Friday 29 March 2013

[wanabidii] PICHA NA HABARI YA JENGO LILILOPOROMOKA KATIKATI YA JIJI LA DAR ES SALAAM

Picture
Kamanda Kova akizungumza na James Mbatia (Mbunge, M/Kiti NCCR-Mageuzi) (picha, maelzo: Habari Mseto blog)
Picture
Picture
Waziri wa Mambo ya Ndani, Dk Emmanuel Nchimbi (kushoto) akipata maelezo kutoka kwa Kamanda Suleima. Kulia ni Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala, Marietha Minangi. (picha, maelzo: Habari Mseto blog)
Picture
Hizi ni aina ya nondo ambazo kimsingi sio imara kuweza kuhimili ujenzi wa ghorofa ndefu kama hili, kuna haja mamlaka husika likatupia macho kampuni za ujenzi ili kuokoa maisha ya wajenzi na watumiaji wa majengo hayo. (picha, maelezo: Habari Mseto blog)
Picture
Picture
Picture
Mtoto Maisamali Karim (6) ambaye ameokolewa kutoka katika madrasa ya Msikiti wa Khoja Shia Ithna Asheri Jamaat ulioangukiwa na jengo (picha, maelezo: Habari Mseto blog)
*NOTE: Taarifa zote zinazowekwa hapa ni kadiri zinavyopatikana kwa ufahamu wa walioko katika tukio na yanayosemwa hapo. Taarifa kamili itatolewa na Jeshi la Polisi watakapokuwa tayari. Vuta subira.

wavuti.com haitamvumilia yeyote wala maoni yoyote yenye lengo la kuwakejeli, kuwadharau na/au kuwavunja moyo watoa habari za awali.

wavuti.com inawashukuru kwa dhati kabisa wote waliotuma raarifa kuchangia taarifa na picha za awali kusambaa.

Kwa mujibu wa taarifa za eneo la tukio, jengo lilikuwa la orofa 16 na hadi sasa (saa tano kasoro), majeruhi ambao idadi yao kamili haijafahamika, wamepelekwa katika hospitali za Muhimbili na nyinginezo binafsi zilizoko karibu na eneo hilo kwa matibabu. Miili ya watu 12 inaripotiwa kupatikana. Inahofiwa kuwa idadi ya watu waliokuwemo ndani ya jengo inakaribia makumi sita, wengi wao wakiwa ni mafundi ujenzi na mama lishe.

Saa 4:06, @MrishoSalma katika tweet yake anatufahamisha kuwa tayari Polisi wameshafika kwenye eneo la tukio. (Shukurani, Salma.) Viongozi mbalimbali pia wapo katika kusaidia kuratibu shughuli za uokozi zonazoendelea japo kwa vifaa duni. Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalumu ya Kipolisi kwa Mkoa wa Dar es Salaam, Suleiman Kova, inaripotiwa kuwa ameomba nguvu kazi ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ).

Appeal/Ombi: Tafadhali piga simu kwa kiongozi yeyote kumfahamisha kuhusu HITAJI LA HARAKA la uokozi wa maisha ya watu walionaswa ndani.

Updates/Taarifa mpya, saa 3:28 asubuhi -- Dk Chaote amefanikiwa kukaribia eneo la tukio na kusikiliza mazungumzo ya watu ambao wanapasha kuwa ndani ya jengo hilo lililokuwa katika ujenzi (under construction), mlikuwemo mafundi ambao inasadikiwa wamenaswa baada ya orofa ya jengo hilo kuporomoka. Kwamba, mafundi hao wakipigiwa simu wanajibu.

Tayati gari la kutoa huduma ya kwanza (ambulance) limeshawasili katila eneo la tukio.

Polisi? Hadi muda huu hakuna taarifa za kuonekana kwao, labda kama wapo upande mwingine ambapo wananchi hawajawaona.

Saa 2:50 asubuhi -- Jengo moja limeshika moto na kuungua (kama inavyoonekana pichani) asubuhi hii mwendo wa saa mbili u nusu, katikati yabjiji la Dar es Salaam, kwenye barabara ya Mororogo, mtaa wa Indira Gandhi (punde tu baada ya Kisutu).

Shukurani ya picha na taarifa: Dk Chaote P.
Picture
Picture
Picture
Picture
Picture
Picture


Source: http://www.wavuti.com/#ixzz2OvQ5DHNS

--
Jobs in Africa - www.wejobs.blogspot.com
International Jobs - www.jobsunited.blogspot.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.
 
 

0 comments:

Post a Comment