Monday 10 June 2013

Re: [wanabidii] TGNP Yaweka Bayana Matokeo Utafiti Vijiji vya Shinyanga, Mbeya na Morogoro


Ninachangia kusema kuwa utafiti wao ni mzuri. ila, Muhimu unapozungumzia vyanzo vya maji na umbali kuvionyesha au kuvielezea na aina ya vyanzo vyenyewe vilivyo. Pia, kuonyesha na hayo mashamba ya mwekezaji na yao wanavijiji. Huenda mwekezaji anatumia tu mbinu za sustainable farming ambapo wao hawatumii ktk mashamba yao lakini wakitumikishwa-hufanya kazi inayohusu kilimo endelevu na hawaigi pia.

Ajira mashambani-unaweza ukakuta hata hiyo ardhi nzuri shinyanga imetokana na mwekezaji kuweka mbolea ambayo wao ndio wanaikusanya kutoka boma zao na kumuuzia, kutumika kuichanganya na kuitandaza ila wao kwao ktk customary land na mashamba yao-kinyesi kinazalisha wadudu hakitumiki. Ndio wanakuja wageni tunawauzia ardhi halafu wao wanatuajiri kisha tunalalamika.

Mimi nimepanda miti rafiki mazingira shambani kwangu. Mbegu unaokota tu kutoka miti hiyo ilipo popote pale. Pia, hubeba mbolea ya kuku na ya ng'ombe nanunua napeleka kwa lori, nimepata veltiva grass, guetemala grass, ninafanya terracing (matuta ya kukinga maji na kuchonga ardhi) na kupanda hayo majani ktk makinga maji-terraces. Nimepanda miti ilindayo ardhi ya kunduchi-salasala liliko shamba. Kuna maeneo wazi ya wenyeji mengi hayajalimwa machaka tu na mashamba ambayo ni sandy soils. Lakini huoni mwananchi kupiga makinga maji anaona kero/tatizo/karaha. Ila wanakuja kukata miti shambani kwangu, kukata majani (guetemala) kuuza kulishia mifugo lakini kwao bare land hawapandi.
Inabidi upambane na watu wasing'oe guetemala ambayo wao wanaweza kuipanda na kupata hela kwa kuiuza na kurutubisha ardhi yao. Mbona anakuja kukata na kuuza? si anajua ubora wake ktk kupata pesa? Asingeyafuata!!


Nimefanikiwa kupita SHY na kufanya kazi Lake zone hadi Serengeti Mkoa wa Mara;
(1985-1988). Baadae (1994, 2003) na miradi mingi ya maji TZ mikoa mingine.

Ninachangia kusema hivi kwa sababu wakati mwingine unakuta kuna vidimbwi vya maji na kuna visima vya maji ambavyo ni traditional water sources na ni cha Mzee Fulani kinaitwa-Kisima cha Mzee Juma au Mwanzage (kwa Mwanzage Well). Kisma cha asili hicho kinakuwa na masharti. Mfano-hakuna kuingia ktk mazingira ya kisima na viatu, hakuna kuchotea ndoo ya chuma bali kata ya kibuyu au ndoo ya plastic utakayoikuta au kata ya kifuu cha nazi (kama kuna minazi). Hii ni kuzuia kuingiza uchafu na kutu kuchafua maji. Sehemu nyingine sheria ni kulipia hela kidogo au kuchuma eneo adjacent to the well ktk kisima kipya. Hii ya kuchimba hutumika sana Serengeti na Musoma Vijijini ambako kuna wafugaji na kila kikundi cha wafugaji hujitahidi kuwa na lambo lao la maji kunyweshea mifugo. Wewe mwenye hitaji la maji mbona hujaweka juhudi na kundi lako kuwa na source yenu? Hivyo, traditional bylaws zinakwambia-wenzako wamechimba a land water reservoir wanachota ya kunywesha mifugo na matumizi ya nyumbani. Basi utoke jasho baada ya kuchimba kibarua eneo utakalopewa ndio uchote hiyo ndoo moja ya maji. Kila ndoo moja-kipande cha kuchimba. Sio dezo. Hii inafanyika.

Huko Musoma rural utakuta kijiji kimoja mfano Masurura kina vibwaya na visima vya jadi 50+ kijiji kimoja na vimezungushiwa wigo wa mimea ya matete. Hii ni enzi hiyo ya 1985-1988 nilipofanikiwa kuwa huko Mara. Ni hivyo niliona maeneo ya Igunga vijijini, Magu, Bunda. Visima vya jadi hulindwa na tuliviboresha kwa kujengea mawe bila ya kutumia cement as a binder (Rock Wells).

Ukiangalia wananchi wanaweza kuchimba na kujengea kisima chao kutumia mawe au tofari za kuchoma kwa kutumia mafundi wao na kulinda eneo na uchafunzi na huwa wanatunga sheria ndogo ndogo na wana adhabu pia za kimila. Ila, watatembea kilometa kadhaa kwenda kisima cha mzee Juma au bwawa chafu ambalo huingiza mifugo, kuoga humo na kufua. Tumenweteka. Visima vya pampu vya deep, medium deep na shallow wells Tanzania vilianzia Shinyanga na Morogoro na kiwanda cha pampu TZ kilikuwa Morogoro. lakini huko kumetokea uharibifu wa kung'oa nati za pampu kuweka ktk plau za ng'ombe na mikokoteni (Shinyanga). Morogoro lack og maintenance unakuta mabomba hayo butu whhite elephants vijijini mpaka kuelekea kilombero. Kupata maji toka pampu muhimu kwani wanalima huko Moro na kutumia pesticides. Matumizi ya madawa ya magugu na ya kuua ukungu katika mazao ya miti.  Ukiangalia takwimu za kifafa zimepata kutokana na madawa haya ya magugu pamoja na ulaji wao wa nyama ya ngurue yenye tape worm. Morogoro yenye mito mingi na wet lands, wanachoma tofari za udongo na wamepata mafunzo vijijini ya kuchoma tofari kwa kutumia pumba za mpunga badala ya kumaliza miti. wanauza tofari sana lakini hawawezi kutumia kujengea visima kulinda uchafuzi. mawe ni mengi pia yale magumu na hutumia kwa foundation ya nyumba zao.

Vijiji vingi pamoja na Morogoro Rural, Machimboni (mawe ya thamani au dhahabu) hata mjijini mikoani Mwanza (Igoma) tunakuta video za matusi na anayeonyesha anajali pesa tu. anaonyesha kwa watoto  hapo sebureni. Pia kuna mabanda ya kuonyesha matusi hayo. Mfano. Kijiji cha Kisanga Morogoro Tarafa ya Mikumi Video za matusi kuangaliwa wakubwa na watoto lilikuwa tatizo no 1 mwaka 2008 katka shughuli za elimua ya ukimwi. Tulipowauliza kama mzazi anakuwepo, viongozi wanajua na wanatazama pia walisema ndio. lakini ni masuala ambayo yapo chini ya uwezo wao WAZAZI, WAZEE WA MILA, EXTENSION STAFF WA KATA HATA KAMA VIONGOZI WA KATA NA KIJIJI (mtendaji Kata, Kijiji na Diwani hawajali wapo corrupt). Waelimishaji jamii-wataalamu kushirikiana na wazee wa mila wanaweza wakakomesha. Ila inaonekana MILA  NA MAADILI HAKUNA. Kiasi kwamba baba na mama watu wazima wanaweza kuangalia picha za malavidavi pamoja na watoto hata kama si watoto wao wa kwao wao wamefungia home-ni Upumbavu  kukosa maadili.

Ukiangalia, mwenye video hiyo ni mtu mwenye hela au madaraka na anatishia wanaomlalamikia. Wengine hufanya siri sebuleni kwao kupata hela. Katika machimbo ni mabanda ya kipato halmashauri ya Kijiji na Wilaya hukusanya mapato daily kama wanavyokusanya kwa wanaouza biashara za chakula barabarani katika uchafu. Vibanda vya video ni vya nyasi. Watoto hufanyakazi ya amalgamation ya dhahamu kupata ujira mdogo, kuponda mawe ili akapate shs 100 akaone video. hapo anachezea mercury inammaliza. anayemfanyisha kazi hii ya mercury ni mama au baba na anayemwonyesha picha za ngono ni baba au baba-anaganga njaa, mwachieni, kajiajiri!! NCHI INAKWENDA KUBAYA.

Kuchangia huduma ya afya ni tatizo. hata kama mtu anakunywa pombe daily (ni tabia vijijini) lakini kutoa 2,000/= kwa card ya afya kwa watu 6 kutibiwa kwa mwaka na wanafunzi watano elfu 2 kwa mwaka ni tatizo. Binafsi, nimegharimia wanawake zaidi ya 20 kutibiwa Fistula bure CCBRT bila ya kupata msaada wa familia. Mume anasema alilipa mahari; familia ilidhania nina hela za mhisani ninataka kuzila peke yangu. Pamoja ya kuwaeleza kuhusu huduma ya bure CCBRT sina mhisani bado wakidhania hivyo. Baada ya kushonwa hao nikaachana nao. Utu wetu upo pembeni, tegemezi daima. Wachache sana walikubali kugharimia angalau nauli ya kuja dar.

Kesi za ubakaji ndio zilishindikana, nimeeleza humu mara nyingi. Inasikitisha sana ndugu zangu. Unakuta usiri na aibu ya kukubali kutoa ushirikiano kwa dhati. hata wewe unayejitolea unachoka kupoteza nauli yako kufuatilia kesi au shauri, unaogopa kuuawa pia. Kuna kukubali kumaliza kienyeji na kuchukua rushwa au kumezea kuficha siri na aibu. Tulitibu watoto wengi wenye magonjwa ya zinaa na kuwafanyia ushauri nasaha. Ubakaji unatokea wakienda na kurudi shule, shamba kuliko kisimani kwani kuchota maji huenda wengi zaidi. Wafanyao ubakaji zaidi ni watu wazima. Ubakaji mwingi ndani ya nyumba wazazi kuwa shamba na kuwaacha watoto na ndugu zao wao huko miezi wakihamia ndege/wanyama pori kulinda mazao wezi wasiibe mpaka wavune. Pia jirani na tegemezi la kukopa dukani kuliko huo ubakaji wa wa nje ya nyumba. Pia kulaza watoto ba vijana wakubwa au watu wazima. Baadhi ya watoto kutumika kufanya biashara kilabuni, kuuza pombe na kuanza klamba vinywaji, biashara magulioni na kurudi usiku njia za mapori. baadhi ya vijiji hukataza wanafunzi kuuza biashara/pombe vilabuni lakini biashara hizo huonekana ndio njia ya kujikimu.Magazeti ya wiki iliyopita imetoa kesi za ubakaji nyingi  pamoja na houseboy kubaka katoto ka miaka 6 na kesi za wanafunzi na jinsi wazazi wanavyoficha ukweli na kupeleka watoto kutibiwa hospitali binafsi bila kuchukua sheria. Pia wahusika wanavyokana tendo ambalo wamefanya na huwa huru pamoja na watoto kutoa vidhibiti. Denial hii ifanyiwe kazi na TGNP na kijamii mpaka wazazi wakubali kuwa wazi ili SOSPA na deski za jinsia zifanikiwe kufanya kinachotegemewa.



  
--- On Mon, 10/6/13, Joachim Mushi <mushijoa@gmail.com> wrote:

From: Joachim Mushi <mushijoa@gmail.com>
Subject: [wanabidii] TGNP Yaweka Bayana Matokeo Utafiti Vijiji vya Shinyanga, Mbeya na Morogoro
To: "Ahmad Michuzi" <amichuzi@gmail.com>, albertgsengo@yahoo.com, "Subi Nukta" <subi@wavuti.com>, "Sigfred Kimasa" <kingkif07@gmail.com>, "Emmanuel Shilatu" <pbuyegu2@gmail.com>, "Seria Tumainiel" <seria.tw@gmail.com>, "Jestina George" <jestinageorge@googlemail.com>, "Josephat Lukaza" <josephat.lukaza@gmail.com>, johnbukuku@gmail.com, "John Badi" <badijohn30@yahoo.co.uk>, "Othman Michuzi" <othmanmichuzi@gmail.com>, uwazi@hotmail.com, "Henry Mdimu" <mdimuz@gmail.com>, "Maggid Mjengwa" <mjengwamaggid@gmail.com>, "zainul mzige" <zainul.mzige21@gmail.com>, "Bashir Nkoromo" <nkoromo@gmail.com>, "Fredy Njeje" <mbeyayetu@live.com>, znzkwetu@gmail.com, "Francis Dande" <dande15us@gmail.com>, "Cathbert Kajuna" <cathbert39@gmail.com>, "francis godwin" <francisgodwin2004@yahoo.com>, father.kidevu@gmail.com, "wanabidii@googlegroups.com" <wanabidii@googlegroups.com>
Date: Monday, 10 June, 2013, 4:49

TGNP Yaweka Bayana Matokeo Utafiti Vijiji vya Shinyanga, Mbeya na Morogoro

Na Thehabari.com

MTANDAO wa Jinsia Tanzania (TGNP), umetoa mrejesho wa utafiti shirikishi uliofanywa na kikosi cha

waraghbishi kutoka mtandao huo katika baadhi ya vijiji kutoka mikoa ya Shinyanga, Mbeya na Morogoro-huku

matokeo yakionesha kuibuka kwa changamoto kadhaa katika maeneo yote ya utafiti.

Akizungumza na waandishi wa habari jana kuelezea matokeo ya utafiti, Mkurugenzi Mtendaji wa TGNP, Usu

Mallya alisema miongoni mwa masuala makuu yaliyojitokeza katika utafiti huo shirikishi na uraghbishi ni

pamoja na changamoto za uwekezaji na mgawanyo mbaya wa ardhi kwa wananchi hususan Kata ya Mshewe Mbeya

Vijijini.

Mallya alisema masuala mengine ni pamoja na ugumu wa upatikanaji wa huduma za maji safi na salama, Ukosefu

wa huduma bora za afya, uongozi mbovu na rushwa maeneo mbalimbali, pamoja na unyanyasaji wa wanawake na

wasichana karibu maeneo yote yaliofanyiwa utafiti.

Akifafanua zaidi alisema utafiti ulibani kuchukuliwa kwa maeneo ya ardhi yenye rutuba Kijiji cha Mshewe

mkoani Mbeya hali inayosababisha wananchi kukosa ardhi ya kutosha kwa kilimo na makazi hivyo kulazimika

wao kuwa vibarua katika mashamba ya wawekezaji ili kujikimu kimaisha. Hali hiyo pia imechangia wanaume

kulazimika kutoa rushwa ya pesa ili kupata kazi katika mashamba.

"Wanawake na wasichana wamekuwa wakifanya vibarua katika mashamba ya wawekezaji kwa ujira mdogo kati ya

shilingi (2,500/- na 3000/- tu kwa siku). Wakati huo huo wanakumbana na ukatili katika ajira hiyo ikiwemo

rushwa ya ngono, hali ambayo inasababisha  ongezeko la  magonjwa ambukizi yakiwemo VVU na Ukimwi.

Alisema licha ya Sera ya Taifa ya Maji kuweka lengo la kupatikana kwa maji katika umbali kwa mita 400; 

bado maji safi na salama ni changamoto kubwa kwa wakazi wa Kishapu na Mshewe kwani hakuna huduma za maji

safi na salama hali inayotishia maisha na afya zao.

"Mfano Kijiji cha Ilota- Mshewe, licha ya uhaba mkubwa wa maji wananchi wanasaka maji katika eneo

hatarishi huku wakichangia maji kidogo yasiyo safi na salama pamoja na mifugo. Cha kusikitisha  wananchi

wamechanga pesa kwa ajili ya maji kwa muda mrefu bila mafanikio. Katika vijiji vya Isoso na Lubaga Kata ya

Kishapu, ukosefu wa maji umesababisha wanawake na wasichana kutembea umbali mrefu na mazingira hatarishi

ambayo yamesababisha ongezeko la mimba za utotoni, ubakaji kwa wanawake na wasichana na vipigo."

Alisema tatizo hilo limeongeza umasikini wa kipato kutokana kutumia muda mwingi na rasilimali kusaka maji.

Kilio chao kikubwa ni kupata vyanzo mbadala vya maji hasa kutoka zi wa Victoria. Aidha aliongeza utafiti ulibainia huduma mbovu za afya kwani katika Kijiji cha Ilota Mkoa wa Mbeya wananchi wamekiri kutokuwepo na zahanati hali inayosababisha wanawake wajawazito kujifungulia majumbani, huku Kata ya Kisaki Morogoro vijijini, tatizo kubwa likiwa ni ukosefu wa dawa na wahudumu wa afya zahanati za vijiji vya Gomero, Station na Nyarutanga licha ya uwepo wa majengo mazuri bila wahudumu, dawa wala vifaa tiba kwa ajili ya uchunguzi. Eneo hilo pia wananchi huchangia gharama kubwa za usafiri wa gari la wagonjwa (shs 70,000) kwenda Morogoro hususan wanawake wanaokwenda kujifungua.

Alisema suala la viongozi kutowajibika na vitendo vya rushwa limejitokeza karibu maeneo yote ya utafiti
ikiwemo uwepo wa usiri wa taarifa za mapato na matumizi, viongozi kutowashirikisha wananchi katika masuala

ya maendeleo, viongozi ngazi za vijiji kuruhusu video za ngono kuoneshwa maeneo yao na kutotekeleza ahadi

zao kwa wananchi.
 
"Unyanyasaji wa kijinsia umejitokeza kama suala mtambuka  katika maeneo yote. Mfano tatizo la maji

linasababisha vipigo kwa wanawake, ubakaji, elimu duni kwa wasichana, mimba za utotoni na ukosefu wa

kipato. Kwa upande wa uwekezaji/ardhi, wanawake na wasichana wamekumbana na rushwa ya ngono, ajira isiyo

na staha pamoja na kipato kidogo na kwa upande wa afya, wanawake wamekuwa wakidaiwa fedha na vifaa wakati

wa kujifungua na hata kujifungulia katika mazingira hatarishi," alisema Mallya.

Aidha alisema lengo kuu la utafiti huo ilikuwa kujenga mifumo mbadala dhidi ya mfumo dume, uliberali mamboleo na mifumo yote kandamizi, huku akidai maafanikio yaliyopatikana ni pamoja na kuendeleza kampeni ya Haki ya Uchumi: Rasilimali Ziwanufaishe Wanawake Walioko Pembezoni ambayo imewezesha kujenga nguvu za pamoja na kuongeza uelewa wa masuala ya kijinsia na ukombozi wa wanawake kimapinduzi katika ngazi mbalimbali hapa nchini na hata nje ya nchi.

*Imeandaliwa na www.thehabari.com

_____________________________________________________________________
Joachim Mushi, Mhariri Mkuu wa gazeti tando la Thehabari.com
Mail address:- mushi@thehabari.com/ jomushi79@yahoo.com/ info@thehabari.com
Mobile:- 0717 030066/ 0786 030066/ 0756 469470
Web:- www.thehabari.com  
          http://joemushi.blogspot.com

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.
 
 

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.
 
 

0 comments:

Post a Comment