Monday 30 September 2013

[wanabidii] Matumizi mabaya ya miito ya simu ya dharula Yamtokea Puani

JESHI la zimamoto na uokoaji limewataka wananchi kuacha matumizi mabaya ya miito ya simu ya dharula kwa Jeshi hilo ili kuepusha usumbufu kwa Jeshi pindi wanapopigiwa simu za dharula.

Wito huo umetolewa na Jeshi hilo baada ya kupata kero za mara kwa mara kutoka kwa wananchi wanaopiga simu kwenye Jeshi hilo wakihitaji huduma za gari hilo lakini wanapofika eneo waliloelekezwa wanakuta hakuna tukio lolote.
Wamekuwa wakipokea simu nyingi za uongo hivyo serikali kuingia gharama kubwa za mafuta ambayo yangetumika kwenye maafa pindi yanapotokea.

Mmoja wa wakazi wa Rugelele kata Rujewa wilaya ya MBARALI DUKA MKWILA[20]ni miongoni mwa wananchi waliopiga simu za uongo katika Jeshi hilo mara kadhaa na kuomba huduma nyingine badala ya ajali ya moto hali iliyofanya Jeshi hilo kumkamata na kumhoji.
DUKA amesema yeye namba hiyo alipewa na mtu mwigine aliyedai kuwa mwenye namba hiyo huwa anatoa pesa za FREE MASON pia dawa za kienyeji kwa matatizo mbalimbali.

Hata hivyo DUKA alikiri kutenda kosa na kuomba msamaha kwa jeshi hilo ambapo aliachiwa huru na kisha kurejea kwao huku akijutia kosa 
alilolifanya na kuahidi kutorudia tena

Na Mbeya yetu

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.

0 comments:

Post a Comment