Saturday, 21 September 2013

[wanabidii] Shaaban Robert Angesemaje Kuhusu Mjadala Wa Katiba...?



Ndugu zangu,

Kama Mwanafasihi na mshahiri mahiri Shaaban Robert angelikuwa hai ,basi, kwenye hili la mjadala wa Katiba yumkini angetamka;
" Turufu huenda kwa mchezaji...!"

Maana, tunaukumbuka mjadala ule kwenye simulizi ya Mfalme Rai. Ni juu ya mjinga na mwerevu. Naam, mkulima ni mjinga na mwenye duka ni mwerevu. Kwa nini kuna wenye kuamini hivyo?

Ndio, wenye kuamini hivyo wanadhani, kuwa kwa vile mkulima anashika jembe tu, basi, hana halijualo.

Na kwa vile mwenye duka anafanya kazi ya kuhesabu pesa, basi ni mwerevu.

Lakini, kama mwenye duka naye hupata hasara, ina maana nae ni mjinga?

Na ni mkulima anayesemwa kuwa ni mjinga ndiye mwenye kuwalisha wengine, wakiwamo wafanyabiashara.

Na kwa vile wakulima wenye kusemwa kuwa ni wajinga ndio walo wengi, basi, hekima na busara ni kwa Mfalme kuhakikisha kuwa hao ndio walio nyuma yake.

Lililo jema ni kuwasikiliza. Maana, turufu siku zote huenda kwa mchezaji.

Maggid.
Iringa.
http://mjengwablog.com

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.

0 comments:

Post a Comment