Monday 4 March 2013

[wanabidii] Re: Kama ikiwezekana kwa Uhuru yatashindikanaje kwa Lowasa

Nastushwa kidogo na matokeo yanayoendelea kutolewa na tume ya uchaguzi Kenya.  Billionea Uhuru Kenyatta anaonekana kuongoza ingawa ni kwa asilimia kidogo. Matokeo haya kwa mtazamo wangu hata kama Uhuru hatashinda uraisi naona yanaweza kuashiria kuwa kigezo cha uadilifu na kufanana na wapiga kura wako si umasikini,bali ni kwa kiwango kipi unaweza kuwasaidia unawaongoza kwa kuchapa kazi sana na kusimamia haki kiadilifu.Katika pitapita zangu mitaani haswa huku kanda ya ziwa hali ya kisiasa kwa tajiri Lowasa inazidi kubadilika siku hadi siku. Umahiri wake unazidi kuongezeka na upendo kwa wananchi wengi pia unazidi kukua. Kuna kila dalili mpka itapofikia 2015,kwa Lowasa tuhuma za ufisadi (tena wa kufikirika) haziwezi kuwa kizingiti cha kumzuia asiteuliwe na chama chake kuongoza. Na hata CCM isipomteua,Lowasa atashida kwa kishindo kwa chama chochote atachoipeperusha bendera yake akitaka. Kwa Lowasa so far tishio pekee  ni Magufuli na Mwakyembe.Ngupula

0 comments:

Post a Comment