Monday 7 January 2013

Re: [wanabidii] Mbunge wa Lushoto azomewa Kanisani *

Bwana salum sio kila kitu cha Kikristo kimeandikwa kwenye Biblia. Ndio maana hata katika Yohana mmoja wa wanafunzi wa karibu wa Yesu (Yohana) alisema yote aliyoyasema na kuyafanya Yesu yangeandikwa, dunia nzima isingetosheleza. Hapo ni Yesu tu, je mitume, je manabii, je wafalme, je waamuzi, je makuhani nk. Mkristo anaongozwa na Roho Mtakatifu anayeregulate mapenzi ya Mungu na Neno lake. Lolote afanyalo Mkristo ambalo halipingani na Wazo kuu la Mungu ndani Biblia ni ruksa. 

Salamu hizi zinaibuka kama njia ya kusalimiana kikristo ambazo nazo hubadilika kulingana na wakati na pia dhehebu. Hata katika Biblia Yesu hakuwa na Salamu maalum ambayo aliitumia kwa kusalimi. Amani iwe kwenu ilitumika mara moja tu alipofufuka basi. 

Lengo kuu la salamu za Kikristo ni kumtakia Mtu heri au baraka iliyobebwa ndani ya maneno katika salamu husika

Mifano ya salamu za BIBLIA
  1. Amani iwe kwenu - Salamu ya Yesu baada ya kufufuka - Luka 24:36
  2. Neema na iwe kwenu na amani zitokazo kwa Mungu Baba, Bwana wetu Yesu Kristo  (Karibu barua zote za Paulo)
  3. Mungu akubariki (Namba 6:24-26)
  4. Uishi milele (2 Samueli 16:16; 1Samueli 10:24)
  5. Amani iwe kwenu na nyumba yako (Luka 10:5; 1Samueli 25:5-6)
  6. Salamu, Kigiriki Hail, kimombo = Greeting -(Mwanzo 29:13; Warumi 16:16; 1Wakorintho 16:20; 2Wakorintho 13:12; 1 Wathessalonike 5:26; 1Petro 5:14). Na hii salamu inaambatana sana na kubusu au kubusiana mfano wa Yuda alipoenda kumsalimia Yesu "Mara akamuendea Yesu akasema, Salamu Rabi, Akambusu Matayo 26:49), Pia Yesu alitumia hii salamu kuwasalimia 
  7. Shalom - Salamu hii hutumia sana na wahayudi na baadhi ya wakristo
  8. Kubusu na kukumbatia ni salamu ya Kikristo pia 1 Petro 5:14

Niishie hapa

Real Change for Real Development,  

Lemburis Kivuyo
+255654650100/078 7665050/0755646470
Website: www.kivuyo.com,  Skype: lekivuyo, Facebook: http://facebook.com/lemburis.kivuyo, Titter: http://twitter.com/lembu1, Linkedin: http://tz.linkedin.com/in/lembukivuyo, Google+: gplus.to/lembukivuyo


2013/1/7 godfred mbanyi <mbanyibg@yahoo.com>
Bw. Matinyi, narudia tena kuchangia juu ya hili!! Huyu Bwana alistahili bakora, kumzomea "it is understatement" kwa kosa alilofanya tena akiwa kanisani!! Dharau za wanasiasa hizo hazivumiliki kwa kiasi hicho!!!




--- On Mon, 1/7/13, Mobhare Matinyi <matinyi@hotmail.com> wrote:

From: Mobhare Matinyi <matinyi@hotmail.com>
Subject: RE: [wanabidii] Mbunge wa Lushoto azomewa Kanisani *
To: "Wanabidii googlegroups" <wanabidii@googlegroups.com>
Date: Monday, January 7, 2013, 8:43 AM


Musa Juma,
 
Suala la dini ya Shekifu halina maana yoyote hapa. Suala kwamba alikuwa na nia njema halina maana yoyote hapa. Suala kwamba waumini walimzomea lina maana kubwa, kwamba wanahisi alifanya kosa, aliwaudhi. Lawama zote zinapaswa kwenda kwa Shekifu kwa sababu hakupaswa kutumia salamu ya dini yoyote pale kanisani (hata ya kikristo) kutokana na hadhi yake ya uanasiasa.
 
Mchungaji au padri angetumia salamu au kauli mbiu za kishabiki kama Asifiwe Bwana Yesu - mara sijui Tumsifu Yesu - hilo lingekuwa ni tatizo lake yeye na kanisa lake lakini huyu Shekifu ni kiongozi wa Watanzania wote kwenye jimbo lake, hivyo alipaswa na anapaswa kutumia salamu za Watanzania wote.
 
Kuleta salamu zenye harufu ya udini ni ukosefu mkubwa wa busara katika zama hizi za udini kuinyemelea nchi yetu. Huyu mtu aache salamu za kipumbavu hizi. Hakuna lugha laini hapa - hizi ni salamu za kipumbavu. Wanasiasa wanaozitumia wapaswa kuzomewa kokote kule. Uanasiasa haufi mtu akiingia kwenye nyumba ya ibada.
 
Kwani sisi Watanzania hatuna salamu za tamaduni zetu katika lugha ya Kiswahili? Hatuna???
 
Matinyi.
 

Date: Mon, 7 Jan 2013 15:43:19 +0300
Subject: Re: [wanabidii] Mbunge wa Lushoto azomewa Kanisani *
From: mussasiwa@gmail.com
To: wanabidii@googlegroups.com

SHEKIFU hakukosea.

WADAU katika mjadala huu, Mbunge huyu, hakukosea kwani salamu hiyo haina tatizo, kwa tafsiri yangu ndogo Mtu kusema: Asalam Aykum humaanisha rehema na amani iwe juu yenu,ukiitikia  wa alaykum salama, kipifu na wewe pia.

Sasa hapa hakuna udini

ni muhimu watu kupunguza jazba katika mambo madogo madogo kama haya kwani hayajengi na kikubwa zaidi Shekifu ni Mkristo sasa kumzomea kwa salamu tu nadhani hajatendewa haki;

 Wadau mjadala huu ni funzo kuwa sasa Taifa liendapo sio salama sisi tuwe watoa elimu sahihi kwani chuki za kidini zimeanza kunutafuta.

Mussa
Arusha

On Thu, Jan 3, 2013 at 1:07 PM, magreth Mulokozi <m.mulokozi@gmail.com> wrote:
Boxbe This message is eligible for Automatic Cleanup! (m.mulokozi@gmail.com) Add cleanup rule | More info

Duu anatafuta kura  za 2015 sasa , duu  pole sana Nd Shekifu


2013/1/3 matinyi@hotmail.com <matinyi@hotmail.com>
....alikariri.....siyo alikalili.




T-Mobile. America's First Nationwide 4G Network


----- Reply message -----
From: "adeladius makwega" <makwadeladius@googlemail.com>
To: "mabadilikotanzania" <mabadilikotanzania@googlegroups.com>, "wanabidii" <wanabidii@googlegroups.com>
Subject: [wanabidii] Mbunge wa Lushoto azomewa Kanisani
Date: Thu, Jan 3, 2013 4:46 am


Shekifu aunza mwaka mpya Vibaya

Mbunge wa  Lushoto Hendry Shekifu ameuunza  mwaka wa 2013 vibaya
baada ya kuzomewa Kanisani  na  waamini katika    sherehe  za  mwaka
mpya baada ya kupewa nafasi ya  kuwasalimu washirika wa Kanisa Kuu  la
KKKT  Lushoto Tanga.

Ibada hiyo ya kuukaribisha  mwaka  mpya ilianza kwa  waumini kupokea
mahubiri  ya  mwaka mpya  yaliyohubiriwa na Mchungaji Walelaza  na
baadae kufuatiwa na ibada  ya ubatizo ambapo watoto wawili kutoka
familia  mbili walibatizwa.

Mara baada ya  ubatizo huo  ibada  ilifuatiwa na utoaji wa  Sadaka
huku  mbunge  huyo wa  Lushoto akionekana  kushiriki  kikamlifu
katika  ibada hiyo .

Akiwa  amevalia  suti  ya rangi  nyeusi  yenye mistari    midogo
midogo  miyeupe Mbunge Shekifu ambaye  aliwahi kushika nyadhifa
mbalimbali zikiwamo ukuu  wa mkoa alipewa nafasi ya kusimama  mbele ya
waamini mithili ya  kasisi.

Nafasi hiyo ilitolewa  wakati wa  Matangazo  huku  mchungaji
akiwaomba  waumini hao  kumsikiliza Mbunge wao ili awasalimu. Basi
Mbunge  Shekifu alisimama  huku akiweka    vizuri koti   kwa kujifunga
vifungo vya koti hili ambalo  lilionekana  kuutosha  mwili wake
mkubwa  uliojengeka  vizuri.

Alikisogelea kipaza sauti  mara  alianza kuongea   kwa
kujiamini."Aslaam Aleikumuuu…" Duu  utangulizi huo  uliharibu  hali ya
hewa  ya kanisa hilo wauumini kuanza  kuzomea na kuguna   kutokana
salaam  hiyo  iliyotolewa  mwanzoni  katika  sehemu  isiyo sahihi.

Hali hiyo iliwafanya waumini hao  kuibua  munkali huo kutokana na
kitendo cha  mbunge  huyo  pengine  kukalili namna  ya kusalimia watu
katika  majukwaa ya kisiasa  bila ya kujua kuwa  sasa  madhari
aliyokuwa nayo ilikuwa  ya  salaam moja  tu   kama sikosei ni Bwana
Yesu asifiwe au  Tumsifu Yesu Kristu.

Hekima  ilitumika   pengine  huku  yule aliyempa nafasi ya kuwasalimu
wauumini wake akijilaumu kuitoa  nafasi hiyo iliyotia  shubiri
kanisani hapo na kuibua  zomeazomea hiyo  ambalo  sio  jambo la
kawaida  kwa waumini kufanya hivyo.

Mchungaji Walelaze  ilibidi  kuinuka na kusema waziwazi  kuwa  Ndugu
Shekifu umekosea  sana kwanza  ulitakiwa  kujitambua kuwa  wewe
japokuwa ni  Kiongozi  pia wewe ni mkiristu   lolote utakalo fanya
popote  pale    tambua     unamajukumu mawili kwanza  ukiristu wako
na pili   kuwa  kiongozi.   Hapa ni kanisani  ulitakiwa kuwasalimia
waashirika  kwa   salaam   yao  siyo salaam hiyo uliyoitoa hapa.

Basi  mchungaji huyo alimaliza  mtafaruku huo huku  mbunge  huyo wa
Lushoto akishuka  katika mimbari ya kanisa  hilo kwa  fedhea na
kurejea  katika kiti chake  ambacho kilikuwa  jirani na  mlango   wa
kutoka  nje  ya  kanisa.

Mara  baada ua  ibada  hiyo  ya mwaka mpaya  mbunge huyo alionekana
kuwa mtu wa  mwisho kuondoka  kanisani  mara baada ya washirika  wote
kuondoka  lakini  washirika  hao  walisema kuwa   mbunge  huyo
amekalili  kusalimia   kwa  salaam    hizo   ndiyo maana  alipitiwa.

"Mimi nilitaka    Mbunge  aombe  msamaha  kwa alilolifanya  sio
kuondoka kimya kimya  tu  hawa wanasiasa  hawana adabu kabisa wanakuja
na   mbwembwe alafu wanapata aibu."alisema mama  mmoja
aliyejitambulisha  kwa  jina moja tu la Mama  Sarah.

Mshirika mwingine alimuunga  mkono mchungaji Waleleza kwa  kumkumbusha
Mbunge  huyo  kuwa  makini sana akiwa  kanisani  na kuheshimu  salaam
 za ibada   za makanisa  sio kuja  na  salaam    za   nyumba  zingine
za ibada.

"Pengine  inawezekana Mbunge huyu  asipewe  tena  nafasi ya
kuwasalimu waumini kanisani kutokana na kosa  hili," aliserma  mzee
mmoja wa makamo ambaye  alidai kuwa hilo ni kosa  baya.

Mwishoni alionekana  Mbunge Shekifu akiingia ndani ya  gari yake
nyeupe  yenye  Bendera ya  CCM ikipeperuka  mkono wa kushoto. Ndani ya
gari hiyo   kukiwa na  akina mama  watatu ambao walionekana  wakifunga
milango na  dereva   wa gari hilo akiondoa  gari  katika eneo la
kanisa  hilo.


Wasalaam  Adeladius Makwega

--
Jobs in Africa - www.wejobs.blogspot.com
International Jobs - www.jobsunited.blogspot.com

Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com  Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma

Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.




--
Jobs in Africa - www.wejobs.blogspot.com
International Jobs - www.jobsunited.blogspot.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
 
 


--
Jobs in Africa - www.wejobs.blogspot.com
International Jobs - www.jobsunited.blogspot.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
 
 



--
Jobs in Africa - www.wejobs.blogspot.com
International Jobs - www.jobsunited.blogspot.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
 
 
--
Jobs in Africa - www.wejobs.blogspot.com
International Jobs - www.jobsunited.blogspot.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
 
 

--
Jobs in Africa - www.wejobs.blogspot.com
International Jobs - www.jobsunited.blogspot.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
 
 

--
Jobs in Africa - www.wejobs.blogspot.com
International Jobs - www.jobsunited.blogspot.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
 
 

0 comments:

Post a Comment