Utamu unakuwa mgawanyiko wa kura, zitayumba, kwa kuwa wanachama wa vyama vyote viwili vya TLP na CCM, watapiga piga tu bila kujipanga kwa ushawishi uliodhaniwa.Mwishowe ni Mbatia anawin.
Naona kama kwa.mtaji huo, Mbatia karahisihiwa kampeni, na kupata kura kibao
SB
On Oct 14, 2015 10:05 PM, 'mpombe mtalika' via Wanabidii <wanabidii@googlegroups.com> wrote:
--
"NDOA isiyo rasmi kisiasa" baina ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) na chama cha upinzani cha Tanzania Labour Party (TLP) mkoani Kilimanjaro imemweka katika mazingira magumu kisiasa James Mbatia wa NCCR-Mageuzi anayegombea Ubunge wa jimbo la Vunjo.
Katika hali isiyotarajiwa kisiasa vyama hivyo viwili vimekuwa katika ushirikiano usio rasmi katika mkoa huo kukabiliana na vyama vinavyounda umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) katika kampeni za uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba 25 mwaka huu.
Ushirikiano huo ulithibitika wiki iliyopita wakati wa mikutano ya kampeni ya mgombea wa nafasi ya Urais wa CCM Dk. John Pombe Magufuli katika jimbo la Vunjo ambapo Mwenyekiti wa TLP Taifa Agustine Lyatonga Mrema alimnadi mgombea huyo wa CCM wakati chama chake kina mgombea anayewani Urais Maxmillan Lyimo.
Akiwa katika mji mdogo wa Himo wiki iliyopita Mrema alimnadi Dk. Magufuli akimwelezea kama mtu anayefaa kuwa Rais wa Tanzania kutokana sifa zake za uchapakazi, uadilifu na ujasiri wa kusimamia uamuzi.
Taarifa zilizofikia Raia Mwema kutoka ndani ya jimbo la Vunjo zinabainisha kuwa ubia huo wa kisiasa baina ya CCM na TLP unaweza kumwathiri na mgombea wa nafasi ya Ubunge katika jimbo hilo kwa tiketi ya NCCR-Mageuzi James Mbatia.
Mbatia, ambaye pia ni Mwenyekiti Mwenza wa Ukawa aliwahi kuwa Mbunge wa Vunjo kati ya mwaka 1995-2000 kabla ya kuangushwa katika uchaguzi wa mwaka 2000 na Jesse Makundi wa TLP.
Mbatia anakabiliwa na upinzani mkali kutoka kwa mgombea wa CCM Innocent Shirima pamoja Agustine Mrema (TLP) ambaye ndiye anayetetea kiti cha Ubunge wa jimbo hilo.
Kwa mujibu wa wakazi wa jimbo hilo katika mikutano yake ya kampeni Mrema amekuwa akikaririwa mara nyingi kuwa kama wananchi wa Vunjo hawatakuwa tayari kumchagua yeye basi wampigie kura mgombea wa CCM Innocent Shirima ambaye anamtaja kama "mjukuu" wake.
Kwa mujibu wa moja wa viongozi wa TLP katika jimbo hilo aliyeomba jina lake lihifadhiwe hatua hiyo Mrema imetokana na kuwepo kwa uhasama mkubwa kisiasa kati yake na Mbatia tangu wakiwa pamoja ndani ya NCCR-Mageuzi kati ya mwaka 1995-1999.
"Mrema na Mbatia ni mahasimu wakubwa kisiasa tangu enzi za NCCR-Mageuzi na Mrema amewahi kulalamika mara nyingi hadharani kuwa Mbatia amekuwa akimfanyia "fitina" za kisiasa katika jimbo lake," kilieleza chanzo chetu.
Taarifa zaidi zinaeleza kuwa ushirikiano huo baina ya Mrema na CCM umemweka katika wakati mgumu kisiasa Mbatia na uwezekano wa kushinda nafasi ya Ubunge katika jimbo hilo umeelezwa kuwa ni finyu.
"Wagombea wote wa CCM na TLP wamekuwa wakimshambulia Mbatia katika majukwaa ya kisasa hali ambayo inamweka katika wakati mgumu Mwenyekiti huyo mwenza wa Ukawa," aliongeza mtoa taarifa wetu.
Aidha Mbati pia amejikuta katika wakati mgumu zaidi kufuatia kuibuka kwa mgogoro baina yake na wagombea Udiwani wa Chadema katika kata 16 za jimbo ambao wamegoma wote kumfanyia kampeni katika kata zao kama sehemu ya makubaliano baina ya vyama vinavyounda Ukawa.
Kwa mujibu wa makubaliano ya awali baina ya vyama vinavyounda Ukawa, Mbatia alipewa heshima ya kuwakilisha umoja huo kugombea Ubunge Vunjo na Chadema walipaswa kumwunga mkono.
Kutokana na kuwepo kwa hali hiyo imeelezwa kuwa Mwenyekiti huyo wa NCCR-
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.
0 comments:
Post a Comment