Thursday 3 January 2013

[wanabidii] Re: Re : TANGAZO LA MKUTANO WA HADHARA WA TAMICO UTAKAOFANYIKA GEITA SIKU YA JUMAMOSI TAREHE 05/01/2013.

Thomas
 
Nashukuru sana nimesoma nanimeelewa anachozungumzia Meneja wa NSSF, napenda ufahamu kwamba sheria haibadilishwi kwa kauli za vikao, kuandika magazetini, vipeperushi au Mbunge au Waziri kutamka kwa mdomo akiwa mahali popote pale. Sheria ina taratibu zake zakubadilishwa, na hii ndio inanifanya nisiamini kauli hizi zilizopamba gazeti hilo lililomwoji Meneja. Anachokisema hapa Meneja wa NSSF ni kuwafanya watu watulize akili na wasifikilie kuacha kazi, binafsi nafahamu umuhimu wakutokuchukua hizo pesa. Lakini nachopinga ni kwamba naona jamaa anaongea uongo, kusema kuwa hilo fao halitofutwa nakataa.
 
Sabau ya pili napenda utambue wazi kuwa sio sheria iliyounda SSRA wala NSSF inayozungumzia fao lakujitoa, hakuna kabisa sehemu katika sheria hizo mbili iliyozungumza. Sheria ya NSSF Kifungu 21 (a) mpaka (g) imetaja aina ya mafao yanayotolewa na NSSF, FAO LAKUJITOA halipo labda kama mimi nasoma sheria nyingine. 
 
Naomba nikurudishe nyumba kidogo wakati swala hili la fao lakujitoa lilipoanza kujadiliwa mwezi Julai 2012. NSSF na PPF walitoa matangazo wakisema kuwa fao lakujitoa litaendela kama ilivyokua mwanza. Tazama kiambatanishi cha kwanza na cha pili hapo juu, labda leo wanazeza kukana sababu vilikua hazina nembo ya mashirika yao. Lakini wote tunakumbuka matamshi hayo yalitoka kwao.
 
Matamshi hayo yalikuja kudhihirika kuwa sio ya kweli pale SSRA walipotoa kauli rasmi wakisema sheria haina fao lakujitoa, kumbuka barua yenye Kumbukumbu Namba AE/164/334/Vol II/2, baadae ikafwatiwa na Taarifa hiyo kiambatanisho namba 3, ambayo ilienda kwa umma, kiambatanisho hicho kinasema "Tangazo hili halitowahusu watu waliojitoa kabla ya tarehe 07 Julai 2012. Wakati huo huo NSSF an PPF walituambia hakuna kitu kama hicho. Ndio maana hata leo inakua ngumu mimi kuamini anachosema Meneja, jamani tukumbuke ukweli utatuweka huru, tusema ukweli kuhusu hili. Sheria inataratibu zake zakubadilishwa na wala sio kwa kusema tu, rahasha! Mimi bado napata wasiwasi kuwa inawezekana mwezi tajwa fao likasitishwa.
 
Hayo ndio maoni yangu, labda tusubiri tarehe tajwa tuone wengine watasema nini? Ila lazima niwepo siku hiyo nisikie kauli gongana za watu waliosahau tulipotoka na swala hili.
 
Asante sana
Jamuhuri Hussein Rungu (Jamuhuri Huru)
From: thomas sabai <thomas_sabai@yahoo.com>
To: Jamuhuri Huru <jamuhurihuru@rocketmail.com>
Sent: Thursday, January 3, 2013 4:39 PM
Subject: Re : TANGAZO LA MKUTANO WA HADHARA WA TAMICO UTAKAOFANYIKA GEITA SIKU YA JUMAMOSI TAREHE 05/01/2013.
Jamhuri huru,
 
Asante kwa feedback ya post yangu. Kwa kuanza naomba upitie japo kauli ya Meneja wa NSSF mkoa wa Kahama kama alivyonukuliwa na Gazeti la habari leo la tarehe 02/01/2013. Niarudi baadaye na ufafanuzi zaidi wa hoja zako.
 
Asante,
Thomas Sabai
 
http://www.habarileo.co.tz/index.php/makala/7823-nssf-yaicheka-bulyanhulu-kutaka-kuacha-kazi-kwa-fao-la-kujitoa--- En date de : Jeu 3.1.13, Jamuhuri Huru <jamuhurihuru@rocketmail.com> a écrit :

De: Jamuhuri Huru <jamuhurihuru@rocketmail.com>
Objet: TANGAZO LA MKUTANO WA HADHARA WA TAMICO UTAKAOFANYIKA GEITA SIKU YA JUMAMOSI TAREHE 05/01/2013.
À: "thomas sabai" <thomas_sabai@yahoo.com>
Date: Jeudi 3 janvier 2013, 5h24

Habari Thomas
 
Nashukuru sana kwa taarifa hizi njema, tena nafarijika kusikia kutoka kwako jinsi ambavyo unatujari wanachama wako.
Kitu nachotamani kukushirikisha ni kwamba, binafsi nanona taarifa zinazoendelea ni za kweli tupu kwa sababu zifuatazo; kama utaniondolea huo utata basi nitakubaliana na wewe kuwa ni uzushi;-
1.    Sheria ya fao lakujitoa lilipojadiliwa Bungeni nakupitishwa hakukua na mabadiriko katika sheria yoyote ile aidha ya Mifuko ya jamii au ile ya SSRA. Sasa kwa ukweli huu hauoni kuwa ni kweli kufika mwezi tajwa hii kitu itasitishwa?
2.    Kama ambavyo inazungumzwa na uzoefu wa nchi zingine duniani kwamba mifuko ya jamii fao lakujitoa huwa linatolewa kwa wale ambao wana umri mkubwa zaidi ambapo ni tofauti na Tanzania kwa sasa. Uoni kwamba hii kitu ilijadiliwa nakupigishwa ili tu kutuliza hasira za watu kwa kipindi kile kifupi, ila huko tuendapo watalitupilia mbali?
 
Ukiweza kunisaidia katika hayo machache nitashuruku sana kwani utakua umerudisha imani yangu dhidi ya hii Serikali pamoja na mifuko ya jamii.
 
Asante
Jamuhuri Huru
 
From: wanabidii@googlegroups.com [mailto:wanabidii@googlegroups.com] On Behalf Of thomas sabai
Sent: Thursday, January 03, 2013 2:42 PM
To: wanabidii@googlegroups.com
Subject: [wanabidii] TANGAZO LA MKUTANO WA HADHARA WA TAMICO UTAKAOFANYIKA GEITA SIKU YA JUMAMOSI TAREHE 05/01/2013.
 
Wadau,
Heri ya mwaka mpya na hongereni kwa majukumu ya ujenzi wa Taifa. Kwa Bahati mbaya huku migodini tumeuanza mwaka 2013 kukiwa na uzushi uliozagaa wa kusitishwa kwa fao la kujitoa ifikapo February 2013. Uzushi huu umezagaa karibu migodi yote ya dhahabu na umesababisha wimbi kubwa la wafanyakazi wa migodini kuacha kazi ili wawahi tarehe hiyo ya kizushi.
Cha kushangaza waajiri wako kimya na wanakubali wafanyakazi wao kujiuzuru kwa uzushi huo pasipo kuwaelimisha na kuwapatia taarifa sahihi wafanyakazi  ambao wamewazalishia mali kwa muda mrefu na kwa faida. Ukimya huu wa waajiri unaibua maswali na mashaka na kudhania yawezekana wakawa na mkono katika uzushi huu ili wanufaike na kupunguza wafanyakazi kwa gharama nafuu.
Binafsi kama kiongozi wa TAMICO nalaani wazushi wenye nia mbaya ya kuhujumu haki za wafanyakazi na jitihada za serikali za kuwapatia wananchi wake ajira na maisha bora, badala yake watu wachache wanatumia mwanya wa kupindisha ukweli kwa lengo la maslahi binafsi.
Kama sehemu ya kuelimisha umma, TAMICO imeandaa mkutano wa hadhara utakaofanyika Jumamosi tarehe 05/01/2013. Mkutano huu utafanyika katika viwanja vya kanisa Katoliki mjini Geita kuanzia saa 8:00 mchana na kuendelea. Mkutano huu unatarajiwa kuhudhuriwa na viongozi na wawakilishi wa TAMICO kutoka sehemu mbali mbali za kazi.
Mgeni rasmi atakuwa ni Mheshimiwa Suleiman Jaffo, mbunge wa Kisarawe na mtoa hoja binafsi ya kutaka  sheria ya marekebisho ya sheria za mifuko ya hifadhi ya jamii,2012 (hususani fao la kujitoa) ipitiwe upya. Wanachama wa mifuko ya hifadhi ya jamii na wafanyakazi wote bila kujali itikadi yoyote ile mnaalikwa kuhudhuria bila kukosa ili kupata ufafanuzi wa kina wa hatma ya fao hilo na kipi kinafanyika kwa sasa kuhusiana na sheria hiyo.
Wote mnakaribishwa kuhudhuria na/ au kutoa maoni ambayo yatanusuru wimbi hili linalowanyima wafanyakazi fursa ya kufanya kazi kwa manufaa ya familia zao na taifa kwa ujumla.
Nawasilisha,
 
Thomas Sabai
Katibu wa TAMICO- Tawi la GGM

0 comments:

Post a Comment