Tuesday 15 January 2013

Re: [wanabidii] JAMANI WAMAMA JIHADHARINI NA KIM


Lakini tufahamu pia kuna watu wanaweza wakamzoea mtu fulani maarufu au mzuri na kujidai au kujisifu kwa wenzao kuwa fulani ni bibi yangu. Hasa wanawake huwakuta haya kama njia ya kuwadhalilisha au kujigamba kuwa ni wangu. Wengine kujisifu mpaka mambo ya ndani na mtu huyo.

Ninakumbuka kuiona kitu ya namna hii in 1970s ya kijana kujidai kuwa msichana fulani wa college fulani ambaye alikua beautiful ni wake. Aliipataje sijui picha yake wakiwa chuoni (labda alipopamba wakati wa birthday kama ilivyokuwa zama hizo ndio ilikuwa fashion kupamba picha zako siku ya sherehe ya birthday yako) akawa anaionyesha jeshini. shoga zake wakamtonya. Ilipokuwa intake yao inaingia yetu inakaribia kutoka mdada alimpa kisago kijana huyo mbele za watu kufuta uongo wake. Mwana dada wa kigogo alikuwa mzuri ile mbaya.

Ni hivi inaonekana hapa kumdhalilisha Dr Mwele Malecela-mwanamke kiongozi, beautiful and intelligent. Hata kama alikuwa na urafiki naye hakuna atakayeweza kuthibitisha ukweli ila hao wawili. Mbona wapo watu wanaojidai kwa kutumia majina ya wakubwa na wakaaminika na wakatapeli watu wengine kumbe hata huko ikulu hawajulikani, kutwa kujidai kwa story za udugu na Mh Kikwete, au urafiki na Ridhiwani au kuwa yeye ni mtoto wa Mkulima PMO toka Rukwa au yeye ni shushushu au police na akafanikiwa kuibia watu kwa kuwatisha au kuwashawishi-baadae akakamatwa ukweli ukajulikana na wengi wakatapeliwa namna hii TZ.  Watu wameuza majumba si yao kwa mpango akaingia humo kimpango, akapata dalali wakaiuza na kumtia mtu hasara mnunuzi. Mwenyewe anamalizia kujenga ahamie anakuta mtu anadai ni yake aliinunua kesi zinaanza.

Hata Ukiwa unasoma Ulaya-upo mtindo wa hasa vwenzetu kutoka Nigeria kila mmoja kujidai kuwa baba yake ni Balozi nchi fulani ili kuwakoga wengine toka africa na wale wa ulaya. Hii ilikuwa inashangaza maana nchi moja ya Nigeria inakuwa na mabalozi zaidi ya 4 nchi moja maana kila ajisifuye ni baba au mjomba wake balozi nchi hiyo hiyo!! ilitumika kuwapata wasichana wa kizungu na waafrika. Hata waliokuwa na ndugu zao baadhi ya Mawaziri bongoland waliokuwa wakitumia vibaya nyadhifa hizo baadhi yao mmojawapo alifungwa USA-North Carolina na kutenganishwa na familia yake kwa vurugu za kuendesha gari hovyo, kula bangi, kupigana, kuzoa mabibi akiwa married akikamatwa-mimi mdogo wake waziri fulani TZ (akiwa wakati huo waziri wa mambo ya ndani).

Hii ya Huyu Kim anaweza kumzoea kiongozi fulani akamsaidia kwa nia ya kujikuza na kutumia jina vibaya. Ingefaa akamatwe. Ila tujifunze matukio haya tuachane na urafiki na watu ambao hakieleweki. Utamuazima gari baada ya yeye kukueleza shida au tukio ikawa nongwa ikatumika kama tangazo la mapenzi kati yenu kumbe si kweli. Au akakupa lift na kukushusha ikaonekana ni wako kwa yeye kujidai-si mnamuona ninamshusha daily? Uswahili na utapeli wa kimataifa!!

Unaweza ukakuta hata wadada wanapigana ngumi-kisa kugombea mwanaume aliyekaa meza fulani wanaempelekea bia kila mmoja akitegemea atakuwa wake ambapo mwenyewe hana mpango na mtu akiwachekea tu na kuwapa offer au tip nzuri kuwasaidia. wao wakaanza ngumi na kugombania bwana.

Aliyeweka suala la Mwele humu ana lake jambo-chuki naye au kitu gani? Anauhakika 100% na hayo ya wengine aliyoyaandika? Story isije ikamgeuka. Maana wengine husimama jukwaani na kuongea kwa uhakika kumbe alipewa story tata ili kummaliza anakuja kulipa mamilioni for damages. Mungu atuepushe na maovu.


--- On Tue, 15/1/13, A S Kivamwo <kivamwo@yahoo.com> wrote:

From: A S Kivamwo <kivamwo@yahoo.com>
Subject: Re: [wanabidii] JAMANI WAMAMA JIHADHARINI NA KIM
To: "wanabidii@googlegroups.com" <wanabidii@googlegroups.com>
Date: Tuesday, 15 January, 2013, 9:41

Kumbe ana-exist?!

From: Neville Meena <nevilletz@gmail.com>
To: wanabidii@googlegroups.com
Sent: Tuesday, January 15, 2013 9:39 AM
Subject: Re: [wanabidii] JAMANI WAMAMA JIHADHARINI NA KIM

Duh hii kali kwelikweli. Binafsi namfahamu Kim nakumbuka kipindi fulani alikuwa Mzee wa Kanisa!

2013/1/15 Abdalah Hamis <hamisznz@gmail.com>
Rachel A. Temu

Hii umeipata ndio stori mjini nakumegea..................


Bi. Mwele Malechela,
Najua utashangaa sana kuusoma huu ujumbe. Usishangae mshukuru Mungu
kwa kuzipata taarifa hizi. Nimeona njia nzuri kukupatia ni kukueleza
ukweli kwa njia hii kuhusu mtu unayejihusisha naye sasa hivi
anayejiita Kim. Majina yake halisi ni Kimbangambanga Julius Mgaya.
Jamaa ni mtu mbaya na hatari sana. Wewe ni mtu mwenye heshima mbele ya
jamii na mkubwa sana kiumri kujihusisha kimapenzi na Kim. Waswahili
wanasema mapenzi hayachagui ni sawa isipokuwa tabia mbaya za mtu huyo
ndio tatizo. Jamaa ameshatapeli sana hapa mjini na kuwarubuni wanawake
wengi wenye nafasi zao kimapenzi na mwisho wa siku anawatapeli na
kuwachuna mali zao.

Kim anafahamika sana hapa mjini kwa kuishi maisha ya kitapeli,
utasikia hadithi nyingi kuwa yupo bize ana mikutano hadi usiku na
wafanyabiashara au viongozi wa serikali kumbe ni uongo, hiyo ni kutaka
kujionyesha kwa watu kuwa ni mtu muhimu na wa maana. Safari nyingi
anazofanya ndani na nje ya nchi ni za kitapeli. Ana wanawake
anaowachuna wapo Marekani na UK. Maisha yake yote ni utapeli na
kupitia wanawake wenye nyadhifa au wafanyabiashara wakubwa.
Kinachomsaidia ni utanashati wake wanawake humnunulia vitu vya
thamani. Kim amesoma hadi kidato cha nne tu hana cheti chochote zaidi
ya hapo. Kim anajifanya ni mbia kwenye biashara kubwa kubwa hapa mjini
akijichanganya na wahindi na viongozi wakubwa. Ukweli ni kwamba hana
kitu na yeye ni kishoka tu anawahangaikia watu mahali walipokwama na
yeye analipwa kamisheni yake. Anatangaza mjini kuwa majengo
yaliyobomolewa kule Masaki ni yakwake, kumbe ni ya mfanyabiashara
mwenye asili ya kihindi. Anasema anamiliki hoteli Arusha inayoitwa
Snowcrest, ukweli ni kwamba hoteli hiyo inamilikiwa na kijana wa
kichaga anayeitwa Willy pamoja na dada yake anayeitwa Theo.
Kujihusisha kwa Kim kwenye hoteli hiyo ni kwa ajili ya kutafuta
biashara na uurafiki wake na mmiliki wa hoteli hiyo lakini amekuwa
anajifanya ni mali yake.

Mama yangu Mwele, nakueleza mambo ya Kim ili usiingie kwenye mtego
wake. Anakuhadaa ili mbadilishane magari, usithubutu. Kwa muda sasa
amekuwa akikushawishi umpe gari lako nayeye akupe gari lake aina ya
Benz . Benz hilo alikuwa amelipaki muda mrefu bila kulitembeza, sio la
kwake. Benz lina kesi maana alimdhurumu mwanamke mmoja na sasa
mwenyewe amechachamaa analitaka gari lake. Sasa kuziba kasheshe hilo
anataka kukuingiza wewe mkenge ili yeye ajitoe. Mama chukua tahadhali
bado mapema. Kim anapenda sana kubadilisha magari lakini
yasikubabaishe, yote unayoyaona sio mali yake ni ya kutaperi na
kubadilishana na watu kama anavyotaka kukufanyia. Alishawahi kuwa na
gari aina ya Hammer lakini halikuwa la kwake, alimtapeli mwanamke
Zanzibar mwenyewe husema kwa watu kuwa ameliuza. Alichukua magari
mawili kwa Chikawe yule waziri wa sheria mojawapo ni BMW X5 ya rangi
ya kibluu hadi leo hajamrudishia na anajizungusha nayo.

Chikawe anamuonea aibu kumdai kwa kuwa alimsaidia kumtafutia nyumba
binti yake. Kim alivyo sasa hivi ana mahusiano ya kimapenzi na binti
huyo wa Chikawe anayeitwa Tamika ameolewa na mzungu lakini utafikiri
Kim ndio mume wake alivyomganda. Kim alikuwa na magari mengine Suzuki
Grand na Mitsubishi ambazo si mali yake. Magari hayo kabla ya
kunyang'anywa na mwenye mali alimtapeli mama mmoja anayefanya kazi
shirika la nyumba NHC, ofisi yake ipo Msasani. Mama huyo mtu mzima
aliingizwa mkenge na Kim baada ya kuingia kwenye uhusiano wa
kimapenzi. Na kwa kuwa mama huyo anafanya kazi NHC alimsaidia Kim
kuipata nyumba ya nationa house anayoishi sasa Kim Chang'ombe. Nyumba
hiyo aliipata kitapeli kwa msaada wa huyo mama, wakaibomoa na kujenga
nyumba nyingine kubwa ambayo ndio anaishi Kim sasa hivi. Huyo mama
aliyafanya yote hayo akijua kuwa wataishi na Kim kama mume na mke.
Nyumba ilipoisha Kim hakumjali tena huyo mama jambo lililomfanya mama
wa watu ajue kuwa ametaperiwa na kumyang'anya magari yake mawili
Suzuki Grand na Mitsubishi. Hivi sasa mama wa watu yupo mbioni
kuikomboa nyumba hiyo ya Chang'ombe maana kaijenga kwa jasho lake.
Kuna gari nyingine tena saloon Progress ambayo nayo haikuwa yakwake.
Gari hiyo alimtapeli dada mmoja anayeitwa Lucy ambaye ameolewa na
Mkorea wanamiliki kampuni inayoitwa TAKAOKA. Kama kawaida yake Kim
alianzisha uhusiano wa kimapenzi na dada huyo huku akimshawishi
wafungue kampuni. Lucy alimpa pesa nyingi Kim, gari na jenereta kubwa
lilifungwa kwenye nyumba ya Kim huko Chang'ombe. Lucy alipomshtukia
Kim akachachamaa na kumnyang'anya gari na jenereta, hataki hata
kumsikia Kim. Mama Mwele ona mifano ya wenzio.

Tabia nyinginewe ya Kim ni umalaya. Kila mwanamke anataka kulala naye,
wengi anawaahidi kuwaoa na hata kuwavisha pete. Anatumia mbinu hiyo
chafu ili kuwanasa nyie dada zetu akishapata anachokitaka anatafuta
pengine pa kuchuna. Kuna mwanamke aliyezaa naye Zanzibar, baada ya
kukorofishana aliondoka na mtoto wake. Sasa hivi amezaa mtoto wa kiume
na mwanamke mwingine polisi traffic anayeitwa Shufaa anakaa Ukonga.
Mwanamke mwingine yupo benki ya NBC, kuna mwingine naye anaishi
Kibangu ni vurugu tupu. Kuna wanawake wawili ambao ana mahusiano nao
bila wao kujijua wanafanya kazi Ifakara health institute. Mmoja wao
anaitwa Rahima Dosa ambaye naye kama walivyo wengine amemtolea posa
baada ya mdosi kuona Kim anamzingua. Rahima ameapiza kuwa hawezi
kumuacha Kim vinginevyo atamuua kwa kua ameshampotezea muda wake
mwingi. Wakati huo huo ana mahusiano ya kimapenzi na wanawake wengi
nitakutajia wachache ninaowafahamu na ambao Kim ameshanitambulisha nao
akina Premi Kibanga yupo ikulu ni mwanamke wake wa muda mrefu, Sofia,
Badra Masud wa Tanesco, Justina Shauri, Shina Sanare, Batilda Buriani
balozi wa Kenya ambaye alikuwa mbunge zamani, Grace, Mange Kimambi na
mama yake Rose Kimambi ambao wote amelala nao na wengineo. Arusha pia
ana wanawake wawili ninaowafahamu mmoja nafanya kazi kwenye hoteli
moja maarufu na mwingine anafanya kazi BOT Arusha.

Kwanini nimesukumwa kukujulisha tabia za Kim, pamoja na udhaifu wetu
wanaume ni kitendo kibaya kuwachanganya wanawake wanaofahamiana au
ndugu. Sijuwi mlikutana wapi na Kim lakini kabla hujaanza kuwa karibu
naye aliwahi kuwa na mahusiano na dada mmoja ambaye sitakutajia ni wa
familia yenu alianzisha uhusiano naye wa kimapenzi akamwambia anataka
kumuoa, dada huyo akapata mimba. Kim akamwambia aitoe mimba dada huyo
akakataa kuitoa. Kim kwa siri alitafuta dawa na kumpa binti atumie
akimdanganya kuwa ni za vitamin zisaidie kukuza mimba hiyo. Dada huyo
kwa mapenzi alitumia dawa hizo na akaanza kuumwa tumbo na damu
kumtoka, alipoenda hospitali aliulizwa ametumia nini naye akaonyesha
dawa alizopewa na Kim kumbe hakupaswa kuzitumia kabisa katika ujauzito
na mimba ilitoka. Dada huyo si mbali na familia yako lakini jamaa
haoni vibaya anachotaka ni kuvuna. Huyo si mwanaume mama achana naye
atakuliza. Kibaya zaidi tabia ya umalaya haogopi hata magonjwa wala
hajifunzi maana mfano mzuri ni watu wake wa karibu ambao ni wazazi
wake walitangulia mbele za haki kutokana na ugonjwa wa ukimwi lakini
yeye hajali.

Sasa hivi kuna watu wanajiandaa kumfungulia mashitaka ya utapeli na
kujipatia mali kwa njia ya udanganyifu. Amewaliza wengi na watu wana
visasi naye. Kwa kupenda maisha ya juu ametengeneza maadui kuliko
marafiki na amekuwa anaishi maisha ya kujifichaficha. Kim hana mwisho
mzuri. Jihadhari sana na Kim anapenda sana ushirikina na waganga wa
kienyeji. Anatumia waganga wengi kutoka Bagamoyo, Zanzibar na Iringa.
Na utapeli wake ni wa kutumia dawa kuwafunga watu wanaomdai na
kuwapumbaza wenye pesa zao ili wasimshtukie. Mwaka jana mwanzoni kuna
taarifa zake zilitoka kwenye vyombo vya habari na magazetini
zikitahadharisha watu kukaa mbali na Kim. Habari hizo zilitumwa kwenya
vyombo vyote vya habari pamoja na picha yake. Habari hizo
naziunganisha hapa chini ili usome kama hukubahatika kuzisoma mwaka
jana. Ningeweza kukueleza mengi kuhusu Kim ni aibu kwa haya machache
huenda ikasaidia kukufungua macho. Jamii inakuheshimu sana na ndicho
kilichoniumiza na nikaamini humjuwi vizuri Kim.

--
Jobs in Africa - www.wejobs.blogspot.com
International Jobs - www.jobsunited.blogspot.com

Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com  Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma

Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.





--
Neville C. Meena,
Secretary General,
Tanzania Editors Forum - TEF,
Dar es Salaam - Tanzania.
Cell: +255 - 787 - 675555
        +255 - 753 - 555556
 
--
Jobs in Africa - www.wejobs.blogspot.com
International Jobs - www.jobsunited.blogspot.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
 
 


--
Jobs in Africa - www.wejobs.blogspot.com
International Jobs - www.jobsunited.blogspot.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
 
 

--
Jobs in Africa - www.wejobs.blogspot.com
International Jobs - www.jobsunited.blogspot.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
 
 

0 comments:

Post a Comment