Juliana Shonza anahitaji kushauriwa kuwa haya anayoyafanya kisiasa yanaweza hata kumharibia kwenye level ya familia......
Ngoja tuendelee kufuatilia!
On Jan 17, 2013 8:10 AM, "Ismael Kimirei" <kiakimirei@gmail.com> wrote:
-- unfortunately sipati printed copy. Natumia online version.
On Thursday, January 17, 2013 8:12:55 AM, nevilletz@gmail.com wrote:
Mwananchi la jana kasome uone iko ukurasa wa ngapi!
Sent from my BlackBerry® smartphone from Vodacom Tanzania
------------------------------------------------------------------------
*From: * Ismael Kimirei <kiakimirei@gmail.com>
*Sender: * wanabidii@googlegroups.com
*Date: *Thu, 17 Jan 2013 08:01:28 +0300
*To: *<wanabidii@googlegroups.com>
*ReplyTo: * wanabidii@googlegroups.com
*Subject: *Re: [wanabidii] Juliana Shonza: Mimi bado ni Makamu
Mwenyekiti BAVICHA *
Meena,
Uliyoyasema juu ya Dr Slaa yanapendeza. Yanatia moyo. Ila cha
kushangaza - huyo huyo Shonza ndo mmempa ukurasa wa mbele kwenye
gazeti lenu kama alivyoomba wakati wa mkutano na wanahabari - kuwa
mkaitangaze vizuri ile habari. Kwangu mimi ile kitu ameandika
haikustahili hata kuwekwa ukurasa wa pili au wa tatu - ningeiweka
katikati huko au karibu na mwisho.
Kim
On 1/17/2013 7:36 AM, nevilletz@gmail.com wrote:
Mtu alikuwa mwanachama siku zote, leo kawekwa pembeni ndo anaamua
kusema kuhusu uozo, hapo the motive behind ni kutimuliwa kwake. Bado
ni binti mdogo, atulie atapata nafasi tena siku zijazo. Kwenda
hadharani na kuwasema viongozi wake wakuu wa Chama ni utovu wa nidhamu.
James Ole Millya alipotoka CCM kwenda Chadema hakuwahi kuwatukana
waliokuwa wakuu wake wa chama JK wala Mukama. Alieleza udhaifu wao na
udhaifu wa chama chake.
Dk Slaa ni mtu anayeaminika siyo ndani ya Chadema tu hata nje ya
chama hicho. Hana record yoyote ya ubadhirifu wa fedha tangu
alipokuwa TEC, Mbunge wala KM Chadema.
Akiwa Mwenyekiti wa LAAC alifanya kazi kubwa na hakuwahi kulala wala
kula kwa fedha za Halmashuri walikokwenda kukagua miradi, si mtoa
fedha kwa waandishi wa habari kama ilivyo kwa wanasiasa wengine,
haombi kuandikwa na vyombo vya habari bali vyombo hivyo humtafuta
kutokana na umuhimu wake.
Aliyoyafanya akiwa TEC kuanzisha Caritas Tanzania, miradi ya maji
kule Karatu na hata fedha alizoingiza pale CCBRT ni ushahid toka
kwamba siyo mbadhirifu wala mbinafsi. Mtu wa aina hii siyo rahisi
kuharibu credibility yake!
Kwa kauli za Shonza dhidi ya Dk Slaa, anajianika kwamba yeye ni mtu
wa aina gani!
Sent from my BlackBerry® smartphone from Vodacom Tanzania
------------------------------------------------------------------------
*From: * Herment Mrema <hmrema11@hotmail.com>
*Sender: * wanabidii@googlegroups.com
*Date: *Wed, 16 Jan 2013 20:37:32 +0000
*To: *<wanabidii@googlegroups.com>
*ReplyTo: * wanabidii@googlegroups.com
*Subject: *RE: [wanabidii] Juliana Shonza: Mimi bado ni Makamu
Mwenyekiti BAVICHA *
Ndugu Wanabidii,
Haya makubwa, lakini tukubali au tusikubali kama haya hayapo siasa
hakuna. Changamoto ni sisi kuchambua ni zipi mbivu na zipi mbichi.
Cheers
Herment
------------------------------------------------------------------------
Date: Wed, 16 Jan 2013 14:05:54 -0600
Subject: Re: [wanabidii] Juliana Shonza: Mimi bado ni Makamu
Mwenyekiti BAVICHA *
From: ngonzy@gmail.com
To: wanabidii@googlegroups.com
Sijui chama hakina taratibu za kushugulikia haya mambo? Yanakera
kweli kuyasoma
2013/1/16 Ireneus Kakuru Mushongi <ireneuskakurumushongi@gmail.com
<mailto:ireneuskakurumushongi@gmail.com>>
Bongo politics...!
Ngoma ya watoto haikeshi... Hivi hamna jinsi yoyote ya kumaliza
matatizo haya?
Mnadhani mnatengeza picha gani kwa mashabiki na wanachama wenu?
Nadhani mwenye timamu hatakuja kuanika mambo haya (yenu)
hadharani tena.
Kuna kubwa gani la kugombania hapa na mnamwakilisha nani?
Kwa hali hii tutarajie ngumi kwenye kikao chochote
kitakachokutanisha makundi haya..
Na huo ndio utakuwa mwisho wa Chdm. Na ushindi mwororo upande wa
pili..
Tafakari..ongozweni na busara, si jaziba matusi na maslahi binafsi..
SIjamwona aliyetumia busara hadi hapo na zaidi tutarajie makubwa
zaidi
UONGOZI UMESHINDWA KUMALIZA HAYA YA WATOTO HAWA NDANI YA CHADEMA
AU NI KWELI NAO NI SEHEMU YA TATIZO?
Siko kwa ajili ya kukosoa au kumfinger point mtu..ila nahisi hii
ni trela na kuna mengi nyuma ya pazia na isipotumika busara, ni
hatari tupu. Safari ya 2015 itabaki ndoto
Kama yale ya Mnara wa Babeli!
Ireneus
On Jan 16, 2013 11:45 AM, "Anthony Masare"
<anthony_masare@yahoo.com <mailto:anthony_masare@yahoo.com>> wrote:
Boxbe <https://www.boxbe.com/overview> This message is
eligible for Automatic Cleanup! (anthony_masare@yahoo.com
<mailto:anthony_masare@yahoo.com>) Add cleanup rule
<https://www.boxbe.com/popup?url=https://www.boxbe.com/cleanup?token%3D0W1YPooSTHaFxyy3tB519K%252BHCpV%252FigMONxLK5PYYn7guXek2LMZ7ER63%252BE5x8Kh%252FCcf6XGgdoJ9IVKmoP2YF5%252BeeR2zLRWsazm0WJ6r7rQsiXVq%252FwMzZo4zdSfX6ZKtuCpRegHBqj%252BK04Bl%252B9kiunA%253D%253D%26key%3DrF%252Fk1CEdZEzePFMmTvh4OamPeDznFfConO%252B3YtzlHcw%253D&tc=13356526385_63802074>
| More info
<http://blog.boxbe.com/general/boxbe-automatic-cleanup?tc=13356526385_63802074>
huyu dada shonza ni mnafiki mkubwa haya yote aliyosema hapa
mbona hakusema akiwa ndani ya chama?amefukuzwa ameaanza
kutapatapa tumpuuze mtu kama huyu hana nia njema na chama
naamini sasa kweli huyu mtu ni kibaraka (mamuluki)
--- On *Tue, 1/15/13, Juma Mzuri /<jumamzuri@gmail.com
<mailto:jumamzuri@gmail.com>>/* wrote:
From: Juma Mzuri <jumamzuri@gmail.com
<mailto:jumamzuri@gmail.com>>
Subject: [wanabidii] Juliana Shonza: Mimi bado ni Makamu
Mwenyekiti BAVICHA
To: "Wanabidii" <wanabidii@googlegroups.com
<mailto:wanabidii@googlegroups.com>>
Date: Tuesday, January 15, 2013, 10:05 AM
TAMKO LA KUTOA UFAFANUZI DHIDI YA TAARIFA BATILI
ZILIZOZALISHWA NA
MWENYEKITI WA BAVICHA
BWANA: JOHN HECHE [WEGESA CHARLES SUGUTA] KUHUSU KUVULIWA
UANACHAMA WA
BAVICHA, NA KUSHABIKIWA NA MH. FREEMAN MBOWE, MWENYEKITI
CHADEMA TAIFA
Nawashukuru sana wanahabari, kwakuchukua muda wenu kuja
kunisikiliza.
Natambua mnakiu ya kusikiliza mambo mengiya kuwaeleza
kutokana na
taarifa zilizosambaa kuhusu hiki
kichefuchefukinachosambazwa kwa
makusudi na virusi vichache vilivyojivika ngozi yaukombozi.
Nimepokea simu nyingi kutoka kwawatu mbalimbali kutoka
ndani na nje ya
Tanzania wakitaka kupata ufafanuzi baadaya kupata taarifa
kupitia
vyombo vya habari kuwa nimevuliwa uanachama naU-Makamu
Mwenyekiti wa
BAVICHA Taifa.Kama mlivyo ninyi, nami pianimeyasikia hayo
kupitia
vyombo vya habari, maana sijapata barua au
mawasilianoyoyote toka kwa
Mwenyekiti wa BAVICHA, Ndugu Wegesa Suguta (John
Heche)aliyetoa tamko
hilo.Kwanza kabisa naomba kuweka wazikwamba sijawahi pewa
shutuma
zozote au mashitaka yoyote yale yanayohusiana nahicho
alichokiongea.
Niliamua kupuuzia kwa sababunamjua Heche ni mlopokaji,
kiongozi
asiyejua wajibu wake, anayetumikiawasiomchagua, mtu asiye
na malengo
na mtegemezi wa siasa ili kuendesha maishayake na ya
familia yake. Pia
nilimpuuza kwa sababu najuasio Mwenyekiti aliyechaguliwa
kidemokrasia,
aliwekwa kwa matakwa ya wakubwazake ambao wanamtumia kwa
malengo
yaliyokusudiwa, ikumbukwe kuwa vijana watatu,Habibu
Mchange, Mtela
Mwampambwa na Grayson Nyakarungu walienguliwa
kimizengweili Heche
ashinde, hivyo kwetu sisi yeye ni sawa na Mwenyekiti wa
kuteuliwa.Hivyo sikumjibu mtu asiyekuwa na sifa sawa na
zangu katika
harakati za kusakademokrasia ya kweli.
Lakini kitendo cha Mwenyekitiwangu, Mh. Freeman Mbowe
kujitokeza
kupitia gazeti mojawapo na kudai madaiyangu ni ya kitoto,
kwanza kimenifedhehesha, ni dharau kwa vijana
walionionanina sifa na
ukomavu na kunipa kura nyingi ili niwe Makamu Mwenyekiti
waBAVICHA
Taifa.
Pili ni kama anahalalisha kikaobatili, kilichokiuka
kanuni na katiba
ya CHADEMA ili kuhalalisha matakwa yaoyenye lengo la kuminya
demokrasia na uhuru wa kujieleza ndani ya chama.
Tatu anahalalisha hoja za vijana,ambazo ndio uhalisia
kuwa Heche
hakuwa na sifa, na uwezo, hivyo alibebwa na Mh.Mbowe ili
akae pale kwa
malengo yake.Ndio maana nilisema ukionakifaranga
kimepanda juu ya figa
ujue mama yake yuko chini, hivyo mama yakekifaranga
kajitokeza
kuhalalisha kifaranga chake kupanda juu ya figa.
MADAI YAALIYODAI MH. MBOWE KUWA NI YA KITOTONiseme wazi
kwamba
nimesikitishwamno na madai aliyoyatoa Mwenyekiti wangu wa
CHADEMA Mh
Freeman Mbowe kupitiagazeti la Mtanzamia la tarehe
12/01/2013 kwamba
madai yangu ni ya kitoto .
Kwanza niweke wazi kabisa kwambanamuheshimu sana Kiongozi
wangu huyu
mkuu ambaye ndiye alipaswa kuwa mstari wa mbele katika
kuhakikisha
kwambahaligawi baraza la Vijana na chama kwa ujumla,
ahakikishe kuna
utawala borandani ya chama, na utendaji haki, lakini cha
kushangaza
ameibuka kumtetea Hechekwa hoja za mwegemeo wa upande
mmojabila
kuangalia maelezo ya upande wa pili.
Niweke wazi kabisa kwamba kaulialiyoitoa dhidi yangu ni
yakiushabiki
maana kama ni madai yangu kuhusu namna
ninavyohujumiwakupitia kwa
Katibu Mkuu yeye anayo nakala ya malalamiko [ushahidi upo],
lakinihakuna hatua ambayo ameichukua.
Namshangaa Mwenyekiti kudai madaiyangu ni ya kitoto sasa
sijui ni
madaiyapi anayazungumzia ? madai ya kitoto ni yapi? na
madai ya
kikubwa ni yapi ? naje madai ya kitoto ni haya mimi
kuhoji kwanini
hatuweki akiba kwenye akauntikwa ajili ya uchaguzi 2015 kama
tulivyokubaliana kwenye baraza kuu mara baadaya uchaguzi wa
2010.Naombaniwajulishe wanachadema kuwa, nimejitahidi
sana kushauri
juu ya
1; Uanzishwaji wa chuo chamafunzo ya uongozi kwa makada
wa CHADEMA ,
badala yake ni matumizi mabaya yafedha za ufadhili wa
wadau tofauti na
hasa mfadhili mkuu ndugu SABODO. Hiiingesaidia pia kulea
ki-mfumo wa
maadili ya uongozi kwa vijana wa umoja wawanafunzi wa
CHADEMA wa vyuo
vikuu yani " CHASO" ambapo mimi ni mwasisi wamkakati huu
nchini.
2; Chama kwa ujumla kutokuwa na jengo letu na hasa makao
makuu yetu.
Niaibu kwa chama kikubwa kama CHADEMA kuwa na ofisi
tulizopanga na
kulipa mamilioni ya fedha za ruzuku na misaada kwa manufaa ya
Mwenyekiti Freeman Mbowena Mkurugenzi wa fedha wanaomjua
mmiliki wa
jengo la makao makuu. Kimsingi mimi natambua chama kina
uwezo mkubwa
wa kuwa na majengo yetu.
3; Kupunguza mshahara wa katibumkuu Ndugu Dk. Slaa ambao
ni zaidi ya
milioni saba kwa mwezi na marupurupu kibao ili pesa hizo
na mamilioni
zielekezwe kujenga chama mikoani kama kweli tunataka2015
tuingie
Ikulu.
4; Kuhakikisha pesa zilizochangishwa kwenye M4C
zinatumika ipasavyo na
si kama zitumikavyo kipindihiki ambapo ni kama tumelewa
wingi wa watu
kwenye mikutano ya hadhara.
5; Kitendo cha Mwenyekiti wa chama kufumbia macho hatua
ya ndugu Slaa
(katibu mkuu) kujikopesha pesa ya ruzuku ya watanzania
zaidi ya
shilingi milioni mia na arobaini.
6; Hatua ya mwenyekiti ndugu Heche kulipwa mshahara na
marupurupu hali
kanuni za chama haziruhusu huku Mbowe akifumbia macho
wakati viongozi
wa mikoa na wilaya hawapewi pesa na vifaa vya uenezi.
7; Kitendo cha mchumba wa Dk.Slaa, Josephine Mushumbusi
kuzunguka
mikoani na kulazimisha kupokelewa kama mke wa mfalme na
kuendesha
vikao vya ndani na mikutano ya hadhara yenye kulenga
kuwajenga
wagombea ubunge anaowataka yeye na katibu mkuu kwa mwaka
2015.
Ndugu wanahabari, je hizi ndo hojaza kitoto anazodai Mh.
Mbowe? Hivyo
basi namtaka Mh. Mbowe sasa asikimbiliekujibu hoja
kiushabiki.
Ajitahidi kuwa na fikra na Busara ili kukisaidia chama
kuvuka kwenye
daraja la sasa la pepo kufukuzana. Atambue Baraka
anazozitoa wanachama
wafukuzwe hovyo na kunyanyaswa ni hatari kwa kuwa
anaandaa kundi kubwa
nje ambalo litageuka mwiba siku za usoni.
UHALISIA ULIOPO:
Ndugu waandishi wa habari,
Naomba kuweka wazi kwamba mimi Juliana Shonza ni Makamu
Mwenyekiti
halali wa baraza la vijana (BAVICHA). Taarifa zozote zile
mlizozisikia
kuhusu kuvuliwa kwangu uanachama, naomba kwa nguvu moja
kupitia
taaluma yenu muwaambie watanzania kwamba wazipuuze. Ni
taarifa
zilizotolewa na kikundi cha kihuni kilicholenga kutimiza
matakwa ya
wakubwa wao. Kikundi hicho hakina mamlaka ya kikatiba
yoyote yale ya
kunivua uongozi huunilio nao.
Kuthibitisha hilo kuwa ni kikundimufilisi, hadi
ninapoandika waraka
huu kwenu sijapewa barua yoyote ile inayonitaarifu kuwa
nimevuliwa
uongozi wangu. Hii ni wazi wanatambua kuwa wanachemka,
wanatengeneza
makundi kwa maslahi wanayoyaona yanawafaa.
Sikuchaguliwa ili niwe chombo cha kuwatumikia watu, na
badala yake
nilichaguliwa ili niwatumikie vijana waCHADEMA na
watanzania kwa
ujumla, na pale nilipoona kuna ukiukwaji na kuhoji ndio
chanzo cha
mizengwe na matamko ya Ndugu Wegesa (John Heche).
Nimekuwa nikiwasumbua viongozi wenzangu kuhusu
kutengeneza kadi za
BAVICHA na kusajili wanachama katika mfumo mzuri
(database) ili tuwe
na kumbukumbu ya wanachama wetu lakini yote
yameshindikana kwasababu
amekuwa akiendeshwa na mfumo dume kandamizi kwa mwanamke,
mara nyingi
nimemshauri kwa ajili ya maendeleo ya Baraza na nimekuwa
nakwamishwa
na Mwenyekiti na Katibu na hata leo sisi wote ni
wanachama kwa
kufikirika (imagination), kwa kuwa bado hatuna kadi za
uanachama kwa
vijana wa BAVICHA zaidi ya kutambulika na katiba ya chama.
KUKIUKWA KWA KATIBA
Ndugu wanahabari, ni wazi kuwakatiba pamoja na mwongozo
wa baraza letu
la vijana bavicha ulikiukwa katikakikao walichokiita
kamati tendaji
iliyokaa tarehe 05/01/2012 ambayo iliongozwa na Bwana
Wegesa Suguta
(John Heche) kama Mwenyekiti, hali inayonilazimu kusema
wazi, bila
kumung'unya maneno kwamba maamuzi yaliyotolewa na kikao hicho
yalikwishapangwa na viongozi wa kitaifa hayakuwa halali.
Nasisitiza
kwamba ni ukweli ulio wazi kwamba agenda na maazimio ya
kikao hicho
yalikwisha amuliwa hata kabla ya kikao hicho kwasababu
kubwa mbili:
1; Taarifa za kufukuzwa kwetuzilikwisha anza kusikika
kwenye mitandao
ya kijamii kama vile jamii forum nafacebook mwezi mmoja
kabla ya kikao
cha kamati tendaji batili.
2; Pili ushahidi wa kimazingirakwa maana ya ukiukwaji
mkubwa wa
kikatiba na mwongozo wa Baraza letu la Vijana uliofanyika
siku ya
kikao.
Ndugu wanahabari,
Ikumbukwe kuwa pamoja na uwepo wa taarifa za kikao mwezi
mmoja kabla
binafsi nililetewa taarifa hizo siku mbili kabla ya
kikao, tena kwa
njia ya ujumbe mfupi wa maandishi {sms} na baadae
kupigiwa simu na
Katibu wa Baraza Bwana Munishi ikinitaka kuhudhuria kikao
hicho
kutokana na kuwa nje ya Dar-es –salaam kwa mambo ya
kifamilia zaidi
niliwataarifu viongozi wenzangu kwa utaratibu maalumu wa
mawasiliano
ya kiuongozi kwa maana ya kuwatumia barua ya udhuru wa
kutohudhuria
kikao.
Lakini cha kushangaza na kustaajabisha kwa viongozi
wenzangu hawa
ambao kwa namna moja ama nyingine napata ugumu wa kuelewa
kama kweli
wana sifa za kuitwa viongozi tena wa idara nyeti sana
katika ustawi wa
chama chetu, kwa makusudi kabisa ama kwa kutumwa kufanya
hivyo ama kwa
utashi wao mdogo wa kiupembuzi yakinifu waliamua kuvunja
na kukiuka
katiba ya chama na kujipa vyeo vya kiunyampara kwa kuamua
kuchukua
maamuzi ya kutuvua uanachama wa kufikirika wa baraza mimi
na vijana
wenzangu Ndugu Mwampamba na Mchange ambao nao hawakupewa
nafasi ya
kusikilizwa, ambao moja kwa moja tunapoteza sifa yakuwa
wanachama wa
CHADEMA.
Ndugu wanahabari,
Naomba sasanijikite katika katiba ya chama changu na
mwongozo wa
baraza la vijana sura ya sita kipengele cha 6.5 ambacho
kinasema
taratibu zifuatazo lazima zifuatwe katika kuchukua hatua
za kinidhamu.
6.5.2 kwa mujibu wa ibara 5.4.3 na .4.4 ya katiba, mwanachama
yeyotehatachukuliwa hatua za kinidhamu ama kuonywa ama
kuachishwa ama
kufukuzwa uanachama bila kwanza
{a} kujulishwa makosa yake kwamaandishi na kutakiwa kutoa
majibu
katika muda usiopungua wiki mbili.
[b] kupewa nafasi yakujiteteakatika kikao kinachohusika.
{c} Mwanachama atajulishwa kwamaandishi uamuzi wa kikao
mnamo wiki
mbili baada ya kusikilizwa.
Ndugu waandishi wa habari,Nisemewazi kwamba hakuna kifungu
kilichofatwa kati ya hivyo niliyoviainisha hapo
juu,hakuna barua
yeyote niliyojulishwa ya hayo waliyoyaita mashitaka yangu
zaidi ya
kuyasoma na kuyasikia kwenye vyombo vya habari baada ya
wao na kikao
chaoharamu kuchukua maamuzi yakunivua uanachama wa Bavicha .
Sikupewa nafasi yakujitetea maanasikuwepo kwenye kikao,
barua ya
udhuru wakutohudhuria walikuwa nayo. Na vilevile mpaka
leo hii
sijajulishwa kwa maandishi uamuzi wa kikao hicho batili
badaa yake
viongozi wenzangu hawa wameamua kuujulisha umma wa
Watanzania na
wanachadema kwa ujumla pasipo kunijulisha mimi kwanza.
Ukiangalia pia
kifungu cha 6.5.6 cha katiba kinasema KIONGOZI YEYOTE
hatachukuliwa
hatua za kinidhamu bila kwanza kupewa mashitaka kwa
maandishi na
mamlaka husika na kupewa nafasi ya kujibu kwa maandishi.
Sasa basi namtaka Bwana Wegesa Suguta awaeleze umma wa
watanzania kama
alivyokurupuka kuwaeleza kwamba Shonza amevuliwa
uanachama wa Chadema
ni wapi na lini yeye kama Mwenyekiti nilipewa barua ya hayo
wanayoyaita mashitaka, na ni lini niliwapa majibu ya
mashitaka hayo.
UHALALI WAKIKAO CHA KAMATI TENDAJI
Ndugu wanahabari,
Ikumbukwe kwambakikao cha juu kuliko vyote kwenye ngazi
ya chama
husika ni Mkutano Mkuu ambao ndio ulioniweka madarakani
kutokana
nakuwa na imani na mimi na kikatiba ndiohaswa ulipaswa
kuniandikia
mashitaka, kunijadili, kunihoji na kutoa maazimio ambayo
yangepelekwa
kamati kuu ambao kimsingi ndiyo yenye mamlaka ya mwisho
yakumvua mtu
yeyote uanachama wake baada ya kujiridhisha na taarifa na
uchunguzi
kutoka kwenye kikao husika kilichomwandikia mwanachama
mashitaka na
kumuhoji.
Ndugu wanahabari ifahamike wazikwamba kikatiba kuna ngazi
mbili tu
zinazoweza kumvua mtu uanachama wake ambazoni ngazi ya
tawi na ngazi
ya kamati kuu.
Hivyo basi namtaka sasa Bwana Wegesa Suguta auambie umma
wa watanzania
kwamba ni lini kamati tendaji ya vijanailigeuka ama
kukaimishwa
madaraka ya ngazi ya tawi, ngazi ya mkutano mkuu
amakamati kuu yakuwa
na uwezo wakumvua kiongozi uanachama wake?
Ndugu waandishi wa habari,
Wajumbe wa kamati tendaji kikatiba ni makatibu wa kamati
za uratibu za
mikoa lakini badala yake Bwana Wegesa Suguta (John Heche)
amekuwa
akiwaita wenyeviti wamikoa na sababu kubwa ikiwa ni
kwamba wengi wa
wenyeviti hao hawastahili kuwepobavicha kutokana na
kwamba umri wao
kuwa zaidi ya miaka 35 hivyo kupoteza sifa za kuwa
viongozi wa BAVICHA
ambayo katiba inamtaka mwanabavicha yeyote kuwa namiaka
18-35, hivyo
basi kwa kuhofia kupoteza nafasi zao hulazimika
kukubaliana na lolote
lile ambalo bwana Wegesa Suguta analitaka hata kama
wakijua kwamba ni
kinyume kabisa na matakwaya katiba na mwongozo wa baraza.
Hivyo kumpa Heche mwanya wakuamua lolote lileanalotaka
ama kutumwa
kulifanya. Kutokana na hilo natangaza wazikwamba kikao
cha kamati
tendaji kilichopita ni batili, chenye wajumbe batili,
kimesimamiwa na
viongozi batili kwa maana ya mwenyekiti na katibu wake maana
wameshindwakuheshimu misingi ya kikatiba katika namna ya
demokrasia ya
chama chetu hivyo basi nachukua nafasi hii kuutangazia
umma wa
watanzania na wanachadema kwa ujumla wao kwamba maamuzi
ya kamati
tendaji yaliyotangazwa na kiongozi kilazana daraja la
viongozi wa juu
bwana Wegesa Suguta ni batili.
Ndugu wana habari,
Sifa ya Mwalimu ni kuweza kubadilisha hali ya umbumbumbu
wa wanafunzi
wake, Heche kama kiongozi, na Mwalimu kitaaluma (nina
wasiwasi na
ufaulu wake katika huo ualimu) alipaswa kuwa mfano bora
kwa vijana wa
Chadema kuwaelekeza na kuwafundisha namna ya kuheshimu
misingi ya
kikatiba ambayo kama chama na baraza tumejiwekea na
tunapaswa kuifuata
ni wazi kuwa Heche ameshindwa kuwa mfano bora kwa vijana,
hajui kanuni
za BAVICHA wala katiba ya CHADEMA, mkurupukaji,
mropokaji, mwenye
uwezo mdogo wa kufikiri, dikteta anayetumia mamlaka
asiyokuwa nayo
(akipewa mamlaka atatuchinja huyu) hivyo hafai kuwa hata
Mwenyekiti wa
serikali za mtaa, wala kuaminiwa popote kupewa nafasi ya
kiuongozi. Ni
wazi ubongo wake yeye nakatibu baraza bwana Munishi
haujapewa tohara
la kisiasa, ifike mahali wakubali kufundwa unyagoni na
manyakanga wa
kisiasa.
KUHUSUKUVULIWA UANACHAMA WA BAVICHA;
Ndugu wanahabari,
Kuhusu kuvuliwauanachama wa Bavicha ambao moja kwa moja
napoteza sifa
ya kuwa mwanachadema namshangaa kiongozi huyu ambaye sifa
yake kuu
siku zote ni ukurupukaji kwa kusema kwamba nimevuliwa
uanachama wa
Bavicha huku akijua wazi Bavicha haijawahi kuwa na kadi
za baraza.
Katika mwongozo wa baraza lavijana kipengele cha 4.4
KUJIANDIKISHA
UANACHAMA 4.4.1 inasema ili kijanaaruhusiwe kujiunga
bavicha ni lazima
awe na sifa zifuatazo
[a] Awe mwanachama wa CHADEMA
[b] Awe na umri kati ya miaka 18 na 35
[c] Awe anakubaliana na misingiya mwongozo wa BAVICHA
4.4.2 Inasema kijana aliyekidhimatakwa hayo hapo juu,
atanunua kadi ya
uanachama wa BAVICHA
Kutokana na kipengele hicho namtaka bwana Wegesa Suguta
auambie umma
wa watanzania na wanaCHADEMA kadi yake yeye ya baraza la
vijana ni
namba ngapi na aliichukulia wapi? Aueleze umma wa
watanzania kadi
yangu ya baraza la vijana ni namba ngapi na niliichukulia
wapi?
Ndugu waandishi wa habari,
Nidhahiri baraza la vijana chadema hatuna kadi ambayo
kimsingi ndiyo
utambulisho wa mwana BAVICHA endapo akishakidhi sifa
zilizoainishwa
hapo juu. Na ni wazikwamba vijana wote wa CHADEMA tuna
sifa za kuwa
wana Bavicha lakini si wanachama wa BAVICHA kutokana na
kwamba
nimekuwa nikimwambia mara kwa mara umuhimu wa kuirasimisha na
kuianzisha ili iwe taasisi kamili kwa kuwa na kadi za
vijana kama
mwongozo wa vijana unavyojieleza.
UELEWA WANGU KUHUSUKUNDI ANALOLIITA NDUGU WEGESA SUGUTA
(JOHN HECHE)
NI "MASALIA"
Ndugu waandishi wa habari,
Hakuna kundi linaloitwa masalia ndani ya Chadema na
BAVICHA. Gazeti la
MWANAHALISI ndilo lililoandika kuwa vijana wote waliofutwa na
kuondolewa kwenye uchaguzi wa BAVICHA mwaka 2011 ni
MASALIA ya Zitto
yanayopukutishwa Chadema. Kimsingi gazeti hili lilikuwa
linafanya kazi
yake ya kipropaganda ndani ya CHADEMA ili kukigawa Chama.
Lilikuwa
linatimiza wajibu wake wa kupika mpasuko ndani ya chama
tena kwa
kuhusisha na viongozi wakubwa ndani ya chadema.
Ni aibu kubwa sana na ni hatari kuona kiongozi kama
Wegesa Suguta
anakuwa mstari wa mbele kushabikia neno masalia, huku
akijua wazi
kufanya hivyo ni kuligawa baraza la vijana. Kwa nguvu
moja nalaani
kitendo hiki cha kipuuzi kinachofanywa na Mwenyekiti huyu
wa BAVICHA
cha kuchekelea upuuzi uliopikwa na gazeti la MwanaHalisi.
Naomba
atumie rasilimali za chama kujenga umoja wa vijana imara,
tushirikiane
kuimarisha Bavicha yenye tija kwa chama na sio kusherekea
mpasuko
ndani ya baraza la vijana.
UELEWA WANGU KUHUSU KITU KINACHOITWA PM7
Ndugu waandishi wa habari,
Naomba kunukuu maneno ya mtu maarufu sana mitandaoni na
kwenye uga wa
habari Mzee Mwanakijiji anasema
"Uongozi imara sio kutegeana, kunyemeleana na kufukuzana.
Uongozi
imara ni kushirikiana".
PM7 ni jina lenye maana ya "PATRIOTIC MOVEMENT" yaani
harakatiza
kizalendo kwa mujibu wa Ndugu Ben saanane ambaye alitumwa
na kiongozi
wa juuwa chama kuja kulitekeleza kwa vijana walioenguliwa
kwenye
uchaguzi wa BAVICHAmwaka 2011 na wanaoonekana kusigana na
kiongozi
huyo kimawazo. PM7 ni wazoliliobuniwa na kiongozi mmoja
wa juu wa
chama akishirikiana na Ben saanane wakinuia kutega mtego
wa kuwanasa
vijana wanaoonekana wapo tofauti kimawazo nakiongozi huyo
wa chama.
Kwa kuwa wazo hilo lilikuwahalina manufaa kwa chama,
halikutekelezwa.
Kiongozi huyo bila kumung'unya maneno ameamua kuwatumia
vijana hao
kuandaa kikao batili cha kamati tendaji ya John Heche ili
awafukuze
vijana hao. Hii ni hatari sana kuona kiongozi wa chama
unageuka simba
na kuanza kuwawinda watoto wake ili uwamalize kisiasa kwa
sababu zako
binafsi.
MAAJABU KATIKAMEDANI ZA SIASA ZA BAVICHA MWAKA 2013
Ndugu waandishi wa habari,
1. Hii ni ajabu sana katika kikaocha kamati tendaji
batili, Ambao
hatukuhojiwa ni watu wawili, mimi Juliana Shonzana kijana
mmoja
anaitwa Exaud Mamuya. Lakini Mimi Juliana Shonza
nimehukumiwa bila
hata kusikilizwa wala kupewa mashitaka na chombo chochote
katika
chama. Wakati huo huo Exaud Mamuya hajahukumiwa kwa madai
hakufika
kwenye kikao. Hii ni dhahiri huu ni mkakati wa kipuuzi ambao
unaendeshwa na watu wapuuzi tena kwa misingi ya kikabila
na kikanda.
2. Muasisi mwenza wa PM7 na kibaraka wa kiongozi wa juu
wa chama
aliyetumika kutoa shutuma chafu kwa Naibu Katibu Mkuu. Kijana
anayefahamika kwa jina la Ben Saanane ameachwa kwa madai
yeye amekiri
mbele ya hiyo kamati tendaji kwamba ni kweli alinuia
kumchafua Naibu
Katibu Mkuu wa chama na kukivuruga chama. Wakati tuhuma zake
zinafananana za Mchange na Mwampamba.
3. Mkakati wa John heche navibaraka wake umejikita
kutukuza ukanda
ndani ya chama tena wa wazi wazi.Ukanda huu
umejidhihirisha kwenye
kutoa hukumu batili za tuhuma kama ifuatavyo.
Vijana waliohukumiwa wote niwale wanaotokea Mbeya, Mbozi
na Kibaha.
Wakati Vijana wa Kilimanjaro wameachwa kwa madai wao wametoa
ushirikiano.
Waliohukumiwa ni:
_Mtela Mwampamba-Mbozi, Mbeya
_Habib Mchange-Kibaha, Pwani
-Juliana Shonza-Mbozi, Mbeya
-Joseph Kasambala – Mbeya mjini (kasimamishwa)
- GWAKISA Mwakasendo –Rungwe, Mbeya (kasimamishwa)
Pamoja na wanachama watatu waliopo Mbeya mjini waliofukuzwa
uanachama.
Waliosamehewa ni:
_Ben saanane-Kilimanjaro
_Exaud Mamuya-Kilimanjaro.
Hii ni dhamira ya wazi kabisa kwamba CHADEMA sasa ni
chama cha
kikanda, Viongozi wa CHADEMA wanatumika kutangaza ukanda kwa
watanzania.
Kwa maana hiyo wale wote wasio wa kaskazini ndani ya Chadema
tusitegemee kutendewa haki.
MAMBO NILIYOMSHAURI HECHE NA KUMUONYA:
Ndugu waandishi wa habari, Sisikama vijana tusigeuze
siasa kuwa ajira
wala chombo cha kuendeshea maisha, ni moja ya vikwazo
katika kukuza
demokrasia ya kweli, maana wengi wanaendekeza njaa na
uhitaji wa
maisha yao ili kupindisha ukweli.
Moja ya maswali yangu kwa Mwenyekiti ni kitendo cha
kubinafsisha gari
alilotoa Naibu Katibu Mkuu kwa ajili ya BAVICHA na badala
yake
akalifisadi, akafanya mali yake binafsi na kumuweka Mdogo
wake Chacha
Heche kuwa dereva wake, nimekuwa nikipinga matumizimabaya ya
rasilimali hiyo kwa manufaa binafsi, na badala yake gari hiyo
ifanyekazi iliyokusudiwa, huu ni msingi wa kuonyesha
tofauti yetu na
wanaotumiarasilimali za serikali (Taifa) kwa manufaa
binafsi nay a
familia zao.
Pia nilimshauri Mwenyekiti awe nakipato halali kama
katiba ya chama
inavyosema Sura 10 MAADILI YA VIONGOZI ibara ya 10
kifungu cha (6)
kinasema Kiongozi anatarijiwa kujitosheleza yeye
nafamilia yake kwa
mapato halali ili kutokuwa ombaomba kwani tabia hiyo
itadhoofisha
uwezo wake wa kutoa uamuzi sahihi, ili kuwa mfano bora
wauwajibikaji
kwa vijana, kama ambavyo Mwalimu Nyerere alivyosema
kipimo cha Utuni
kufanya kazi, badala yake ametelekeza taaluma ya ualimu,
aliyotumia
pesa za walipa kodi kwa kusoma na muda wote ni kupiga
soga bila
uzalishaji na kujipatia kipato halali, na badala yake
anategemea
mshahara usio halali kuishi, ni wazi Mwenyekiti ni cheo
cha kisiasa na
hatakiwi kulipwa mshahara, wala kulipiwa nyumba kwa
mujibu wa kanuni.
Badala yake majibu anafikiri ni kufanya njama na
waliopindisha
taratibu hizo ili alipwe mshahara kwa maslahi yao ya
kisiasa. Na
tumekuwa tukilipinga hilo kwani tunataka tuwe mfano wa
utawala bora
kwa vitendo na si maneno peke yake.
MWISHO:
Ndugu waandishi wa habari,
Nipokwenye mchakato na wanasheria wangu kushughulikia
swala la
kumpeleka mahakani Bwana John Heche na gazeti la Tanzania
Daima toleo
namba 2958 kwa kuniita msaliti wa CHADEMA, natumiwa na
CCM na kuwa
nina mahusiano (natumiwa) na Wassira tena bila kunihoji
mimi Juliana
Shonza. Kwa maana hiyo wamenichafua na kunidhalilisha
mbele ya umma wa
watanzania.
Pili naomba kuweka wazi kwambanatarajia kuomba ufafanuzi
wa kikatiba
juu ya shutuma zilizotolewa kwenye vyombo vya habari
dhidi yangu na
bwana Wegesa Suguta (John heche) ili aseme ni aminisho
lipi la
kuthaminisha na kusakidikisha mtazamo wa maono yake ili
bongo za
watanzania zijue ukweli. Mimi Makamu Mwenyekiti wa
BAVICHA natangaza
rasmi Mtela Mwampamba na Habib Mchange ni wanachama hai
na halali wa
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).
Hivyo nawaomba waendelee na kazizao za ujenzi wa chama
kwenye majimbo
yao na taifa kwa ujumla. Nawaomba wananchi na wanachama
wote wa
CHADEMA waendelee kuwa na imani dhidi ya vijanahawa. Kama
mlivyomwamini Mwampamba na kumpa kura 32000 na kama
mlivyo mwamini
Mchange na kumpa kura 10,400 kwenye uchaguzi wa Ubunge
mwaka 2010.
Vivyo hivyo naowaombamuendelee kushirikiana nao
kuhakikisha wanatimiza
adhima ya ukombozi mwaka2015.
Wenu katika ujenzi wa demokrasia makini
Juliana Daniel Shonza
M/Kiti BAVICHA-Tanzania Bara.
--
Jobs in Africa - www.wejobs.blogspot.com
<http://www.wejobs.blogspot.com>
International Jobs - www.jobsunited.blogspot.com
<http://www.jobsunited.blogspot.com>
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com
<http://us.mc1411.mail.yahoo.com/mc/compose?to=unsubscribe%40googlegroups.com>
Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole
responsibility for any legal consequences of his or her
postings, and hence statements and facts must be
presented responsibly. Your continued membership
signifies that you agree to this disclaimer and pledge to
abide by our Rules and Guidelines.
--
Jobs in Africa - www.wejobs.blogspot.com
<http://www.wejobs.blogspot.com>
International Jobs - www.jobsunited.blogspot.com
<http://www.jobsunited.blogspot.com>
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com
<mailto:wanabidii%2Bunsubscribe@googlegroups.com> Utapata
Email ya kudhibitisha ukishatuma
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility
for any legal consequences of his or her postings, and hence
statements and facts must be presented responsibly. Your
continued membership signifies that you agree to this
disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
--
Jobs in Africa - www.wejobs.blogspot.com
<http://www.wejobs.blogspot.com>
International Jobs - www.jobsunited.blogspot.com
<http://www.jobsunited.blogspot.com>
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com
<mailto:wanabidii%2Bunsubscribe@googlegroups.com> Utapata Email
ya kudhibitisha ukishatuma
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for
any legal consequences of his or her postings, and hence
statements and facts must be presented responsibly. Your
continued membership signifies that you agree to this disclaimer
and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
--
Jobs in Africa - www.wejobs.blogspot.com
International Jobs - www.jobsunited.blogspot.com
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha
ukishatuma
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any
legal consequences of his or her postings, and hence statements and
facts must be presented responsibly. Your continued membership
signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by
our Rules and Guidelines.
--
Jobs in Africa - www.wejobs.blogspot.com
International Jobs - www.jobsunited.blogspot.com
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha
ukishatuma
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any
legal consequences of his or her postings, and hence statements and
facts must be presented responsibly. Your continued membership
signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by
our Rules and Guidelines.
--
Jobs in Africa - www.wejobs.blogspot.com
International Jobs - www.jobsunited.blogspot.com
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha
ukishatuma
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any
legal consequences of his or her postings, and hence statements and
facts must be presented responsibly. Your continued membership
signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by
our Rules and Guidelines.
--
Jobs in Africa - www.wejobs.blogspot.com
International Jobs - www.jobsunited.blogspot.com
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha
ukishatuma
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any
legal consequences of his or her postings, and hence statements and
facts must be presented responsibly. Your continued membership
signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our
Rules and Guidelines.
--
Jobs in Africa - www.wejobs.blogspot.com
International Jobs - www.jobsunited.blogspot.com
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha
ukishatuma
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any
legal consequences of his or her postings, and hence statements and
facts must be presented responsibly. Your continued membership
signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our
Rules and Guidelines.
--
Jobs in Africa - www.wejobs.blogspot.com
International Jobs - www.jobsunited.blogspot.com
Kujiondoa Tuma Email kwenda wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
Jobs in Africa - www.wejobs.blogspot.com
International Jobs - www.jobsunited.blogspot.com
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
0 comments:
Post a Comment