shehena ya makasha.

(iii)Kuunganisha wateja katika mtandao mmoja wa mawasiliano ya kompyuta (PortCommunity System).

(iv)Kuimarisha ulinzi na usalama bandarini kupitia mradi wa “Integrated Security System.”

(v)Kuboresha mifumo ya kompyuta kwa ajili ya upakuaji, upakiaji, na uotaji wa mizigo bandarini.Tayari mifumo ya kompyuta yaHarbour view, Cargo system na billing system inafanya kazi. Mfumo wa billing system umewezesha wateja kulipa malipo moja kwa moja kupitia benki, k.m. CRDB.

(vi)Kuendelea kutoa elimu kwa wafanyakazi ili kuboresha ujuzi wao.

(vii)Kujenga maeneo ya kuhudumia shehena ya makasha (Mfano; Kisarawe ICD naEx-Copper Yard).

(viii)Ujenzi wa matanki ya kuhifadhi mafuta (tank farms) huko Ras Mjimwema.

(ix)Ujenzi wa kituo cha kuhudumia mizigo cha Kisarawe (CFS). Wilaya ya Kisarawe imeipa TPA eneo la eka 1,760 za ardhi. TPA imeomba Halmashauriya Kisarawe kuthamini na kutoa gharama za fidia.

(x)Kushirikisha sekta binafsi katika uwekezaji na uendeshaji wa shughuli zabandari.

7.HITIMISHO

Serikali kupitia Mamlaka ya usimamizi wa Bandari Tanzania itaendelea kuwekeza katika bandari ya Dar es salaam kwa kujenga uwezo wa rasilimali watu namiundombinu pamoja na vitendea kazi vya kutosha na vya kisiasa. Msisitizo umewekwa katika matumizi ya TEHAMA ili kuhakikisha bandari hii inatoa huduma bora kwa wateja wake.

IMETOLEWA NA
MAMLAKA YA USIMAMIZI WA BANDARI TANZANIA

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

0 comments:

Post a Comment