Friday 28 June 2013

Re: [wanabidii] TAFAKARII


Kwa watanzania, tafakari ni jambo baya na haliwezekani ndugu yangu. Vichwa vyetu vina matatizo ndani kuna kitu gani sijui. Unafikwanna jangwa la moto, mnapoteza mali. gari la zima moto lilifika lakini lilikosa pa kupita kutokana na mbanano wan nyumba. Likaona limwage maji kimpango nyumba nyingine jirani zilowe ili moto usivamie kuokoa usambaaji moto. Ulikkoanza moto kila kitu kinateketea. Hata hivyo, baada ya moto kuisha, kila mmoja anajenga na kubananisha zaidi kila nafasi-hakuna kujifunza hata kutokana na hatari iliyopita. Ukiangania hilo eneo-lilikuwa limepimwa na kulikuwa na barabara za kokoto au lamu safi, maeneo wazi ya kucheza watoto, viwanja vya shule na huduma nyingine. Aidha kulijengwa nyumba za NHC na kuuziwa wananchi. Hata GVT ilipojenga nyumba hizo za NHC iliishia mbali na bonde. wao sasa open space garages, welding etc; baa mpaka karibu na shule na viosk vya music vinavyosumbua wanafunzi kwa makelele na huyo ni mzazi afanyaye hivyo. Akibomolewa-kulipiza kisasi lakini sheria anaijua haimruhusu kufanya hivyo.

Kukipakwa rangi-bomoa-habomoi anafuta rangi. Akilipwa mafao abomoe alijenga pasiporuhusiwa-anamuuzia mtu kitu ambacho kinatakiwa kubomolewa, ameshalipwa, anatoa rushwa anapata mashahidi feki, mtu anaibiwa hela. Tingatinga likija huyu mnunuzi mpa anaishitaki GVT kuwa kaonewa. Anatakiwa amshitaki aliyemuuzia, amkamate.

Na wale wa Ubungo Mataa-Kimara Temboni-kuanzia 1994 hawajavunja na zimeongezeka. Subiri uone tingatinga linavunja nyumba na makabati na kila kitumkimo ndani halafu uone maandamano na mapigano na police upate sababu ya kukuzia chama chako kipate wateja zaidi na utakapochukua wewe nchi iwe squatter zaidi-uwaachie wajenge hata katikati ya barabara si wanaganga njaa!! lazima sasa tuende ktk utii wa sheria sector zote. Sheria ya space, indoor air quality, zima moto, ujenzi. Huwezi ukajenga maghorofa mbanano na nyumba ndogo katikati, maradhi ya mapafu, TB yatakuwa mengi. Ukiwa na uhifadhi misitu kama mipango ya Mkuhumi, kuwa na misitu mijini, uwe na maghorofa marefu sana lazima uwe na helikopya ya zima moto-tunazo? Huwezi kuwa na karakana ya mbao, vyuma katibu na nyumba unatumia rangi za kutoa fumes, mbao za kutoa vumbi laini la mbao na nondo zitoazo vumbi la chuma watoto wanavuta pumbi ya unga huo ndani hakuna kiyoyozi.

Kemikali toka kiwandani haziendi katika mfumo takiwa bali kuingia mitoni, watu wanakatiza mtoni, kuchota maji-kifafa, cancer, magonjwa ya ngozi, kunywa sumu na kufa vifo visivyotambuliwa sababu zake. Watu wanauza chakula wazi barabarani kunakojengwa barabara na kuna mavumbi yanayotimuliwa na magari yapitayo. Unamkuta mtu anakula na mainzi kibao licha ya vumbi na moshi wa lead utokao ktk magari ambapo lead inaathiri ubongo na kuleta sumu ktk damu na mtu kuathirika vibaya.

Watu wameondoa fence za waste stabilization ponds wamejenga nyumba wapo usiku na mchana kwenye mbu culex kisha dawa zimetolewa tar 22 hakuna watu kunywa.tunawaona mitaana na vyandarua wakiokotea tupa sio waokotee kifaa vya viroba no-chandarua. Kulipiza kisasi ndio kunawafanya viongozi wa mitaa, vijiji kuogopa kuchukua sheria ktk makazi yao hata kama sio corrupt. Na sasa -Kisasi kwa kumwagia tindikali. kama tunashindwa Mtaani kuonyanya, kukubari kurekebishana, kumuonya mwana familia aliyeweka garage pasipofaa, kuvamia open space hadi anatoka ktk TV kulalamikiwa-familia, koo imekaa kimya-nchi itajaza jela wangapi; nchi itakuwa nna polisi wangapi kila mtaa na kila nyumba, kila plot? Nani atalipia gharama hii hata kama ulinzi shirikishi, PPP inashindikana kutokana na tabia, desturi, mawazo na mwenendo wa Uswahili?

Ukishitakiwa mahakamani-baadhi ya magazeti aminika kuwa vioo vya jamii eti yanatangaza-Dawa ya kushinda kesi Mahakamani! Dawa ya biashara mafanikio siku tatu-huku umeiweka biashara pasipo takiwa!

Subiri Obama aondoke-watarudi barabarani kuliko ilivyokuwa zamani. Wenye majimbo yao Kelele Bungeni tu sio kutumia raslimali wapewazo kutafuta eneo kwa kuwashirikisha hao wapiga kura wao na halmashauri kujenga banda kubwa kila mtu ahamie huko na meza yake hao wawatewteao wajikimu. Ni kusifia utetezi waachiwe walipo wagange njaa. Wawaelimishe kuwa-ukitoka barabarani kuondoka hapa e.g. tandale, mabibo soko la ndizi na manzese-uzuri na mitumba-nami nitahusika kukukamata!! Mteja atakuja tu ulipo, atanunua wapi asipokuja huko? Kodi pia itakusanyika ili impunguze bei kupanda kwa vitu vingine muhimu.

Mungu atuondolee Mtindio Akili huu.
 


From: Sylvanus Kessy <frkessy@yahoo.com>
To: "wanabidii@googlegroups.com" <wanabidii@googlegroups.com>
Sent: Friday, 28 June 2013, 22:28
Subject: Re: [wanabidii] TAFAKARII

Bwana Alexanda
asante sana kwa tahadhari hii. Ni kweli watanzania tumeathirika kuunga mkono au kupinga mambo ya maendeleo. Tuna hitaji miji na majiji yenye mpango na yaliyo safi. Ukitembelewa kwa wenzetu usafi unawezekana kirahisi kwa sababu ya mpango mji ulivyo.

Moto umekuwa ni janga la Taifa kwa Tanzania. Kwa umakini huduma ya zima moto haifikii jamii muda muafaka sababu ya miundombingu yetu mibovu. Kila mtu anajenga na kufanya biashara apendavyo.

Tukubali ni lazima miji na majiji yetu yawe na mpango. Ukiambiwa umejenga eneo la barabara, au karibu na nguzo ya umeme au karibu na kiwanda kinachomwaga sumu, au kwenye mkondo wa maji; tii amri ya kuondoka eneo hilo.





From: Hildegarda Kiwasila <khildegarda@yahoo.co.uk>
To: "wanabidii@googlegroups.com" <wanabidii@googlegroups.com>
Sent: Wednesday, June 26, 2013 4:06 PM
Subject: Re: [wanabidii] TAFAKARII

NINAUNGA MKONO HOJA


From: alexander chipalazya <chipalazya@yahoo.com>
To: "wanabidii@googlegroups.com" <wanabidii@googlegroups.com>
Sent: Wednesday, 26 June 2013, 15:42
Subject: Re: [wanabidii] TAFAKARII

Jamani tunapaswa kuzingatia sheria, kila kipande cha ardhi ya mji kinatakiwa kitumike kama ilivyokusudiwa, hatupaswi kukubaliana na hii habari ya kila eneo la mji kuwa sehemu ya biashara. Watu wanapanga samaki, mboga-mboga sakafuni kando ya barabara na hata kwenye reserve road. Magari yetu mengi tuyatumiayo yako chini ya kiwango maana ni second car, yanatoa moshi kibao na kuathiri hata hizi bidhaa  tunazozitumia hasa vyakula? Muda mwingine tusikubali na kusuport  kila kitu kwa kisingizio cha ugumu wa miasha.



From: Hildegarda Kiwasila <khildegarda@yahoo.co.uk>
To: "wanabidii@googlegroups.com" <wanabidii@googlegroups.com>
Sent: Wednesday, June 26, 2013 2:03 PM
Subject: Re: [wanabidii] TAFAKARII


Nidhamu ya usafi wa miji na land use plans zake lazima uwepo na sheria izingatiwe.

Sijawahi kwenda mjini posta na maeneo ya kariakoo kwa muda mrefu. Nilipita Jumamosi last week kuelekea Buguruni. Niliona kimawazo hapa DSM kuwa- City Council na municipals zake na Mzee mkali Regional Commissioner mji umewashindwa. Hao City, Municipal Health Officers and Environmental Engineers, NEMC kulikoni nikajiuliza.

Vi nchi vidogo vinapigana vita vinakuja nyuma yetu vinatushinda. Hiyo Public, Private Partnership (PPP) katika waste collection and city cleansing activities- ni kipofu na gonjwa. Stormwater drainage system-imejaa mataka ya kila aina. watu wamepanga biashara barabarani, pembeni ya barabara pa kupita hakuna. Ninawahurumia wenye maduka kama wanafanya biashara kweli maana bidhaa zimepangwa mbele ya maduka yao hata pa kupita tabu. Hata kama kuna kuganga njaa-tugange kwa kuzingatia sheria na usafi.
Hebu fikiria gari likikosea njia au kuharibika kitu lije liingie pembeni litaua wangapi? Ni makorokoro, viosk, vibanda mitaa yote ya Manzese, kariakoo, karume, msimbazi na biashara mpaka buguruni pande 2 za barabara. Hatuna ethics za kufuata sheria si za miji tu hata vijiji, hata ya conservation.

Ni kubananisha majengo, vibanda na kuchanganya biashara. Moto ukizunga hauchagui. Pamoja na magari kutoa moshi wenye lead, upepo kutimua vumbi kupeperuka pande zote-watu wanauza chakula kikiwa wazi na mainzi yanaonekana kutua. Utaona pale matikiti kila mtu amekata vipande hayafunikwi. ukifika ubungo Mandera road landmark area-vyakula wazi, vumbi, inzi; maandazi wazi, mifereji uchafu wa kuzalisha maishi na mbu wa matende umejaa despite big size ya stormwater drainage system ya ubungo. Mitaro hiyo ipo clogged na uchafu maji yametuama.

Sehemu nyingine ukipita ni harufu ya kinyesi tu na malundo ya taka. Pia, wapo wanaochakula taka hizo bila protective gear na hapo pia kuna electronic na dispensary waste. Bado hao wafanyakazi wa makampuni wanaonyonywa na local companies kufanyishwa kazi za ufagizi na uzoaji takangumu bila ya protective gear anakula vumbi lenye usafi wa kila aina na lenye wadudu wa kila aina.

Huko manzese wanakojenga barabara-wametandaza barabarani wakati greda linafanyakazi. kampuni inakwama kujenga kwa vile watu wametandaza biashara barabarani. Jee, greda au lori likipinduka na kuua idadi kadhaa ya watu hapo barabarani atalaumiwa nani. Muda wa kampuni unakwisha kutokana na biashara barabarani na msongamano wa magari na meza za biashara. IFIKE MAHALI KIFANYIKE KITU CHA KUJENGA NIDHAMU ZA AINA ZOTE PAMOJA NA UTII WA SHERIA ZA BIASHARA, AFYA NA MAZINGIRA ILI MIJI NA TOWNSHIPS ZETU NA VIJIJI VIWE MAHALA PA KUISHI NA PA KUTAZAMIKA. Tusitete uchafu kwa visingizio vya kuganga njaa. Ganga kwa nidhamu itakiwayo ya sekta husika. Hata nyumbani-usitembee bila nguo eti kwa vile upo nyumbani kwako. Maadili hayakuruhusu, wakati wowote anaweza akatokea mtoto, mpita njia, mgeni. Ni hivyo ktk biashara na environmental, business, health ethics and laws.

TZ inakaribia kuwa kama miji mingine michafu ya Bombay/India. NGO za jamii zishirikiane na Serikali kufufua makambi ya vilema na wazee na kujenga eneo kubwa fenced. Wawape vifaa na kuwafundisha ujasiriamali, walime mazao ya bustani, waweke dukani kwao hapo mapambo hayo mikeka, majamvi, vipepeo, viti, viatu, mchicha, kabichi, machungwa, asali etc na kuwapa tender ya kupeleka mboga na matunda, asali mashuleni, hospitali kwa kutumia gari yao watakayo wanunulia ktk hicho kituo. wafufue shule za ufundi za vilema ili ziwe kama zamani kupunguza ombaomba ambao baadhi wana viungo kamilifu kabisa wanatesa watoto kuzurura juani kutwa. Kuiua social welfare dept tatizo maana ombaomba analala barabarani na watoto na tunapita tunaangalia tu.

Bado kuna kazi kubwa ya kufanya kuleta maendeleo na nidhabu ya utii wa sheria, usimamiaji majukumu sawasawa katika sekta mbali mbali hata environment..
Nani anahaki ya kuuza biashara katikati ya barabara? Ifike kwamba, maeneo ya biashara ndogondogo yakijengwa halafu waondoke warudi barabarani-Pinda strategy itumike kuleta nidhamu-waondoe kwa nguvu. Maeneo ya kupita kwa mguu wakipanga biashara-ondoa; ikipita gari, pikipiki, bajaji eneo la kupita kwa mguu-kamata toza faini kubwa ili kujenga nidhamu. Tatizo ya kutekeleza sheria bongoland ni-Rushwa!! Lakini-inawezekana.
 
From: Jonas Kiwia <jonaskiwia39@gmail.com>
To: wanabidii@googlegroups.com; mabadilikotanzania@googlegroups.com
Sent: Wednesday, 26 June 2013, 12:51
Subject: [wanabidii] TAFAKARII

Hii ni haki jamani,nimepita hapa magomeni muda sio mrefu na kukuta wamachinga wenye vibanda vyao wakikamatwa na askari mgambo. Na vibanda vyao kuvunjwa vunjwaa.
Kulikua hamna namna mbadala ya kulishughulikia hili mpaka na maaskari wakiwa na mabomu  pia?
Mboona nguvu nyingi kwa vitu vidogo?
Nawaza
--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.
 
 


--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.
 
 


--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.
 
 


--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.
 
 


--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.
 
 


0 comments:

Post a Comment