Sunday 30 August 2015

RE: [wanabidii] Kuelekea uchaguzi Mkuu 2015: UKAWA yadhibitisha-Lowasa anaumwa.

Ninaomba kutoa rai kwa wanabidii.  Kwanza tukubali kuwa hii nchi siyo ya CCM wala UKAWA, peike yake hivyo ni ya watanzania wote.  Tumeona ilani za uchaguzi za kambi mbili muhimu yaani CCM na UKAWA.

Kinachotakiwa ni sisi Watanzania tuje na vipaumbele vitano ambavyo kwa yeyote ambaye atachukua hii nchi lazima avitekeleze ama sivyo atakuwa ameshindwa kazi hivyo ashughulikiwe ipasavyo.

Mimi nitaanza na naomba tuchangie mawazo yetu:

Vipengele 5 Muhimu:

1. Mabadiliko ya mfumo tuliorithi kutoka kwa wakoloni na kuwa na mfumo wa kiuchumi, kijamii, kihaki, kisheria na kimaendeleo unaolinda na kugawa rasimali zetu (equitably) kwa kila Mtanzania.

2. Katiba Mpya ambayo itaonesha kwa uwazi kipengele kilichopo hapo juu (Katiba ya Warioba)

3.  Siasa ya kujitegemea kikweli kweli kwa kutumia rasimali zetu bila kutegemea misaada ya nje ambayo inaelezea sisi tuna mlengo gani wa kiuchumi, ama wa kiubepari, kiujamaa, mchanganyiko  na kukata mnyororo wa ukoloni mamboleo ambao kwa miaka 54 umeendelea kutuathiri kama taifa.

4.   Mkakati wa kutenganisha biashara na siasa kuhakikisha mwanasiasa hapati nafasi ya kutumia nafasi yake kutunga au kuinfluence utungaji au untengenezaji wa sera na sheria zitakazomnufaisha mfanyabiashara binafsi au marafiki zake wa karibu.  Vile vile Mfanyabiashara hatakuwa na fursa ya kuinfluence directly or indirectly untengenezaji wa sera au sheria zitakozumnufaisha yeye binafsi au watu au marafiki wake wa karibu.

5.  Mganywanyo wa madaraka kati ya Dola (Serkali) Bunge, Na Mahakama ambao unahakikisha hii mihimili mitatu inajitegemea.

Tuachane na huu ushabiki wa wewe CCM, mimi UKAWA, tulijaza au hamkujaza uwanja tujadili vitu vya msingi ambayo ndio muhimu kwa maendeleo yetu.  Tulazimishe makundi haya mawili makubwa watusikilize.  Ambaye ataweza kujenga hoja nasi tukamuelewa kwa hoja zake tumpe kura.

Ahsante

Herment A. Mrema


Date: Sun, 30 Aug 2015 03:45:56 -0700
Subject: Re: [wanabidii] Kuelekea uchaguzi Mkuu 2015: UKAWA yadhibitisha-Lowasa anaumwa.
From: dekleinson@gmail.com
To: wanabidii@googlegroups.com

Nisamehewe kwa typing errors zote ndani ya siku 2 hizi.
Maana naona naboronga ila nipo safarini barabara za CCM mawimbi mengi. sijui lini tutanywea chai kwenye barabara zetu.


--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

0 comments:

Post a Comment