Sunday 23 June 2013

[wanabidii] Tafadhali Usininukuu...



Ndugu zangu,

Nahofia, kuwa Watanzania tumejikita kwenye ndoto ya utajiri wa gesi na mafuta. Hivyo, kusahau kilimo chetu. Hiyo ni hatari kwa uchumi wetu.

Tunafikiria utajiri wa gesi na mafuta kana kwamba katika dunia hii ni sisi tu Watanzania ndio wenye utajiri wa akiba ya gesi na mafuta. Hatujui, kuwa katika dunia hii kuna nchi zilizo na akiba hizo za mafuta na gesi lakini bado uchumi wao hauwafanyi watu wao wawe ni wenye neema tu.

Nao wanafikiria pia kwenye vyanzo vingine vya kuinua uchumi wao ikiwamo kilimo. Na ukweli tunaoishi nao sasa ni huu, kuwa gesi na mafuta bado havijawa uti wa mgongo wa taifa letu. Kilimo kimekuwa na huenda kitabaki kuwa UTI WA MGONGO WA TAIFA LETU. Na ndio UHAI WETU.
Maggid Mjengwa,
Iringa.
0754 678 252
http://mjengwablog.com

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.
 
 

0 comments:

Post a Comment