Monday 3 June 2013

RE: [wanabidii] MRADI WA MJI MPYA WA KIGAMBONI , SERIKALI IFUATE SHERIA SIO UBABE

Naomba kujua;

Kimbiji hii ni ile iliyojengwa na walihamishwa kutoka jijini Dar na Mzee Mustafa Songambele (wasio na kazi, miaka ya 70), sawa na Songasonga, Gezaulole, Mwanadilatu na Tegeta?

Kama ndiyo; wananchi hawa wanahitaji kupata msaada wa utetezi wa kisheria.

 

------------------------------

Marcus Falinzungu

Mob: +255 754 929460

             +255 655 929460

-----------------------------

 

From: wanabidii@googlegroups.com [mailto:wanabidii@googlegroups.com] On Behalf Of denis Matanda
Sent: Monday, June 03, 2013 2:02 PM
To: wanabidii
Subject: Re: [wanabidii] MRADI WA MJI MPYA WA KIGAMBONI , SERIKALI IFUATE SHERIA SIO UBABE

 

Wizara imevunja sheria ipi? Nijuavyo mimi ardhi ni mali ya serikali. Haki yangu mimi kama mwananchi ni kwenye fidia tu!

 

2013/6/2 Wanakijiji Kimbiji <wanakijijikimbiji@yahoo.com>

 

 

        Mradi wa Mji mpya wa Kigamboni ,Wizara ya Ardhi lazima ifuate Sheria 

        Sio Kutumia ubabe katika kuchukua ARDHI ya wananchi

 

        HAIWEZAKANI UWAONDOE WAZAWA ,ARDHI UMPE MGENI

 

 

 

Wizara ya Ardhi imejikuta kuwa mvunjivu wa sheria za nchi,na kutumia nguvu,

na kuwatisha wananchi wa wilaya Temeke  kwa kutaka kuwanyang'anya Ardhi

katika kutekeleza mradi wa mji mpya Kigamboni (KDA).

 

Malalamiko na vilio vya wananchi wa maeneo yanayokadiliwa kuanzia ekali

6,000 hadi 50,000 wilaya ya Temeke,vilio vya wananchi hao ambao wanatishiwa

kuondelewa katika makazi au ardhi zao ,vimekuwa vilio vya samaki machozi

yanakwenda na maji.

 

Sura mpya ya kutisha inayowaletea mashaka wakazi  Kigamboni na maeneo

mengine ambayo Waziri wa Ardhi Prof.Anna Tibaijuka ametangaza kuwa

yatachukuliwa kwa ajili ya ujenzi wa mji mpya Kigamboni,wananchi

wamekuwa wakijiuliza hivi serikali inaivunja sheria ya nchi kwa kupitia

wizara ya Ardhi? na kuwatosa wananchi wake katika wingu la giza !

 

Utata unakuja pale waziri Anna Tibaijuka anapozitaja kata za Pemba Mnazi,

Kisarwe II,Kimbiji, wilaya Temeke,kuwa kata hizo zitachukuliwa

ili kuongezea utanuzi wa mradi mji mpya Kigamboni,wakati maeneo ya awali

yaliotajwa jatika mradi,kata Kimbiji,pemba mnazi,kisarawe II haziku

wepo. Wananchi wa maeneo hayo wanajiuliza maswali mengi ambayo majibu

yake hakuna,

Hivi Serikali itachukua ardhi na kuwafukuza wananchi katika maeneo hayo

bila ridhaa ya wenye mali au makubaliano ?

Je ?kufanya hivyo Serikali itakuwa inavunja  "sheria za utwaaji Ardhi Na.47 ya mwaka 1967

na Sheria ya Mipango Mji Na.8 ya mwaka 2007."

 

Sheria za utwaaji Ardhi sura ya 118 inauhusu upangaji vizuri na ujenzi wa makazi tu na

siyo viwanda, maofisi,maghorofa ma tahasisi za Umma !

sasa kama sheria ndiyo hii ,Wananchi wa maeneo yaliyotajwa na Waziri Anna Tibaijuka

kwa nini waondelewe pale ? harafu wawekwe akina nani?

 

Sheria hii hairuhusu Serikali kuleta watu wengine ili kuwaendeleza kwa 

kisingizio chochote kile hata cha uwekezaji. Ardhi ikitwaliwa chini ya sheria

hii itagawanywa kwa wakazi walewale waliokuwapo baada ya kutenga maeneo ya

ardhi kwa ajili ya miundombinu.

 

Wizara ya Ardhi isijinye kichwa ngumu katika kuvunja sheria hizi na kuwa wasiri

wa kuwastukiza wanachi baadala ya kuwashirikisha katika miradi ya maendeleo,

Sheria ya Mipango Miji Na.8 ya mwaka 2007 hisitumike kama mwanya wa

kuwanyang'anya Ardhi wananchi na kuigawa na itakayobaki kuwapa

marafiki au wawekezaji,kufanya hivyo ni kuwadhurumu wapiga kura na

wananchi wa maeneo usika. ni vema taratibu za kisheria zifuate kuliko

Wizara Ardhi kutumia Ubabe.kwa sababu kifungu namba 8 cha sheria hiyo

kinataka kabla ya kutangazwa eneo kuendelezwa lazima wananchi waitwe

na waelezwe na kukubali mpango au mradi huo. 

Kinyume cha ni kuvunja sheria

 

Tangazo la serikali la 24 Oktoba 2008 kwenye gazeti la Serikali Na. 43 Vol. 89 lilikuwa na taarifa ya

 amri ambayo ilianisha mipaka ya eneo litakalokumbwa na ujenzi wa mji mpya kuwa ni kata tano

 za Somangila, Kigamboni, Vijibweni, Kibada na Mji Mwema.  http://www.youtube.com/watch?v=Jh2jQcnWcQo

tumsikilize Rais Kuhusu Kigamboni http://www.youtube.com/watch?v=UaviGdsJJNI

 

 

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.
 
 




--

Wasalaam,

 

Denis Matanda,

Mine Planning Supt,

Tanzania.

 

" Low aim, not failure, is a crime"

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.
 
 

0 comments:

Post a Comment