Sunday, 12 June 2016

Re: [wanabidii] Kampuni ya kigeni inapotumia mbinu chafu kuidhalilisha serikali

Hivi serikali yetu itakosa mapato gani kwa kupiga marufuku uwindaji wa kitalii? Na kwa nini tunaruhusu kampuni za kigeni kupewa vitalu vya uwindaji wa kitalii?
Miaka kadhaa nyuma kampuni ya Kijapani iliomba kukodisha eneo la mbuga za Wanyama Marekani kwa ajili ya utalii na starehe Wamarekani wakawakatalia.
Kwa nini ni sisi tu Afrika tunaoruhusu kuwa playground za foreigners?
em

2016-06-12 11:18 GMT-04:00 'Hildegarda Kiwasila' via Wanabidii <wanabidii@googlegroups.com>:
Kampuni ya kigeni ukiona inafanya hivi ujue wana kichwa juu yao. Kuna mkubwa amenunua ubia humo anakula nao na anawafanya wawe na kichwa kikubwa.

Wametumbua mengi sasa wakubwa hao wataaibika. Hakuna tena ubia na mihela na kuwapeleka nyumba ndogo shopping Dubai na UK. Tunapowaachia wapande juu ya vichwa vyetu wanaingia kutuvua hata nguo.

Sio hao wa kuwekeza katika utalii, ni mpaka contractors na kufikia kujenga chini ya kiwango haulizwi. Si ameshampa mkubwa mafao-gari la kisasa, scholarship kwa mwanae anasoma ulaya, mihela ya kujichana-utamweleza nini?
 Mnakuwa katika consultancy work na kampuni ya kizungu inawanyanyaza wazawa hivi hivi eti tunamezea kwa vile huo mradi unagharimiwa na nchi yao! Hukwe kwenye utalii tunawasaidia mpaka kuwinda kupita kiwango kilichowekwa. Karuhusiwa Kongoni 5 anaua 10 na tunambebea na anasafishisha wanyama wazima hata waliokatazwa. Game scout wa serikali wapo na maofisa wakuu wao.

Ndio hapo pia tumeona vibari vya kununua punda na kuuza nyama yake wakati anayepewa kibali hana shamba la mifugo ya punda. Kama hana ranch ya Punda unampaje kibali cha kununua na kuuza? Si mpe eneo la donkey ranch? Ndio inabidi watu waibe punda wa watu wakamuuzie!

Unatoaje kibali cha kukata mbao, milingoti ya miti, kuuza mkaa kwa mtu asiye na shamba la miti ambalo umelikagua? Leseni bila ya shamba unafanikisha uvamizi na ukataji miti kutoka protected forests. Halafu-climate change, degradation enhancing negative climate chage effects?! Miji hakuna maji-wakati unawapa leseni za kuchimba madini mpaka misitu maji na upo unapita unakusanya kodi/ushuru kila siku mpaka wa bar na majumba ya video huko migodini-Nyumbu!

Yaani mgeni na kampuni yake akunyanyase mwenyeji na serikali ya nchi alikokuja ambake sio kwao? Hata ikiwa kwao-azingatie sheria husika. Kama Obama atatunyima misaada kutokana naye-sawa!! Tuwe masikini jeuri!!

Kulikuwa na mzungu Kijiji cha Kisiwani -Mkomazi Pare eti Volunteer wa Kiholanzi akitoa na vimsaada vidogo, kajenga na nyumba pale kaadopt na mtoto. Na mwingine alikuwa kijiji cha Mnazi Gonja. Huyu wa Kisiwani akipiga makofi mpaka wanaume wababa wa watu-Dharau. Mimi kufika kumuhoji shughuli za NGO yao akaniitia polisi kusema kavamiwa na jambazi. Pilisi wakaja na M/Kiti kijiji ambaye alishangaa kuona jambazi ni mimi aliyenisindikiza pale ktk kazi zangu sasa  anaongozana na police kuona hao wavamizi ananikuta mimi-alipigwa butwaa. Tusiwaache wapumbavu kama hawa. Thanks kwa DC wa Same wakati ule Mh Peter Kangwa-vituko vya huyu mholanzi alikuja kupewa masaa 24 None Persona Grata! Oyeee! Yupo barabarani anasimamishwa anaambia anaongea na DC anadharau akamwamia yy ndio mwakilishi wa Rais barua hii masaa 24. Kajaribu kurudi kwa njia zote mara 5 ameshindwa kuingia TZ. Nyumba ya fahari aliyoijenga ipo karibu na ofisi ya Kata Kisiwani. Jambazi mimi? Niliwaambia mMimi mtanzania, nimezaliwa Tanzania, nitafia Tanzania nchi yangu!! Mara Mungu akazusha tija kwa mtu mlinzi ya nchi yake DC Peter Kangwa. Yule wa  Gonja-Mnazi naye alisepeshwa!

Kuna baadhi ya wafanyakazi katika miradi ambao ni wageni wanafanya kutembelewa na jamaa zao kila mara wanajazana na wanatumia magari ya mradi kuwatembeza mbugani weeken. Lakini hao hasa ni watalii, wanawalipa wao hela kuweka  ktk accounts zao midola au hela za kwao huku anawapokea kama jamaa zake kumbe UONGO nchi inakosa hea.

Wanaotoa ardhi kwa utalii, kilimo na shughuli nyingine bila ya kuzingatia sheria ya ardhi, utalii na uwindaji, ya NIC ya uwekezaji-watumbuliwe. Tumejimaliza wenyewe miaka mingi sasa iwe mwisho!!

Inawezekana-Timua hiyo kampuni for Good!! Tumbua na huyo mshirika/mbia wake anayempa kiburi.

Kama Kawaida

--------------------------------------------
On Sun, 12/6/16, Joachim Mushi <mushijoa@gmail.com> wrote:

 Subject: [wanabidii] Kampuni ya kigeni inapotumia mbinu chafu kuidhalilisha serikali
 To: "avila kakingo" <avila.kakingo@gmail.com>, "Krantz Mwantepele" <krantzcharles@gmail.com>, "Daniel Mbega" <brotherdanny5@gmail.com>, "Bukoba Wadau" <bukobawadau@gmail.com>, "Bashir Nkoromo" <nkoromo@gmail.com>, "Binagi Online Tv" <binagimediagroup@gmail.com>, "Haki Ngowi" <Haki.yako@gmail.com>, "uwazi@hotmail.com" <uwazi@hotmail.com>, "Josephat Lukaza" <josephat.lukaza@gmail.com>, "Luke Joe" <djlukejoe@gmail.com>, "johnbukuku@gmail.com" <johnbukuku@gmail.com>, "Jestina George" <jestinageorge@gmail.com>, "Muhidin Sufiani" <sufianimafotoblog@gmail.com>, "Subi Nukta" <subi.nukta77@gmail.com>, "Sophia Mbeyu" <sophiembeyu@msn.com>, "zainul mzige" <zainul.mzige21@gmail.com>, zainul@modewjiblog.com, zai_mzige@yahoo.com, "Swahili Villa" <swahilivilla@gmail.com>, "william malecela" <willymalec@gmail.com>, "wanabidii@googlegroups.com" <wanabidii@googlegroups.com>, "Deogratius Rweyunga" <drweyunga@gmail.com>, "Robert Okanda" <rokanda01@gmail.com>, "Richard Mwaikenda" <rmwaikenda@yahoo.com>, "Adam Mzee" <thamani80@gmail.com>, "Fredy Tony Njeje" <latestnewstz@live.com>, "info@dewjiblog.com" <info@dewjiblog.com>, "Francis Dande" <dande15us@gmail.com>
 Date: Sunday, 12 June, 2016, 16:52

 Kampuni ya
 kigeni inapotumia mbinu chafu kuidhalilisha serikali

 <table align="center"
 cellpadding="0" cellspacing="0"
 class="tr-caption-container"
 style="margin-left: auto; margin-right: auto;
 text-align:
 center;"><tbody><tr><td
 style="text-align: center;"><a href="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiw4Q9ZxRO6-dwg_PKDFjt2U63nNRQ8ncBvHMgjz81s-EOWV9g0lYkA-AOqUCeN81CaMQGKqVILCy-gt81FGkrXsui_LKIL8B9DSA4w3KK9G_07XrQkPQPTuJoqXY0XvzRdDNq0DCunw4U/s1600/Gari+la+Kampuni+ya+Wengert+Windrose+Safaris+likiwa+limeshikiliwa+kituo+cha+polisi+mkoani+Arusha+baada+ya+kukutwa+na+shehena+ya+bangi..JPG"
 imageanchor="1" style="margin-left: auto;
 margin-right: auto;"><img border="0"
 height="360" src="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiw4Q9ZxRO6-dwg_PKDFjt2U63nNRQ8ncBvHMgjz81s-EOWV9g0lYkA-AOqUCeN81CaMQGKqVILCy-gt81FGkrXsui_LKIL8B9DSA4w3KK9G_07XrQkPQPTuJoqXY0XvzRdDNq0DCunw4U/s640/Gari+la+Kampuni+ya+Wengert+Windrose+Safaris+likiwa+limeshikiliwa+kituo+cha+polisi+mkoani+Arusha+baada+ya+kukutwa+na+shehena+ya+bangi..JPG"
 width="640"
 /></a></td></tr><tr><td
 class="tr-caption" style="text-align:
 center;"><span style="font-size:
 small;">Gari la Kampuni ya Wengert Windrose Safaris
 likiwa limeshikiliwa kituo cha polisi mkoani Arusha baada ya
 kukutwa na shehena ya
 bangi.</span></td></tr></tbody></table><br
 /><b>Na Mwandishi Wetu</b><br
 /><br
 /><b>BIASHARA</b> ya utalii
 imekuwa na ushindani mkubwa si nje bali hata ndani ya nchi
 yetu. Ushindani wa kibiashara unadhihirishwa na jinsi
 ambavyo makampuni ya ndani na nje yanavyopigana vikumbo
 kutafuta njia na mbinu za kuwapiku washindani wao.<br
 />Hilo ni jambo la kawaida kabisa.<br
 /><br />Hakika pale ambako
 hapana ushindani basi ni wazi pia kwamba hapatakuwapo na
 tija kwani mama wa biashara huria ni ushindani na hilo
 hakuna wa kubishana. Hata hivyo, kuna mvutano ambao
 umeanzishwa na kampuni ya Wengert Windrose Safaris Limited,
 kampuni tanzu ya Friedkin Conservation Fund (Friedkin Family
 Tanzania) dhidi ya serikali ya Tanzania ambao hauna tija kwa
 pande zote mbili na ambao unahitaji kumalizwa kwa sababu
 umeendelea kuikosesha nchi mapato.<br
 /><br />Kampuni nyingine ni
 Tanzania Game Trackers Safaris Limited na Mwiba Holdings
 Limited.<br />Kampuni hiyo imeingia katika
 mvutano na serikali kuanzia mwaka 2013 wakati msimu mpya wa
 uwindaji wa kitalii ulipoanza, hasa pale walipokosa moja ya
 vitalu walivyoomba katika utaratibu wa ushindani. Kitalu
 hicho kilijulikana kwa jina la Lake Natron Game Controlled
 Area (North). Baadaye kitalu hiki kilikuja kujulikana kama
 Lake Natron Game Controlled Area (East), ambacho kiligawiwa
 kwa Green Mile Safari Company Limited baada ya
 ushindani.<br /><br
 />Kitalu hiki cha uwindaji wa kitalii ndicho
 kimekuwa luba na kufanya mahusiano kati ya kampuni hiyo na
 serikali kuyumba sana hadi leo takriban miaka mitatu baada
 ya kampuni hiyo kukosa umiliki katika mchakato wa ushindani.
 Katika mazingira ya kawaida kampuni ya kigeni inayofanya
 biashara hapa nchini kwa kutumia sheria za Tanzania haina
 budi kukubaliana na sheria, na kama kuna kutoridhika na
 chochote inatakiwa kwenda mahakamani kutafuta haki.<br
 /><br />Hata hivyo, baada ya
 kampuni hiyo kwenda mahakamani mara kadhaa kutafuta haki ya
 kumilikishwa kitalu hicho ikashindwa kuipata imeamua
 kuendeleza vita dhidi ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa
 Tanzania kupitia vyombo vya habari. Tena vita hiyo ambayo
 inaendeshwa kwa kutumia vyombo vya habari vya ndani na nje
 ya nchi ilihamishiwa hadi katika Baraza la Congress la
 Marekani.<br /><br
 /><table align="center"
 cellpadding="0" cellspacing="0"
 class="tr-caption-container"
 style="margin-left: auto; margin-right: auto;
 text-align:
 center;"><tbody><tr><td
 style="text-align: center;"><a href="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgnnmCP6UHB2d9M7tzTpXfVBhheJXuOknpUPwGKF7Tn5M3z9uxjPEeErIT0eiyCxWKJYtT6IISeP9KCQl-cDPPikuiLyqYXzvpTXEoUMpSf4Ji1L5yq_EWwBHRzJilT7XhEOJvWA9o-ad0/s1600/IMG-20150325-WA0002.JPG"
 imageanchor="1" style="margin-left: auto;
 margin-right: auto;"><img border="0"
 height="360" src="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgnnmCP6UHB2d9M7tzTpXfVBhheJXuOknpUPwGKF7Tn5M3z9uxjPEeErIT0eiyCxWKJYtT6IISeP9KCQl-cDPPikuiLyqYXzvpTXEoUMpSf4Ji1L5yq_EWwBHRzJilT7XhEOJvWA9o-ad0/s640/IMG-20150325-WA0002.JPG"
 width="640"
 /></a></td></tr><tr><td
 class="tr-caption" style="text-align:
 center;"></td><td
 class="tr-caption"><span
 style="font-size: small;">Shehena ya bangi
 ikishushwa kwenye gari la Kampuni ya Wengert Windrose
 Safaris katika kituo cha polisi mkoani Arusha baada ya
 kukamatwa.</span></td></tr></tbody></table>Baraza
 la Congress liliaminishwa na wamiliki wa kampuni hiyo ya
 Wengert ambayo ni ya Kimarekani kwamba Tanzania ni nchi ya
 hovyo ambayo sheria hazifuatwi hata kidogo.<br
 />Kampuni ya Wengert ikafikia hatua ya
 kuliaminisha Baraza hilo kwamba imetendewa ndivyo sivyo
 nchini kwa kunyang'anywa kitalu kinyume cha sheria na
 kwamba kitendo hicho kimefanyika kinyume cha sheria.<br
 /><br />Katika
 kulighadhibisha Baraza hilo Wengert wakadai kwamba
 imenyang'anywa kitalu na kupewa kampuni nyingine ya
 kigeni. Hiyo ya kudai kwamba imenyang'anywa kampuni ya
 Kimarekani na kupatiwa kampuni nyingine ya kigeni ni katika
 ile ile tabia ya kutaka kuwachochea watunga sheria hao wa
 Marekani kwa kutumia kigezo cha kwamba wao ni bora zaidi
 hivyo haiyumkiniki akanyang'anywa Mmarekani halafu apewe
 mgeni mwingine!<br />Uchochezi huo
 ukatumika kwa malengo ambayo kampuni ya Wengert
 ilitaka.<br /><br />Baraza
 la Congress la Marekani lilimwandikia Rais wa Marekani,
 Barack Obama, barua likiituhumu Idara ya Wanyamapori kwa
 kuinyanga'anya kampuni ya Wengert kitalu na kukitoa isivyo
 halali kwa Kampuni nyingine, jambo ambalo halikuwa kweli.
 Hata hivyo, ukweli ni kwamba kampuni iliyogawiwa kitalu
 hicho ni ya Kitanzania.<br />Kampuni hiyo
 haikutaka kusema ukweli kwamba uamuzi wa kutogawiwa
  kitalu ulitokana na maamuzi ya kamati ya ugawaji
 wa vitalu na kamwe sio kutokana na uamuzi wa Idara ya
 Wanyamapori.<br /><br
 />Vitalu hugawiwa na Waziri wa Maliasili na
 Utalii baada ya kushauriwa na kamati ya ugawaji wa vitalu.
 Tuhuma hizo za uongo zilipelekwa mbele ya Baraza la Congress
 baada ya rufaa yao waliyokata kupinga ugawaji wa vitalu
 kukataliwa. Ni wazi kabisa kwamba ushawishi uliofanywa kwa
 Baraza la Congress kwa kutumia mbinu chafu na uongo
 uliokithiri ulilenga katika kuiweka katika shinikizo
 serikali ya Tanzania ili iende kinyume na maamuzi yake
 halali yaliyofanayika kwa mujibu wa sheria.<br
 /><br />Wengert walikwenda
 mahakamani mara kadhaa kupinga maamuzi hayo ya serikali na
 mara zote wamegonga ukuta. Wiki iliyopita walishindwa kwa
 mara ya nne mahakamani katika jitihada zao za kutaka
 kuthibitisha kwa kutumia vielelezo wanavyodai ndivyo halali
 kwamba kuna makosa katika ugawaji wa vitalu katika eneo la
 Lake Natron Game Controlled Area. Imefikia hatua kampuni ya
 Wengert inadai kwamba nyaraka rasmi za Serikali ya Tanzania
 ni batili na kwamba yenyewe ndiyo ina ramani halali na
 nyaraka mbalimbali kutoka serikalini.<br
 /><br />Inachekesha sana
 kwamba kampuni ya kigeni inakuja nchini na kuamua kupambana
 na serikali yetu kwa ajili ya kulazimisha umiliki wa kitalu
 cha uwindaji wa kitalii kwa kila njia ikiwa ni pamoja na
 kuvifunga midomo vyombo vya habari kwa kutumia mbinu chafu.
 Kwa taarifa rasmi za kiserikali ni kwamba kampuni hiyo,
 pamoja na kampuni nyingine za Friedkin Family Tanzania,
 zimekuwa zikiwatumia watumishi wake na mawakala mbalimbali
 kufanya vitendo vya hujuma dhidi ya makampuni mengine ya
 uwindaji wa kitalii.<br /><br
 />Aidha, kampuni hiyo pia imekuwa ikiendesha
 kampeni chafu dhidi ya viongozi mbalimbali wa Wizara ya
 Maliasili na Utalii kwa lengo la kutaka kuthibitisha kwamba
 viongozi hao wanafanya maamuzi yasiyozingatia sheria. Ukweli
 ni kwamba kampuni hizo ndiyo zimekuwa mstari wa mbele
 kutotii sheria za nchi.<br /><br
 />Tabia hii ilishamiri sana wakati wa awamu
 iliyopita. Kumekuwapo na jitihada za kuitaka kampuni hiyo
 iendelee kufanya shughuli zake za kitalii katika maeneo
 halali iliyokabidhiwa na serikali ya Tanzania lakini kila
 uchao kumekuwapo na tuhuma za kila aina dhidi ya wadau
 wengine wa sekta ya utalii na serikali kutoka kwa kampuni
 hizo.<br /><br /><table
 align="center" cellpadding="0"
 cellspacing="0"
 class="tr-caption-container"
 style="margin-left: auto; margin-right: auto;
 text-align:
 center;"><tbody><tr><td
 style="text-align: center;"><a href="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEii7NrMY2t_5XIJwphGQJ0F1vUCQRw_hMMU-qbECigVt3lfgUs1PS-4GN0vPYmUv7JgPAegmd6opG9IriUs4JZB82iagc8j5ZJLozeZPX4DLKM7iBRvjHisD4ZtFhZm6TJWSN1NTJPzDHQ/s1600/Mtuhumiwa.JPG"
 imageanchor="1" style="margin-left: auto;
 margin-right: auto;"><img border="0"
 height="640" src="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEii7NrMY2t_5XIJwphGQJ0F1vUCQRw_hMMU-qbECigVt3lfgUs1PS-4GN0vPYmUv7JgPAegmd6opG9IriUs4JZB82iagc8j5ZJLozeZPX4DLKM7iBRvjHisD4ZtFhZm6TJWSN1NTJPzDHQ/s640/Mtuhumiwa.JPG"
 width="360"
 /></a></td></tr><tr><td
 class="tr-caption" style="text-align:
 center;"><span style="font-size:
 small;">Mtuhumiwa ambaye ni dereva wa gari hiyo
 akiwa ameshikiliwa na
 polisi.</span></td></tr></tbody></table>Inasikitisha
 kwamba kampuni hizo hazioni kwamba ni bora kuachana na
 malumbano yasiyokuwa na tija na badala yake kuendelea na
 kazi kama zinapenda kuendelea kuwekeza Tanzania vinginevyo
 kama zinafikiri zinaonewa ziondoke nchini kwa sababu
 Tanzania sio nchi pekee ambayo wanaweza kufanya biashara ya
 uwindaji wa kitalii. Katika kuthibitisha kwamba kampuni hizi
 hazina hata chembe ya ustaarabu, wamediriki kuwafuata wageni
 wa kampuni shindani na kuwafanyia fujo jambo ambalo
 liliripotiwa serikalini.<br /><br
 />Aidha, katika kuthibitisha uwezo wake wa
 kufanya mambo ya hovyo upo ushahidi kwamba watumishi au
 mawakala wa kampuni hiyo walichimba mashimo katika kiwanja
 kidogo cha ndege kilichopo kwenye moja ya vitalu vya
 washindani wao eti tu kwa sababu uwanja huo waliutengeneza
 wao wakati wanamiliki kitalu hicho.<br
 /><br />Swali kubwa
 linalojitokeza katika vurugu hizi za makampuni haya ya
 Kimarekani ni kwamba nani anayewachochea na kuwavimbisha
 kichwa kiasi cha kuidhalilisha serikali ya Tanzania huku
 wakiwa nchini? Kwa nini hadi leo hatusikii hatua za
 kinidhamu na hata kisheria dhidi ya kampuni hizii ambayo
 inaonekana kila uchao yanazidisha mapambano dhidi ya
 serikali yetu? Tusiruhusu mwekezaji yeyote yule kutupanda
 kichwani, hata kama anatoka taifa linalojigamba kuwa taifa
 kubwa duniani! Tunachohitaji kwa wawekezaji ni wao wanufaike
 na sisi pia tunufaike.
 ___________________________________________________________________________________Joachim
 Mushi, Mwenyekiti wa Tanzania Bloggers Network (TBN) na
 Mhariri Mkuu wa Thehabari.com.
 Mail address:-
 mushi@thehabari.com/
 jomushi79@yahoo.com/
 info@thehabari.com
 Mobile:- 0717
 030066 / 0756 469470
 Web:- www.thehabari.com  

           http://joemushi.blogspot.com




 --

 Send Emails to wanabidii@googlegroups.com

  

 Kujiondoa Tuma Email kwenda

 wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com  Utapata Email ya
 kudhibitisha ukishatuma

  

 Disclaimer:

 Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility
 for any legal consequences of his or her postings, and hence
 statements and facts must be presented responsibly. Your
 continued membership signifies that you agree to this
 disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.

 ---

 You received this message because you are subscribed to the
 Google Groups "Wanabidii" group.

 To unsubscribe from this group and stop receiving emails
 from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.

 For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com

Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com  Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma

Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

0 comments:

Post a Comment