Thursday 11 August 2016

Re: [wanabidii] KESI YA CHADEMA YA KUTAKA MAANDAMANO YATUPWA NA KORTI KUU

Katabazi;
Naona maendeleo makubwa katika uandishi wako,naomba nikupe hongera Mdada.
Ukiwa na mada ambayo inasomeka kwa mtiririko mzuri huleta hamu ya kuisoma hata iwapo ni ndefu zaidi ya wastani.
 
Reuben



On Thursday, August 11, 2016 1:26 PM, 'mohamed mnzava' via Wanabidii <wanabidii@googlegroups.com> wrote:


Hawa CHADEMA wanajichanganya sana, . . . . . na wanatuhanganya sisi tusiojua sharia.

Wanashindwa hata kuwakilisha Hoja ktk Kesi nzito kama hiyo. Sasa tuwategemee wapi na vipi iwapo wanashindwa hata kusoma, kutafsiri na kutumia Sheria zilizopo wazi!!
Watambue na wakumbuke kuwa "Kesi ni malumbano ktk Hoja", kesi sio malumbano ya majukwaa ya siasa.

Mhhh, wahenga walisema "papara Ureke"


On Thursday, August 11, 2016 1:11 PM, 'Happiness Katabazi' via Wanabidii <wanabidii@googlegroups.com> wrote:



KESI YA CHADEMA YA KUTAKA MAANDAMANO YATUPWA NA KORTI KUU

Na Happiness Katabazi
HATIMAYE Mahakama Kuu Kanda ya Dar Es Salaam, imelifukuza kwa gharama ombi  la kuiomba Mahakama hiyo iwapatie Kibali  cha Kufungua mahakamani hapo ombi la kuomba Mahakama hiyo iifute  amri /uamuzi wa Inspekta Jenerali wa Polisi Ernest Mangu ya kuzuia maandamano na mikutano ya kisiasa nchini  kwasababu ya dosari za kisheria .

Uamuzi huo ulitolewa Juzi na Jaji Kiongozi Fredinand Wambali  wakati  Katika ombi Na. 52/2016 lilowasilishwa Mbele yake na Baraza la Udhamini la Chadema lilokuwa kikitetewa na wakili wa kujitegemea Peter Kibatara dhidi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Inspekta Jenerali wa Polisi waliokuwa wakitetewa na Mawakili wa serikali Haruna Matagane na Daniel Nyakeha.

Jaji Wambali  alisema mlalamikaji  alikuwa na Maombi mawili.Ombi la kwanza Chadema ilikuwa ikiomba Mahakama hiyo iwapatie Kibali cha Kufungua Kesi ya kupinga amri na uamuzi wa IGP wa Kuzuia mikutano na maandano ya vyama Vya siasa nchini na ombi la pili waliomba Mahakama hiyo itoe tamko la Kusema  amri na uamuzi Huo wa IGP Si halali kisheria.

Uamuzi huo ulitolewa Juzi na Jaji Kiongozi  Fredinand Wambali  ambapo alisema amekubaliana mapingamizi yaliyowasilishwa na upande wa utetezi kwamba huwezi kuomba amri ya mapitio ya amri ya IGP Mahakamani hapo wakati    mlalamikaji alikuwa na Mlango mwingine wa kupinga amri ya IGP na Mlango huo ni kwa mlalamikaji Kupenda kupinga amri ya IGP kwa Waziri wa Mambo ya Ndani  na alishindwa kufanya hivyo.

" Chadema walipaswa kukatia rufaa amri hiyo ya IGP ya Kuzuia maandamano ya vyama Vya siasa Kwa Waziri wa Mambo ya Ndani na sio kwenda kushitaki mahakamani' alisema Jaji Wambali na hiyo ikapatikana Katika Kifungu Cha 43(6) sura 322  ya Mwaka 2002 ya Judicial Review .

Aidha Jaji Wambali alisema anakubaliana na pingamizi la pili la Mawakili wa serikali ambalo lilidai Kuwa ombi Hilo la Chadema litupwe kwasababu ombi Hilo la Chadema halikuambatanishwa na maelezo ya mlalamikaji  NA hayo maelezo ya Kidhi matakwa ya Kanuni ya 5(2) of The Judicial Reviews Rules of 2014 ambayo inataka hiyo hati ya mlalamikaji if afanue maelezo na jina la mlalamikaji.

" Chadema Katika shauri Hili hayo yote walishindwa kuyafanya  hivyo Mahakama hii inatupilia Mbali ombi Lao la kutaka Mahakama hii itamke amri ya IGP Kuzuia maandamano ni batiri kwa gharama kwasababu ombi la Mlalamikaji halijakidhi matakwa ya kisheria.

Chanzo: Facebook: Happiness Katabazi

11/8/2016.









Sent from my iPad

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com

Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com  Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma

Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.


0 comments:

Post a Comment