Monday, 3 August 2015

Re: [wanabidii] Haya ndio maneno ya mnyika juu ya ufisadi wa Lowasa miaka miaka 7 iliyopita leo hii wnadai amekuwa mtakatifu

hatari sana, ndionakubali sana maneno ya Mh Arfi alipomwambia Mh Lisu kuwa aweke akiba ya maneno

2015-08-02 13:00 GMT+03:00 'ELISA MUHINGO' via Wanabidii <wanabidii@googlegroups.com>:
Jamani muda tu ndio utaamua. Kinachoniumma ni watanzania kukikosa chama chao walichokipenda kwa sababu ya kumkaribisha ndugu yetu huyu basi.
--------------------------------------------
On Sun, 8/2/15, Ireneus Kakuru Mushongi <ireneuskakurumushongi@gmail.com> wrote:

 Subject: Re: [wanabidii] Haya ndio maneno ya mnyika juu ya ufisadi wa Lowasa miaka miaka 7 iliyopita leo hii wnadai amekuwa mtakatifu
 To: "wanabidii@googlegroups com" <wanabidii@googlegroups.com>
 Date: Sunday, August 2, 2015, 11:12 AM

 "Kwa
 niaba ya Baraza la Vijana wa CHADEMA (BAVICHA), kwa taarifa
 hii tunarudia
 kukemea jitihada zozote za kumlinda na kumtangaza Lowassa
 kuwa shujaa katika taifa letu kwani hali hii ikiachwa kuendelea inatoa
 mfano mbaya kwa vijana wa Tanzania. Tusingependa kwa namna yoyote katika taifa
 letu, mtuhumiwa wa ufisadi aliyetajwa pia katika orodha ya
 mafisadi(list of shame) kulindwa na kuenziwa kama shujaa wa
 Taifa letu kwani ni kuharibu maana nzima ya ushujaa katika
 uwajibikaji."



 Omukunirwa
 Ireneus 



  

 2015-08-02 9:31 GMT+03:00
 'mpombe mtalika' via Wanabidii <wanabidii@googlegroups.com>:


 Wednesday, September 3, 2008


 SERIKALI IACHE KUMLINDA LOWASSA


 Siku chache zilizopita. Nilitoa taarifa hii kwa vyombo
 vya
 habari. Hata hivyo, kwa sababu ambazo sizifahamu, habari hii
 haikutoka katika
 magazeti mengi ya kila siku. Pengine inaweza ikawa ni njia
 iliyotumika
 kufikisha ujumbe(barua pepe) lakini kuna uwezekano mkubwa
 sababu ikawa ni kuwa
 Lowassa hakutajwa kuchukuliwa hatua kama hizi ambazo
 nimezieleza hapa katika
 yale Maazimio 23 ya Bunge.



 Yeye aliambiwa tu atakafakari na kuchukua maamuzi
 ambayo
 ataona yanafaa. Yeye akaamua kujiuzulu. Lakini bado
 siridhiki sana na sababu
 hii kwa kuwa maazimio hayo 23 hayajasema Karamagi na Msabaha
 wachunguzwe kuhusu
 Rushwa kama serikali ilivyoamua. Kama imeamualiwa na
 Serikali hawa wachunguzwe,
 kwanini serikali haikumjumuisha na Lowassa? Hii inafanya
 niamini kwamba bado
 msimamo huu hapa chini ni mwafaka:

  

 TAARIFA KWA UMMA

  

 SERIKALI IACHE KUMLINDA
 LOWASSA                                               


  

     Ni mmoja wa mizizi
 ya ufisadi wa Richmond

     Akamatwe,
 ahojiwiwe na achukuliwe hatua za kisheria.

  

 Tarehe 25 Februari, 2008 Vijana wa CHADEMA tulitoa
 taarifa
 kwa umma tukikemea jitihada zilizokuwa zikiendelea za
 Lowassa kujisafisha na
 kusafishwa na tukahimiza achukuliwe hatua za haraka kutokana
 na tuhuma za
 ufisadi na/ama matumizi ya madaraka katika kashfa ya
 RICHMOND. Pamoja na
 taarifa yetu hiyo kwa umma katika kipindi chote ambacho
 Serikali ilipewa na
 Bunge kutekeleza maazimio ya Bunge kuhusu suala hilo hatua
 tulizopendekeza
 hazikuchuliwa.
  Aidha
 tumefadhaishwa zaidi na Taarifa ambayo Waziri Mkuu,
 Mheshimiwa Mizengo ameiwasilisha Bungeni Alhamisi 28 Agosti,
 2008 pamoja na
 kutaja hatua ambazo zimechukuliwa kuhusu watuhumiwa wengine
 ikiwemo kuandikiwa
 Barua za kujieleza na/ama kuanza kuchunguzwa na vyombo vya
 dola/usalama; Waziri
 Mkuu hakueleza hatua ambazo zimeaanza kuchukuliwa dhidi ya
 Bwana Lowassa.


 Tunatambua kuwa Waziri Mkuu katika taarifa yake
 ameeleza
 kuhusu hatua ambazo serikali imeanza kuchukua ikiwemo za
 marekebisho ya Sheria
 ama mifumo ya uwajibikaji, ikiwemo ile ya manunuzi. Hata
 hivyo, tungependa
 kuweka bayana kwamba matatizo ya msingi ya taifa letu
 hayasababishwi na
 mapungufu katika sheria pekee, ila kwa kiasi kikubwa
 yanasababishwa na kulegea
 kwa misingi ya utawala wa sheria na uwajibikaji miongoni mwa
 viongozi
 . Hivyo,
 tunapenda kuwajulisha Watanzania kuwa kama watuhumiwa wa
 ufisadi
 hawatachukuliwa hatua mapema, misingi ya utawala wa sheria
 itazidi kutetereka
 na matokeo yake ni kuwa mageuzi yoyote katika mifumo ya
 kiutawala
 hayatatekelezwa kikamilifu. Kwa ujumla tunaamini kwamba
 utamaduni huu wa
 kulindana katika serikali unatoa mfano mbaya kwa vijana wa
 kitanzania kuhusu
 uongozi na utawala bora.

  

 Tungependa kusisitiza kuwa Bwana Lowassa, akiwa Waziri
 Mkuu
 wa nchi yetu wakati huo alikuwa mmoja wa mizizi mikuu ya
 ufisadi wa RICHMOND.
 Hivyo, tunaona kuwa Taarifa ya Utekelezaji ya Waziri Mkuu
 Pinda imejikita
 katika kushughulikia matokeo badala ya mzizi wa tatizo
 lenyewe na hivyo kama
 hali hii ikiendelea itaporomosha nidhamu na uwajibikaji
 katika taifa letu.

 Tunaamini kwamba kama Bwana Lowassa aliyekuwa kinara wa
 Serikali wakati huo,
 ataweza kuchukuliwa hatua kikamilifu basi itakuwa rahisi kwa
 waliokuwa chini
 yake kuweza kuchukuliwa hatua za haraka na hatimaye
 kurejesha maadili katika
 utawala. Lakini kama Serikali itaendelea kumlinda Bwana
 Lowassa na kuwatoa
 kafara maafisa wa chini, bado haitakuwa imetekeleza
 kikamilifu dhana ya
 uwajibikaji na utawala wa Sheria. Kujiuzulu kwa Waziri Mkuu
 na mawaziri wenzake
 kadhaa ni hatua ndogo sana katika kashfa iliyohusisha
 uvunjaji wa Sheria za
 nchi yetu, mazingira ya ufisadi na hasara kubwa kwa
 taifa.

  

 Sisi tunaona kutotajwa kikamilifu kwa hatua
 zilizochuliwa
 juu ya Bwana Lowassa ni mwendelezo wajitihada za miezi ya
 karibuni za Bwana
 Lowassa(Mb) kupita akijitetea kuanzia katika hotuba yake
 alipokwenda Jimboni
 Monduli na kunukuliwa na vyombo mbalimbali vya habari na
 hata mahojiano yake
 maalumu na Televeshioni ya Taifa(TVT).

  

 Aidha, taarifa ya Waziri Mkuu Pinda imeakisi uamuzi wa
 Waziri Mkuu aliyejiuzulu Bwana Edward Lowassa kujitokeza
 miezi ya karibuni
 kujitetea kuhusu kuhusika kwake katika kashfa ya Richmond
 ambayo kwa ujumla ni
 ishara ya unafiki wa kisiasa.
  Itakumbukwa kuwa baada ya Kamati
 Teule
 kuwasilisha taarifa yake, Bwana Lowassa alipata nafasi
 bungeni takribani mara
 mbili kama kiongozi wa shughuli za serikali bungeni wakati
 akiwa Waziri
 kuzungumzia suala hili lakini hakutoa utetezi ambao Mwezi
 Februari alijaribu
 kuutoa kwa umma
  Waziri Mkuu Pinda inabidi auleze
 Umma kama uamuzi wa
 kumtomtaja katika Taarifa yake ya utekelezaji kuhusu hatua
 ambazo amechuliwa ni
 ishara kuwa serikali imekubaliana na utetezi wa Bwana
 Lowassa.

  

 Itakumbukwa kuwa Vijana wa CHADEMA tulieleza wazi
 kwamba
 katika kujitetea kwake mwezi Mei, Bwana Lowassa
 alithibitisha wazi uzembe na
 matumizi mabaya ya madaraka ambayo aliyafanya alipokuwa
 Waziri Mkuu wakati wa
 sakata zima la Richmond. Hivyo, tunarudia kutoa mwito kwa
 vyombo vya dola
 kuweza kumkamata, kumhoji na kumchukulia hatua za kisheria
 dhidi ya uzembe na
 matumizi hayo mabaya ya madaraka kwa mujibu wa sheria za
 nchi yetu.
 Badala ya
 Bwana Lowassa kuendelea kupita akijitetea kuwa Kamati Teule
 haikumuita kuweza
 kujieleza; vyombo vya dola vimkamate akatoe maelezo yake
 panapohusika. Vyombo vya
 dola vimekuwa vikiwakamata raia wa kawaida wenye taarifa za
 uhalifu kuweza
 kuisadia polisi, inashangaza Bwana Lowassa amejieleza wazi
 kuwa alikuwa
 anafahamu uhalifu uliokuwa ukitendeka lakini bado yuko nje
 akijitetea na pia
 Taarifa za kiserikali zikielekea kumlinda
 . Tunaamini akikamatwa yeye,
 atawezesha watuhumiwa wakuu wa kashfa ya Richmond kuweza
 kupatikana. Tulieza
 wazi katika tamko letu na Mwezi Februari kuwa , jitahada
 zozote za kumlinda na
 kumtetea zingeweza kuathiri mwekekeo wa hatua ambazo
 zitanatarajia kupendekezwa
 na Kamati ya Waziri Mkuu mpya Mheshimiwa Mizengo Pinda.
 Kutokana na Taarifa ya
 Waziri Mkuu Pinda aliyowasilisha Bungeni Alhamisi tarehe 28
 Agosti, 2008 ni
 wazi kuwa kuna kila dalili kuwa mwelekeo huo umeanza
 kuathiriwa, hivyo
 tunarudia tena kutaka Bwana Lowassa achukuliwe hatua kabla
 ya Bunge la Mwezi
 Novemba, 2008.

  

 Bwana Lowassa akiwa Waziri Mkuu amethibitisha kwamba
 maneno
 yake mwenyewe kuwa alikiuka Sheria ya Maadili ya Viongozi wa
 Umma ya mwaka 1995
 na Sheria ya Makosa ya Udhibiti wa Uhujumu wa Uchumi wa nchi
 ya Mwaka 1984.

  

 Bwana Lowassa alikiri kwamba alikuwa anafahamu kwamba
 Richmond ni kampuni ya kitapeli, lakini katika kipindi chote
 cha uongozi wake
 aliinyamazia hali hii na kwa kiasi kikubwa aliitetea kampuni
 hiyo mbele ya
 macho ya umma. Wakati wa Viongozi mbalimbali wa upinzani
 walipoweka bayana
 kwamba Richmond ni kampuni isiyo na uwezo, serikali ilitetea
 kampuni hiyo.
 Vyombo mbalimbali vya habari vilimtuhumu Bwana Lowassa mwaka
 2006 na 2007 kama
 kiongozi wa Shughuli za serikali bungeni, kwamba alishiriki
 'kuwaziba midomo'
 wabunge wa CCM wasijadili suala hili.
  Pia, ni Bwana Lowassa huyo huyo,
 alinukuliwa akiwa Arusha akiwataka watanzania wasiijadili
 kampuni ya Richmond
 baada ya mvua kuanza kunyeshaKama Bwana Lowassa wakati wote
 huo alijua kama
 ni kampuni ya kitapeli kama anavyojaribu alivyojaribu
 kujitetea, uamuzi wake wa
 kuwaasa watanzania wasiijadili ulikuwa ni wa kulinda ufisadi
 ambao aliufahamu.
 Inashangaza pia ni Lowassa huyo huyo alisema alijua kuwa
 Richmond ni kampuni ya
 kitapeli; ni Lowassa huyo huyo alisema kwamba alishauriwa
 vibaya na watumishi
 wa umma aliowataja kuhusu uwezo wa Richmond; Ni Lowassa huyo
 huyo aliyesema
 kwamba alijua kuwa TANESCO chini ya Menejimenti ya Net Group
 Solution walitaka
 kuhujumu mchakato wa tenda na hivyo
 'kuwanyang'anya'.
  Lakini ni Lowassa huyo
 huyo aliyekuwa Waziri Mkuu ambaye angeweza kuviagiza vyombo
 vya dola kumwezesha
 kuthibitisha 'utapeli wa Richmond'; hivyo, maelezo ya
 sasa yanayotolewa kuhusu
 ushiriki wake yanaonyesha kuwa sasa kuna mwelekeo wa
 kumlinda.

  

 Tunaendelea kushangazwa na Serikali na Bwana Lowassa
 kutumia
 utetezi wake kueleza tu nia yake ya kutaka mkataba wa
 Richmond usitishwe; nia
 ambayo kama ni kweli alikuwa na uwezo wa kuitekeleza na
 hakuitekeleza.

 Tunaitaka Serikali na Bwana Lowassa kuweka bayana ni kwa
 vipi Richmond ilipewa
 tenda hiyo na kwa shinikizo la nani. Bwana Lowassa anakwepa
 kuyazungumzia haya
 kwa kuwa anajua kabisa kwamba ni yeye aliyetumia madaraka
 yake vibaya alipokuwa
 Waziri Mkuu kwa kukiuka Sheria na Taratibu za Ununuzi kwa
 'kupora' mchakato
 uliokuwa ukiendeshwa na TANESCO, 'kuunda kamati yake' na
 kuzisukuma mamlaka za
 ununuzi hali iliyopelekea Richmond kupewa tenda ili hali
 haikuwa na uwezo
 uliotakiwa.
  Ni uzembe
 huu ambao umelisababishia hasara taifa kwa kulipa
 shilingi milioni 152 kila siku kwa kampuni ya Dowans
 iliyohamishiwa mkataba wa
 kitapeli wa Richmond; na takribani bilioni 172 kwa ujumla
 ambazo taifa
 linawajibika kuzilipa kutokana na kukodisha mitambo hiyo.
 Hvyo tunarudia tena
 rai yetu ya kutaka fedha zilizozilipwa kizembe mpaka sasa
 kurejesghwa
 serikalini.
  Kwa
 vyovyote vile, jitihada za Bwana Lowassa za kuhamasisha
 ujenzi
 wa Sekondari Kata, na utumishi wake kama Waziri Mkuu katika
 kipindi cha miaka
 miwili, haviwezi kuzidi hasara aliyosababisha katika uchumi
 wetu kipindi chote
 tulichokosa umeme wa dharura na wala hailingani na hasara
 ambayo tunaendelea
 kuilipa kila siku iendayo kwa Mungu. Maamuzi haya ya Bwana
 Lowassa yanaendelea
 kuwaumiza wananchi wote ikiwemo wa Jimbo lake la Monduli
 ambao wanataabika kwa
 mzigo wa gharama za umeme.

  

 Tunarudia tena kumkumbusha Rais Kikwete kwamba Sheria
 ya
 Maadili ya Viongozi wa Umma inamtaka Rais kuhakikisha kwamba
 taratibu
 zinatengenezwa zitakazojenga maadili na kuongeza imani ya
 wananchi kwa uadilifu
 wa viongozi wa umma na katika taratibu za utoaji maamuzi
 ndani ya Serikali na
 katika sekta ya umma.

 Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma vile vile imeweka
 kanuni zinazotakiwa kuongoza utendaji wa viongozi wa umma:
 kwamba wanapokuwa
 madarakani, viongozi wa umma watakuwa waadilifu, wenye
 huruma, utulivu, umakini
 na watakaoendeleza viwango vya juu vya maadili ili kujenga
 na kuendeleza imani
 ya umma kwa uadilifu wa Serikali.
  Kuhusiana na utoaji wa maamuzi,
 viongozi wa
 umma watatekeleza wajibu wao kufuatana na sheria na kwa
 maslahi ya umma. Hivyo,
 taarifa ya Waziri Mkuu Pinda kutokueleza bayana hatua ambazo
 Bwana Lowassa
 ameshachukuliwa au atachukuliwa ni ishara kuwa kauli ya Rais
 Kikwete aliyoitoa
 wakati akizungumza na Wazee wa CCM mkoani Dar es Salaam
 kwamba Bwana Lowassa
 amepata tu 'ajali ya kisiasa', na kumsifu kwa utumishi
 wake imechangia kumlinda
 mhusika huyu mkubwa katika sakata zima la
 RICHMOND.
  Vijana wa
 CHADEMA
 tulitarajia kuwa, baada ya Bwana Lowassa kukiri mwenyewe
 hadharani kuhusu
 uzembe wake na matumizi mabaya ya madaraka Rais Kikwete
 angelekeza hatua za
 kuchukuliwa dhidi yake badala ya kuendelea kumpamba kama
 "shujaa wa uwajibikaji',
 kinyume na hayo tutaamini kwamba serikali yake inaendeshwa
 kwa 'ubia wa
 kulindana'.
  Aidha
 tunarudia kutoa rai kwamba Rais Kikwete kuwafukuza kazi
 watumishi wote wa umma waandamizi ambao wametajwa na Bwana
 Lowassa kushiriki
 uzembe na matumizi mabaya ya madaraka; watumishi ambao
 walitajwa pia na Kamati
 Teule ya Bunge lakini mpaka sasa wanaendelea kutumikia
 nafasi zao mbalimbali.

 Kwa kuwa Waziri Mkuu Pinda ameshatangaza kwamba kwa wale
 wateule wa Rais,
 Kamati yake imeshapeleka suala zima kwake, tunategemea Rais
 atachukua hatua za
 haraka ili kuonyesha mfano kwa viongozi wengine wa chini
 yake wanaotarajiwa
 kuchukua hatua kwa watumishi wa chini.


 Kadhalika tunapenda kuvikumbusha tena vyombo vya dola
 kwamba
 Sheria ya Udhibiti wa Makosa ya Kuhujumu Uchumi ya mwaka
 1984 inatamka makosa
 yafuatayo kuwa baadhi ya makosa ya kuhujumu uchumi ni pamoja
 na yale yote yenye
 kusababisha hasara kwa mamlaka ya Serikali. Pia Sheria ya
 Kuzuia na Kupambana
 na Rushwa Na. 11 ya mwaka 2007 inatamka kuwa ubadhirifu
 na/au ufujaji wa mali
 ya umma unaofanywa na watumishi wa umma na Matumizi mabaya
 ya madaraka kwa
 ajili ya manufaa binafsi, ni sehemu ya
 ufisadi.
  Bwana
 Lowassa alithibitisha
 kwamba maneno yake kwamba wapo viongozi waandamizi wa
 Serikali ambao amewataja
 kwa majina wamefanya maamuzi ya kifisadi, kitendo chake cha
 kunyamazia ufisadi
 huo- kinafanya iwe vigumu kwa yeye kutenganishwa na tuhuma
 za ufisadi zilizomo
 katika mchakato mzima wa kupewa tenda kwa kampuni ya
 Richmond na mambo yote
 yaliyotokea baada ya Mkataba huo kuhamishiwa kwa kampuni ya
 Dowans.


 Aidha tumefadhaishwa na Taarifa ya Waziri Mkuu Pindi
 kwamba
 kujiuzulu kwa Waziri Mkuu na Baadhi ya Mawaziri ilikuwa ni
 ishara ya hatua
 ambazo serikali imechukua kutekeleza maazimio ya Bunge
 kuhusu suala husika.
 Tunarudia kukumbusha kwamba toka sakata la Richmond
 lilipoanza zaidi ya mwaka
 mmoja uliopita tulimtaka Bwana Lowassa kujiuzulu kulinda
 heshima yake lakini
 alikaidi na kuitetea kampuni ya Richmond.
  Uamuzi wa yeye kujiuzulu baada ya
 kashfa yote kuwa hadharani, umesaidia tu kuilinda serikali
 ya CCM lakini katu
 hauwezi kumpatia heshima ya uwajibikaji na wala hakuwezi
 kuwa ishara ya kwamba
 Maazimio ya Bunge yameshatekelezwa.


 Kwa niaba ya Baraza la Vijana wa CHADEMA (BAVICHA), kwa
 taarifa hii tunarudia kukemea jitihada zozote za kumlinda na
 kumtangaza Lowassa
 kuwa shujaa katika taifa letu kwani hali hii ikiachwa
 kuendelea inatoa mfano
 mbaya kwa vijana wa Tanzania. Tusingependa kwa namna yoyote
 katika taifa letu,
 mtuhumiwa wa ufisadi aliyetajwa pia katika orodha ya
 mafisadi(list of shame)
 kulindwa na kuenziwa kama shujaa wa Taifa letu kwani ni
 kuharibu maana nzima ya
 ushujaa katika uwajibikaji.


 "Inasikitisha kwamba vijana wezi wadogo wadogo
 wakijazana
 magerezani. Vijana wamachinga kuendelea kukosa mitaji na
 maeneo ya kufanyia
 biashara; wanafunzi wa elimu ya juu wakipandishiwa ada na
 wengine kukosa
 mikopo- huku fedha za walipa kodi zikiendelea kuteketea kwa
 ufisadi na
 watuhumiwa wa ufisadi wakiendelea kutamba
 hadharani.
  Hali hii
 ikiachwa,
 itaharibu utawala wa sheria na kuleta matabaka katika taifa
 letu. Vijana
 tusingependa kuona nchi yetu inatumbukia kwenye migawanyiko
 kwa sababu ya
 kuwalinda watu wachache kwa kisingizio cha haki za
 binadamu"

  

 Imetolewa tarehe 31 Agosti 2008 safirini Kenya
 na:

 John Mnyika

 Mkurugenzi wa Vijana

 0754694553





 --

 Send Emails to wanabidii@googlegroups.com

  

 Kujiondoa Tuma Email kwenda

 wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com
  Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma

  

 Disclaimer:

 Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility
 for any legal consequences of his or her postings, and hence
 statements and facts must be presented responsibly. Your
 continued membership signifies that you agree to this
 disclaimer and pledge to abide by our Rules and
 Guidelines.

 ---

 You received this message because you are subscribed to the
 Google Groups "Wanabidii" group.

 To unsubscribe from this group and stop receiving emails
 from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.

 For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.






 --

 Send Emails to wanabidii@googlegroups.com

  

 Kujiondoa Tuma Email kwenda

 wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com  Utapata Email ya
 kudhibitisha ukishatuma

  

 Disclaimer:

 Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility
 for any legal consequences of his or her postings, and hence
 statements and facts must be presented responsibly. Your
 continued membership signifies that you agree to this
 disclaimer and pledge to abide by our Rules and
 Guidelines.

 ---

 You received this message because you are subscribed to the
 Google Groups "Wanabidii" group.

 To unsubscribe from this group and stop receiving emails
 from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.

 For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.


--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com

Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com  Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma

Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

0 comments:

Post a Comment