Monday 11 July 2016

[wanabidii] Re: VIJANA NA MAGARI YA MIKOPO

On Tuesday, January 20, 2015 at 3:01:50 AM UTC-8, Juma Mzuri wrote:
> VIJANA NA MAGARI YA MIKOPO
> Vijana wengi wakiingia kwenye soko la ajira kitu cha kwanza wanachofikiria kufanya ni kununua gari. Kuna wachache wanazichanga na kununua gari lakini wengi wao wamenunua magari kwa mkopo, Vijana wengi hapa mujini wanaendesha magari ya mkopo. Utakuta mtu badala ya kuchukua mkopo ili afungue biashara ya kumuingizia kipato, wao wanakopa magari ili waonekane wapo juu kimaisha. Gari lenyewe unalolikopa badala likuingizie kipato lenyewe ndio linakukaanga, kila siku lazima uliingize sheli kununua mafuta, kila mwezi lazima mshahara wako ukatwe kulipia gari ulilokopa, gari lenyewe nalo linahitaji kufanyiwa service. Watu wanafanya kazi, wanalipwa kipato kizuri lakini mishahara yao haiwatoshi kwasababu ya magari waliokopa.
>
> Mtu unachukua mkopo wa gari wakati unaishi nyumba ya kupanga na huna hata kipande cha ardhi cha kujenga choo.. Pumbavu... Kwanini usichukue mkopo ukanunua ardhi ukaanza kujenga nyumba yako taratibu?? au kwanini usichukue mkopo ukafanya biashara ili upate njia nyingine ya kujiingizia kipato?? Shida ya vijana mlio wengi, mademu mnakopa magari kuwaringishia mashoga zenu mtaani na wanaume mnakopa magari ili muwapate kiurahisi mademu coz hapa mujini kama una gari ukitongoza demu hakatai... Wengi mnakopa magari eti kwasababu hamtaki kupanda daladala

BWANA JUMA MZURI USITUMIE MBINU ZA ZAMANI KWENYE CHANGAMOTO ZA LEO KILA JAMBO NA WAKATI WAKE WAKATI WEWE UNAKIWANJA MWENZIO ANAGARI WEWE HUNA NA YEYE HANA KIWANJA SIKU AKINUNUA KIWAJA WW UTAKUWA UNANUNUA GARI KWAHIYO MAISHA NI MPISHANO TU HUNA HAJA YA KUWA NA HASIRA NA MAISHA YA MWINGINE MIMI NILIANZA KUNUNUA GARI NIKIWA NAISHI KWA BABA NA SIKUWA NA KITU LKN LEO NINAKWANGU NA VYOTE HIVYO NINAVYO NA NIMEMNUNULIA NA YEYE GARI NA ARDHI WAKATI NILIANZA NA GARI NIKIWA KWAKE SO ACHA MAWAZO YA ZAMANI KWENYE ULIMWENGU WALEO UKITUMIA MBINU ZA ZAMANI KWENYE CHANGAMOTO ZA LEO UTAFELI

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com

Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma

Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

0 comments:

Post a Comment