Wednesday 29 January 2014

Re: [wanabidii] MRITHI WA JK HUYU HAPA/ MIZANI TOLEO 31/01/2014

Utabiri kuwa Lowasa ndiye mrithi wa kiti cha uraisi ni wa kweli..Mungu hawezi kulazimika kuingilia kati na kunyosha mapito ya mgombea wa uraisi kupitia CCM ashinde kama mtu huyo ni mnafiki na asiyekuwa na tija naye...Ni ukweli kuwa Lowasa anapendwa na hata Mungu mwenyewe kwani ni muwazi,mkweli na hana majungu.Si mnafiki na haishi kwa kutegemea kudra za wanadamu bali wakati wote humtegemea Mungu...Ndani ya Lowasa Tanzania yenye neema tele inawezekana...karne ya viongozi waoga na wasiokuwa na tija ifike mwisho jamani...Ngupula


On Wednesday, 29 January 2014, 21:54, Emmanuel Muganda <emuganda@gmail.com> wrote:
Kila mtu ana haki yake ya kuota. Nisingetumia muda wote na paragraph lukuki kumnadi Lowassa.  
em

Sent from my iPhone

On Jan 29, 2014, at 1:24 PM, Steven Stey <parokostey@gmail.com> wrote:

On Jan 29, 2014 7:08 PM, "Magora Hassan" <magorah15@gmail.com> wrote:
Rgrds
Magora
---------- Forwarded message ----------
From: "musa khamis" <mizanimedia@yahoo.com>
Date: Jan 29, 2014 7:05 PM
Subject: MRITHI WA JK HUYU HAPA/ MIZANI TOLEO 31/01/2014
To: "Magora" <magorah15@gmail.com>

TUSIUMIZE VICHWA BURE
MRITHI WA RAIS KIKWETE HUYU HAPA
 
Na Mwandishi Maalum
Mwenendo wa upepo wa kisiasa ni vigumu kuwa na utabiri wa kuaminika kutokana na ukweli kuwa wakati wowote hubadilika na kugeuza mwelekeo. Hali hii inatokana na ukweli ambao hauzuiliki unaotokana na hali ya kimaumbile ya binadamu ya kuwa daima ya hamu ya kutaka mabadiliko hata bila ya kujua atafaidikaje na mabadiliko hayo.
Ni kwa silika hii baadhi ya watanzania hasa vijana wasiojua nchi ilikotoka, imefikia wapi na inataraji nini sasa na kwa mustakbali, waliweka matumaini yao kwenye vyama vya upinzani kama njia ya kufikia mapinduzi ya hali zao hasa za kiuchumi kwa dhana kuwa hali ngumu ya uchumi waliyonayo inasababishwa na chama tawala CCM.
Matumaini ya wenye nadharia ya kuhitaji mabadiliko kwa mujibu kisilika ya kibinadamu tu,  na ambao  wengi wao ni vijana wadogo, wameweka tumaini lao kwenye vyama vya upinzani hususan chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), ambacho katika chaguzi zilizopita kilifanya vizuri ukilinganisha na vyama vingine vya upinzani.
Hata hivyo matumaini hayo yamefifia katika kipindi cha zaidi ya mwaka mmoja uliopita, baada ya kuzuka malumbano makubwa na kutoaminiana baina ya viongozi wa ngazi ya juu wa chama hicho.
Katika kipindi cha mwaka mzima wa 2013 viongozi wa Chadema wamejishughulisha zaidi na mapambano ya ndani badala ya kuimarisha chama, kitendo ambacho kimekidhoofisha na kukirejesha nyuma lakini pia kuwakatisha tamaa watanzaniajuu ya uwezekano wa chama hicho kukiangusha Chama tawala katika uchaguzi wa mwaka 2015.
 Hali ya mapambano ndani ya chama hiki kikuu cha upinzani kumekinufaisha chama cha Mapinduzi ambacho watendaji wake wakuu walitumia mwanya huo kukiimarisha chama chao na kuwajengea wananchi dhana ya kupuuza upinzani huku serikali ikishadidisha kusimamia miradi ya maendeleo ambayo ni mtaji wenye nguvu kisiasa mbele ya jamii.
Kitendo cha kutuhumiwa Mbunge wa Kigoma kaskazini Zitto Kabwe na wenzake kuwa wasaliti wa chama hicho kwa kutumiwa na CCM, kitaendeleza dhana mbili endelevu zilizo muhimu na zinazohitaji tafakuri.
Kwanza ni kuwa, kuna udhaifu mkubwa ndani ya uongozi wa Chadema ngazi ya Taifa kwa kiasi kwamba CCM imeweza kupenya na kuingia ndani na kufaulu kujenga dhana ya kutoaminiana na kuusambaratisha uongozi.
Pili, Chadema watapaswa kufahamu kuwa ikiwa vyanzo vyao vya uchunguzi vimebaini kuwa CCM ilijipenyeza ndani yao kwa kiasi kinachoelezwa, ni wazi pia bado ndani ya Chadema kuna CCM wengine ambao wana jukumu la kuendeleza wimbi la kutoaminiana na hivyo hali ya mambo bado si shwari.
Kwa ujumla katika uwanja wa siasa za vyama vingi bado CCM inatawala kwa kigezo cha ukweli kuwa inamiliki serikali na vyombo vyake na hakuna shaka kuwa vyombo hivyo kwa pamoja vitaendelea kuhakikisha vinailinda Ikulu kuangukia mikononi mwa wapinzani na njia mojawapo ni kuwasambaratisha wapinzani kama walivyofanya kwa NCCR-Mageuzi.
NCCR-MAGEUZI ni chama kilichokuwa na nguvu kubwa lakini kama ambavyo kila mmoja wetu anafahamu hadi leo chama hicho  kinachechemea baada ya kutokea machafuko ya ndani kama haya tunayoyaona sasa ya Chadema ambayo kuna kila dalili inayoonyesha virusi vya ugonjwa huu kiasili vinategenezwa na CCM.
Chama cha Wananchi (CUF) kama vyama vingine vya upinzani kinaendelea kushuka chati baada ya kuwa na magomvi ya ndani ambayo tunaweza kuyaita ni maradhi ya wapinzani. Chama hiki katika sura yake halisi kinaonyesha uhai wake uko mikononi mwa mtu binafsi.
Ukiondoa visiwani Zanzibar ambako Maalim Seif Shariff Hamad ni mwanasiasa nyota anayeng'ara kwa siasa za upinzani visiwani humo, CUF hakina mvuto wa kisiasa popote Tanzania Bara na kila uchaguzi mkuu wa Rais unapofanyika Chama hicho huzidi kupoteza umaarufu wake na kudidimia.
Kwa upande wa demokrasia ndani ya vyama vyote viwili vikuu vya upinzani CUF na Chadema havina demokrasia ya kweli ndani yake ukilinganisha na CCM. Mfano mdogo ni huu kwamba haihitajiki mkutano mkuu ndani ya Chadema wala CUF kumtambua nani atakuwa mgombea wa kiti cha Urais kwa Bara au Visiwani na anayejaribu kuhoji jambo hilo hapana shaka atafukuzwa si tu uongozi bali hata uanachama wa chama chenyewe.
Sasa kama nilivyotanguliza kusema awali upepo wa kisiasa hubadilika, lakini hadi sasa kuelekea uchaguzi Mkuu wa Rais wa mwaka 2015 hakuna matumaini yanayoonyesha kuwa mrithi wa Dk Jakaya Kiwete atatokea chama cha upinzani, bali bado upepo unaashiria kuendelea utawala wa CCM.
Kuwapo kwa wanasiasa wengi wenye kujikweza kwenye dhana ya sifa za kugombea nafasi hiyo, kunakiweka chama cha Mapinduzi katika wakati mgumu kutokana na makundi yaliyomo ndani kugombea nafasi hiyo muhimu katika taifa.
Ukweli wenyewe ni kuwa Rais JK ana wakati mgumu sana katika shughuli ya kuutua mzigo wa uongozi wa Chama chake kwa sababu huenda chama hicho kikasambaratika kabisa au kikapata ushindi kiduchu utakaokipa serikali dhaifu yenye kutegemea maridhiano na upinzani endapo vita ya kugombea urithi wa kiti cha rais ndani ya CCM haitodhibitiwa.
Ndani ya CCM kuna hazina kubwa ya viongozi wenye maadili na uwezo mkubwa kiuongozi lakini wamekuwa kimya na hawaoni busara ya kujitokeza na kujitangaza kufaa kwao kwa sababu maadili mema hayamfundishi mtu mwadilifu kujitukuza na kujinaki kwa kujipa sifa mwenyewe.
Pengine wapenzi wa wanasiasa wa kambi mbali mbali hawawezi kufurahia uchambuzi huu, lakini ni ukweli usioepukika kuwa Edward Lowassa kwa sasa anatambulika kuwa ndiye mwana-CCM aliyejipanga na kufanikiwa kuwarubuni wana-CCM wengi kuamini kuwa yeye ndiye rais ajaye.
Lowassa anafahamika kama mwanasiasa hodari, mwenye haiba na shakhsiya, hutambulika pia kama mtu mwenye maamuzi na uwezo mkubwa wa kusimamia maamuzi yake. Mwandishi wa uchambuzi huu ni mmoja wa watu ambao wasingependa Lowassa ashike nafasi ya Urais, lakini chuki na utashi wake binafsi hauna nguvu ya kuzuia ukweli kusimama mahala pake.
Lowassa ameshikilia turufu kutokana na uwezo wake mkubwa kifedha ambao ameutumia bila ajizi kuugawa kwa mahitaji ya kijamii hususan kupitia taasisi za kidini na kumfanya Lowassa kukubalika zaidi Makanisani.
Lakini hata hivyo Lowassa bado hajamaliza tofauti zake na Waislamu wanaomtazama kama mdini kutokana na kusaini mkataba  (Memorandum of understanding) baina ya Serikali na Wakristo unaoipa jamii hiyo fursa ya kufaidika na fedha kutoka serikalini.
Lowassa ambaye alijiuzulu nafasi ya waziri mkuu kutokana na kashfa ya kampuni iliyodaiwa kuwa hewa ya kufua umeme ya Richmond, licha ya kugawa mamilioni ya fedha kila anapoalikwa bila ukomo, amekuwa akikanusha kuwa yeye si tajiri na kwamba nyuma yake wako watu ambao anawaita marafiki wanaochangia mamilioni hayo.
Jambo ambalo wengi wanajiuliza bila kupata jibu kuhusu suala la fedha  anazogawa Lowassa ni je, hawa marafiki zake wanaojitolea mamilioni haya wana nia gani katika utoaji wao? Marafiki hawa wema kiasi hicho ni watanzania au ni raia wa kigeni? Nini madhumuni yao katika kumjenga Lowassa kupitia njia ya kumwaga mapesa?
Wanategemea kupata nini kwa Lowassa akishaingia Ikulu? Akiwa Ikulu Lowassa anategemea kuwa na hiyari juu ya wafadhili wake hao? Wafadhali hao hawawezi kuwa na kauli yoyote juu ya mfadhiliwa? Je haiwezi kuwa watu hawa wana nia ya kumfanya Lowassa akubalike ili baadae ajikute kuwa rais wakala wa wawezeshaji wake?
Uchunguzi wa uhakika wa mwandishi wa dodoso hili unaonyesha kuwa uongozi wa CCM katika mikoa mingi unamuunga mkono Lowassa kwa kiwango kwamba kuna tetesi kuwa kuna baadhi ya viongozi kimkoa wanapata posho zao ama kwa Lowassa mwenyewe au kwa watu wanaodhaniwa kuwa wapenzi wake.
Kwa kuzingatia udhaifu wa vyama vya upinzani, na dhana kuwa mgombea wa CCM ndiye mwenye nafasi kubwa ya kuwa rais, na kwa namna Lowassa alivyojipanga ndani ya chama, na ukweli kuwa endapo jina la Lowassa litaingizwa katika mkutano mkuu hakuna wa kumshinda, basi hapana shaka Lowassa ana nafasi ya kuwa mrithi wa Rais Jakaya Kikwete.
Hii si maana yake kuwa Edward Lowassa ndiye pekee mwana-CCM anayefaa kwa nafasi hiyo. Wapo wengine wanaotajwa tajwa na ambao wana sifa bila dosari za wazi japo hawana mamilioni ya kumwaga akiwemo Benard Membe,  Dk Hussein Mwinyi, Dk Emmanuel Nchimbi na Dk Asha Rose Migiro.
Wengine ambao wanatajwa kuwa wanafaa ni pamoja na Dk Harison Mwakyembe, Anne Makinda, Dk John Magufuli, na pia kuna wengine kama Samuel Sitta na waziri mkuu mstaafu Fredirick Sumaye.
Kwa kadiri ya mjadala huu utakavyoendelea jambo kubwa la msingi linaloweza kutokea ni CCM kusambaratika baada ya jina la Lowassa kuondolewa katika kinyang'anyiro cha urais na Lowassa naye akajibu kwa kuamua kujiondoa ndani ya chama hicho.
 Endapo jambo hilo litatokea CCM itagawanyika vipande ambavyo ama vitawapa nguvu wapinzani kuchukua nchi au CCM kupata ushindi kiduchu utakaokifanya kuwa na rais atakayekuwa na wabunge wachache na hivyo kuongoza serikali dhaifu.
Naomba nihitimishe makala hii kwa kuwakumbusha wanaogombea nafasi ya urais na wapambe wao kuwa mbali na kampeni zao wenyewe wasije wakasahau kuzihusisha jitihada zao na matakwa ya Rais Kikwete kama kiongozi wa nchi, lakini pia Kikwete kama mtu mwenye shakhsiya na mvuto maalum wenye nguvu na ushawishi wake binafsi.
Lakini kubwa kuliko yote msilolijua wagombea masikini na matajiri, ni hilo la kuwa Rais wa Tanzania atakayemrithi Jakaya Kikwete ni huyo hapa, "Mgombea ambaye ataungwa mkono na Jakaya mwenyewe iwe wakati huo kikatiba anaruhusiwa kumfanyia kampeni au haruhusiwi.
Nafahamu kuwa wako watakaosema ya kuwa hata viongozi waliomtangulia JK walishindwa kuwaweka warithi waliowataka wao kwa kuwa walikinzana na upepo wa kisiasa. Lakini upepo wa kisiasa unaotoa ishara ya kubadilishana uongozi baina ya Rais Kikwete na mrithi wake uko wazi kuwa miongoni mwa watu anaowafikiria yeye basi mmoja wao ndiye atakayemrithi.  Kama wengine walishindwa kuna kila uwezekano JK hatoshindwa. Kwa hiyo usisumbuke na kuumiza kichwa chako bure atakayeungwa mkono na Kikwete mwenyewe ndiye rais ajaye.
 
 
 
 
 
 
 
 
 
--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.
--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.
--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.


0 comments:

Post a Comment