Thursday 27 June 2013

Re: [wanabidii] DRAFT - MUUNDO MPYA WA UTUMISHI WA WALIMU

Yataka moyo

On 24 Jun 2013 12:37, "Felix Mwakyembe" <fkyembe@gmail.com> wrote:
hahahahahahahaha, nasubiri kukuona ukiwa wa kwanza kurudi kwenye chaki, Vincent!!!

Felix


2013/6/24 Vincent Mhangwa <vmhangwa@gmail.com>
Eee unaweka kalamu chini unabeba chaki na rula ndefu ya ubao.


2013/6/24 Ntunaguzi Ntiyakunze <ntunaguzin96@gmail.com>
Mhhhhhh

Tutarudi kweli????


2013/6/23 Vincent Mhangwa <vmhangwa@gmail.com>
Ikiwa hivi  tutarudi kwenye fani, dah!


2013/6/23 Felix Mwakyembe <fkyembe@gmail.com>
Paul,

Hizo hadithi za miaka nenda rudi, graduate ananzia laki nane lini hiyo, mwakani wakati yule mfagizi bandarini anachukua milioni, kwa nini basi naye huyu mwalimu graduate asiende kufagia pale bandarini, si kila mtu anahitaji maisha bora.

Kuna kipindi graduate wa kilimo walikimbilia kuuza magazeti kama maafisa mauzo, kisa walivutiwa na package tofauti na ilivyokuwa kilimo. Wengine walikimbilia kuhesabu pesa benki, kisa inalipa na leo hii tafuta wataalamu wa kilimo kama utawapata vijana!!

Felix


2013/6/23 paul lawala <pasamila292000@gmail.com>
Mwakyembe
 
Si wanasema graduate ataanzialaki nane?ingawa bado ni danganya toto


2013/6/23 Felix Mwakyembe <fkyembe@gmail.com>
Hizi nadharia za wakalia ofisi hazitainua elimu, ni ubabaishaji ule ule.

Weka package nono uone kama watu hawatafundisha na walio nje kukimbilia huko.

Mwalimu Mhitimu wa chuo kikuu, 500,000/= kwake ni ndoto, wakati maeneo mengine ni chini ya mshahara wa kada ya chini kabisa kama vile mfagizi wa ofisi.

Felix


2013/6/23 Vincent Mhangwa <vmhangwa@gmail.com>
Hii tamu! Lakini imetolewa na nani? Mwl VM upo hapa pia? Turudi nini? imetolewa na nani? Tupe source
Vin


2013/6/22 Abdalah Hamis <hamisznz@gmail.com>

1.      UTANGULIZI

 

Kwa muda mrefu Sekta ya Elimu nchini imeendelea kukabiliwa na changamoto mbalimbali, ikiwemo ya uhaba wa Walimu katika shule na Vyuo.  Tatizo linalojitokeza lina sura mbili; Kwanza ni kupatikana wahitimu wa shule za Sekondari wenye kupenda kujiunga na mafunzo ya Ualimu.  Pili waliomo katika ajira ya Ualimu kutopenda kujiunga na mafunzo kubakia na kuendelea na kazi ya Ualimu.  Aidha, wale wanaondelea na kazi ya Ualimu kupungukiwa na ari ya utendaji kazi kunakosababishwa na mazingira ya kazi yasiyovutia.

 

Kwa upande mwingine Serikali imekuwa ikifanya jitihada za kupanua Elimu ya Msingi au Sekondari kwa kuongezea mikondo shuleni, kuongeza uandikishaji wa wanafunzi, kupanua kuboresha miundombinu kwa kushirikisha nguvu za wanachi na mipango maalumu ya Serikali kama vile Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Msingi (MMEM) na Mpango wa Maendeleo ya Elimu ya Sekondari (MMES).

 

Pamoja na jitihada hizi za serikali bado kuna changamoto ambazo zinaathiri maendeleo ya Elimu katika ngazi zote.  Changamoto hizo ni pamoja;-

 

i.       Sekta ya Elimu kutowavutia na kutowabakiza kazini Walimu

Hali halisi ya kazi na uzito wa majukumu ya Mwalimu ni kama ifuatavyo:-

·         Muda wa kuanza kazi na kumaliza kazi usio na mpaka.  Mwalimu hufundisha darasani, husahihisha husimamia mwenendo wa kazi za wanafunzi hata wawapo nje ya darasa, huandaa masomo kwa ajili ya siku inayofuata na hushiriki shughuli nyingine za kijamii.

·         Ugumu wa kazi na mazingira ya kufanyia kazi (kama shule kuwa kwenye maeneo yasiyofikika kirahisi kutokana na miundombinu duni ambayo iko nje ya uwezo wa Wizara ya Elimu) kunaifanya kazi ya ualimu isiwe na mvuto kwa wengi.

·         Kutokakana na hali iliyoelezwa hapo juu, baadhi ya Walimu wanapopata nafasi ya kuajiriwa kwenye maeneo yanayovutia kimazingira na malipo mazuri zaidi, huacha kazi Serikalini na kuajriwa kwenye shule zisizo za Serikali au kupata ajira zilizo nje ya ualimu.

·         Zaidi ya hayo, Walimu wengi hupendelea kuajriwa maeneo ya mijini, ambako kuna fursa za kuanzisha shughuli za ziada zinazowaongezea kipato (nje ya mishahara yao) pamoja na mazingira ya kuvutia zaidi.

 

 

 

ii       Uwiano wa Walimu na Wanafunzi

Kuongezeka kwa idadi kubwa ya wanafunzi wanaoandikishwa shuleni kusikolingana na idadi ya Walimu kunasababisha ongezeko la kazi na uzito wa majukumu kwa Walimu (Mfano: idadi ya wanafunzi wa Shule za Msingi iliongozeka kutoka 7,959,884,(2006) hadi 8,313,080(2009) ikiwa na uwiano wa 1:54 na Wanafunzi wa Shule za sekondari za kutoka 490,492 (2006) hadi 1,293,691 (2009) ikiwa na uwiano wa 1:49.  Hali hii inaathiri ufanisi wa Mwalimu na kufanya asiifurahie kazi yake.  Aidha, wanafunzi nao hukosa fursa ya usimamizi wa karibu wa kazi zao.

 

Kwa upande wa mafunzo ya Ualimu wa ngazi zote idadi ya wahitimu ni ndogo ikilinganishwa na mahitaji yao kwenye soko la ajira (Mfano: mwaka 2007 wahitimu wa vyuo vya ualimu na vyuo vikuu walikuwa 23,900 na mahitaji yalikuwa 35,000 Aidha, sekta binafsi inaonekana kuvutia zaidi na hivyo walimu wengi huvutiwa kuajiriwa kwenye sekta hiyo. Vile vile walimu wengine huamua kuajiajiri au kuajiriwa kwenye fani nyingine zisizo za Ualimu ambako nako kuna vivutio vya mishahara mikubwa zaidi na marupurupu mengine.

 

Sanjari na hilo, lipo ongezeko la wanafunzi lisilolingana na miundombinu iliyopo na vitendea kazi.  Hali hii inasababisha wanafunzi kulundikana kwenye vyumba vya madarasa, huku Walimu wakishindwa kuwafikia kwa urahisi . Aidha, wanafunzi hukosa fursa murua ya kupokea masomo kwa kushindwa kuandika nukuu (notes) au kuwa na usikivu hafifu (lack of concentration due  to congestion). Hali hii inakuwa mbaya zaidi kwa wanafunzi wenye mahitaji maalum.

         

          iii.     Changamoto ya Kuinua Masomo ya Sayansi

Imejidhihirisha kuwa idadi ya wanafunzi wanoamua kusoma mchepuo wa Sayansi inazidi kupungua mwaka hadi mwaka wakati mahitaji ya kitaifa ya wanasayansi ni makubwa.  Hii inasababishwa na mambo yafuatayo:-    

 

(a)          Uhaba wa Walimu wa Sayansi, unatokana na wale waliohitimu masomo hayo kutopenda kwenda kufundisha masomo ya sayansi.

(b)          Masomo ya Sayansi katika Shule za Sekondari na Vyuo vya ualimu yanafundishwa  kwa nadharia pasipo mafunzo vitendo ya kutosha kutokana na kutokuwepo kwa Mafundi Sanifu wa Maabara.

(c)          Kukosekana kwa Mafundi Sanifu wa Maabara katika shule za Sekondari kunaongeza mzigo kwa Walimu wanaofundisha masomo ya sayansi ambao hulazimika kufanya maandalizi ya mafunzo ya Sayansi kwa vitendo wenyewe.

(d)          Ongezeko hili la majukumu linamlazimisha Mwalimu kufanya kazi zake na zisizokuwa za kwake, kwa malipo ya mshahara wake tu.

(e)          Kukosekana kwa mafunzo kwa vitendo kwa wanafunzi kunalazimisha kuwepo kwa mitihani mbadala kwa vitendo (Alternative to Practicals).  Hali hii husababisha mwanafunzi kutoiva vizuri katika masomo ya sayansi, na hivyo kujenga woga kujiunga na masomo hayo.

(f)           Walimu waliohitimu kupitia utaratibu wa mitihani mbadala kwa vitendo wanapokwenda kufundisha kwenye shule zenye maabara na vifaa hukwepa kufundisha masomo hayo kwa vitendo kwa vile wanashindwa kutumia vifaa hivyo.

 

(iv)    Kada ya Fundi Sanifu Maabara katika Sekta ya Elimu

Ili kuboresha ufundishaji wa masomo ya sayansi shuleni na kukabili ongezo la majukumu kwa Walimu wa masomo ya sayansi, kuna umuhimu wa kuanzisha utaratibu wa kuwaajiri Fundi Sanifu wa Maabara.  Aidha, watumishi wa kada hii wawe na Muundo wa Utumishi chini ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi.  Kwa umuhimu huohuo, inapendekezwa kuwa Mafundi Sanifu wa Maabara wawekwe chini ya Idara za kitaaluma za shule ili waweze kupata fursa ya mafunzo ya kuwaongoza na kusimamia wanafunzi katika masomo ya sayansi kwa vitendo, kwenye vyuo vinavowafundisha Mafundi Sanifu wa Maabara.

 

2.      Dhamana ya Mwalimu katika Jamii

Ili kuwa na taifa lililoelimika, tunahitajika kuwekeza katika elimu kwa kuwa na Walimu bora wa kutosha na kuweza kuwabakiza na kuwaendeleza ndani ya utumishi wa sekta ya elimu.  Changamoto zilizoainishwa hapo juu hazitengenezi mazingira chanya ya kuwawezesha Walimu kulinda na kukidhi dhamana waliyopewa na jamii.

 

3.      Umuhimu wa Mabadiliko katika Miundo

Umuhimu wa mabadiliko katika miundo yanalenga kukabiliana na changamoto zinazojitokeza katika sekta nzima ya elimu.  Changamoto hizo ni pamoja na kuwapata Walimu wenye sifa wa kutosha katika Shule za Msingi na Shule za Sekondari, kuwavutia walimu kujiunga na kubakia katika ajira ya ualimu serikalini na kuinua ufaulu na ari ya kusoma masomo ya Hisabati, Sayansi na Ufundi.

 

4.      Hitimisho

Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi inaleta mapendekezo ya kuhuisha na kuanzisha Miundo ya Utumishi ya kada za ualimu, Wakufunzi, Mafundi Sanifu Maabara, na Wakutubi katika ngazi za Shule za Msingi, Sekondari na Vyuo vya Ualimu.

 

Mapendekezo haya yanalenga kutanzua changamoto zilizotambuliwa na kuainishwa kwa lengo la:-

·         Kufanya kazi ya ualimu iweze kuwavutia Walimu kujiunga:

·         Kuvutia Walimu kubakia katika kada hiyo; na

·         Kuinua ari ya kazi ya ualimu kwa lengo la kuinua ubora wa elimu itolewayo.

 

Hivyo, vianzia na ukomo wa ngazi za mishahara vinashauriwa virekebishwe kama ifuatavyo:-

 

Cheo

Kianzia Ngazi ya Mshahara cha zamani

Kianzia Ngazi ya Mshahara kinachopendekezwa

Mwalimu

TGTS. B

TGTS. D

Afisa Elimu Msaidizi

TGTS. C

TGTS. E

Afisa Elimu 

TGTS. D

TGTS. F

 

Aidha, Maafisa Elimu Wasaidizi/ Maafisa Elimu wa masomo ya Sayansi watakuwa na kianzia chenye kidato cha 5 cha Ngazi ya mshahara husika.

 

Muundo mpya unaopendekezwa wa Mafundi Sanifu Maabara za Shule (School Laboratory Technician) ni kwa lengo la kuinua kiwango cha ufundishaji wa masomo ya Sayansi kwa shule za sekondari na vyuo vya ualimu kwa kuwa kada hiyo haikuwepo na ni muhimu katika mchakato mzima wa ufundishaji wa Sayansi kwa vitendo.

 

Miundo iliyoboreshwa ni:-

(i)           Muundo wa Maafisa Elimu;

(ii)          Muundo wa Maafisaelimu Wasaidizi;

(iii)        Muundo wa Walimu;

 

Muundo mipya inayopendekezwa

(i)           Muundo wa Mafundi Sanifu wa Maabara ya Shule

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

MIUNDO ILIYOBORESHWA

 

Jedwali Na. 1: Muundo wa Utumishi wa Maafisa Elimu (Education Officers)

 

Cheo cha Sasa

Ngazi ya Mshahara

Ngazi ya Mshahara inayopendekezwa

Afisa Elimu Daraja la II

TGTS. D

TGTS. F

Afisa Elimu Daraja la I

TGTS. E

TGTS. G

Afisa Elimu Mwandamizi

TGTS. F

TGTS. H

Afisa Elimu Mkuu Daraja la II

TGTS. G

TGTS. I

Afisa Elimu Mkuu Daraja la I

TGTS. H

TGTS. J

 

 

Jedwali Na. 2: Muundo wa Utumishi wa Maafisa Elimu Wasaidizi (Assistant Education Officers)

Cheo cha Sasa

Ngazi ya Mshahara ya Sasa

Ngazi ya Mshahara inayopendekezwa

Afisa Elimu Msaidizi  Daraja la III

TGTS. C

TGTS. E

Afisa Elimu Msaidizi  Daraja la II

TGTS. D

TGTS. F

Afisa Elimu Msaidizi Daraja la I

TGTS. E

TGTS. G

Afisa Elimu Msaidizi Mwandamizi

TGTS. F

TGTS. H

 

 

Jedwali Na. 3 Muundo wa Utumishi wa Walimu (Teachers)

 

Cheo

Ngazi ya Mshahara ya Sasa

Ngazi ya Mshahara inayopendekezwa

Mwalimu Daraja la III

TGTS. B

TGTS. D

Mwalimu Daraja la  II

TGTS. C

TGTS. E

Mwalimu Daraja la  I

TGTS. D

TGTS. F

Mwalimu Mwandamizi

TGTS. E

TGTS. G

 

 

 

 

 

 

 

 


MIUNDO YA UTUMISHI YA MAAFISA ELIMU

(EDUCATION OFFICERS)

 

UTARATIBU WA KUAJIRIWA NA KUPANDISHWA VYEO

 

1.      Afisa Elimu Daraja la II – TGTS. F

          (a) Sifa za Kuingilia moja kwa moja

Kuajiriwa wenye Shahada ya Sayansi, Hisabati, Uhandisi, Sanaa, au Biashara, na somo la Ualimu kwa kila fani kutoka vyuo vya Elimu ya Juu vinavyotambulika na Serikali.  Wale wenye masomo ya Sayansi  wataanzia na kidato cha tano (5) cha ngazi hii ya mshahara (TGTS F. 5).

          (b)      Sifa ya kuingilia waliomo kazini:

(i)       Kubadilishwa kazi Maafisa Elimu Wasaidizi waliopata sifa za (a) hapo juu

Au

(ii)      Kubadilishwa vyeo watumishi wenye Shahada ya Sanaa/Uchumi/ Biashara/Uhasibu waliopata Stashahada ya Uzamili katika fani ya Ualimu.

          (c)      Kazi ya Kufanya:

(i)       Kufundisha katika Shule za Sekondari, kufuatana na masomo aliyosomea.

(ii)      Kuandaa maazimio ya kazi, maandalio ya masomo, zana za kufundishia/kujifunzia, mazoezi ya wanafunzi na majaribio;

(ii)          Kutunga, kusimamia na kusahihisha mitihani kwa lengo la kutathmini maendeleo ya wanafunzi.

(iii)        Kuandaa, kuwapangia kazi wanafunzi na kusahihisha mazoezi

(iv)         Kuandaa taarifa kuhusu kazi za wanafunzi na kuwasilishwa kwa uongozi wa shule

(v)          Kuandaa na kutunza kumbukumbu za maendeleo ya wanafunzi na kuwasilisha katika mamlaka husika.

(vi)         Kuratibu shughuli za shule kwa zamu

(vii)       Kusimamia vyama vya masomo (Associations)

(viii)     Kusimamia "clubs" za masomo

(ix)        Kuandaa mpango wa kazi na kutoa kipaumbele kwa majukumu kulingana na upatikanaji wa nyenzo;

(x)          Kutunza na kudhibiti matumizi ya vifaa katika sehemu aliyokabidhiwa

(xi)        Kufanya shughuli za ukuzaji mitaala;

(xii)       Kulea wanafunzi kwa:-

·         Kuwaandaa kiakili, kimwili na kijamii ili waweze kujua wajibu wao kwa jamii

·         Kufundisha tabia na mwenendo mzuri:

·         Kutoa ushauri nasaha kwa wanafunzi;

(xiii)     Kujenga mazingira yanayofaa kufundishia na kujifunzia shuleni;

(xiv)      Kufundisha Elimu ya Watu Wazima; na

(xv)       Kazi nyingine atkazopangiwa na Mkuu wa Shule

 

(xvi)    Elimu Maalum

Walimu watakaofundisha Elimu Maalum watafanya kazi zifuatazo:

(a)      Kuchapisha katika maandishi ya nukta nundu (Braille) mitihani ya wanafunzi wasioona;

(b)      Kuandaa michoro na ramani mguzo kwa ajili ya kufundishia na kujifunzia wanafunzi wasioona'

(c)      Kuchukua "ear impression" na kutengeneza "ear moulds" kwa viziwi;

(d)      Kufanya matengenezo ya shimesikio (Hearing aids) za wanafunzi viziwi; na

(e)      Kutunza kumbukumbu za matatizo ya wanafunzi wenye ulemavu yatokanayo na ulemavu yatokanayo na ulemavu walionao.

 

2.      Afisa Elimu Daraja la I – TGTS . G

          (a)      Sifa za kuingilia waliomo kazini:

Kupandishwa cheo Maafisa Elimu Daraja la II waliotumikia katika cheo hicho kwa muda usiopungua miaka mitatu (3) na utendaji mzuri kulingana na Tathmini ya Wazi ya Utendaji (OPRAS) na kusajiliwa katika chombo cha usajili wa Walimu.

au

(b)          Kubadilishwa vyeo watumishi wenye Shahada ya Hisabati/Sayansi/Uhandisi/Sanaa waliopata Stashahada ya Uzamili katika fani ya ualimu.

au

(c)          Kubadilishwa na kupandishwa Cheo Maafisa Elimu Wasaidizi waliopata sifa za (a) hapo juu.

 

(d)          Kazi za kufanya:

((i)      Kufundisha katika Shule za Sekondari, kufuatana na masomo aliyosomea.

(ii)      Kuandaa maazimio ya kazi, maandalio ya masomo, zana za kufundishia/kujifunzia, mazoezi ya wanafunzi na majaribio;

(iii)        Kutunga, kusimamia na kusahihisha mitihani kwa lengo la kutathmini maendeleo ya wanafunzi.

(iv)         Kuandaa, kuwapangia kazi wanafunzi na kusahihisha mazoezi

(v)          Kuandaa taarifa kuhusu kazi za wanafunzi na kuwasilishwa kwa uongozi wa shule

(vi)         Kuandaa na kutunza kumbukumbu za maendeleo ya wanafunzi na kuwasilisha katika mamlaka husika.

(vii)       Kuratibu shughuli za shule kwa zamu

(viii)     Kusimamia vyama vya masomo (Associations)

(ix)         Kusimamia "clubs" za masomo

(x)          Kuandaa mpango wa kazi na kutoa kipaumbele kwa majukumu kulingana na upatikanaji wa nyenzo;

(xi)        Kutunza na kudhibiti matumizi ya vifaa katika sehemu aliyokabidhiwa

(xii)       Kutoa ushauri wa kitaalamu kwa ngazi za juu kuhusu masuala mbalimbali kulingana na majukumu aliyopewa;

(xiii)     Kufanya shughuli za ukuzaji mitaala;

(xiv)      Kulea wanafunzi kwa:-

·         Kuwaandaa kiakili, kimwili na kijamii ili waweze kujua wajibu wao kwa jamii

·         Kufundisha tabia na mwenendo mzuri; na

·         Kutoa ushauri nasaha kwa wanafunzi;

(xv)       Kujenga mazingira yanayofaa kufundishia na kujifunzia shuleni;

(xvi)      Kufundisha Elimu ya Watu Wazima; na

(xvii)    Kazi nyingine atakazopangiwa na Mkuu wa Shule

(xviii)Elimu Maalum

Walimu watakaofundisha Elimu Maalum watafanya kazi zifuatavyo:-

(a)      Kuchapisha katika maandishi ya nukta nundu (Braille) mitihani ya wanafunzi wasioona;

(b)      Kuandaa michoro na ramani mguzo kwa ajili ya kufundishia na kujifunzia wanafunzi wasioona'

(c)      Kuchukua "ear impression" na kutengeneza "ear moulds" kwa wanafunzi viziwi;

(d)      Kufanya matengenezo ya shimesikio (Hearing aids) za wanafunzi viziwi; na

(e)      Kutunza kumbukumbu za matatizo ya wanafunzi wenye ulemavu yatokanayo na ulemavu yatokanayo na ulemavu walionao.


3.      Afisa Elimu Mwandamizi – TGTS. H

          (a)      Sifa za kuingilia waliomo kazini

Kupandishwa cheo Maafisa Elimu Daraja la I waliotumikia katika cheo hicho kwa miaka isiyopungua mitatu (3) na wenye utendaji mzuri wa kazi kulingana na Tathmini ya Wazi ya Utendaji Kazi (OPRAS).

          (b)      Kazi za kufanya:

((i)      Kufundisha katika Shule za Sekondari, kufuatana na masomo aliyosomea.

(ii)      Kuandaa maazimio ya kazi, maandalio ya masomo, zana za kufundishia na kujifunzia, mazoezi ya wanafunzi na majaribio;

(iii)        Kutunga, kusimamia na kusahihisha mitihani kwa lengo la kutathmini maendeleo ya wanafunzi.

(iv)         Kuandaa, kuwapangia kazi wanafunzi na kusahihisha mazoezi

(v)          Kuandaa taarifa kuhusu kazi za wanafunzi na kuwasilishwa kwa uongozi wa shule

(vi)         Kuandaa na kutunza kumbukumbu za maendeleo ya wanafunzi na kuwasilisha katika mamlaka husika.

(vii)       Kufanya tafiti mbalimbali za kielimu

(viii)     Kuratibu shughuli za shule kwa zamu

(ix)        Kusimamia vyama vya masomo (Associations)

(x)           Kusimamia "clubs" za masomo

(xi)        Kuandaa mpango wa kazi na kutoa kipaumbele kwa majukumu kulingana na upatikanaji wa nyenzo;

(xii)       Kutunza na kudhibiti matumizi ya vifaa katika sehemu aliyokabidhiwa

(xiii)     Kutoa ushauri wa kitaalamu kwa ngazi za juu kuhusu masuala mbalimbali kulingana na majukumu aliyopewa;

(xiv)      Kufanya shughuli za ukuzaji mitaala;

(xv)       Kufanya shughuli za ukaguzi wa shule

(xvi)      Kulea wanafunzi kwa:-

·         Kuwaandaa kiakili, kimwili na kijamii ili waweze kujua wajibu wao kwa jamii

·         Kufundisha tabia na mwenendo mzuri:

·         Kutoa ushauri nasaha kwa wanafunzi;

(xvii)    Kujenga mazingira yanayofaa kufundishia na kujifunzia shuleni;

(xviii)  Kufundisha Elimu ya Watu Wazima; na

(xix)     Kazi nyingine atakazopangiwa na Mkuu wa Shule

 

 

(xx)      Elimu Maalum

Walimu watakaofundisha Elimu Maalum watafanya kazi zifuatayo:-

(a)      Kuchapisha katika maandishi ya nukta nundu (Braille) mitihani ya wanafunzi wasioona;

(b)      Kuandaa michoro na ramani mguzo kwa ajili ya kufundishia na kujifunzia wanafunzi wasioona'

(c)      Kuchukua "ear impression" na kutengeneza "ear moulds"  kwa viziwi;

(d)      Kufanya matengenezo ya shimesikio (Hearing aids) za wanafunzi viziwi; na

(e)      Kutunza kumbukumbu za matatizo ya wanafunzi wenye ulemavu yatokanayo na ulemavu yatokanayo na ulemavu walionao.

UTEUZI:

(i)           Kutegemeana na utendaji/nidhamu, Afisa Elimu Mwandamizi anaweza kuwa Mkuu wa Idara, Taaluma, Nidhamu, Michezo na Miradi katika Shule ya Sekondari yenye kidato cha IV

(ii)          Afisa Elimu Mwandamizi anaweza kuteuliwa kuwa Mkaguzi wa Shule ngazi ya Wilaya baada ya kuhudhuria mafunzo ya Ukaguzi ya miezi mitatu (3).

(iii)        Endapo mtumishi huyu atateuliwa kushika apewe nyongeza moja ya Ngazi ya mshahara (Duty Post).

4.      Afisa Elimu Mkuu Daraja la II – TGTS. I

          (a)      Sifa za kuingilia waliomo kazini:-

Kupandishwa cheo Maafisa Elimu Waandamizi waliotumikia cheo hicho kwa muda usiopungua mika mitatu (3) na wenye Shahada ya Uzamili pamoja na utendaji mzuri wa kazi kulingana na Tathmini ya Wazi ya Utendaji Kazi (OPRAS)

          (b)      Kazi za kufanya

((i)      Kufundisha katika Shule za Sekondari, kufuatana na masomo aliyosomea.

(ii)      Kuandaa maazimio ya kazi, maandalio ya masomo, zana za kufundishia na kujifunzia, mazoezi ya wanafunzi na majaribio;

(iv)         Kutunga, kusimamia na kusahihisha mitihani kwa lengo la

kutathmini maendeleo ya wanafunzi.

(v)          Kuandaa, kuwapangia kazi wanafunzi na kusahihisha

           mazoezi

(vi)         Kuandaa taarifa kuhusu kazi za wanafunzi na kuwasilishwa

           kwa uongozi wa shule

(vii)       Kuandaa na kutunza kumbukumbu za maendeleo ya wanafunzi na kuwasilisha katika mamlaka husika.

(viii)     Kufanya tafiti mbalimbali za kielimu

(ix)        Kuratibu shughuli za shule kwa zamu

(x)          Kusimamia vyama vya masomo (Associations)

(xi)        Kusimamia "clubs" za masomo

(xii)       Kuandaa mpango wa kazi na kutoa kipaumbele kwa majukumu kulingana na upatikanaji wa nyenzo;

(xiii)     Kutunza na kudhibiti matumizi ya vifaa katika sehemu

aliyokabidhiwa

(xiv)      Kutoa ushauri wa kitaalamu kwa ngazi za juu kuhusu masuala mbalimbali kulingana na majukumu aliyopewa;

(xv)       Kufanya shughuli za ukuzaji mitaala;

(xvi)      Kushughulikia maswala ya utumishi katika kituo chake;

(xvii)    Kuandaa Andiko Mradi;

(xviii)  Kuandaa bajeti ya Shule

(xix)     Kuandaa taarifa mbalimbali za shule;

(xx)       Kusimamia ukusanyaji mapato na matumizi ya fedha za shule;

(xxi)     Kutoa mafunzo kwa watumishi walio chini yake

(xxii)    Kufanya tathmini ya ufundishaji;

(xxiii)  Kufanya ukaguzi wa shule wa ndani;

(xxiv)   Kulea wanafunzi kwa:-

·         Kuwaandaa kiakili, kimwili na kijamii ili waweze kujua wajibu wao kwa jamii

·         Kufundisha tabia na mwenendo mzuri:

·         Kutoa ushauri nasaha kwa wanafunzi;

(xxv)    Kujenga mazingira yanayofaa kufundishia na kujifunzia shuleni;

(xxvi)   Kufundisha Elimu ya Watu Wazima; na

(xxvii) Kazi nyingine atkazopangiwa na Mkuu wa Shule

xxvii.          Elimu Maalum

Walimu watakaofundisha Elimu Maalum watafanya kazi zifuatayo:-

(a)      Kuchapisha katika maandishi ya nukta nundu (Braille) mitihani ya wanafunzi wasioona;

(b)      Kuandaa michoro na ramani mguzo kwa ajili ya kufundishia na kujifunzia wanafunzi wasioona'

(c)      Kuchukua "ear impression" na kutengeneza "ear moulds"  kwa viziwi;

(d)      Kufanya matengenezo ya shimesikio (Hearing aids) za wanafunzi viziwi; na

(e)      Kutunza kumbukumbu za matatizo ya wanafunzi wenye ulemavu yatokanayo na ulemavu yatokanayo na ulemavu walionao.

UTEUZI:     

i.       Kutegemea na utendaji/nidhamu, Afisa Elimu Mkuu Daraja la II anaweza kuwa Mkuu wa Idara, Taaluma, Nidhamu, Michezo na Miradi katika Shule ya Sekondari yenye kidato cha VI.     

ii.       Afisa Elimu Mkuu Daraja la II anaweza kuteuliwa kuwa Msaidizi wa Katibu wa Idara ya Tume ya Utumishi wa Walimu (TSD) Mkoa, Mkaguzi Mkuu wa Shule wa Kanda, Afisa Mtendaji katika Makao Makuu ya Wizara au Tume ya Utumishi wa Walimu.  Aidha anaweza kuteuliwa kushika kazi za madaraka makubwa zaidi ya uongozi katika Wizara.

iii.      Afisa Elimu Mkuu Daraja II anaweza kuteuliwa kuwa Mkaguzi wa Kanda.  Nafasi ya uteuzi zitapendekezwa kufuatana na sifa na utendaji wenye matokeo.

iv.      Endapo mtumishi huyu atateuliwa kushika wadhifa apewe nyongeza moja ya Ngazi ya mshahara (Duty Post).

 

5.           Afisa Elimu Mkuu Daraja la I – TGTS. J

(a)  Sifa za Kuingilia waliomo kazini:

Kupandishwa cheo Maafisa Elimu Wakuu daraja la II waliotumikia katika cheo hicho kwa miaka isiyopungua mitatu (3) na utendaji mzuri wa kazi kulingana na Tathmini ya Wazi ya Utendaji Kazi (OPRAS). 

 

(i)       Kufundisha katika Shule za Sekondari, kufuatana na masomo aliyosomea.

(ii)      Kuandaa maazimio ya kazi, maandalio ya masomo, zana za kufundishia na kujifunzia, mazoezi ya wanafunzi na majaribio;

(iii)        Kutunga, kusimamia na kusahihisha mitihani kwa lengo la

kutathmini maendeleo ya wanafunzi.

(iv)         Kuandaa, kuwapangia kazi wanafunzi na kusahihisha mazoezi

(v)          Kuandaa taarifa kuhusu kazi za wanafunzi na kuwasilishwa kwa  uongozi wa shule

(vi)         Kuandaa na kutunza kumbukumbu za maendeleo ya wanafunzi na kuwasilisha katika mamlaka husika.

(vii)       Kufanya tafiti mbalimbali za kielimu

(viii)     Kuratibu shughuli za shule kwa zamu

(ix)        Kusimamia vyama vya masomo (Associations)

(x)           Kusimamia "clubs" za masomo

(xi)        Kuandaa mpango wa kazi na kutoa kipaumbele kwa majukumu kulingana na upatikanaji wa nyenzo;

(xii)       Kutunza na kudhibiti matumizi ya vifaa katika sehemu

aliyokabidhiwa

(xiii)     Kutoa ushauri wa kitaalamu kwa ngazi za juu kuhusu masuala mbalimbali kulingana na majukumu aliyopewa;

(xiv)      Kufanya shughuli za ukuzaji mitaala;

(xv)       Kushughulikia maswala ya utumishi katika kituo chake;

(xvi)      Kuandaa Andiko Mradi;

(xvii)    Kuandaa bajeti ya Shule

(xviii)  Kuandaa taarifa za shule na kuwa

...

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.
 
 

0 comments:

Post a Comment