Thursday 27 December 2012

Re: [wanabidii] TAARIFA KWA UMMA JUU YA MAAMUZI YA BARAZA LA MADAKTARI KUHUSU MADAKTARI WALIOGOMA

49 ni wale walioomba msamaha kupitia vyombo vya habari

2012/12/27 Yona F Maro <oldmoshi@gmail.com>
UTANGULIZI

Kutokana na mgomo wa madaktari uliotokea kati ya tarehe 23 na 29 mwezi
juni 2012.Wizara iliwasilisha malalamiko kwenye Baraza la madaktari
Tanganyika ili lifanye uchunguzi kuhusu madaktari hao .Idadi ya
madaktari wote waliogoma walikuwa 394, kati yao madaktari 376 walikuwa
ni madaktari walio katika mafunzo kwa vitendo (Interns) kutoka
hospitali za Muhimbili, K.C.M.C. Bugando, Mbeya Rufaa, St.Francis -
Ifakara, Dodoma, Temeke, Mwananyamala, Amana, Haydom na Sekou Toure.
Aidha, Madaktari waajiriwa(Registrar) 18 walishiriki katika mgomo huo
kutoka hospitali ya Rufaa ya Mbeya.

Baraza lilipitia malalamiko yote na limetoa adhabu stahiki kwa kila
daktari aliyethibitishwa kushiriki katika mgomo huo.  Adhabu hizo
zilikuwa katika makundi yafuatayo; onyo, onyo kali na kusimamishwa
udaktari kwa muda wa kati ya mwezi mmoja na miezi sita.Vile vile kuna
Madaktari ambao hawakuwa na hatia ya kushiriki katika mgomo na hivyo
walifutiwa mashtaka.

MCHANGANUO WA ADHABU

•       Waliofutiwa mashitaka madaktari 49
•       Waliopewa onyo  madaktari 223
•       Waliopewa onyo kali madaktari 66
•       Kusimamishwa kwa muda madaktari 30
•       Mashitaka yaliyoahirishwa kutokana na wahusika kuhitaji ushauri wa
kisheria madaktari 4
•       Mashitaka yasiyosikilizwa kutokana na wahusika kutofika walipoitwa
na Baraza madaktari 22

Wizara inakamilisha taratibu za kinidhamu kwa mujibu wa Kanuni za
Utumishi wa Umma kwa Madaktari wote waajiriwa ambao walipatikana na
hatia mbele ya Baraza la Madaktari.   Wizara pia imeridhia kuwapa
Madaktari waliokuwa katika mafunzo kwa vitendo fursa nyingine ya
kuendelea na mafunzo hayo katika hospitali za Umma walizokuwepo kabla
ya kuondolewa.  Hata hivyo fursa hii haitawahusu Madaktari wote
waliopewa adhabu za kusimamishwa na Baraza la Madaktari, hadi hapo
watakapomaliza kutumikia adhabu zao.

HITIMISHO
Kwa taarifa hii madaktari wote waliofutiwa mashtaka na wale waliopewa
onyo na onyo kali wanatakiwa kuwasilisha kwa Katibu Mkuu Wizara ya
Afya na Ustawi wa Jamii barua kutoka kwa msajili wa Baraza la
Madaktari ikithibitisha kurejeshewa usajili  na kuruhusiwa kuendelea
na mafunzo kwa vitendo. Vile vile madaktari waajiriwa(Registrar)
wanatakiwa pia kuripoti kwa Katibu Mkuu Wizara ya Afya ili kupewa
barua zao kulingana na Adhabu walizopewa.  Barua hizi zitatolewa
kuanzia tarehe 2 Januari, 2013.Madaktari wote walio katika mafunzo kwa
vitendo wanatakiwa kuanza kazi katika vituo vyao vya awali  ifikapo
tarehe 14 Januari, 2013.Hakuna muda utakaoongezwa kwa kipindi
kilichobakia cha mafunzo kwa vitendo. Kwa wale wote waliopewa adhabu
wataanza kutumikia adhabu hizo kuanzia tarehe ya adhabu hiyo
ilivyotolewa.

Nsachris Mwamwaja
Msemaji
WIZARA YA AFYA NA USTAWI  WA JAMII
27/12/2012

--
Jobs in Africa - www.wejobs.blogspot.com
nafasi mpya za Kazi www.kazibongo.blogspot.com
Habari na Picha www.patahabari.blogspot.com

DELL LATITUDE D 620 & D30

80 GB HardDisk ,CORE 2 DUO , 2.0 GHZ CPU ,1 GB RAM
DVD/CD - RW ,WINDOWS 7 /WINDOWS XP ,WIRELESS , BLUE TOOTH .

TSHS : 380,000 , 1 YEAR WARRANTY

CALL : 0786 806028
Free Delivery in Dar es salaam

Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com  Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma

Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.



--
Jobs in Africa - www.wejobs.blogspot.com
nafasi mpya za Kazi www.kazibongo.blogspot.com
Habari na Picha www.patahabari.blogspot.com
 
DELL LATITUDE D 620 & D30
 
80 GB HardDisk ,CORE 2 DUO , 2.0 GHZ CPU ,1 GB RAM
DVD/CD - RW ,WINDOWS 7 /WINDOWS XP ,WIRELESS , BLUE TOOTH .
 
TSHS : 380,000 , 1 YEAR WARRANTY
 
CALL : 0786 806028
Free Delivery in Dar es salaam
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
 
 

0 comments:

Post a Comment