Saturday 1 December 2012

[wanabidii] Timu za Tanzania zatinga robo fainali CECAFA

Timu zetu zote mbili zimeingia robo fainali ya michuano ya Kombe la Chalenji kwa wakubwa mwaka 2012 zinazofanyika nchini Uganda.
 
Michuano ya Robo Fainali itakuwa kama ifuatavyo (kwa mujibu wa tovuti ya Soccer Way):
 
Jumatatu kipute cha kwanza: TANZANIA BARA  na Rwanda
.........................ndinga la pili: Uganda na Sudan
 
Jumanne kipute cha kwanza: TANZANIA ZANZIBAR na Burundi
.........................ndinga la pili: Kenya na Malawi
 
Nusu Fainali ya Kwanza: Natabiri itacheza TANZANIA BARA na Uganda
Nusu Fainali ya Pili: Nabashiri itacheza TANZANIA ZANZIBAR na Malawi
 
Mchezo wa Mshindi wa Tatu: Uganda na Malawi
 
Fainali: TANZANIA BARA na TANZANIA ZANZIBAR.
 
Hongera Tanzania Bara kwa kuifunga Somalia 7-0 huku mshambuliaji wa Simba, Mrisho Ngassa, akipiga magoli matano peke yake na golikipa wa Simba, Juma Kaseja, akiokoa magoli elfu. Hadi sasa Tanzania Bara ndiye yenye magoli mengi katika michuano hii kama ifuatavyo:
Mrisho Ngassa ........... 5
Boko wa Azam ........... 4
 
Wachezaji wa Yanga bado hawana mchango kwa timu yetu, wazungukazunguka tu!
 
Matinyi.
 
 
 

0 comments:

Post a Comment