Monday 7 January 2013

Re: [wanabidii] Re: Mbunge wa Lushoto azomewa Kanisani *

Yona,
 
Sahihisho kidogo. Kwangu mimi salamu hiyo au salamu nyingine yeyote, sina tatizo nayo. LAKINI unachotakiwa kujua ni kuwa tofauti ya uislam na ukristo ni kwamba ukristo ni maisha ya kiroho, uislam ni mfumo wa maisha ya kila siku. Ni mfumo unaoelezea mwana-Adam aishi vipi, avae vipi, serikali iendeshwe vipi. Ndiyo maana huwezi kutofautisha uarabu na uislam. Ndiyo maana asalam aleikum ni salamu ya kiarabu na hivyo ni salamu ya kiislam. Au Yona unaijua salamu ya kiislam zaidi ya asalam aleikum.
 
Mimi najiuliza, hata kama nikisalimiwa kwa salamu ya kiislam au kilokole au hata ya kijadi inanidhuru au kuniathiri nini. Kwangu sioni tatizo kama ninajua namna ya kuitikia. Lakini kwa Shekifu ambaye kusalimia kwa salamu ya kiarabu/kiislam wakati yeye mwenyewe si muislam wala mwarabu, anaowasalimia si waislam wala waarabu, is very awkward. Ningeweza kuelewa kama ambaye aliitoa salamu angekuwa muislam/mwarabu akiwasalimia wakristo au waswahili, au mkristo akiwasalimia waislam/waarabu, au muislam/mwarabu akiwasalimia waislam/waarabu. Kwa mkristo kuwasalimia waislam kwa salamu ya kiislam au kinyume chake inapendeza maana inaonesha jinsi jamii yetu ilivyochanganyika, inavyoheshimiana na kuthaminiana katika kile ambacho mwenzie anakiamini.
 
Bart     
From: Yona F Maro <oldmoshi@gmail.com>
To: Wanabidii <wanabidii@googlegroups.com>
Sent: Tuesday, January 8, 2013 12:12 AM
Subject: [wanabidii] Re: Mbunge wa Lushoto azomewa Kanisani *

Mbunge shekifu hakuwa na sababu yoyote ya kuomba radhi kwa kutamka
asalam aleikum , Hii sio salamu ya kidini ni salamu ya lugha ya
kiarabu inayotamkwa dunia nzima na kwa maeneo kama ya Tanga ukanda wa
pwani hiyo imezoeleka sana .

Naungana na ndugu Matinyi alivyosema watu kutanguliza utaifa badala ya
dini na makabila .

On Jan 7, 11:23 pm, Edgar Mbegu <emb...@hotmail.com> wrote:
> Matinyi
> Huyu bwana alienda Kanisani siku ya Jumapili, na si katika Mkutano wa hadhara aliouitisha yeye. Kanisani kuna salamu zake ambazo si za "kishabiki" au za "kipumbavu" kama unavyodai wewe, maadamu zinatolewa mahali panapohusika. Si ndiyo uhuru wa kuabudu huo kadiri ya Katiba yetu ambao hata wanasiasa wanao?
> Kama unadhani alipaswa kuwasalimu kwa salamu za "kitanzania" , angeitisha mkutano wa hadhara na kuwasalimu watu kwa salamu hizo. Kama ni mwanasiasa tu na hana dini alikwenda Kanisani kufanya nini? Maadamu alienda Kanisani, siku ya Jumapili katika Ibada, na yeye pengine ni muamini wa Kanisa hilo, alipaswa kuwasalimu kwa salamu ya Kanisa husika; na waamini walimzomea kwa sababu alitoa salamu ambayo huwa haitumiki Makanisani hata kama maana yake ni nzuri namna gani. Isipokuwa, katika vyombo vya habari vya taifa, unasikia mtangazaji kabla ya kuanza kipindi anatoa salamu zinazohusika na dini fulani, hapo nadhani siyo mahali pake. Au katika semina za kiserikali... hapo salamu hizo hazihusiki. Mimi naona, aliyekosea  ni yule aliyemualika huyo bwana  aongee katika hadhira ile, kama nani? Kama ni muamini wa kanisa hilo, si alienda kusali tu kama wengine? Kwa nini apewe nafasi ya pekee ya kusalimia au kuongea? Ina maana katika Kanisa hilo kila mgeni hupewa nafasi kama hiyo?
>
> From: mati...@hotmail.com
> To: wanabidii@googlegroups.com
> Subject: RE: [wanabidii] Mbunge wa Lushoto azomewa Kanisani *
> Date: Mon, 7 Jan 2013 16:43:13 +0000
>
> Musa Juma,
>
> Suala la dini ya Shekifu halina maana yoyote hapa. Suala kwamba alikuwa na nia njema halina maana yoyote hapa. Suala kwamba waumini walimzomea lina maana kubwa, kwamba wanahisi alifanya kosa, aliwaudhi. Lawama zote zinapaswa kwenda kwa Shekifu kwa sababu hakupaswa kutumia salamu ya dini yoyote pale kanisani (hata ya kikristo) kutokana na hadhi yake ya uanasiasa.
>
> Mchungaji au padri angetumia salamu au kauli mbiu za kishabiki kama Asifiwe Bwana Yesu - mara sijui Tumsifu Yesu - hilo lingekuwa ni tatizo lake yeye na kanisa lake lakini huyu Shekifu ni kiongozi wa Watanzania wote kwenye jimbo lake, hivyo alipaswa na anapaswa kutumia salamu za Watanzania wote.
>
> Kuleta salamu zenye harufu ya udini ni ukosefu mkubwa wa busara katika zama hizi za udini kuinyemelea nchi yetu. Huyu mtu aache salamu za kipumbavu hizi. Hakuna lugha laini hapa - hizi ni salamu za kipumbavu. Wanasiasa wanaozitumia wapaswa kuzomewa kokote kule. Uanasiasa haufi mtu akiingia kwenye nyumba ya ibada.
>
> Kwani sisi Watanzania hatuna salamu za tamaduni zetu katika lugha ya Kiswahili? Hatuna???
>
> Matinyi.
>
> Date: Mon, 7 Jan 2013 15:43:19 +0300
> Subject: Re: [wanabidii] Mbunge wa Lushoto azomewa Kanisani *
> From: mussas...@gmail.com
> To: wanabidii@googlegroups.com
>
> SHEKIFU hakukosea.
>
> WADAU katika mjadala huu, Mbunge huyu, hakukosea kwani salamu hiyo haina tatizo, kwa tafsiri yangu ndogo Mtu kusema: Asalam Aykum humaanisha rehema na amani iwe juu yenu,ukiitikia  wa alaykum salama, kipifu na wewe pia.
>
> Sasa hapa hakuna udini
>
> ni muhimu watu kupunguza jazba katika mambo madogo madogo kama haya kwani hayajengi na kikubwa zaidi Shekifu ni Mkristo sasa kumzomea kwa salamu tu nadhani hajatendewa haki;
>
>  Wadau mjadala huu ni funzo kuwa sasa Taifa liendapo sio salama sisi tuwe watoa elimu sahihi kwani chuki za kidini zimeanza kunutafuta.
>
> Mussa
> Arusha
>
> On Thu, Jan 3, 2013 at 1:07 PM, magreth Mulokozi <m.mulok...@gmail.com> wrote:
>
>   This message is eligible for Automatic Cleanup! (m.mulok...@gmail.com) Add cleanup rule | More info
>
> Duu anatafuta kura  za 2015 sasa , duu  pole sana Nd Shekifu
>
> 2013/1/3 mati...@hotmail.com <mati...@hotmail.com>
>
> ....alikariri.....siyo alikalili.
>
> T-Mobile. America's First Nationwide 4G Network
>
> ----- Reply message -----
> From: "adeladius makwega" <makwadelad...@googlemail.com>
> To: "mabadilikotanzania" <mabadilikotanzania@googlegroups.com>, "wanabidii" <wanabidii@googlegroups.com>
> Subject: [wanabidii] Mbunge wa Lushoto azomewa Kanisani
> Date: Thu, Jan 3, 2013 4:46 am
>
> Shekifu aunza mwaka mpya Vibaya
>
> Mbunge wa  Lushoto Hendry Shekifu ameuunza  mwaka wa 2013 vibaya
> baada ya kuzomewa Kanisani  na  waamini katika    sherehe  za  mwaka
> mpya baada ya kupewa nafasi ya  kuwasalimu washirika wa Kanisa Kuu  la
> KKKT  Lushoto Tanga.
>
> Ibada hiyo ya kuukaribisha  mwaka  mpya ilianza kwa  waumini kupokea
> mahubiri  ya  mwaka mpya  yaliyohubiriwa na Mchungaji Walelaza  na
> baadae kufuatiwa na ibada  ya ubatizo ambapo watoto wawili kutoka
> familia  mbili walibatizwa.
>
> Mara baada ya  ubatizo huo  ibada  ilifuatiwa na utoaji wa  Sadaka
> huku  mbunge  huyo wa  Lushoto akionekana  kushiriki  kikamlifu
> katika  ibada hiyo .
>
> Akiwa  amevalia  suti  ya rangi  nyeusi  yenye mistari    midogo
> midogo  miyeupe Mbunge Shekifu ambaye  aliwahi kushika nyadhifa
> mbalimbali zikiwamo ukuu  wa mkoa alipewa nafasi ya kusimama  mbele ya
> waamini mithili ya  kasisi.
>
> Nafasi hiyo ilitolewa  wakati wa  Matangazo  huku  mchungaji
> akiwaomba  waumini hao  kumsikiliza Mbunge wao ili awasalimu. Basi
> Mbunge  Shekifu alisimama  huku akiweka    vizuri koti   kwa kujifunga
> vifungo vya koti hili ambalo  lilionekana  kuutosha  mwili wake
> mkubwa  uliojengeka  vizuri.
>
> Alikisogelea kipaza sauti  mara  alianza kuongea   kwa
> kujiamini."Aslaam Aleikumuuu…" Duu  utangulizi huo  uliharibu  hali ya
> hewa  ya kanisa hilo wauumini kuanza  kuzomea na kuguna   kutokana
> salaam  hiyo  iliyotolewa  mwanzoni  katika  sehemu  isiyo sahihi.
>
> Hali hiyo iliwafanya waumini hao  kuibua  munkali huo kutokana na
> kitendo cha  mbunge  huyo  pengine  kukalili namna  ya kusalimia watu
> katika  majukwaa ya kisiasa  bila ya kujua kuwa  sasa  madhari
> aliyokuwa nayo ilikuwa  ya  salaam moja  tu   kama sikosei ni Bwana
> Yesu asifiwe au  Tumsifu Yesu Kristu.
>
> Hekima  ilitumika   pengine  huku  yule aliyempa nafasi ya kuwasalimu
> wauumini wake akijilaumu kuitoa  nafasi hiyo iliyotia  shubiri
> kanisani hapo na kuibua  zomeazomea hiyo  ambalo  sio  jambo la
> kawaida  kwa waumini kufanya hivyo.
>
> Mchungaji Walelaze  ilibidi  kuinuka na kusema waziwazi  kuwa  Ndugu
> Shekifu umekosea  sana kwanza  ulitakiwa  kujitambua kuwa  wewe
> japokuwa ni  Kiongozi  pia wewe ni mkiristu   lolote utakalo fanya
> popote  pale    tambua     unamajukumu mawili kwanza  ukiristu wako
> na pili   kuwa  kiongozi.   Hapa ni kanisani  ulitakiwa kuwasalimia
> waashirika  kwa   salaam   yao  siyo salaam hiyo uliyoitoa hapa.
>
> Basi  mchungaji huyo alimaliza  mtafaruku huo huku  mbunge  huyo wa
> Lushoto akishuka  katika mimbari ya kanisa  hilo kwa  fedhea na
> kurejea  katika kiti chake  ambacho kilikuwa  jirani na  mlango   wa
> kutoka  nje  ya  kanisa.
>
> Mara  baada ua  ibada  hiyo  ya mwaka mpaya  mbunge huyo alionekana
> kuwa mtu wa  mwisho kuondoka  kanisani  mara baada ya washirika  wote
> kuondoka  lakini  washirika  hao  walisema kuwa   mbunge  huyo
> amekalili  kusalimia   kwa  salaam    hizo   ndiyo maana  alipitiwa.
>
> "Mimi nilitaka    Mbunge  aombe  msamaha  kwa alilolifanya  sio
> kuondoka kimya kimya  tu  hawa wanasiasa  hawana adabu kabisa wanakuja
> na   mbwembwe alafu wanapata aibu."alisema mama  mmoja
> aliyejitambulisha  kwa  jina moja tu la Mama  Sarah.
>
> Mshirika mwingine alimuunga  mkono mchungaji Waleleza kwa  kumkumbusha
> Mbunge  huyo  kuwa  makini sana akiwa  kanisani  na kuheshimu  salaam
>  za ibada   za makanisa  sio kuja  na  salaam    za   nyumba  zingine
> za ibada.
>
> "Pengine  inawezekana Mbunge huyu  asipewe  tena  nafasi ya
> kuwasalimu waumini kanisani kutokana na kosa  hili," aliserma  mzee
> mmoja wa makamo ambaye  alidai kuwa hilo ni kosa  baya.
>
> Mwishoni alionekana  Mbunge Shekifu akiingia ndani ya  gari yake
> nyeupe  yenye  Bendera ya  CCM ikipeperuka  mkono wa kushoto. Ndani ya
> gari hiyo   kukiwa na  akina mama  watatu ambao walionekana  wakifunga
> milango na  dereva   wa gari hilo akiondoa  gari  katika eneo la
> kanisa  hilo.
>
> Wasalaam  Adeladius Makwega
>
> --
> Jobs in Africa -www.wejobs.blogspot.com
> International Jobs -www.jobsunited.blogspot.com
>
> Kujiondoa Tuma Email kwenda
> wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com  Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
>
> Disclaimer:
> Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
>
> --
> Jobs in Africa -www.wejobs.blogspot.com
> International Jobs -www.jobsunited.blogspot.com
>
> Kujiondoa Tuma Email kwenda
> wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
>
> Disclaimer:
> Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
>
> --
> Jobs in Africa -www.wejobs.blogspot.com
> International Jobs -www.jobsunited.blogspot.com
>
> Kujiondoa Tuma Email kwenda
> wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
>
> Disclaimer:
> Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
>
> --
> Jobs in Africa -www.wejobs.blogspot.com
> International Jobs -www.jobsunited.blogspot.com
>
> Kujiondoa Tuma Email kwenda
> wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
>
> Disclaimer:
> Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented ...
>
> read more »

--
Jobs in Africa - www.wejobs.blogspot.com
International Jobs - www.jobsunited.blogspot.com

Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com  Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma

Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.




0 comments:

Post a Comment