Tuesday, 4 August 2015

Re: [wanabidii] Lipumba, Mbatia na Mbowe mnanidai Mijeledi

we Mpombe watakutoa kucha na meno hao we shauri yako, watu wameiga dili we unawaandama

2015-08-04 9:13 GMT+03:00 'eid omari' via Wanabidii <wanabidii@googlegroups.com>:
Duh, safi sana. Nimependa namna ulivyowakilisha.


Omary Iddy,DAGROFORESTRY RESEARCH TANZANIA FORESTY RESEARCH INSTITUTE(TAFORI)P.O BOX 1257,SHINYANGATANZANIA.Tel:+255 28 276 3249MOBILE:+255 713 728 672FAX:+255 28 276 2198EMAIL:eidomari@yahoo.com

--------------------------------------------
On Tue, 8/4/15, 'mpombe mtalika' via Wanabidii <wanabidii@googlegroups.com> wrote:

 Subject: [wanabidii] Lipumba, Mbatia na Mbowe mnanidai Mijeledi
 To: "ELISA MUHINGO' via Wanabidii" <wanabidii@googlegroups.com>
 Date: Tuesday, August 4, 2015, 12:36 AM





                                        Lipumba, Mbatia na Mbowe mnanidai Mijeledi
                                Luqman
 Maloto












                                                        Juzi, nikiwa nimeketi sebuleni natazama taarifa ya
 habari, upande
  wa pili mtoto wangu Nyambo alikuwa anafanya 'homuweki'
 yake. Kila mmoja
  alikuwa 'bize' na majukumu yake ya kumalizia siku.



 Ila yeye alikuwa ananisumbua, "baba hii ni nini?" Shule
 afundishwe yeye,
  majibu nitoe mimi. Nyambo anadhani baba yake ni
 'jiniaz',
 ananiporomoshea 'viingereza' vyake "what is this?"
 Habari kwamba umande
 ulinitesa nikatoka nduki hana!



 Nilikuwa natazama Televisheni ya Al Jazeera idhaa ya
 Kiingereza, labda
 kwa kuona hivyo ndiyo akadhani 'kiinglishi' kinapanda.
 Nikimwambia sijui
  mtoto anakuwa mkali, "teacher said you should help me"
 hapo ikabidi
 niwe mkali nikamwambia "tusitukanane mtoto, ohoo!"



 Nikabadilisha 'chaneli', nikarudi kikwetukwetu! Si ndiyo
 nikakutana na
 habari moto ya Ukawa kumsafisha Waziri Mkuu aliyejiuzulu,
 Edward Ngoyai
 Lowassa! Mchana wake nilisikia minong'ono kuwa
 ameshajiunga na Chama cha
  Demokrasia na Maendeleo (Chadema). Hapo nikaamini safari
 imekwiva!



 Baba mtu nikaanza kupayuka: "Yeees CCM kwisha, 2015 CCM
 out!" Mtoto
 akanihoji: "Unashangilia Lowassa kwenda upinzani au Ukawa
 kumsafisha
 Lowassa?" Nikamjibu: "Hapa ngoma inogile mwanangu,
 Matumaini ameondoka,
 CCM vipandevipande, CCM siwapendi walimkata Matumaini."



 "Bora wewe huipendi CCM, mimi nawachukia Ukawa ni waongo
 sana," Nyambo
 alisema kwa sauti yenye ghadhabu, ikabidi nimrudi: "Wewe
 fanya homuweki
 yako achana na haya mambo ya wakubwa, unapiga kura
 wewe?"



 "Mengine yatapita, hili halipiti baba, Ukawa waongo sana
 na ukiendelea
 kuwatetea, siku nikisema uongo nisikuone unanishikia fimbo,
 patachimbika," alisema akiwa anawaka, akafunga daftari kwa
 hasira na
 kuondoka.



 Nikaona dogo anataka kunipanda kichwani, nikamwita sauti ya
 kwanza
 kimya, ya pili hakujibu akawa anaenda tu, mara ya tatu
 nikakaza sauti
 kiume, akaitika, nikamwambia arudi haraka.



 Akaja 'kinundanunda', nikamuuliza kinachomtatiza, maana
 'testi' yote ya
 Matumaini kutoka CCM ilikuwa imetoweka kwa ajili yake.
 Akanijibu: "Wewe
 kila siku nikikuongopea unanichapa halafu wengine wakisema
 uongo
 unawashangilia." Ile sauti ya Nyambo ilikaa kulialia na
 macho yalilengwa
  machozi, kama baba ninayempenda mtoto wangu, nilijisikia
 vibaya,
 ikabidi niwe mpole.



 "Kwani hao Ukawa wamekudanganya nini mwanangu?" Swali
 langu liliamsha
 mizuka ya Nyambo, alikuwa mkali kama pilipili kichaa.
 "Huyu Profesa
 Ibrahim Lipumba wa Cuf si ni yeye aliyesema CCM imewakosea
 Watanzania
 kwa kumpa Lowassa fomu ya kuomba kuteuliwa kuwa mgombea
 Urais?



 "Tena alisema mtu aliyepaswa kuwa jela kwa kosa la ufisadi
 anajitokeza
 kugombea Urais na anakwenda kuchukua fomu anapewa. Hawa
 akina James
 Mbatia wa NCCR-Mageuzi na Dk. Emmanuel Makaidi, si walikuwa
 wanatangaza
 huku na huko Lowassa fisadi? Leo hii wanamsafisha bila
 aibu!"



 Nilikosa cha kuzungumza kwa muda nikawa namtazama Nyambo,
 nikawaza sijui
  katumwa kunishawishi nibaki CCM! Alipoona nimekaa kimya
 akazidi
 kumiminika: "Siku ile Juni 18, mwaka huu kwenye mdahalo wa
 wakuu wa
 vyama vya siasa, ulioandaliwa na Taasisi ya CEO Roundtable,
 si ilikuwa
 Mwezi Mtukufu wa Ramadhan?"



 Nikapiga hesabu, nikamjibu ndiyo. Akasema: "Basi Lipumba
 hakufunga siku
 hiyo, maana nilimuona kwenye runinga akiwa amekaza misuli
 akielezea
 jinsi Lowassa anavyostahili kuwa jela, leo hapa anamsafisha,
 anasema
 kama ni mchafu mbona hajapelekwa mahakamani, huyu babu
 vipi?"



 "Homuweki yako umemaliza?" Nilimhoji ili asiendelee
 kukoroma, mtoto
 mdogo anakoroma mbele ya mkubwa, nilimuona ananikata
 'stimu'. Jibu
 nililokutana nalo lilinikata maini. Nyambo wa siku hiyo si
 sawa na wa
 siku zote: "Nitafanya homuweki ukiniahidi na hao Ukawa
 utawachapa kwa
 kusema uongo kama vile ambavyo huwa unanichapa
 nikiongopa."



 Nikamtolea macho, jamani mimi nina ubavu gani wa kuwacharaza
 viboko
 Ukawa! Tatizo la watoto wanadhani sisi wazazi wao tuna nguvu
 za kupiga
 dunia nzima. Alipoona nipo kimya akanisisitiza: "Tena yule
 Mwenyekiti wa
  Chadema Freeman Mbowe na katibu wake Dk. Willibroad Slaa
 ndiyo uwachape
  mijeledi mingi."



 Aliposema hivyo alikimbilia chumbani kwangu, aliporejea
 alikuwa
 ameshikilia nakala tatu za gazeti linalomilikiwa na Mbowe.
 "Baba unaona
 jinsi hawa watu wasivyofaa kuaminika? Hapa Mbowe anasema
 Lowassa dhaifu
 hatakiwi Ukawa kwa sababu ni bubu. Hili lingine linasema
 Lowassa
 anakaribishwa Ukawa.



 "Hili la tatu linasema Slaa amekataa watakaokatwa na CCM
 kwa sababu ni
 makapi, Ukawa hawatasimamisha mgombea aliyekatwa na CCM. Leo
 naona
 chereko za Ukawa kumpokea Lowassa na kumsafisha. Kuna uongo
 mkubwa
 kuliko huu? Kuudanganya umma wa Watanzania."



 Nyambo ndiye alikuwa nyota wa mazungumzo yetu siku hiyo,
 aliteleza kama
 amekanyaga ganda la ndizi: "Septemba 15, 2007 nilikuwa
 sijazaliwa ila
 baada ya kuzaliwa na kukuta Dk. Slaa anaitwa shujaa,
 niliamua 'kugugo'
 niuone ushujaa wake ulianzia wapi.



 "Nikakuta aling'ara kwa kuanika majina 11 ya watu
 wanaofilisi nchi.
 Orodha ya Mafisadi, List of Shame! Katika majina hayo
 aliyoyataja,
 Lowassa ni namba tisa na washirika wake Rostam Aziz na Adrew
 Chenge pia
 wamo!



 "Katika Uchaguzi Mdogo wa ubunge Arumeru Mashariki mwaka
 2012, Slaa
 alisisitiza Lowassa ni fisadi na ndiyo maana baada ya
 kutajwa kwenye
 orodha ya mafisadi mwaka 2007 hakwenda mahakamani. Akasema
 Lowassa
 amejijengea ofisi binafsi ya mbunge yenye thamani ya
 shilingi milioni
 800 wakati wanafunzi wa Monduli wanakaa chini, vilevile
 alipora mradi wa
  maji Arumeru na kuupeleka Monduli.



 "Sasa baba huyu aliyetupiwa kashfa zote hizo anasafishwaje
 leo na watu
 haohao? Fisadi papa wa jana, leo amekuwa kamanda, kivipi?
 Juni mwaka
 huu, Slaa aliandika kwenye akaunti yake ya Twitter jinsi
 ambavyo Lowassa
  hafai kwa sababu ana madoa ya uadilifu."



 Mtoto akachukua kompyuta mpakato, akatafuta vya kutafuta
 kisha
 akanionesha 'twiti' za Slaa, zilisomeka: "Lowassa
 tumemtaja katika
 Orodha ya Mafisadi walioifikisha nchi hii katika hali mbaya
 kabisa.
 Kilele kikiwa sakata la Richmond."

 Nyingine ikasomeka: "Suala kwamba watu wenye madoa ya
 uadilifu wanaota
 Urais wa nchi ni wazi kwamba kupita katika chama chao si
 uadilifu."



 Akaniuliza: "Umeona?" Kwa sauti ya iliyokosa unyoofu
 nilimjibu: "Ndiyo
 mwanangu." Kwa hakika Nyambo alinithibitishia kuwa yeye ni
 mzaliwa hasa
 wa kizazi cha kuhoji. Kwa siku hiyo alinitoa 'nokauti'
 kwa hoja zake
 nzito. "Sijui shuleni kwao mwalimu huwa anawapigisha stori
 za siasa,"
 niliwaza, maana kwenye madaftari yake hakuna somo la
 siasa.



 Nyambo katika ubora wake: "Nilisoma pia Mwenyekiti wa
 Chadema Kanda ya
 Mashariki, Mabere Marando alimhusisha moja kwa moja Lowassa
 na ufisadi
 wa fedha Benki Kuu kwenye Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA),
 vilevile
 Mwanasheria wa Chadema, Tundu Lissu amekuwa mshereheshaji
 sana wa
 ufisadi wa Lowassa. Sasa leo tunaona nini?



 "Sasa chama kipi ambacho hakizingatii maadili katika
 kupitisha majina ya
  wagombea? CCM au Ukawa? Mtu ambaye kwa zaidi ya miaka nane
 ameimbwa
 nchi nzima kuwa ni fisadi, leo hii anasafishwa kienyeji tu!
 Eti mbona
 hakupelekwa mahakamani, walitaka apelekwe na nani kama
 waimbaji ni wao
 wenyewe?



 "Yaani wewe mwenyewe utoe tuhuma halafu baadaye umsafishe
 uliyemtuhumu
 kwa sababu hakupelekwa mahakamani na unaongezea hakuna
 mwenye ushahidi
 aliwahi kujitokeza. Kwa hiyo ulikuwa unatoa tuhuma za uongo
 kufurahisha
 genge? Unajijenga kisiasa kwa uongo! Yaani baba usipowachapa
 hawa Ukawa
 na mimi hunichapi tena."



 Kwa sauti ya unyenyekevu, nilimwambia: "Basi mwanangu
 malizia homuweki
 tukalale." Akaja juu: "Nimekwambia simalizii mpaka
 uniahidi utawachapa
 mijeledi Ukawa, waongo sana! Yule Godbless Lema aliwahutubia
 wananchi
 Arusha kuwa kumkataa na kumzomea Lowassa ni jambo lenye
 heshima kubwa
 kwa nchi kwa sababu ni fisadi, leo anatamba kuwa Safari ya
 Matumaini
 inaendelea Chadema, huyu naye ni muongomuongo lazima
 umchape.



 "Wanajitetea eti Lowassa hakuwa tatizo bali mfumo uliopo
 CCM, wakati
 kila siku walimtaja moja kwa moja kwamba ni tatizo. Naibu
 Katibu Mkuu wa
  Chadema, John Mnyika alisema CCM inamlinda Lowassa kwa
 sababu upo
 ushahidi wa ufisadi wake, leo hii CCM wamemkataa kuwa
 mgombea Urais,
 Chadema na Ukawa wamemkubali, nani anamlinda?"



 Nilimwangalia, akanisistiza nijibu swali. Nikamwambia sijui,
 akaendelea:
  "Hujui eeh! Hivi Ukawa wanaposema tatizo ni mfumo, mfano
 mtu akiwa
 anaishi nyumba jirani, kila siku mnalamika hamlali
 anawaibia, siku
 akihamia nyumbani kwenu ndiyo mnasema tatizo la wizi wake
 lilisababishwa
  na nyumba aliyokuwa anaishi? Baba nijibu utawachapa
 huwachapi?"



 Kwa upole ikabidi nimwambie: "Nitawacharaza mijeledi
 waongo sana hao."
 Nilijibu hivyo ili kumaliza ubishi. Akasema: "Hapo sawa,
 nami namalizia
 homuweki yangu nikalale. Usipowachapa hatutaelewana, siyo
 unaniitikia
 tu. Na ukiwachapa uwaambie mimi ndiye niliyekutuma

  JamboLeo









 --

 Send Emails to wanabidii@googlegroups.com

  

 Kujiondoa Tuma Email kwenda

 wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com  Utapata Email ya
 kudhibitisha ukishatuma

  

 Disclaimer:

 Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility
 for any legal consequences of his or her postings, and hence
 statements and facts must be presented responsibly. Your
 continued membership signifies that you agree to this
 disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.

 ---

 You received this message because you are subscribed to the
 Google Groups "Wanabidii" group.

 To unsubscribe from this group and stop receiving emails
 from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.

 For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.


--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com

Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com  Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma

Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

0 comments:

Post a Comment