Friday 28 December 2012

[wanabidii] TAMKO LA BAVICHA MKOA WA TANGA KUHUSU Deogratias Kisandu

*TAARIFA KWA UMMA* 

NAPENDA kutoa taarifa kwa umma kutokana na habari zinazoandikwa kwenye 
baadhi ya vyombo vya habari, huku chanzo cha habari hizo kikiwa ni Katibu 
wa BAVICHA Mkoa wa Tanga, Bwana Deogratias Kisandu, ambazo zimekuwa 
zikionesha kuwa vijana wa Mkoa wa Tanga tuna walakini katika chama chetu 
cha CHADEMA. 

Leo katika baadhi ya vyombo vya habari, Bwana Kisandu amenukuliwa akitoa 
taarifa kuwa yeye pamoja na makatibu wenzake nchi nzima, wamepanga kufanya 
maandamano ya kuupinga uongozi wa juu wa kitaifa wa BAVICHA. 

Kwa kutambua na kuheshimu kuwa moja ya misingi muhimu ya uendeshaji wa 
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) pamoja na mabaraza yake ni 
vikao, ambavyo vipo kwa mujibu wa Katiba, miongozo, taratibu, kanuni na 
itifaki za chama, vijana wa CHADEMA Mkoa wa Tanga, ambao mimi ndiye msemaji 
wao kikatiba, tunaamini Bwana Kisandu anazidi kupotoka. 

Kwa hiyo basi, kama ambavyo nimeshapokea malalamiko kutoka kwa vijana wa 
Tanga baada ya hatua yake ya awali ya Bwana Kisandu kutoa taarifa kwa 
vyombo vya habari, bila kuzingatia katiba, maadili na itifaki ya chama, 
akibeba propaganda nyepesi za Sekretarieti ya CCM, juu ya suala la kadi 
mbili kwa Katibu Mkuu wetu Dkt. Willibrod Slaa, kuna haja ya kufanya vikao 
kuangalia na kujadili mwenendo wa kiongozi mwenzetu huyo. 

Kwa sababu kama vijana makini wa CHADEMA, chama ambacho kinaamini katika 
kutoa utumishi bora, mikakati madhubuti, sera imara kwa ajili ya maendeleo 
endelevu ya Watanzania wote, ambao wamekosa uongozi bora na siasa safi 
kutokana na ufisadi na ubadhirifu wa CCM, lazima tuwe makini na kila 
mwenzetu yeyote yule ambaye anaonekana kufanya kazi ya CCM kwa kutumia jina 
la CHADEMA. 

Tunapenda kumkumbusha Bwana Kisandu kuwa atumie muda wake pia kuisoma vyema 
katiba ya CHADEMA hasa katika Sura ya 10 inayozungumzia Maadili ya 
Viongozi, Sifa mahususi za viongozi na maadili ya wanachama, kifungu 
10.1(1-13), toleo la mwaka 2006. 

Kuhusu masuala ya ushiriki wa vijana kwenye shughuli mbalimbali za chama 
ikiwemo mikutano ya M4C, Bwana Kisandu anapaswa kuelewa kuwa vijana 
kutokana maeneo mbalimbali ya nchi, ukiwemo Mkoa wa Tanga tumekuwa 
tukishirikishwa, kupitia utaratibu maalum unaopangwa na Ofisi ya Katibu 
Mkuu, ambao tunaamini mpaka sasa umetoa fursa kwa wanachama wote, wakiwemo 
wazee, wanawake na vijana kukieneza na kukiimarisha chama maeneo mbalimbali 
ya nchi. 

Na maamuzi yote ya msingi kwa uendeshaji wa Baraza hasa kwa Mkoa wa Tanga 
yatafanyika kupitia vikao na hatua zitachukuliwa kwa kufuata katiba, 
kanuni, maadili, itifaki na miongozo ya chama. 

 *Aron J Mashuve* 

*Mwenyekiti wa BAVICHA* 

*Mkoa Wa Tanga* 

--
Jobs in Africa - www.wejobs.blogspot.com
nafasi mpya za Kazi www.kazibongo.blogspot.com
Habari na Picha www.patahabari.blogspot.com
 
DELL LATITUDE D 620 & D30
 
80 GB HardDisk ,CORE 2 DUO , 2.0 GHZ CPU ,1 GB RAM
DVD/CD - RW ,WINDOWS 7 /WINDOWS XP ,WIRELESS , BLUE TOOTH .
 
TSHS : 380,000 , 1 YEAR WARRANTY
 
CALL : 0786 806028
Free Delivery in Dar es salaam
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
 
 

0 comments:

Post a Comment