Saturday, 1 August 2015

Re: [wanabidii] RE: [Mabadiliko] NINAMUUNGA MKONO LOWASSA KUGOMBEA URAIS

Lakini jamani hayo maneno kasema Lowasa mmeyakubali siku anao watuhumu wakikanusa mnasemaje?
Kwenye mkanganyiko kama huo ndiyo huwa kuna haja ya mahakama.
Kwani katika hali ya kawaida unategemea Lowasa aseme nini?


Walewale

On Aug 1, 2015 10:41 PM, "'ELISA MUHINGO' via Wanabidii" <wanabidii@googlegroups.com> wrote:
Kama Lowasa akipona la Richmond anaweza kujiosha na fedha alizokuwa akizisambaza makanisani na misikitini na kwingineko?? alipoulizwa akasema anachangiwa na rafiki zake. lakini hakujibu lengo la marafikizake hao ni nini. Bado anaungwa mkono kwa saabu ya kujibu la richmond?
--------------------------------------------
On Sat, 8/1/15, Ireneus Mushongi <ireneuskakurumushongi@gmail.com> wrote:

 Subject: [wanabidii] RE: [Mabadiliko] NINAMUUNGA MKONO LOWASSA KUGOMBEA URAIS
 To: mabadilikotanzania@googlegroups.com
 Cc: "WANA BIDII" <wanabidii@googlegroups.com>
 Date: Saturday, August 1, 2015, 10:45 AM

 Mama
 Nkya
 Haya yote Ni marudio Tu. Tumeshayasikia
 tokea vinywa mbali mbali.

 Kwanini mnapindisha ukweli? Huyu huyu Dr Slaa
 alisema kuwa Ana ushahidi kuhusu Richmond Na Yuko tayari
 kuuwasilisha  mahakamani kama tu ENL atapelekwa kwa
 pilato.

 Mbona hamuhoji hayo
 tena au siyo ya msingi sababu Mkaskazini huyu keshakuwa
 malaika na automatically msafi kwa kubadili jezi? Hawa jamaa
 ni wajanja wamecheza na nyakati wamehit kwenye msumari wa
 moto ukiwa haujapoa. Watu wamecheza na fursa adimu. Kimsingi
 wana malengo tofauti. Huyu ana hasira ya kuikomoa CCM hawa
 wanacheza na akili hiyo kujijenga kisiasa zaidi kwani
 popularity itaongezeka, status itapanda, watavuna wafuasi
 wengi at ago na si lazima waingie ikulu but watakuwa
 wamegain sana hata kuongeza wabunge 50 from the current
 number.

 Next move atakuja
 Chenge. Ukihama CCM si unatakasika automatic? Huyu bwana ana
 team oliyojiuzuru naye. Sijawasikia wao kuhama au wanapima
 upepo bado hadi ufanyike uchaguzi. Hawa wote ndani ya Ukawa
 ni watukufu na wasafi hivi karibuni watajoin majeshi na
 kubadili jezi. Hawa hawa waliokuwa wanawaponda
 watawashangilia sana na kuwaita majembe!

 Ninaamini Mbowe, Slaa,
 Lipumba, Mbatia,  na UKAWA top yote hawampendi ENL ila
 wametumia fursa hii kuachieve strategy zao za kisiasa. Time
 will tell. Kumsafisha au kutomsafisha haihusu sana.
 Washasema ilikuwa ni mambo ya kisiasa zaidi so watapima
 matokeo baadaye! Muhimu ni kugain tu kwa sasa kabla ENL
 hajarudi kwenye normal senses.

 Tutaona mwisho wa haya... Heri sisi
 tusiofungamana na kipande yoyote.... Tunahitaji mabadiliko
 ya kweli sio ya kinafiki. Msituchanganye! Jana mlikuja
 kivingine, Leo mnakuja hivi kesho hatujui mtakuja na lipi.
 Tuonyeshe dira na dhamira sio mikakati ya fursa za zimamoto.

 Umesababisha mke wa mtu aachwe,  alipopewa
 talaka tu, eti ndio na wewe unatangaza ndoa halafu eti
 tukuchangie. Tutafika? Siasa mchezo mchafu!From:
 'ananilea
 nkya' via Mabadiliko Forum
 Sent:
 ‎01/‎08/‎2015
 01:21
 To:
 mabadilikotanzania@googlegroups.com
 Cc:
 WANA
 BIDII
 Subject:
 [Mabadiliko] NINAMUUNGA MKONO
 LOWASSA KUGOMBEA URAIS

 Mimi Ananilea Nkya tatizo langu kubwa kwa
 Lowassa lilikuwa ni ufisadi wa Richmond uliotafuna zaidi ya
 shilingi bilion 172 za wananchi. Baada ya kusikia kauli yake
 alipohojiwa na wanahabari siku alipojiunga na CHADEMA, na
 baada ya kujiridhisha kuwa kama alikuwa amehusika na ufisadi
 wa Richmond leo angelikuwa jela kama Yona na Mramba,
 namuunga mkono kugombea Urais. Naamini hata Dr Slaa
 amemkubali Lowassa kuwa mgombea Urais wa vyama vinanyounda
 UKAWA baada ya kujiridhisha kuwa mamlaka ya juu ilimbebesha
 Lowassa kashfa ya Richmond ili kunusuru serikali nzima
 kuanguka.

 Lakini zaidi
 nimeongeza imani yangu kwa Lowassa baada ya kubaini kuwa
 hata Baba wa Taifa Julius Kambarage Nyerere alimuona kama
 kijana makini mwenye maono na dhamira safi ya kuwatumikia
 Watanzania. Mwaka 1995 wakati Rais mstaafu Ali Hassan Mwinyi
 anamaliza muda wake  mwandishi wa habari Mwita Matinyi
 alimuliza Mwalimu Nyerere alikuwa anafikiri ni nani angeweza
 kumrithi Mwinyi kuiongoza Tanzania. Mwalimu alijibu Matinyi
 hivi. Nanukuu:
 Ni kweli Mzee Mwinyi
 anaondoka lakini ndani ya CCM kuna viongozi wengi wenye sifa
 za kuwaongoza Watanzania, kikubwa tu awe na dhamira kwa
 mfano wapo wakina Warioba, Mzee Msuya na Mark Bomani na wapo
 vijana hodari na wenye upeo mkubwa sana kama Mkapa, Kikwete
 na Lowassa ni jambo la heri sana CCM kuwa na watu kama hawa
 (Majira 26/5/1995) ukurasa wa 3; na Nipashe 26/5/95 ukurasa
 wa 3).

 Pia nikiwa ripota
 Radio Tanzania Dar es Salaam niliwahi kufanya kazi na
 Lowassa katika miaka ya 90. Nilivyouona utendaji wake wa
 kazi zama hizo nashawishika kwamba anafaa kuwa kiongozi wa
 nchi yetu. Nilishuhudia akijituma kweli kweli kwenye kazi za
 umma zama hizo.

 Kadhalika
 namuunga mkono Lowassa kwa sababu hagombei Urais kupitia
 chama cha CCM ambacho kinakumbatia mfumo wa kuwadhawau na
 kuwafukarisha wananchi huku watawala wachache wakineemeka
 kwa kutumia rasilimali za nchi kama vile nchi hii ni mali ya
 watawala, familia zao na marafiki za. Ninaamini kwa kugombea
 Urais kupitia UKAWA, CCM itapunguziwa dharau na jeuri yake
 dhidi ya wananchi ambao ndio wenye mamlaka ya mwisho kuhusu
 hatma ya nchi yetu. Mfano CCM mwaka jana 2014 ilionyesha
 dharau kubwa sana kwa wananchi kwa kuizika Rasimu ya Katiba
 iliyotengenezwa kwa kutumia maoni ya wananchi wakati fedha
 zaidi ya bilioni 130 zilitumika. Kwa kutumia mabilioni hayo
 bila Katiba Mpya kupatikana ni kufisadi mali za wananchi
 mchana kweupe. Haikubaliki.

 Vile vile namuunga mkono Lowassa kwa kwa sababu
 anaukataa hadharani umaskini wa kuchongwa ambao watawala
 wanautumia kwa faida yao ili waendelee kuwanunua wananchi
 mafukara wakati wa uchaguzi na wakishapata madaraka
 waendelee kujineemesha na mali za nchi.

 Nchi yetu siyo maskini bali watawala
 wanaendekeza matakwa ya wawekezaji (wakoloni wa zama hizi za
 utandawazi wizi) ambao wanaliibia taifa rasilimali nyingi na
 na hatimaye nchi za wawekezaji hao (donors)wanawapoza
 watawala kwa vijimisaadaa uchwara. Ni aibu sana kwa kiongozi
 wa Tanzania kijipitisha nchi moja hadi nyingine Marekani,
 Ulaya, China, India na Ausralia n.k kutembeza bakuli (omba
 omba kama matonya vile) huku nchi yetu ikiwa na rasilimali
 tele. Tena wakati watawala wanakwenda kuomba eti wanapanda
 ndege daraja la kwanza. Huu ni wenda wazimu. Ni kuiaibisha
 Tanzania na Afrika.

 Sina
 chama cha siasa ninachofungamana nacho kwa sasa, lakini
 namuunga mkono Lowassa kugombea Urais kupitia UKAWA kwa
 sababu naamini akiwa Rais wa nchi yetu upuuzi huu wa
 kuendekeza umaskini kwa kuomba omba nchi za nje huku tukitoa
 mali za nchi honyo hovyo kwa wageni na kuamini kuwa
 maendeleo ya nchi yetu yataletwa kwa misaada kutoka nje,
 kutakomeshwa. Naamini hata hao wakoloni wa zama hizi za
 utandawazi wizi wanajua Lowassa hatachekacheka nao.

 Lakini zaidi namuunga mkono
 Lowassa kwa sababu Watanzania wakiridhia kwenye sanduku huru
 la kura hapo Oktoba awe Rais wa Tanzania, vyama vinavyounda
 UKAWA vitasimamia kuhakikisha kuwa mamlaka ya wanannchi
 hayaporwi hivyo hovyo tena. Kwa hiyo Rasimu ya Katiba ya
 wananchi itaheshimiwa na nchi yetu itapata Katiba Mpya
 inayotokana na maoni ya wananchi. Kwa kufanya hivyo taifa
 hili litaanza kupiga hatua kubwa ya kuondoa ufukarishwaji wa
 wananchi walio wengi unaofanya na watawala wa CCM kwa
 kushirikiana na wakoloni wa zama hizi za utandawazi wizi.

 Naridhia andiko langu hili
 lichapishwe na yeyote anayetaka
 Ananilea
 Nkya
  E-mail:ananilea_nkya@yahoo.com

 --
 Unapokea
 Email hizi kwa sababu umejiunga na Jukwaa la
 'Mabadiliko'.
 Kuchangia mada tuma kwenye
 Email hii: mabadilikotanzania@googlegroups.com


 For more
 options, visit this group at:
 http://groups.google.com/group/mabadilikotanzania?hl=en?hl=en
 ---
 You received this message
 because you are subscribed to the Google Groups
 "Mabadiliko Forum" group.
 To
 unsubscribe from this group and stop receiving emails from
 it, send an email to
 mabadilikotanzania+unsubscribe@googlegroups.com.
 To post to this group, send email to
 mabadilikotanzania@googlegroups.com.
 Visit
 this group at
 http://groups.google.com/group/mabadilikotanzania.
 To view this discussion on the web visit
 https://groups.google.com/d/msgid/mabadilikotanzania/1438381307.95951.YahooMailBasic%40web121006.mail.ne1.yahoo.com.
 For more options, visit
 https://groups.google.com/d/optout.


 --

 Send Emails to wanabidii@googlegroups.com

  

 Kujiondoa Tuma Email kwenda

 wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com  Utapata Email ya
 kudhibitisha ukishatuma

  

 Disclaimer:

 Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility
 for any legal consequences of his or her postings, and hence
 statements and facts must be presented responsibly. Your
 continued membership signifies that you agree to this
 disclaimer and pledge to abide by our Rules and
 Guidelines.

 ---

 You received this message because you are subscribed to the
 Google Groups "Wanabidii" group.

 To unsubscribe from this group and stop receiving emails
 from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.

 For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.


--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com

Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com  Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma

Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

0 comments:

Post a Comment