Tatizo la wanaojiita wazanzibari wengi hawaelewei wanachokidai na kwa nini wanakidai. Ukiwauliza karibu wote watakwambia wananyonywa na bara, sasa sijui ni kipi kilichopo zanzibar ambacho hakipo bara na ambacho kinafaidisha bara kuliko zanzibar. Wengine wanadai wanatawaliwa na hapa ndipo nnapokuwa na utata na definition yao ya kutawaliwa. Nnachoamini kuna kakundi kadogo ka watu zanzibar ambao wanaelewa nini hasa wanakitafuta kwa maslahi ya wanachama wa hicho kikundi. Ili kufanikisha malengo wanatumia uelewa duni wa wazanzibari wengi kwa kutumia sababu tofauti kutokana na ukweli kwamba sababu halisi haziwezi kusemwa hadharani.
Suala kama hili la kuvunja muungano linahitaji utafiti wa ndani "detailed assessment" na wa muda mrefu tena na wataalamu na sio wanasiasa wala mambumbumbu wenye kujua kupiga kelele. Utafiti uonyeshe faida na hasara za wakati huu wa muungano na baada ya kuvunika kwa muungano kwa zanzibar na wananchi wake. Utafiti ulinganishe faida na hasara kwa nyakati hizo mbili ila usitoe mapendekezo yake ili maamuzi ya wakati upi mzuri ubaki kwa mwananchi. Mwisho utafiti uwe wazi kwa wazanzibari wote halafu wapewe nafasi ya kuamua (referendum) huku wakijua nini hasa matokeo ya uamuzi wao (informed decision).
Lakini hili la kuwalisha sumu wananchi ambao wengi hawajafika hata darasa la saba ni uonevu kwa sababu wanakuwa wanashabikia kitu wasichokifahamu kwa kina. Hakuna kitu kibaya kama kujutia maamuzi yaliykwishafanyika.
Vile vile kuna ukweli kwenye maelezo ya Matinyi someni vizuri.
Nnachokiona BAADHI ya wazanzibari wamepokea haya mapendekezo kama vile ndio yamepitishwa. Jamani Tanzania ina watu wengi wenye mitazamo na uelewa tofauti. Wengine ni wana Chadema lakini si lazima mtazamo wako ufanane na wa uongozi wako ambao kwao vile vile kunaweza kuwa na tofauti ila demokrasia tu imetumika i.e. wengi wape.
On Thursday, January 10, 2013 10:55:17 AM UTC+3, Said Issa wrote:
--Kaka Matinyi,>sisi tunataka NDOA kamili.
Kama unataka ndoa kamili, basi bora utafute mwari mwengine, kwani huyu keshatoroshwa!...bin Issa.From: Mobhare Matinyi <mat...@hotmail.com>
To: Wanabidii googlegroups <wana...@googlegroups.com>
Sent: Wednesday, January 9, 2013 10:59:14 PM
Subject: RE: [wanabidii] Wazanzibari wasema - " Ahsante Chadema"!
--John, nenda kawape wenzako jibu hili linaloanza hivi:
Jamani Watanzania wenzangu, huku ni kuchanganyikiwa ingawa kunatia moyo kwamba watu bado mnautaka Muungano wetu.
Mfumo wa serikali tatu kama shirikisho ni sera ya vyama vyote vya upinzani na baadhi ya Watanzania na hata CUF wamekuwa wakiihubiri kwa miaka yote hadi pale Maalim Seif alipobadilika na kuanza kuuhubiri muungano wa mkataba kana kwamba kuna miungano isiyokuwa na mikataba.
Hoja ya muungano wa mkataba inataka mambo ambayo yakitekelezwa huu muungano hautakuwepo na ndicho ambacho watu wa Tume - akina Warioba - huwa wanawauliza wanaoutaja muungano wa mkataba kwamba wanamaanisha hivyo au vinginevyo.
Mfano wa muungano wa mkataba unaotolewa eti ni EU na hiki kilichosemwa na Chadema hakina sura ya EU bali sura ya shirikisho kama yalivyo mashirikisho ya nchi nyingi duniani, mfano Nigeria, Sudan, Ujerumani, India, Kanada, Brazil, Marekani, n.k. Mashirikisho haya pamoja na hili la Chadema yana "sovereign state" moja yenye serikali zaidi ya moja LAKINI huu muungano wa mkataba unaosemwa eti utakuwa na sovereign states zaidi ya moja na hakutakuwa na serikali ya shirikisho bali mfumo kama wa EU ambao ni kama huu wa AU na huu si muungano kamili bali ushirikiano tu.
Hii ni tofauti kubwa mno na kama watu hamuijui, basi ni kweli kwamba hata mnachokidai hamkijui.
Tofauti ya shirikisho la Chadema na haya ni kwamba shirikisho la Chadema lina serikali kuu dhaifu mno inayozungukwa na serikali mbili zenye nguvu. Huwezi kudumu katika mfumo wenye serikali kuu dhaifu kiasi hiki na pengine tujiulize kwa nini serikali za mashirikisho mengine duniani hazina hii sura? Kumbukeni Muungano wa Kisovieti, kwamba pale ulipokuwa na serikali ya shirikisho dhaifu ndipo hapo ulipovunjikilia mbali.
Huo muungano wa mkataba unaodaiwa bila kueleweka na hata wanaousema ni mwepesi kuliko mfumo uitwao "confederation" ambao huziunganisha nchi katika masuala ya ulinzi na sera za nje/uhusiano wa kimataifa, kama zile jamhuri za iliyokuwa USSR. Mkishakuwa na sovereignty states zaidi ya moja, na hamna vitu hivi viwili vya pamoja, basi mnaweza kweli mkawa kama EU au AU iwapo mtakubaliana kushirikiana lakini huo si MUUNGANO tunaoutaka siye wengine; sisi tunataka NDOA kamili.
Matinyi.
Date: Wed, 9 Jan 2013 09:51:07 -0800
From: nkumb...@yahoo.com
Subject: [wanabidii] Wazanzibari wasema - " Ahsante Chadema"!
To: wana...@googlegroups.com
Wazanzibari wasema - " ahsante chadema"!
--
Jobs in Africa - www.wejobs.blogspot.com
International Jobs - www.jobsunited.blogspot.com
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+...@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
Jobs in Africa - www.wejobs.blogspot.com
International Jobs - www.jobsunited.blogspot.com
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+...@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
Jobs in Africa - www.wejobs.blogspot.com
International Jobs - www.jobsunited.blogspot.com
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
0 comments:
Post a Comment