Kuna usemi Ngupula kuwa-Debe Tupu Haliishi Kuvuma.. Hivi kwa mfano itokee msichana anajitangaza kuwa-mwanaume fulani ananipenda sana ananipenda anamwambia kila mtu na kujiandaa na vivalo vya ndoa. Ikija kutokea huyo mwanaume akaoa mke/msichana mwingine kwa sherehe kubwa waziwazi kila mtu akishuhudia jee atajinyonga? Atahama mji au ataamua kumuua huyo bwana na mke huyo mpya? Kama kuzuia mvua kwa mkono haiwezekani-kaa ndani kimya usitoke nje kwenye mvua! Maama, utaloa mpaka bukta ya ndani uaibike!! Akili za kuazima-Changanya na zako!! Eti unashindwa kulipia kadi ya afya shs 10 elfu kwa mwaka kutibu watu 6 wa kaya yako; kuchangia madeski shs 5 elfu kwa mwaka au kuchangia madarasa, kisima cha kupata maji cha kijiji cheni kila mtu umri miaka 18+ kuchangia elfu moja kwa mwezi au 12 kwa mwaka, ila unaweza kuchangia gharama ya mafuta, chakula, matengenezo ya bodaboda, kula vumbi pua na mdomo, pancha utakazopata kutoka Mbeya hadi Dodoma kumsifu mtu km 600+
Mabomba ya maji ya visima vya handpump toka vijengwe in mid 1980 na kukamilika mid 1990 havikarabatiwi mnakunywa maji na mifugo inayokoka dip-hamna hela, serikali itujengee!! Leo hii mnagharimia MISIFA!! Excuse me! kama demokrasia ndio hii wa watu kupoteza muda wa kilimo, kuzalisha mali, kusaidia kuchangia jamii yao iendelee hata kununua mitumba kwa ajili ya zahanati ambako wake zao wanajifungua hakuna pazia, shuka (za mitumba zipo) ni kulala juu ya godoro alilodorozea mwenzake mwingine-leo muda na fedha ni kwa ajili ya kuonekana tu!!?? inakera, kinyaa na aibu. Basi ikifika kila mtarajiwa abebwe kwa maandamano watu kutoka mikoa mbali mbali kila mtu na wao-tutakuwa sawa na taahira wa bangi. Kalivuta mwenyewe sasa anafaidi matunda yake. Bora wangekusanyana na kuandamana mpaka shule yao ya msiki yenye matatizo wakashindwa kutwa wanakarabati au kufyatua tofari za kukarabati, kupanda miti, kuweka wigo wa shule mifugo isiharibu mazingira ya shule na
kupumzika darasani wanafunzi wakiwa hawapo ng'ombe na mbuzi zipo darasani zinakula kivuri!! Wangelima shamba la shule hiyo mijibaba watoto wapate uji maana chakula shuleni kinaongeza attendance and passing rate. Nchi za kiafrika-tuna matatizo.
Kikwete ampe baraka wakati wachaguzi ni sisi? mbona Nyerere alisema 'wewe bado tulia' lakini wewe hufai kabisa hata iweje usitegemee!! Chuki binafsi hakuna ila wazee bakini kuwa washauri waachieni vijana. Kujitafutia kufa ghafla kwa pressure tu utakapoona jina halikupita au limepita hukupata kula kuona unapendwa kumbe 'changa la macho'. Wekeni asiotakiwa kikweli na wananchi CCM itapata matunda ya uchaguzi wa serikali za mitaa-kukipigia chama pinzani mradi tyu huyo asiyetakiwa wa CCM asipite!! Na sasa wenzetu wenye ualbino wanawekewa vidigitali cha kumonita wapo wapi, makaburi yana ulinzi-mtamaliza familia zetu kuweka watu mizukule na ushindi usipatikane-aah lakini Gwajima wa kutoa mizukule yupo. Hata hivyo Mvua na Jua vinazuilika kwa mkono kushika mwamvuli wa kufunika mwili labda iwe ya mawe kama hiyo ya Kahama/Geita kwenye mauaji ya ajabu ajabu.
--------------------------------------------
On Thu, 26/3/15, 'ngupula' via Wanabidii <wanabidii@googlegroups.com> wrote:
Subject: Re: [wanabidii] Lowassa ana baraka za Kikwete?
To: wanabidii@googlegroups.com
Date: Thursday, 26 March, 2015, 13:42
Sometimes mtu mnapomzungumzia saana
ni dalili kuwa mnamuogopa. Mtu wenye matunda hupigwa
mawe.Kama mnahis Lowasa hata kitu and is unfit fanyeni kazi
zenu majumbani na kama mna wagombea wengine mnaowapenda
muwapiganie hao kwa hoja zenye nguvu.....Ngupula.
'lesian mollel' via Wanabidii
<wanabidii@googlegroups.com> wrote:
Hawajakutana bara barani
hawa-fullstop
From: Juma Mzuri
<jumamzuri@gmail.com>
To:
wanabidii@googlegroups.com
Sent:
Tuesday, March 24, 2015 6:06 AM
Subject:
[wanabidii] Lowassa ana baraka za Kikwete?
Lowassa
ana baraka za Kikwete?
Ilikuwa kama tetesi kuwa Lowassa anatarajia kuwania kiti cha
urais kumrithi Kikwete baada ya muhula wake kuisha. Tetesi
hizo zilisindikizwa na shughuli za harambee kuchangia
maendeleo ya asasi za kidini, binafsi hata makundi kwenye
jamii. Tetesi hizo ziliwaibua wasaka urais ambao walitaraji
kupenyeza majina yao katika mchujo wa chama (CCM) wakati
utakapowadia, lakini badala yake walikimbizana na tetesi
hizo huku wakijinasibu kutaka kugombea urais 2015. Ikumbukwe kwamba Lowassa
bado ni mtuhumiwa namba moja wa sakata la RICHMOND ambalo
liliiangusha serikali Bungeni na kumlazimisha rais kuunda
upya Baraza la Mawaziri.Hatimaye walidhibitiwa kwa
kuwekwa kiti-moto na hatimaye kufungiwa mwaka mmoja
kuendeleza harakati zao huku wakiangaliwa nyendo zao. Ila
washangiliaji hawajui ni nini hasa walichofungiwa maana kama
kujitangaza walishajitangaza na pia wameendelea kufanya
siasa za Chama bila kubugudhiwa na yeyote.Hata kabla kifungo
chao kuisha mzee wa Monduli ameibuka kwa kasi ya ajabu huku
makundi ya kijamii yakitumika kushinikiza kukubalika kwake
na akilazimishwa kuchukua fomu huku akichangiwa pesa ya ada
ya kuchukua fomu ndani ya chama chake. Yamesemwa mengi ndani
na nje ya Chama lakini washereheshaji hawajabaki nyuma
kukebehi na kunasibu kuwa siyo Lowassa anayetaka kugombea
bali ni wanachi....Haya yote
yanafanyika mbele ya Rais ambaye pia ni Mwenyekiti wa Taifa
wa Chama cha Mapinduzi. Haya yanafanyika huku kanuni za
kuhusu kutangaza nia na ratiba za kuchukua fomu
hazikurekebishwa hivyo kuonyesha wazi ukiukwaji wake. Haya
yanafanyika sambamba na kujitakasa kwa Lowassa tena kwa
tambo nyingi kwamba kujiuzulu kwake kulikuwa kwa lazima ili
kuokoa serikali isianguke yote. Na wapambe wake wanapita
huku na huko wakisema kuwa 'BWANA MKUBWA' anahusika
na "ishu" ile. Hakuna aliyesimama kukemea wala
kutoa ufafanuzi wa propaganda zinazoenezwa mitaani.
Haiyumkiniki sasa yametimia kuhusu ule usemi kwamba
'Uongo ukirudiwa rudiwa sanahugeuka
ukweli'Ninagoma na pia
ninasita kuamini kwamba nguvu kubwa ya Lowassa inatokana na
uswahiba alionao na mkuu wa nchi, kwani alishawahi kusema
"...mimi na JK hatukukutana barabarani...."
Inawezekana sana sisi wananchi tunazugwa kwamba hawa
waheshimiwa hawapatani kumbe jioni wanakunywa kahawa pamoja,
inawezekana kabisa kwamba Lowassa ndiye chaguo la Kikwete
kurithi kile kiti pale magogoni.Nasema hayo kwa
sababu, hatujaona JK kukerwa na tambo, harakati na hatimaye
propaganda za kambi ya Lowassa hasa zinapopambamoto kipindi
hiki kuelekea uteuzi wa ndani ya Chama na hatimaye Uchaguzi
mkuu hapo Oktoba. Chama cha CCM kinaweza kuungana ama
kugawanyika kwa kiwango cha kutisha kupitia uteuzi wa
mgombea wa Urais mwaka huu.Kazi kwenu
Wananchi kumkubali mteule wa JK au kumchagua mtu makini
ambaye hajatumia kununua umaarufu ili apewe nafasi ya kuwa
rais wetu baada ya JK.Bila CCM imara,
nchi itayumba. - By NyerereLeo nchi
inayumba....
--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya
kudhibitisha ukishatuma
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility
for any legal consequences of his or her postings, and hence
statements and facts must be presented responsibly. Your
continued membership signifies that you agree to this
disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the
Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails
from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.
--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya
kudhibitisha ukishatuma
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility
for any legal consequences of his or her postings, and hence
statements and facts must be presented responsibly. Your
continued membership signifies that you agree to this
disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the
Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails
from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.
--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.
0 comments:
Post a Comment