Monday 31 December 2012

Re: [wanabidii] Mbeya kwawaka moto tena

Poleni sana wana mbeya

Sent from my iPad

On 31 Des 2012, at 10:22, Hildegarda Kiwasila <khildegarda@yahoo.co.uk> wrote:

Jee hii itatufundisha? Huenda hatutojifunza na ndio maana inajirudia rudia mahala pamoja mara nyingi. Licha ya hii dharura ya mbeya, ipo kuchomeana nyumba zaidi ya kumi vijijini. Labda huenda hii hutokea mara nyingi kama kumkomoa mtu fulani apate hasara kama inavyotokea Kilombero kwa wakulima wa miwa kuchomeana mashamba ili fulani asipate hela ya miwa maana amelima imepamba sana atakula mahela.

Tutabananisha tena majengo ya sokoni au maeneo ya biashara bila ya kujali hasara tuliyopata, mahitaji ya zimamoto na njia ya kupita-why. Tutajaza mafuta ya kila aina na mikaa na kupikia mkaa katika ujazo wa makorokoro, kuunganisha umeme kinyemela labda. Ifike wakati serikali inunue helikopta ya zima moto ili mibanano ya majengo isizuie uokoaji watu na mali. Sheria ya ujenzi kimataifa inataka inapofika ujenzi wa ghoroka kadhaa kuwe na helikopta ya zima moto na uokoaji. Kuwe na landing stage juu na kama hospitali iwe na air strip kushusha na kuchukua wagonjwa toka juu au eneo kona dulani kama moto unawaka jengoni na lift zimesimamishwa. TZ inaangalia mbanano, unawaka leo na kesho tunajenga mbanano. Ghorofa 50+ zinajengwa hatuma hizo zima moto za helikopta. Ni mpira gani utapanda huko juu maghorofa yafukayo nchini? Haya mabanda tu yanatuka kazi moto ukiwaka, jee ghorofa?

Walaaniwe hao waliokuwa wakipiga polisi na walinzi, kubomoa magari vioo kuwakomoa waliowazuia kuiba. Twahitaji kujenga utii wa sheria za ujenzi, jihadhari za moto na utu katika majanga. Angalia soko la Mwenge, biashara za Mwenge hadi kituo cha daladala na roshani za hoteli zinazozuka ktk mbanano huo. Tazama soko la Tandale, Tegeta na mbanano na makazi ya watu. Angalia mbanano Sinza barabara yote na mtaa wa kutokea kwa Kakobe kwenda sinza-bar za kuchoma nyama, viwanda vya useremala, maduka ya nguo, saluni, bar, petrol station, maghorofa, makazi. Ni hivi DSM na miji mingine. Jee, tunajifunza? Hongera kwa juhudi zilizopita-Mioto hii itufundishe wengineo tulipo.
Twawapa pole waadhirika. Mikopo watalipaje na biashara zimeungua? Mungu awape ujasiri moyoni na utulivu wa akili. Mwaka unaanza vibaya Mbeya.

--- On Mon, 31/12/12, richard bahati <ribahati@gmail.com> wrote:

From: richard bahati <ribahati@gmail.com>
Subject: [wanabidii] Mbeya kwawaka moto tena
To: wanabidii@googlegroups.com
Date: Monday, 31 December, 2012, 6:45

Imekuwa ni mazoea sasa kusikia kwamba moto umezuka katika masoko ya wafanya buashara huko Mbeya.
Haikuwa jambo la kushangaza jana umati mkubwa wa watu waliokuwa wanashuhudia moto ukiteketeza bidhaa za mamilioni ya fedha katika soko la Mwajnlwa Jijini Mbeya.
Hii hali inayojitokeza mara kwa mara itatukwamua kwenye umaskini  kweli?
Fuatilia zaidi kisa hiki hapa:

 http://goldentz.blogspot.com/2012/12/maghala-ya-kuhifadhia-bidhaa-za-wafanya.html

--
Jobs in Africa - www.wejobs.blogspot.com
nafasi mpya za Kazi www.kazibongo.blogspot.com
Habari na Picha www.patahabari.blogspot.com
 
DELL LATITUDE D 620 & D30
 
80 GB HardDisk ,CORE 2 DUO , 2.0 GHZ CPU ,1 GB RAM
DVD/CD - RW ,WINDOWS 7 /WINDOWS XP ,WIRELESS , BLUE TOOTH .
 
TSHS : 380,000 , 1 YEAR WARRANTY
 
CALL : 0786 806028
Free Delivery in Dar es salaam
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
 
 

--
Jobs in Africa - www.wejobs.blogspot.com
nafasi mpya za Kazi www.kazibongo.blogspot.com
Habari na Picha www.patahabari.blogspot.com
 
DELL LATITUDE D 620 & D30
 
80 GB HardDisk ,CORE 2 DUO , 2.0 GHZ CPU ,1 GB RAM
DVD/CD - RW ,WINDOWS 7 /WINDOWS XP ,WIRELESS , BLUE TOOTH .
 
TSHS : 380,000 , 1 YEAR WARRANTY
 
CALL : 0786 806028
Free Delivery in Dar es salaam
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
 
 

0 comments:

Post a Comment