Tuesday 30 July 2013

[wanabidii] CHADEMA KATIKA KASHFA NYINGINE

Kwanza naomba radhi kwa video hiyo hapo chini lakini nimewaza ni kwanini imesambaa mitandaoni na pia ni kwanini imehusicha chama cha CHADEMA.
Pengine ni kwa kuwa mhusika ni kada wa CHADEMA.
Imenibidi nijiulize kama chama cha siasa ni taasisi ya dini ambayo inaangalia maadili ya kila siku ya wanachama wake. Siasa na maadili ya mtu binafsi ni vitu viwili tofauti. Sijaona mantiki ya mitandao mbali mbali kuhusisha chama cha CHADEMA katika hili. Hata hivyo mhusika katika video yake ya home made, hakuvaa vazi la chama wala bendera ya chama wala hakutaja chama.
Ni busara tujadili hili kama mojawapo ya mmomonyoko wa maadili katika jamii na sio kuhusisha chaka kwa mambo kama haya. Chama kinapokewa wanachama mbalimbali ila sidhani kama chama cha siasa kinahusika katika kurekebisha tabia binafsi za watu.
Pamoja na kusikitikia jambo hilo kuwa si ziri, lakini watoa habari si vyema kuhusisha chama cha siasa na mambo binafsi ya watu
Video na maelezo hapa:
http://goldentz.blogspot.com/2013/07/maisha-binafsi-ya-mtu-si-jukumu-la.html

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.
 
 

0 comments:

Post a Comment