Wednesday 3 October 2012

Re: [wanabidii] Watanzania Mabingwa Wa Kiswahili? - Mwanzo

Ha ha ha ha...Mzee Matinyi..Paul pia ni Bingwa wa kiswahili kwani ametoa malenga yake kama ifuatavyo ".......LENI MKANONE"...ha ha ha ha...! Huoni kuwa yeye  ni Bingwa? Je hahitaji kusifiwa kwa hilo?


2012/10/3 lucas haule <kisacha2003@yahoo.com>
Pauliay
Hufahamu kuwa, uwezo wa kuchapa kitabu ni tofauti na uwezo wa lugha au taaluma. Hapo umezungumzia utunzaji katika maandishi, lakini kiswahili kwa watanzania ni nyumbani, ni mabingwa. Bingwa ni kwasababu, tunacheza na kiswahili tunavyotaka, tunakuza lugha yetu kama tunavyotaka, ndiyo maana hukusema mtunzi au watunzi wa mashahiri ya kiswahili wametoka Kenya au ghana.

--- On Tue, 10/2/12, Mobhare Matinyi <matinyi@hotmail.com> wrote:

From: Mobhare Matinyi <matinyi@hotmail.com>
Subject: RE: [wanabidii] Watanzania Mabingwa Wa Kiswahili? - Mwanzo
To: "Wanabidii googlegroups" <wanabidii@googlegroups.com>, uchunguzionline@yahoogroups.com, progressive-kenyans@googlegroups.com, giving-it-straight@googlegroups.com
Date: Tuesday, October 2, 2012, 10:53 AM


Paul,
 
Usipoteze muda wako bure tu - kwa kigezo chochote kile huwezi kuwalinganisha Watanzania na watu wa taifa ama kundi lolote lile duniani. Soma uliyoandika uone ulivyovuruga Kiswahili humo kwenye ujumbe wako pamoja na ubishi wako au sijui niite kuwaonea gere Watanzania.
 
Watanzania, ama tuwaite mabingwa au jine lolote lile, ndio miamba ya Kiswahili duniani. Kubishia jambo la wazi ni kupoteza muda bure!
 
Asante,
 
Matinyi.
 

Date: Tue, 2 Oct 2012 09:20:00 -0700
From: pauliyai@yahoo.com
Subject: Re: [wanabidii] Watanzania Mabingwa Wa Kiswahili? - Mwanzo
To: wanabidii@googlegroups.com; uchunguzionline@yahoogroups.com; progressive-kenyans@googlegroups.com; giving-it-straight@googlegroups.com


Kwa wapenzi wote wa Lugha ya Kiswahili,
Ninasikitika sana nisomapo mambo ambayo ndugu zetu Watanzania wanaendelea kuyaandika hapa kuwa wao ni mambingwa wa Kiswahili. Sasa basi ninyi ndo mabigwa basi leni mkanone! Nakumbuka katika idhaa ya taifa ya Sautu ya Kenya kulikuwa na kipindi kimoja cha lugha ya Kiswahili kilichoitwa Mabingwa wa Kiswahili, kipindi hiki kilikuwa kizuri sana katika maendelezo ya Lugha lakini kule kujitapa kwao kulileta hoja mbali mbali. Wale wote waliokuwa wakijadili katika kipindi hiki wakiwemo, Mwalimu Walter Mbotela, Kazungu Katana, Ireri Mbaabu, Abdala Mwasimba, Abdala Baruwa na wengine wengi wakaamua kubadilisha jina la kipindi hicho kwa sababu walikubaliana kuwa hakuna mtu yeyote yule ambaye anaweza kusema kuwa yeye ndiye bingwa wa lugha kwa sababu lugha ni hai na inakua kila kukicha. Watanzania hawawezi kuwa mabingwa wa lugha hii kwani hawaujui msamiati wote wa lugha ya Kiswahili.

Kule Kukitumia Kiswahili katika nyanja mbalimbali hakuwezi kuwafanya Watanzania kuwa mabingwa. Vitabu vinavyotumiwa katika kufundishia Fasihi ya Kiswahili ni vitabu vinavyoteuliwa na jopo maalumu katika Taasisi ya Elimu ya Kenya na vitabu vinatoka kote. Vitabu vilivyotumiwa miaka ya awali kama Mashimo ya Mfalme Suleimani Cha Alan Paton, Mabepari wa Venisi,cha William Shakespear tafsiri ya Marehemu Mwalimu Nyerere, Mkaguzi Mkuu wa Srikali cha Nikolai Gogol, Masaibu ya Ndugu Jero cha Wole Soyinka ni baadhi ya vitabu vilivyotumiwa katika kufundishia fasihi. Vitabu hivi havikuandkwa na Watanzania.

Watanzania hawawezi kuwa mabingwa wa Lugha kwa sababu ya kuwa vitabu vinavyotumia katika Fasihi sasa viliandikwa na wao. Things Fall Apart cha Chinua Achebe, The River Between, cha Ngugi wa Thiongo, The Concubine cha Elechi Amadi ni riwaya za Kiingreza zilizotumiwa kufundishia Fasihi katika Kiingereza katika Nchi nyingi zikiwemo nchi za Afrika Mashariki. Kuandika riwaya au Tamthilia katika Lugha fulani hakuwanyi watu wa Taifa lolote kuwa mabingwa wa Lugha hiyo. Wakenya si Mabingwa wa Kiingereza kwa sababu wameandika Vitabu vingi katika Kiingereza.

Hata hivyo vitabu vingi vinavyotumiwa kufundishia Lugha ya Kiswahili nchini Kenya vimeandikwa na Wakenya wenyewe. Hata baadhi ya vitabu vya fasihi  viliandikwa na wakenya wenyewe vikiwemo, Siku Njema cha Ken Walibora Waliaula, Kaburi bila Msalaba,Mtawa Mweusi, Visiki, Kilio Cha Haki,Kwahivyo Ndugu zetu Watanania acheni kujitapa bure. Leopold Sengor wa Senagal alikifahamu kifaransa barabara lakini hawezi kuitwa Bingwa wa Kifaransa. Natamatisha mchango wangu kwa mada hii nikisema kuwa Kiswahili ni lugha ya wote, yenye chimbuko lake katika Pwani ya Afrika Mashariki na ni lugha inayo zidi kukua. Na ninasema hapa kuwa niliweza Kufundishwa kiswahili na Mwalimu kutoka Tanzania ambaye kwakweli alitupotezea muda wetu bure. Kama hatungepata Mkenya amabaye alituzamisha katika Mashairi ya Vitabu kama Dafina ya Umalenga, Kina Cha Maisha, na vinginevyo, tungeufeli mtihani.
Paulo 

From: Magiri paul <kiganyi@gmail.com>
To: wanabidii@googlegroups.com
Sent: Tuesday, October 2, 2012 11:31 AM
Subject: [wanabidii] Watanzania Mabingwa Wa Kiswahili? - Mwanzo

Kwa mpenzi yeyote wa Kiswahili ni sharti azingatie stadi nne za lugha hiyo. Yaani kuzungumza, kusoma kuandika na kuelewa lugha ya Kiswahili.
Hata hivyo baadhi ya wakenya wamekuwa wakilamika kuwa vitabu vingi vya Watanazani vimekuwa vikitahiniwa nchini Kenya hususan katika vidato vya tatu na vinne. Ukweli ni kuwa Watanzania wamewabwaga wakenya na ipo mifano ya kutajika kuhusiana na hilo katika vitabu hususan vya fasihi. Swali ni je Wakenya wamepewa fursa ya kuandika au la? Ni nani anastahili kuwaambia waandike vitabu vya Kiswahili, na je wachapishaji vitabu wako radhi kuzichapisha kazi za Wakenya? Kuanzia miaka ya themanini hadi sasa, idadi ya vitabu vya Watanzania vilivyotahiniwa katika kunga za riwaya, tamthilia na ushairi ni kubwa kushinda vya Wakenya.

http://wotepamoja.com/archives/7833#.UGptucPAMEw.gmail --
Karibu Jukwaa la www.mwanabidii.com
Pata nafasi mpya za Kazi www.kazibongo.blogspot.com
Blogu ya Habari na Picha www.patahabari.blogspot.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
 
 



--
Karibu Jukwaa la www.mwanabidii.com
Pata nafasi mpya za Kazi www.kazibongo.blogspot.com
Blogu ya Habari na Picha www.patahabari.blogspot.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
 
 
--
Karibu Jukwaa la www.mwanabidii.com
Pata nafasi mpya za Kazi www.kazibongo.blogspot.com
Blogu ya Habari na Picha www.patahabari.blogspot.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
 
 

--
Karibu Jukwaa la www.mwanabidii.com
Pata nafasi mpya za Kazi www.kazibongo.blogspot.com
Blogu ya Habari na Picha www.patahabari.blogspot.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
 
 

--
Karibu Jukwaa la www.mwanabidii.com
Pata nafasi mpya za Kazi www.kazibongo.blogspot.com
Blogu ya Habari na Picha www.patahabari.blogspot.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
 
 

0 comments:

Post a Comment