Hivi serikali yetu itakosa mapato gani kwa kupiga marufuku uwindaji wa kitalii? Na kwa nini tunaruhusu kampuni za kigeni kupewa vitalu vya uwindaji wa kitalii?
Miaka kadhaa nyuma kampuni ya Kijapani iliomba kukodisha eneo la mbuga za Wanyama Marekani kwa ajili ya utalii na starehe Wamarekani wakawakatalia.
Kwa nini ni sisi tu Afrika tunaoruhusu kuwa playground za foreigners?
em
2016-06-12 11:18 GMT-04:00 'Hildegarda Kiwasila' via Wanabidii <wanabidii@googlegroups.com>:
Kampuni ya kigeni ukiona inafanya hivi ujue wana kichwa juu yao. Kuna mkubwa amenunua ubia humo anakula nao na anawafanya wawe na kichwa kikubwa.
Wametumbua mengi sasa wakubwa hao wataaibika. Hakuna tena ubia na mihela na kuwapeleka nyumba ndogo shopping Dubai na UK. Tunapowaachia wapande juu ya vichwa vyetu wanaingia kutuvua hata nguo.
Sio hao wa kuwekeza katika utalii, ni mpaka contractors na kufikia kujenga chini ya kiwango haulizwi. Si ameshampa mkubwa mafao-gari la kisasa, scholarship kwa mwanae anasoma ulaya, mihela ya kujichana-utamweleza nini?
Mnakuwa katika consultancy work na kampuni ya kizungu inawanyanyaza wazawa hivi hivi eti tunamezea kwa vile huo mradi unagharimiwa na nchi yao! Hukwe kwenye utalii tunawasaidia mpaka kuwinda kupita kiwango kilichowekwa. Karuhusiwa Kongoni 5 anaua 10 na tunambebea na anasafishisha wanyama wazima hata waliokatazwa. Game scout wa serikali wapo na maofisa wakuu wao.
Ndio hapo pia tumeona vibari vya kununua punda na kuuza nyama yake wakati anayepewa kibali hana shamba la mifugo ya punda. Kama hana ranch ya Punda unampaje kibali cha kununua na kuuza? Si mpe eneo la donkey ranch? Ndio inabidi watu waibe punda wa watu wakamuuzie!
Unatoaje kibali cha kukata mbao, milingoti ya miti, kuuza mkaa kwa mtu asiye na shamba la miti ambalo umelikagua? Leseni bila ya shamba unafanikisha uvamizi na ukataji miti kutoka protected forests. Halafu-climate change, degradation enhancing negative climate chage effects?! Miji hakuna maji-wakati unawapa leseni za kuchimba madini mpaka misitu maji na upo unapita unakusanya kodi/ushuru kila siku mpaka wa bar na majumba ya video huko migodini-Nyumbu!
Yaani mgeni na kampuni yake akunyanyase mwenyeji na serikali ya nchi alikokuja ambake sio kwao? Hata ikiwa kwao-azingatie sheria husika. Kama Obama atatunyima misaada kutokana naye-sawa!! Tuwe masikini jeuri!!
Kulikuwa na mzungu Kijiji cha Kisiwani -Mkomazi Pare eti Volunteer wa Kiholanzi akitoa na vimsaada vidogo, kajenga na nyumba pale kaadopt na mtoto. Na mwingine alikuwa kijiji cha Mnazi Gonja. Huyu wa Kisiwani akipiga makofi mpaka wanaume wababa wa watu-Dharau. Mimi kufika kumuhoji shughuli za NGO yao akaniitia polisi kusema kavamiwa na jambazi. Pilisi wakaja na M/Kiti kijiji ambaye alishangaa kuona jambazi ni mimi aliyenisindikiza pale ktk kazi zangu sasa anaongozana na police kuona hao wavamizi ananikuta mimi-alipigwa butwaa. Tusiwaache wapumbavu kama hawa. Thanks kwa DC wa Same wakati ule Mh Peter Kangwa-vituko vya huyu mholanzi alikuja kupewa masaa 24 None Persona Grata! Oyeee! Yupo barabarani anasimamishwa anaambia anaongea na DC anadharau akamwamia yy ndio mwakilishi wa Rais barua hii masaa 24. Kajaribu kurudi kwa njia zote mara 5 ameshindwa kuingia TZ. Nyumba ya fahari aliyoijenga ipo karibu na ofisi ya Kata Kisiwani. Jambazi mimi? Niliwaambia mMimi mtanzania, nimezaliwa Tanzania, nitafia Tanzania nchi yangu!! Mara Mungu akazusha tija kwa mtu mlinzi ya nchi yake DC Peter Kangwa. Yule wa Gonja-Mnazi naye alisepeshwa!
Kuna baadhi ya wafanyakazi katika miradi ambao ni wageni wanafanya kutembelewa na jamaa zao kila mara wanajazana na wanatumia magari ya mradi kuwatembeza mbugani weeken. Lakini hao hasa ni watalii, wanawalipa wao hela kuweka ktk accounts zao midola au hela za kwao huku anawapokea kama jamaa zake kumbe UONGO nchi inakosa hea.
Wanaotoa ardhi kwa utalii, kilimo na shughuli nyingine bila ya kuzingatia sheria ya ardhi, utalii na uwindaji, ya NIC ya uwekezaji-watumbuliwe. Tumejimaliza wenyewe miaka mingi sasa iwe mwisho!!
Inawezekana-Timua hiyo kampuni for Good!! Tumbua na huyo mshirika/mbia wake anayempa kiburi.
Kama Kawaida
--------------------------------------------
On Sun, 12/6/16, Joachim Mushi <mushijoa@gmail.com> wrote:
Subject: [wanabidii] Kampuni ya kigeni inapotumia mbinu chafu kuidhalilisha serikali
To: "avila kakingo" <avila.kakingo@gmail.com>, "Krantz Mwantepele" <krantzcharles@gmail.com>, "Daniel Mbega" <brotherdanny5@gmail.com>, "Bukoba Wadau" <bukobawadau@gmail.com>, "Bashir Nkoromo" <nkoromo@gmail.com>, "Binagi Online Tv" <binagimediagroup@gmail.com>, "Haki Ngowi" <Haki.yako@gmail.com>, "uwazi@hotmail.com" <uwazi@hotmail.com>, "Josephat Lukaza" <josephat.lukaza@gmail.com>, "Luke Joe" <djlukejoe@gmail.com>, "johnbukuku@gmail.com" <johnbukuku@gmail.com>, "Jestina George" <jestinageorge@gmail.com>, "Muhidin Sufiani" <sufianimafotoblog@gmail.com>, "Subi Nukta" <subi.nukta77@gmail.com>, "Sophia Mbeyu" <sophiembeyu@msn.com>, "zainul mzige" <zainul.mzige21@gmail.com>, zainul@modewjiblog.com, zai_mzige@yahoo.com, "Swahili Villa" <swahilivilla@gmail.com>, "william malecela" <willymalec@gmail.com>, "wanabidii@googlegroups.com" <wanabidii@googlegroups.com>, "Deogratius Rweyunga" <drweyunga@gmail.com>, "Robert Okanda" <rokanda01@gmail.com>, "Richard Mwaikenda" <rmwaikenda@yahoo.com>, "Adam Mzee" <thamani80@gmail.com>, "Fredy Tony Njeje" <latestnewstz@live.com>, "info@dewjiblog.com" <info@dewjiblog.com>, "Francis Dande" <dande15us@gmail.com>
Date: Sunday, 12 June, 2016, 16:52
Kampuni ya
kigeni inapotumia mbinu chafu kuidhalilisha serikali
<table align="center"
cellpadding="0" cellspacing="0"
class="tr-caption-container"
style="margin-left: auto; margin-right: auto;
text-align:
center;"><tbody><tr><td
style="text-align: center;"><a href="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiw4Q9ZxRO6-dwg_PKDFjt2U63nNRQ8ncBvHMgjz81s-EOWV9g0lYkA-AOqUCeN81CaMQGKqVILCy-gt81FGkrXsui_LKIL8B9DSA4w3KK9G_07XrQkPQPTuJoqXY0XvzRdDNq0DCunw4U/s1600/Gari+la+Kampuni+ya+Wengert+Windrose+Safaris+likiwa+limeshikiliwa+kituo+cha+polisi+mkoani+Arusha+baada+ya+kukutwa+na+shehena+ya+bangi..JPG"
imageanchor="1" style="margin-left: auto;
margin-right: auto;"><img border="0"
height="360" src="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiw4Q9ZxRO6-dwg_PKDFjt2U63nNRQ8ncBvHMgjz81s-EOWV9g0lYkA-AOqUCeN81CaMQGKqVILCy-gt81FGkrXsui_LKIL8B9DSA4w3KK9G_07XrQkPQPTuJoqXY0XvzRdDNq0DCunw4U/s640/Gari+la+Kampuni+ya+Wengert+Windrose+Safaris+likiwa+limeshikiliwa+kituo+cha+polisi+mkoani+Arusha+baada+ya+kukutwa+na+shehena+ya+bangi..JPG"
width="640"
/></a></td></tr><tr><td
class="tr-caption" style="text-align:
center;"><span style="font-size:
small;">Gari la Kampuni ya Wengert Windrose Safaris
likiwa limeshikiliwa kituo cha polisi mkoani Arusha baada ya
kukutwa na shehena ya
bangi.</span></td></tr></tbody></table><br
/><b>Na Mwandishi Wetu</b><br
/><br
/><b>BIASHARA</b> ya utalii
imekuwa na ushindani mkubwa si nje bali hata ndani ya nchi
yetu. Ushindani wa kibiashara unadhihirishwa na jinsi
ambavyo makampuni ya ndani na nje yanavyopigana vikumbo
kutafuta njia na mbinu za kuwapiku washindani wao.<br
/>Hilo ni jambo la kawaida kabisa.<br
/><br />Hakika pale ambako
hapana ushindani basi ni wazi pia kwamba hapatakuwapo na
tija kwani mama wa biashara huria ni ushindani na hilo
hakuna wa kubishana. Hata hivyo, kuna mvutano ambao
umeanzishwa na kampuni ya Wengert Windrose Safaris Limited,
kampuni tanzu ya Friedkin Conservation Fund (Friedkin Family
Tanzania) dhidi ya serikali ya Tanzania ambao hauna tija kwa
pande zote mbili na ambao unahitaji kumalizwa kwa sababu
umeendelea kuikosesha nchi mapato.<br
/><br />Kampuni nyingine ni
Tanzania Game Trackers Safaris Limited na Mwiba Holdings
Limited.<br />Kampuni hiyo imeingia katika
mvutano na serikali kuanzia mwaka 2013 wakati msimu mpya wa
uwindaji wa kitalii ulipoanza, hasa pale walipokosa moja ya
vitalu walivyoomba katika utaratibu wa ushindani. Kitalu
hicho kilijulikana kwa jina la Lake Natron Game Controlled
Area (North). Baadaye kitalu hiki kilikuja kujulikana kama
Lake Natron Game Controlled Area (East), ambacho kiligawiwa
kwa Green Mile Safari Company Limited baada ya
ushindani.<br /><br
/>Kitalu hiki cha uwindaji wa kitalii ndicho
kimekuwa luba na kufanya mahusiano kati ya kampuni hiyo na
serikali kuyumba sana hadi leo takriban miaka mitatu baada
ya kampuni hiyo kukosa umiliki katika mchakato wa ushindani.
Katika mazingira ya kawaida kampuni ya kigeni inayofanya
biashara hapa nchini kwa kutumia sheria za Tanzania haina
budi kukubaliana na sheria, na kama kuna kutoridhika na
chochote inatakiwa kwenda mahakamani kutafuta haki.<br
/><br />Hata hivyo, baada ya
kampuni hiyo kwenda mahakamani mara kadhaa kutafuta haki ya
kumilikishwa kitalu hicho ikashindwa kuipata imeamua
kuendeleza vita dhidi ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania kupitia vyombo vya habari. Tena vita hiyo ambayo
inaendeshwa kwa kutumia vyombo vya habari vya ndani na nje
ya nchi ilihamishiwa hadi katika Baraza la Congress la
Marekani.<br /><br
/><table align="center"
cellpadding="0" cellspacing="0"
class="tr-caption-container"
style="margin-left: auto; margin-right: auto;
text-align:
center;"><tbody><tr><td
style="text-align: center;"><a href="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgnnmCP6UHB2d9M7tzTpXfVBhheJXuOknpUPwGKF7Tn5M3z9uxjPEeErIT0eiyCxWKJYtT6IISeP9KCQl-cDPPikuiLyqYXzvpTXEoUMpSf4Ji1L5yq_EWwBHRzJilT7XhEOJvWA9o-ad0/s1600/IMG-20150325-WA0002.JPG"
imageanchor="1" style="margin-left: auto;
margin-right: auto;"><img border="0"
height="360" src="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgnnmCP6UHB2d9M7tzTpXfVBhheJXuOknpUPwGKF7Tn5M3z9uxjPEeErIT0eiyCxWKJYtT6IISeP9KCQl-cDPPikuiLyqYXzvpTXEoUMpSf4Ji1L5yq_EWwBHRzJilT7XhEOJvWA9o-ad0/s640/IMG-20150325-WA0002.JPG"
width="640"
/></a></td></tr><tr><td
class="tr-caption" style="text-align:
center;"></td><td
class="tr-caption"><span
style="font-size: small;">Shehena ya bangi
ikishushwa kwenye gari la Kampuni ya Wengert Windrose
Safaris katika kituo cha polisi mkoani Arusha baada ya
kukamatwa.</span></td></tr></tbody></table>Baraza
la Congress liliaminishwa na wamiliki wa kampuni hiyo ya
Wengert ambayo ni ya Kimarekani kwamba Tanzania ni nchi ya
hovyo ambayo sheria hazifuatwi hata kidogo.<br
/>Kampuni ya Wengert ikafikia hatua ya
kuliaminisha Baraza hilo kwamba imetendewa ndivyo sivyo
nchini kwa kunyang'anywa kitalu kinyume cha sheria na
kwamba kitendo hicho kimefanyika kinyume cha sheria.<br
/><br />Katika
kulighadhibisha Baraza hilo Wengert wakadai kwamba
imenyang'anywa kitalu na kupewa kampuni nyingine ya
kigeni. Hiyo ya kudai kwamba imenyang'anywa kampuni ya
Kimarekani na kupatiwa kampuni nyingine ya kigeni ni katika
ile ile tabia ya kutaka kuwachochea watunga sheria hao wa
Marekani kwa kutumia kigezo cha kwamba wao ni bora zaidi
hivyo haiyumkiniki akanyang'anywa Mmarekani halafu apewe
mgeni mwingine!<br />Uchochezi huo
ukatumika kwa malengo ambayo kampuni ya Wengert
ilitaka.<br /><br />Baraza
la Congress la Marekani lilimwandikia Rais wa Marekani,
Barack Obama, barua likiituhumu Idara ya Wanyamapori kwa
kuinyanga'anya kampuni ya Wengert kitalu na kukitoa isivyo
halali kwa Kampuni nyingine, jambo ambalo halikuwa kweli.
Hata hivyo, ukweli ni kwamba kampuni iliyogawiwa kitalu
hicho ni ya Kitanzania.<br />Kampuni hiyo
haikutaka kusema ukweli kwamba uamuzi wa kutogawiwa
kitalu ulitokana na maamuzi ya kamati ya ugawaji
wa vitalu na kamwe sio kutokana na uamuzi wa Idara ya
Wanyamapori.<br /><br
/>Vitalu hugawiwa na Waziri wa Maliasili na
Utalii baada ya kushauriwa na kamati ya ugawaji wa vitalu.
Tuhuma hizo za uongo zilipelekwa mbele ya Baraza la Congress
baada ya rufaa yao waliyokata kupinga ugawaji wa vitalu
kukataliwa. Ni wazi kabisa kwamba ushawishi uliofanywa kwa
Baraza la Congress kwa kutumia mbinu chafu na uongo
uliokithiri ulilenga katika kuiweka katika shinikizo
serikali ya Tanzania ili iende kinyume na maamuzi yake
halali yaliyofanayika kwa mujibu wa sheria.<br
/><br />Wengert walikwenda
mahakamani mara kadhaa kupinga maamuzi hayo ya serikali na
mara zote wamegonga ukuta. Wiki iliyopita walishindwa kwa
mara ya nne mahakamani katika jitihada zao za kutaka
kuthibitisha kwa kutumia vielelezo wanavyodai ndivyo halali
kwamba kuna makosa katika ugawaji wa vitalu katika eneo la
Lake Natron Game Controlled Area. Imefikia hatua kampuni ya
Wengert inadai kwamba nyaraka rasmi za Serikali ya Tanzania
ni batili na kwamba yenyewe ndiyo ina ramani halali na
nyaraka mbalimbali kutoka serikalini.<br
/><br />Inachekesha sana
kwamba kampuni ya kigeni inakuja nchini na kuamua kupambana
na serikali yetu kwa ajili ya kulazimisha umiliki wa kitalu
cha uwindaji wa kitalii kwa kila njia ikiwa ni pamoja na
kuvifunga midomo vyombo vya habari kwa kutumia mbinu chafu.
Kwa taarifa rasmi za kiserikali ni kwamba kampuni hiyo,
pamoja na kampuni nyingine za Friedkin Family Tanzania,
zimekuwa zikiwatumia watumishi wake na mawakala mbalimbali
kufanya vitendo vya hujuma dhidi ya makampuni mengine ya
uwindaji wa kitalii.<br /><br
/>Aidha, kampuni hiyo pia imekuwa ikiendesha
kampeni chafu dhidi ya viongozi mbalimbali wa Wizara ya
Maliasili na Utalii kwa lengo la kutaka kuthibitisha kwamba
viongozi hao wanafanya maamuzi yasiyozingatia sheria. Ukweli
ni kwamba kampuni hizo ndiyo zimekuwa mstari wa mbele
kutotii sheria za nchi.<br /><br
/>Tabia hii ilishamiri sana wakati wa awamu
iliyopita. Kumekuwapo na jitihada za kuitaka kampuni hiyo
iendelee kufanya shughuli zake za kitalii katika maeneo
halali iliyokabidhiwa na serikali ya Tanzania lakini kila
uchao kumekuwapo na tuhuma za kila aina dhidi ya wadau
wengine wa sekta ya utalii na serikali kutoka kwa kampuni
hizo.<br /><br /><table
align="center" cellpadding="0"
cellspacing="0"
class="tr-caption-container"
style="margin-left: auto; margin-right: auto;
text-align:
center;"><tbody><tr><td
style="text-align: center;"><a href="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEii7NrMY2t_5XIJwphGQJ0F1vUCQRw_hMMU-qbECigVt3lfgUs1PS-4GN0vPYmUv7JgPAegmd6opG9IriUs4JZB82iagc8j5ZJLozeZPX4DLKM7iBRvjHisD4ZtFhZm6TJWSN1NTJPzDHQ/s1600/Mtuhumiwa.JPG"
imageanchor="1" style="margin-left: auto;
margin-right: auto;"><img border="0"
height="640" src="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEii7NrMY2t_5XIJwphGQJ0F1vUCQRw_hMMU-qbECigVt3lfgUs1PS-4GN0vPYmUv7JgPAegmd6opG9IriUs4JZB82iagc8j5ZJLozeZPX4DLKM7iBRvjHisD4ZtFhZm6TJWSN1NTJPzDHQ/s640/Mtuhumiwa.JPG"
width="360"
/></a></td></tr><tr><td
class="tr-caption" style="text-align:
center;"><span style="font-size:
small;">Mtuhumiwa ambaye ni dereva wa gari hiyo
akiwa ameshikiliwa na
polisi.</span></td></tr></tbody></table>Inasikitisha
kwamba kampuni hizo hazioni kwamba ni bora kuachana na
malumbano yasiyokuwa na tija na badala yake kuendelea na
kazi kama zinapenda kuendelea kuwekeza Tanzania vinginevyo
kama zinafikiri zinaonewa ziondoke nchini kwa sababu
Tanzania sio nchi pekee ambayo wanaweza kufanya biashara ya
uwindaji wa kitalii. Katika kuthibitisha kwamba kampuni hizi
hazina hata chembe ya ustaarabu, wamediriki kuwafuata wageni
wa kampuni shindani na kuwafanyia fujo jambo ambalo
liliripotiwa serikalini.<br /><br
/>Aidha, katika kuthibitisha uwezo wake wa
kufanya mambo ya hovyo upo ushahidi kwamba watumishi au
mawakala wa kampuni hiyo walichimba mashimo katika kiwanja
kidogo cha ndege kilichopo kwenye moja ya vitalu vya
washindani wao eti tu kwa sababu uwanja huo waliutengeneza
wao wakati wanamiliki kitalu hicho.<br
/><br />Swali kubwa
linalojitokeza katika vurugu hizi za makampuni haya ya
Kimarekani ni kwamba nani anayewachochea na kuwavimbisha
kichwa kiasi cha kuidhalilisha serikali ya Tanzania huku
wakiwa nchini? Kwa nini hadi leo hatusikii hatua za
kinidhamu na hata kisheria dhidi ya kampuni hizii ambayo
inaonekana kila uchao yanazidisha mapambano dhidi ya
serikali yetu? Tusiruhusu mwekezaji yeyote yule kutupanda
kichwani, hata kama anatoka taifa linalojigamba kuwa taifa
kubwa duniani! Tunachohitaji kwa wawekezaji ni wao wanufaike
na sisi pia tunufaike.
___________________________________________________________________________________Joachim
Mushi, Mwenyekiti wa Tanzania Bloggers Network (TBN) na
Mhariri Mkuu wa Thehabari.com.
Mail address:-
mushi@thehabari.com/
jomushi79@yahoo.com/
info@thehabari.com
Mobile:- 0717
030066 / 0756 469470
Web:- www.thehabari.com
http://joemushi.blogspot.com
--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya
kudhibitisha ukishatuma
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility
for any legal consequences of his or her postings, and hence
statements and facts must be presented responsibly. Your
continued membership signifies that you agree to this
disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the
Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails
from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.
--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.
0 comments:
Post a Comment