Tuesday 8 January 2013

[wanabidii] TANGAZO LA MKUTANO WA HADHARA WA TAMICO UTAKAOFANYIKA GEITA SIKU YA JUMAMOSI TAREHE 05/01/2013

Pamoja na mvua kubwa iliyonyesha Geita lakini tulifanikiwa kufanya mkutano wa ndani katika ukumbi wa kanisa katoliki Geita kama ambavyo ulipangwa. Mvua hiyo ilianza majira ya saa 8:45 hadi saa 10 alasili muda ambao wafanyakazi wengi walikuwa njiani kuelekea kwenye viwanja vya kanisa katoliki ambapo mkutano wa TAMICO ulipangwa awali ufanyikie. Hata hivyo baada ya hali ya hewa kubadilika tuliamua kuutumia ukumbi ambao ulihimili watu zaidi ya 250 walikuwa wameishafika kwenye mkutano.
 

Mgeni rasmi, Mheshimiwa Suleiman Said Jaffo mbunge wa Kisarawe  aliwahakikishia wafanyakazi hao waliohudhuria mkutano huo kwamba habari zilizosambaa migodini na kusababisha wafanyakazi kuacha kazi si za kweli kwani kwa sasa serikali ipo katika mchakato wa kuandaa mswada wa marekebisho kwa maelekezo ya bunge ili uletwe bungeni kwa kujadiliwa. Na kwa utaratibu mswada unatakiwa kusomwa mara mbili pasipo kujadiliwa na mara ya tatu ndio unasomwa na kujadiliwa na hatimaye unapitishwa na kusubiri Rais ausaini kuwa sheria na baada ya rais kusaini, waziri mwenye dhamana anautungia kanuni na kutangaza tarehe ya sheria kuanza kutumika kwenye gazeti la serikali.

Kwa mchakato huo, hakuna ukweli wowote kwamba mswada uletwe kwenye kikao cha mwezi February 2013 na kuupitisha. Na hata kama mswada utapitia hatua zote hizo na bado serikali ikaweka kipengele cha fao la kujitoa namna ambavyo kinapigiwa kelele bado wabunge watakuwa na fursa ya kukipinga kwa kuzingatia hoja mbali mbali zilizokwisha wasilishwa na wadau katika nyakati tofauti zikipinga kipengele hicho kutokana na  upekee wa sekta binafsi hususani migodi,NGO's na sekta zingine zenye changamoto zinazofanana na hizo.

Pia alitoa angalizo juu ya wimbi la wafanyakazi migodini kuacha kazi ambalo limepelekea wafanyakazi zaidi ya 300 kuacha kazi katika migodi ya dhahabu ya Bulyanhulu,Geita, North Mara,Tulawaka na Buzwagi katika kipindi kisichozidi miezi miwili. Mgodi wa Bulyanhulu ndio umeathilika zaidi ambapo wafanyakazi zaidi ya 200 tayari wameishaacha kazi na athali za uzalishaji tayari zimeanza kujitokeza.Alionya kama wimbi hili litaendelea la kuacha kazi kwa uvumi tu basi tutarajie nafasi hizo  kuchukuliwa na wageni kutoka nje na kunyima fursa vijana wa kitanzania.

Mwisho, aliahidi kuifanyia kazi hoja iliyoibuliwa kwenye mkutano ya ya black listing inayofanyw na waajiri migodini kumzuia mfanyakazi aliefukuzwa au kuachishwa kazi mgodi mmoja ashindwe kuajiriwa mgodi mwingine hata kama ameachishwa kazi kwa kuonewa au kusingiziwa jambo ambalo kiuhalisia hakulifanya. Kuna wasiwasi mkubwa kama jambo hili lisipofanyiwa kazi kikamilifu hata hawa wanaoacha kwenye wimbi hili la fao la kujitoa wakakumbwa na kikwazo hiki pale ambapo watapata tena fursa ya kuajiliwa tena katika mgodi mwingine au huo huo waliotoka.

Aidha aliwashauri wafanyakazi kuchangamkia fursa mbali mbali zilizopo nchini kwa ajili ya ustawi wao wenyewe na taifa kwa ujumla. Aliwaasa kila mfanyakazi ajiwekee lengo la kumiliki ardhi walao heka tano na kuhakikisha wanamiliki viwanja katika miji ambayo tayari imeishaunganishwa na mtandao wa barabara.

Thomas Sabai

Katibu wa TAMICO- Tawi la GGM
--- En date de : Jeu 3.1.13, thomas sabai <thomas_sabai@yahoo.com> a écrit :


De: thomas sabai <thomas_sabai@yahoo.com>
Objet: TANGAZO LA MKUTANO WA HADHARA WA TAMICO UTAKAOFANYIKA GEITA SIKU YA JUMAMOSI TAREHE 05/01/2013
À: "mabadiliko groupmail" <mabadilikotanzania@googlegroups.com>
Date: Jeudi 3 janvier 2013, 3h33

Wadau,

Heri ya mwaka mpya na hongereni kwa majukumu ya ujenzi wa Taifa. Kwa Bahati mbaya huku migodini tumeuanza mwaka 2013 kukiwa na uzushi uliozagaa wa kusitishwa kwa fao la kujitoa ifikapo February 2013. Uzushi huu umezagaa karibu migodi yote ya dhahabu na umesababisha wimbi kubwa la wafanyakazi wa migodini kuacha kazi ili wawahi tarehe hiyo ya kizushi.

Cha kushangaza waajiri wako kimya na wanakubali wafanyakazi wao kujiuzuru kwa uzushi huo pasipo kuwaelimisha na kuwapatia taarifa sahihi wafanyakazi  ambao wamewazalishia mali kwa muda mrefu na kwa faida. Ukimya huu wa waajiri unaibua maswali na mashaka na kudhania yawezekana wakawa na mkono katika uzushi huu ili wanufaike na kupunguza wafanyakazi kwa gharama nafuu.

Binafsi kama kiongozi wa TAMICO nalaani wazushi wenye nia mbaya ya kuhujumu haki za wafanyakazi na jitihada za serikali za kuwapatia wananchi wake ajira na maisha bora, badala yake watu wachache wanatumia mwanya wa kupindisha ukweli kwa lengo la maslahi binafsi.

Kama sehemu ya kuelimisha umma, TAMICO imeandaa mkutano wa hadhara utakaofanyika Jumamosi tarehe 05/01/2013. Mkutano huu utafanyika katika viwanja vya kanisa Katoliki mjini Geita kuanzia saa 8:00 mchana na kuendelea. Mkutano huu unatarajiwa kuhudhuriwa na viongozi na wawakilishi wa TAMICO kutoka sehemu mbali mbali za kazi.

Mgeni rasmi atakuwa ni Mheshimiwa Suleiman Jaffo, mbunge wa Kisarawe na mtoa hoja binafsi ya kutaka  sheria ya marekebisho ya sheria za mifuko ya hifadhi ya jamii,2012 (hususani fao la kujitoa) ipitiwe upya. Wanachama wa mifuko ya hifadhi ya jamii na wafanyakazi wote bila kujali itikadi yoyote ile mnaalikwa kuhudhuria bila kukosa ili kupata ufafanuzi wa kina wa hatma ya fao hilo na kipi kinafanyika kwa sasa kuhusiana na sheria hiyo.

Wote mnakaribishwa kuhudhuria na kutoa maoni ili tunusuru wimbi hili linalinyima wafanyakazi haki yao ya kufanya kazi kwa kisingizio cha fao la kujitoa.

Nawasilisha,

Thomas Sabai

Katibu wa TAMICO-Tawi la GGM

--
Jobs in Africa - www.wejobs.blogspot.com
International Jobs - www.jobsunited.blogspot.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
 
 

0 comments:

Post a Comment