Thursday 20 June 2013

Re: [wanabidii] CCM DHIDI YA SERIKALI 3

Ngupula Zanzibar ya sasa inasumbua. Ili uiingize kuikubali serikali moja inabidi kupitia serikali tatu.
Nje ya serikali tatu hakuna muungano. Naupenda sana muungano ndiyo maana naziunga mkono serikali tatu. Zanzibar ya sasa ni shida kwenye muungano. ukiiendeleza serikali mbili. na Rais wa zanzibar akaendelea kushauriana na 'mwenzake wa Tanzania automatically Tanzania inakuwa bara

--- On Wed, 6/19/13, Godfrey Ngupula <ngupula@yahoo.co.uk> wrote:

From: Godfrey Ngupula <ngupula@yahoo.co.uk>
Subject: Re: [wanabidii] CCM DHIDI YA SERIKALI 3
To: "wanabidii@googlegroups.com" <wanabidii@googlegroups.com>
Date: Wednesday, June 19, 2013, 8:48 PM


Kwa hili nafikiri tuwaache CCM wajaribu karata yao.Tupo wananchi wengi ambao hatutaki hata kusikia kitu kinachoitwa serikali 3...Zanzibar ya sasa hata katika muundo wa serikali 2 inasumbua,ikishindikana serikzli 2 twende kwenye moja. kama kweli tunapendana .Ngupula

From: Enock P.Ndunguru <ep.ndunguru@yahoo.com>
To: wanabidii@googlegroups.com
Sent: Thursday, 13 June 2013, 18:45
Subject: Re: [wanabidii] CCM DHIDI YA SERIKALI 3



----------
Sent from my Nokia phone

------Original message------
From: Gikaro Ryoba <gikaroryoba@yahoo.com>
To: "wanabidii@googlegroups.com" <wanabidii@googlegroups.com>
Date: Wednesday, June 12, 2013 2:31:22 PM GMT-0700
Subject: [wanabidii] CCM DHIDI YA SERIKALI 3

CCM DHIDI YA SERIKALI 3
Chama tawala
nchini Tanzania, CCM bado kinaonekana kuendeleleza sera yake ya kupinga muundo
wa serikali tatu ambao hivi sasa unapendekezwa pia katika rasimu ya Katiba Mpya
iliyowasilishwa mwanzoni mwa wiki iliyopita. Itakumbukwa kwamba hapo kabla tume
mbili zilizoundwa zilipendekeza mfumo wa serikali tatu katika muungano kati ya
iliyokuwa Tanganyika na Zanzibar lakini mapendekezo yao hayakutekelezwa .
 
Rasimu ya Katiba
Mpya imezingatia maoni yaliyotolewa na wananchi wa Tanzania ambao ndio wenye
maamuzi juu ya hatima ya nchi yao. Tume ya Nyalali na Jaji Kisanga zilipata
maoni kutoka kwa wananchi, ambao ndio waliotaka uwepo wa serikali tatu. Inasikitisha
kwamba CCM wanataka kuwaamulia wananchi aina ya serikali wanayaoitaka wao. Huku
ni kusigina demokrasia na ni dharau kubwa kwa wananchi. Siku zote CCM inadhani
kwamba wananchi ni mazezeta na kwamba hawawezi kujiamulia mambo yao wenyewe Sasa
ikiwa wananchi ndio wanaotaka serikali tatu, iweje kikundi kidogo cha wanachama
wa CCM wajifungie chumbani huko Dodoma na kuazimia kuchakachua maoni ya
wananchi?
 
Nchi hii ina
jumla ya watanzania million 45. Wanachama wote wa CCM hawazidi million 5! Iweje
kikundi cha watu million 5 watake kuchakachua maoni ya watanzania million 45? Hii
ndiyo demokrasia kweli? CCM wanataka kubaka maoni ya wananchi kwa manufaa ya
mafisadi wachache kama walivyozoea kuwatumikia mafisadi huku wakiwaacha solemba
wananchi. Hii haikubaliki hata kidogo. Ifike wakati wananchi waone kwamba CCM
haiweki maslahi ya wananchi mbele isipokuwa wanalinda maslahi ya wachumia tumbo
wachache ndani ya chama na serikali. Hii maana yake ni kwamba serikali haina
nia njema na ustawi na mustakabali wa wananchi bali inawatumia kama ngazi ya kutimizia
haja zao za kiutawala na kinyonyaji!
 
Maoni yaliyozaa
rasimu ya katiba hii yalitolewa na wananchi wote bila kujali dini, kabila,
kanda, vyama, jinsia au hali zao. Kwa hivyo, sio busara hata kidogo kwa CCM
kuwaelekeza wanachama wake wakatae muundo wa serikali 3 wakati ni wanachama hao
hao ndio waliohojiwa na kukubali kuwa na muundo wa serikali 3! Kufanya hivyo ni
sawa na kuwashikia akili watanzania na kuwaona kama hawakuwa na akili nzuri
wakati wanatoa maoni ya kuwa na serikali 3. Na nitawashangaa sana wananchi na wanachama
wa CCM watakaokubali kushikiwa akili na kubatilisha maoni yao ya awali ya kuwa
na serikali 3.
 
Tujiulize ni kwa
nini tume zote tatu (Tume ya Warioba, Jaji Kisanga na Nyalali) waliamua
kukusanya maoni ya wananchi badala ya kuwaachia CCM wawaamulie wananchi kama
wanavyotaka. Kama hali ni hiyo basi ni bora tume hizi zisingeundwa na kutumia
mamilioni ya walipakodi katika kusaka maoni ya wananchi. Basi tungewaachia CCM
(wajuzi wa kila jambo) wajifungie ukumbi wa Chamwino huko Dodoma watuamulie watanzania
aina ya katiba tunayopaswa kuwa nayo—jambo ambalo ni kubaka demokrasia
waziwazi.
 
Enyi wanaCCM/wananchi,
akili za kuambiwa changanya na za kwenu. Saa ya ukombozi ni sasa. Msikubali kamwe
kulamba matapishi yenu wenyewe. Acheni msimamo wenu wa kuwa na serikali 3 ubaki
hivyo hivyo. Nina imani kwamba kipindi mnatoa maoni yenu mlikuwa watu wazima na
mlikuwa na akili timamu. Wapuuzeni hao wanasiasa wanaotaka kuchakachua maoni
yenu kwa maslahi ya mafisadi na wachumia tumbo wachache. Wekeni maslahi ya nchi
mbele ya maslahi ya chama. Vyama vinazaliwa na kufa lakini taifa la Tanzania litadumu
milele. Tafakari, chukua hatua!

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com

Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com  Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma

Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.



--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com

Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com  Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma

Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.



--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.
 
 

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.
 
 

0 comments:

Post a Comment