Wednesday 19 June 2013

[wanabidii] Re: [Wanazuoni] MILIPUKO TULIITEGA WENYEWE

Kuichoka serikali ndio ushambulie kwa mabomu na hujuma nyingine ?

Hata huko misri hatujasikia mabomu wala wakivunja miundombinu yao 


2013/6/19 Baruani Mshale <baruani.mshale@gmail.com>
 

swala hili ni pana zaidi. Si la Tanzania peke yake. Duniani kote wananchi wamechoshwa na serikali zisizoheshimu haki za raia na binadamu kwa ujumla. Angalia kinachoendelea Brazil. La msingi ni walioko serikali watumie kwa busara nguvu walizopewa na wananchi kuendesha taifa si kutafuta nani wa kumlaumu. Sote tunaona yanayotokea nchi zingine na kwetu yanaingia taratibu. serikali yetu imejipangaje? 


2013/6/19 Yona Maro <oldmoshi@gmail.com>
 

Nakumbuka mwaka 2010 baada ya uchaguzi mguu kupita mtu katika mijadala ya ndani kulikuwa na hisia kwamba ule uadui uliojengwa mwaka ule ungeendelea zaidi ya pale kwahiyo wadau tujiandae kwa miaka 3 ijayo baada ya uchaguzi .

Kilichofuatia ilikuwa ni kujaribu kujenga hali ya amani kwenye mitandao ya kijamii kwanza maana hii mitandao ndio sura ya wanajamii wa kitanzania wote bila kujali ubaguzi wowote .

Baadhi ya watu hawakuelewa haswa vijana wenzangu pale tulipojaribu kuwaonya na kuwaambia kuhusu mwenendo wao wa kuchangia hoja mbalimbali , kuleta habari mbali mbali kwenye mitandao hii kwa maslahi ya vyama vyao vya siasa .

Makundi ya NGO nayo hayakuwa nyuma nayo yalitumia kila hila na nafasi kujipenyeza kwenye mitandao ya kijamii kuweka watu wao na kuhubiri chuki na utengano huku wakiendelea kufagilia watu wao na mkundi yao .
Viongozi wa dini nao waliendeleza yale ya mwaka 2010 kuendelea kupromoti wale waliowaunga mkono katika uchaguzi huo na kuendelea kushambulia upande wa pili kwa lugha wanazojua wao wenyewe .

Mwaka huu nilikutana na rafiki yangu mmoja baada ya kusoma habari ya mauaji wa kiongozi wa dini hapa Zanzibar , huyu rafiki akataka kujua maoni yangu kuhusu suala lile .

Nikamweleza hayo niliyoandika hapo juu na kuongeza kwamba sasa inayofuatia ni mauaji na hujuma za kisiasa , siku si nyingi tutaanza kusikia watu wakiuwawa , wakiteswa , wakilipuliwa na hata kupata usumbufu mwingine wa aina mbalimbali .

Kile ambacho  baadhi yetu wamekuwa wakihubiri kwa siri au kwa uwazi kwa kipindi cha miaka 3 iliyopita sasa kimeanza kuzaa matunda ndio hii milipuko ambayo tuliitega wenyewe .

Sasa tusianze kulaumiana kwa kushikana mashati na kutafuta mchawi , hii nchi ni yetu sote ,wote tunawajibika kuhakikisha nchi yetu inarudi kwenye hali ya amani na utulivu ili kila mtu aweze kuwa huru na ashiriki maendeleo ya nchi yake .

Tusiwafuate sana viongozi wa siasa maana wao watoto wao wanasoma ulaya , wengine wana uraia wa nchi mbili , wengine wanalindwa na sheria mbalimbali kama viongozi .


--
www.wejobs.blogspot.com Jobs in Africa
 www.naombakazi.blogspot.com International Job Opportunities




--
Baruani Mshale
Doctoral Program
SNRE
University of Michigan

__._,_.___
Reply via web post Reply to sender Reply to group Start a New Topic Messages in this topic (2)
Recent Activity:
.

__,_._,___



--
www.wejobs.blogspot.com Jobs in Africa
 www.naombakazi.blogspot.com International Job Opportunities

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.
 
 

0 comments:

Post a Comment