Toka zama za zamani-kinaeleweka kuna nyumba nyingi za mitaa fulani mmojawapo ni eneo la kariakoo, Ilala-biashara ya umalaya ilikuwepo. Waheshimiwa wana nyumba zao maalum ambapo huenda huko kukutana na wanawake zao. Nyumba hizo ni za watu wa mchanganyiko fulani sitoutaja hapa. Wanapika masalo na kujua jamaa fulani anakuja saa ngapi na kukutana na mtu wake fulani ambae humkuta tayari hapo. hao wamama wanapika masalo ya hatari na kuilisha hiyo couple. wanafanya mambo yao na kuondoka. hivyo huwa ni vyumba vya familia. Watoto huteseka sana na kulala usiku wa manane sana. Huo ulikuwa mfumo wa Jamii hiyo akina amma wakiishi kwa mtindo huo kama kipato chao. Pia wakipika na kuuza chapati, karimati, samaki za kukaanga. Tabia ingine ni ile ya matajiri wa Kihindi kukodisha nyumba Kurasini Low density na maeneo mengine ya maficho. analipia kwa mwezi au mwaka mzima na kuweka mlinzi. kila jioni au atakapo huenda na changu doa zake huko akavinjari baadae kurudi kwa familia yake. Nyumba hizo zikitumika na wageni wa jamii hiyo kutoka nchi mbalimbali wakija bongoland kibiashara. anaweza akafikia enzi hizo Kilimanjaro hotel lakini akatayarishiwa burudani na changudoa huko katika nyumba hizo ili asionekane kule hotelini. Miunganisho mingine ikifanywa na hao telephone operators wa hotel wana marafiki zao wanaounganishwa na wababa wajao wanaotaka changudoa au mama wa kustarehe naye na ambao huja kibiashara na hao wenye kukodi nyumba za starehe. ukiwaona hao wengine wanavilemba na matasbihi mkononi. ukielezwa huko wanakokwenda chango doa-anakunywa mapombe, kaandaliwa pochopocho huwezi kuamini hilo lemba na tasbihi vya nini kama sio geresha. Wakati ilipotokea kesi ya wazungu kumlazimisha changudoa afanye ngono na mbwa miaka ile-alitokea mama mmoja kuwaambia wenzetu fulani kama huko zamani mtindo huo walikuwepo nao wazungu. akawaonyesha makovu yake mapajani jinsi mbwa wa bosi wake alivyokuwa akimrarua wakati wa tendo. akawaeleza kuwa-nyumba alizokuwa nazo Dar ambazo akipangfisha na kupata kipato alijengewa na huyo mzungu ambaye hakutaka mbwa wake awe anakwenda na vimbwa koko vya DSM. hayo yalikuwa mateso ambayo jamii haikuijua wakati ule. Pia wakati wa ukoloni-kulikuwa na wamama ambao, walikuwa wanakwenda bandarini kujipeleka kwa mabwana wazungu mabaharia na wageni wengine walikuja wakati huo. Kwenda kwao ilikuwa nia ni kutongozwa ili apate mimba azae katoto chotara. akisha kupata ujauzito-alimtoroka bwana wa kizungu na kukimbia kwenda kijijini kwao au mji mwingine asionekane. Hawa nia yao ilikuwa kupata katoto keupe kenye macho ya bluu bluu etc. Wanaofanyakazi katika baadhi ya makundi ya jamii fulani fulani nchini wanateseka kwa ngono za kulazimishwa. Kila aingiapo mpya kuendelea na kazi-hulazimishwa kutoa huduma hiyo. Kuna miaka ya nyumba kesi hizi zilitoka magazetini na baadhia yao walionyesha watoto waliozaa. Walifukuzwa kazi walipopata ujauzito. Kama akikataa kufanyiwa hivyo kutoa ngono inapotakiwa-alisingiziwa kuiba kitu hasa hela nyingi sana na kupelekwa polisi kabla hayaenda yeye kushitaki kutaka kubakwa. Mateso ya ngono yalikuwepo na ngozo za kujiuza na kuuza watu pia. Rural prostitution nayo inakuwa kwa kasi vijijini na ubakaji mwingi usiotolewa taarifa au kesi zake` kuwa ngumu kutokana na mahakama kuwa mbali, nauli kutoa uende huko kwa gharama zako na inatajwa haiishi haraka. wengine huchukua hongo na kuacha kesi ife kifo halisi. Mijini brothels nyingi na baadhi ya lodges unasikia kuwa -chumba hicho kina wenyewe mpe chumba kingine. ukiuliza chemba utasikia ni cha watu gani na kuwaona daily wakiingia na kutoka. Lodges za vijijini unaweza ukarudi ghafla ukakuta chumbani kwako ulikopanga kuna watu. wahudumu wanatumia chumba chako ulichopanga na kulipia kujipatia hela extra. unakuta walioingia humo mama amevaa khanga yako ulioiacha hapo, anajipaka mafuta yako. Kama hukuwakuta-unaona dalili si za kawaida na chanuo lina nywele zi zako. kianchokuja kutokea unapowakuta-unahama lodge. Mwenye lodge anakuona unatokea kwingine na mlishaanza kuzoeana naye mnamueleza kwa nini mmehama anashangaa haelewi kama kinaendelea hicho hapo kwake. lakini umalaya ni kipato kwa wahusika na wanaowapa nafasi ya vyumba. Kwa sasa `maisha yalivyo magumu, watu wanauza ardhi hovyo, halmashauri zinachukua customary land ya vizee na kupima viwanja. Mpaka mabonde ya kulima mpunga na mbogamboga wakati mpunga ukisha kuvunwa-umalaya na kuuza vichanga, ushoga utakua sana. taifa haliangalii kwamba ni kawaida ya mwafrika wa bongoland kulima eneo totauti mazao tofauti ya kujikimu kulingana na ecological niche. Anakaa kariakoo analima Mbezi makabe, Kibaha mazao mbali mbali. anakaa Bagamoyo Mjini analima Kiromo mihogo na ana shamba la minazi an Mikorosho huko; analima mto Ruvu mpunga na analima Kiwangwa huko ana ekari za mananasi. Kote kunachukuliwa na hawezi kulipia thamani ya viwanja hivyo inakula kwake- ardhi ni ya serikali ipo chini ya Rais. Mji/Miji imekuwa hivyo no Mashamba. Mbona ulaya kuna Cities with farms why not Africa-Tanzania? Tunauongeza umasikini na uchangudoa hadi kwa vichanga. Bibi kizee atakula wapi mashamba ya minazi na mikoroso na ya mpunga, mihogo, viazi yamekuwa house plots!! Atabaki kuviuza vijukuu maana wazazi wao wamefariki, yatima naye hana uwezo na hana ardhi. Vibabu na vijana vitakuwa vinaingia nyumbani hapo kuvibaka na kumpa bibi hela-brothels za aina yake hizo zinaanza kushamiri. Planners, land and social welfare officers, community Dev workers wanaona hii trend ya fertile lands mpaka wetland na mashamba yake kupimwa viwanja vya nyumba na wasio na ajira kukosa pa kujikimu lakini wanakula jiwe. Mtanzania anaweka mipango na policies za kuua watanzania wenzake waliomaskini bila kujali. Unapogeuza Kibaha kuwa mji na michungwa na minazi ile yote ikatwe, unapitia watu kijijini hapo plot za 25x25 feet unategemea atalima wapi na ale nini? Ahamehame aende wapi. Unapopima viwanja vya nyumba vya namna hivyo mabonde ya Morogoro yanayofaa kwa kilimo unafikilia wakale wapi. wakipanda milimani wanaondolewa au watafanya milima dongo liporomoke liwazike mvua ikinyesha. Waende wapi kama sio kuongeza ujambazi mji ambao una mabonde mazuri ya kilimo ambayo sasa ni house plots. wizi na ujambazi na uchangudoa umeongezeka. Wadada huvizia kuwepo Bunge Dodoma na kuwabamba wajapo kulala Morogoro Msamvu na kuwaibia hela!! Brothels na uchangu-tunautengeneza na zitakua zaidi. Rudisha pia mfumo wa kwenda JKT, jenga nyumba za bei ya chini ktk mashamba yale zamani yalikuwa chini ya mamlaka za mazao fulani-pamba, kahawa, chai, minazi; mashamba ya prisons, katani. Waweke huko vijana wakitoka JKT-std 7, 12, form six wape elimu ya ujasiriamali walime mazao for export na local use. wafundishe na weka viwanda vya kufunga bidhaa, kuweka label na magari ya kusafirisha nchi jirani na kwa ndege. Hakikisha hunyanga'nyi watu ardhi wanayoitegemea. maisha bora hayaji kwa mtu kupewa bali kujituma na kuwajibika kwa maendeleo yake na kwa sera na mikakati ya maendeleo ya nchi kuwa yanaona mbali jinsi ya kuwawezesha. Maisha bora ni pamoja na kukubali kujituma sio kupewa. . --- On Thu, 11/4/13, Jovias Mwesiga <ngonzy@gmail.com> wrote:
|
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.
0 comments:
Post a Comment