yesu sio mungu yes mama yake sio mama wamungu sawa fundisho hili linatupelekaje mbinguni?
Hakuna mwaka ambao Yesu alianza kuitwa Mungu. Bali Yesu alizaliwa akiwa Mungu na atabaki kuwa hivyo. Ukitaka kuzijua sifa za Yesu soma Isaya 9:6-10. Kuyajua mafumbo ya Mungu na kuyaelewa ni kipawa cha Mungu. Na kipawa hicho hupewa watoto wa Mungu baada ya kuthibitika kwa Mungu. Mtu mwovu awaye yeyote hawezi kumuelewa Yesu na akidhani anamuelewa, basi anamuelewa vibaya. Kuendelea kuelezea uungu wa Yesu kwa kadamnasi ni kumwaga lulu mbele ya nguruwe na hakuna cha zaidi bali ni kulaluliwa na kuumizwa. .. Ngupula.
Tracy John Kimambo <tracykwetu@gmail.com> wrote:Watu wengi hutangaza hadharani kwamba Yesu ni Mungu hali hiyo hutokana na mtu kutokuwa na Elimu ya kutosha kuhusu chanzo cha Yesu kuitwa Mungu katika nafsi ya Pili .
MASLAHI ya Dunia hii yamewafanya watu wengi wenye elimu kuhusu Yesu kuwa Mungu washindwe kuwaeleza watu ukweli kuhusu Umungu wa Yesu wameamua kuwadanganya makusudi.
Siri zilizomo Kanisani ambazo zinamzuwiya Kiongozi kuwafundisha watu ukweli na nidhamu ya woga iliyojengwa ndani ya Wafuasi inamfanya mtu akubali jambo bila kulielewa kabisa akiuliza husomewa Yohana 1:1-5 na kupewa tafsiri potofu lazima akubaliane na Kiongozi wake hiyo ndiyo Sera ya kudanganya watu na kweli wamedanganyika kama unavyowaona ukimwambia ukweli yuko tayari kupigana na kuuwa mtu, hata hivyo lazima ukweli tuuseme tu kwa kumuogopa Mungu. Mataya 10:26-27.
Kwa kuzingatia umuhimu wa somo hili inabidi tuligawe katika sehemu Nne ili kupata ushahidi wa fundisho la imani ya utatu wa Mungu mmoja. Sehemu hizo ni kama ifuatavyo:-
Matamshi ya Yesu mwenyewe kuhusu Uungu wake. Anasemaje?
Wanafunzi wa kwanza wa Bwana Yesu walimfahamu kwamba ni Mungu au vipi?
Maaskofu waliofuata baada ya wanafunzi wa kwanza tangu Karne ya kwanza hadi karne ya tatu je? Walifundisha vipi kuhusu Yesu.
Imani ya utatu ilivyoanza hadi kuwa fundisho kamili na kanuni ya Wakristo Duniani pote.
Yesu anasemaje katika Injili yake:
Yohana 17:3 imeandikwa hivi – uzima wa milele ndiyo huu wakujue Mungu wa pekee na Yesu uliyemtuma. Katika Aya hii Yesu anasema kwamba ili kupata uzima lazima tumjue kwanza Mungu wa pekee na umjue Yesu Kristo aliyetumwa na Mungu, hapa Yesu hasemi lolote kuhusu yeye kuwa nafasi ya pili ya Mungu ila anakiri wazi yeye ametumwa na Mungu mmoja wa pekee.
Luka 2:40 imeandikwa hivi:- Yule mtoto akakua akaongezeka nguvu amejaa hekima na neema ya Mungu ilikua juu yake.
Katika Aya hii tunaambiwa kwamba Yesu alijaa hekima na neema ya Mungu. Tahadhari ufikirie vizuri kwa makini sababu hapa inayonyesha kwamba bila ya Mungu kumpa neema Yesu asingelikuwa na hekima hii inaonyesha wazi Yesu ni kiumbe aliyeteuliwa na Mungu na hii ni kawaida yake Mwenyezi Mungu kwa Mitume na Manabii wake kuwapa neema na hekima.
Yohana 13:13 imeandikwa hivi:- Nanyi mwaniita Mwalimu na Bwana nanyi mwasema vema maana ndivyo nilivyo. Maneno hayo yatueleza wazi kwamba alikuwa anajua wazi kwamba yeye ni Mwalimu na Bwana ndiyo maana anawasifu wanafunzi wake, NANYI MWASEMA VEMA.
Matayo 23:9 imeandikwa:- Wala msimwite mtu Baba maana Baba yenu ni mmoja wa Mbinguni wala msiitwe Kiongozi maana Kiongozi wenu ni mmoja naye ndiye Yesu Kristo, hapa Yesu anaendelea kutuonyesha jinsi alivyo tofauti na Mungu hayuko sawa na Mungu daima Mungu ni Baba lakini Yesu ni Kiongozi tu.
Ufunuo: 1:1-2 imeandikwa hivi:- Ufunuo wa Yesu Kristo aliopewa na Mungu awaonyeshe watu wake……Naye akatuma Malaika akamuonyeshe Mtumwa wake Yohana……..Wakati ufunuo unatolewa na Mungu na kupewa Yesu wakati huo Yesu ameshatoka Duniani yuko Mbinguni, lakini bado inaonyesha Mungu ndiye mkubwa Yesu bado ni wakutumwa ili awaonyeshe watumwa kuhusu mambo yao yatakayokuja kama tulivyosoma. Zipo Aya nyingi sana zinazoo
--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.
0 comments:
Post a Comment